Mchungaji Gwajima na tabiri zake: 'Tanzania Mpya' inakuja

Asante

JF-Expert Member
Dec 18, 2009
2,084
1,076
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Kawe, Mch.Josephat Gwajima amesema Tanzania mpya yenye matumaini inakuja.

Akihubiri Kanisani hapo leo alisema ingawa yeye ni mwana CCM na vyombo vyote vilivyotumika kwenye mkutano wa ccm Jangwani jana vilitoka Kanisani kwake, alisema chama cha siasa cha ccm kipo katika wakati mgumu na kimepoteza kabisa mwelekeo na uwezo wa kuongoza dola.

Amewaonya wanasiasa wanaojiona ni wasafi na bado wanang'ang'ania ccm, wajue mwisho wao kisiasa upo ukingoni, aliwaonya Mwakyembe, Sita na wanasiasa wangine kuwa hali ya ccm ilivyo sasa ni sawasawa na samaki aliye ndani ya bwawa na maji ambalo linakaribia kukauka.

"Tanzania mpya inakuja" ulikuwa ndio ujumbe wake wa leo.

Tanzania yenye uwezo wa kukomesha rushwa inakuja.

Tanzania yenye uwezo wa kujali afya za wananchi wake inakuja.

Tanzania yenye uwezo wa kukomesha wizi wa mali za uma inakuja.

Tanzania yenye uwezo wa kuwapatia vijana wake elimu bora inakuja.

Tanzania yenye uwezo wa kuwalisha wananchi wake inakuja.

Amewatakia wananchi wote afya njema, wapate kuipokea Tanzania mpya.

Tanzania mpya inakuja - AMINA.

BAADAE: Juni 14, 2012

Kwa wale mnaomfahamu mchungaji Gwajima mtakubaliana nami kuwa ni moja ya wachungaji wenye upako wa ajabu Tanzania na wanaozungumza mambo yaliyofunuliwa kwao na Mungu.

Katika mahubiri yake ya Jumapili na jana jioni alisema kwamba amefunuliwa kuwa Sitta na Mwakyembe kwakuwa ni watu waadilifu watashindwa ku-survive ndani ya CCM maana watakuwa wanachukiwa sana na kuwekewa mizengwe na hivyo watajiunga CHADEMA kabla ya uchaguzi mkuu 2015. Pia alitabiri CCM inakwenda kuanguka na utawala utakaojali maslahi ya nchi kuundwa.

Natamani mwaka 2015 ufike haraha ili tushuhudie unabii ukitimia! Ili ukubaliane na Mchungaji kuwa CCM inakwenda kuanguka, angalia kadi za CHADEMA zinavyotafutwa kama dhahabu mitaani. Kila mtu anaulizia kadi zinapatikana wapi, maji yamebadili mkondo, hakuna anayevutiwa tena na CCM
 
Huu ndio ukweli wa mambo. Kama wanaccm wanasoma mtandao na specifically habari hii, basi WAFICHE UPUMBAVU WAO.
HII HAIHITAJI DAKIKA KUFIKIRI.
 
Huu ndio ukweli wa mambo. Kama wanaccm wanasoma mtandao na specifically habari hii, basi WAFICHE UPUMBAVU WAO.
HII HAIHITAJI DAKIKA KUFIKIRI.

wafuasi wa ccm ni wapumbavu na unajua siku zote mpumbavu haelimiki
 
Gwajima ndio mkodishaji wa vyombo vya muziki na matangazo kwaajili ya mkutano wa CCM?
 
kwanza atuambie issue ya msukule wa marehemu amina chifupa iliishia wapi....
 
tatizo kasema maneno hayo kama nani?

1. kama nabii?
2. kama kada wa CCM aliyetoa vyombo vya mkutano?
 
Huo ni uongo. Huyu ni mzushi na muongo. Anachosema ni cha kutunga ili kufurahisha watu. Hebu toa ushahidi zaidi.

Acheni bwana kutufanya sisi kama hatujui vitu. Watumishi wa Mungu wanautaratibu wao wa kuongelea viongozi.

Eti ametaja na majina ngoja tumuulize yeye maana na yeye yumo humu.
 
Hivi huyu GWAJIMA si ndo LUKUVI alienda kumuomba amuombee KIKWETE mapepo yasimvamie Ikulu? atakuwa amesoma lile andiko linalosema KWELI ITAKUWEKA HURU!
 
Huo ni uongo. Huyu ni mzushi na muongo. Anachosema ni cha kutunga ili kufurahisha watu. Hebu toa ushahidi zaidi.

Acheni bwana kutufanya sisi kama hatujui vitu. Watumishi wa Mungu wanautaratibu wao wa kuongelea viongozi.

Eti ametaja na majina ngoja tumuulize yeye maana na yeye yumo humu.

Hakuna uzushi wa uongo wowote, ccm imefika mwisho wa reli.
 
Back
Top Bottom