Mchungaji Faustine aliyefukuzwa Tanzania na kukimbilia Kenya

Mapengo 17

R I P
Mar 28, 2014
1,232
609
Nimekuwa nikisikia tetesi kuwa Mchungaji Faustine Munishi alifukuzwa Tanzania na akakimbilia nchini Kenya na nilikuwa natamani sana kujua sababu iliyofikisha hapo ni nini?

Wakuu leo kwa bahati nzuri wakati naangalia tv nimemuona Mchungaji Munishi na Juliani wakihojiwa live katika chanel ya KBC1 iliyoko Kenya, na kwa bahati nzuri swali la mwisho aliloulizwa na mtangazaji ni kuhusu mahusiano yake na Nchi ya Tanzania yakoje?

Munishi akajibu kuwa mahusiano yake na Tanzania kwa upande wa kisiasa hayako vizuri, na mgogoro huo ulianza punde tu aliporecord wimbo unaosema CCM imezeeka.

Kwa hiyo viongozi wa CCM ambao ndio watawala ndio hayuko nao vizuri, jambo linalomsababisha hata akija huku Tanzania asipewe heshima na sanaa yake isipewe kipaumbele, lakini akabainisha kuwa yeye na watanzania wako na mahusiano mazuri wala hawana tofauti yeyote.

Aliendelea kusema kuwa uwepo wake wa Kenya haina maana kuwa yeye ni mkimbizi na wala hataki kuchukua uraia wa nchi yeyote maana yeye ni Mtanzania na anaipenda Tanzania.

Mchungaji Munishi au maarufu kwa jina la wimbo wake wa Malebo akaendelea kusema kuwa pamoja na kuwa na migogoro na wanasiasa lakini yeye hapo alipo hana kadi ya chama chochote na wala sio mwanasiasa, ila tu serikali ya CCM kwasababu inatawaliwa na mabepali ingawa wanaigiza kama wanatawala kwa mfumo wa ujamaa ndio wanaomletea zengwe hilo, ila anaamini siku moja wataondoka madarakani na yeye atarudi nyumbani kwao Tanzania na kuishi vizuri tena kwa amani.

Baada ya Mchungaji Munishi kuongea maneno hayo yote nikajiuliza maswali haya, "Viongozi wa CCM wamepata wapi madaraka ya kumfukuza mtu nchini kwake? Kwanini serikali hii inaendeshwa kibabe wakati Tanzania ni nchi ya kidemocrasia? Kuna dhambi gani kwa mchungaji au kwa raia kutoa mawazo yake ya kuikosoa serikali au chama tawala?

attachment.php

Huyu ndiye Mchungaji Munishi aliyekimbilia Kenya baada ya kufukuzwa Tanzania

 

Attachments

  • Munishi.jpg
    Munishi.jpg
    23 KB · Views: 4,272
Mkuu, mbona kwenye maelezo yake hakuna mahala ambapo amesema kuwa alifukuzwa? Kinachoonekana ni kwamba mauzo ya kazi zake za kisanaa ya,eshika kutokana na kuegemea upande mmoja wa kisiasa. Kama mwimbaji wa nyimbo za injili, alipaswa kutambua kuwa wateja wake wapo ccm na upinzani. Kitendo cha kuikashifu ccm ambayo ina wateja wake wengi ni kujiua kisanii. Hivyo akaona bora akajaribu soko lake Kenya ambako mambo yanaendelea kumuwia vigumu. Wasanii mjifunze
 
toka pepo la ccm!! hata mimi namkubali sana huyu jamaa..
haswa nyimbo zake
mfano..
*mashirika ya bima (Yesu ni bima tosha)
*injili na siasa
*wanamwabudu nani?
*gazeti sio ugali..

hata mimi namsubiri kwa hamu atakaporudi nyumbani..
WELCOME TZ nchi ya maziwa na asali.
 
Mkuu, mbona kwenye maelezo yake hakuna mahala ambapo amesema kuwa alifukuzwa? Kinachoonekana ni kwamba mauzo ya kazi zake za kisanaa ya,eshika kutokana na kuegemea upande mmoja wa kisiasa. Kama mwimbaji wa nyimbo za injili, alipaswa kutambua kuwa wateja wake wapo ccm na upinzani. Kitendo cha kuikashifu ccm ambayo ina wateja wake wengi ni kujiua kisanii. Hivyo akaona bora akajaribu soko lake Kenya ambako mambo yanaendelea kumuwia vigumu. Wasanii mjifunze
mlifanya fitna....
 
toka pepo la ccm!! hata mimi namkubali sana huyu jamaa..
haswa nyimbo zake
mfano..
*mashirika ya bima (Yesu ni bima tosha)
*injili na siasa
*wanamwabudu nani?
*gazeti sio ugali..

hata mimi namsubiri kwa hamu atakaporudi nyumbani..
WELCOME TZ nchi ya maziwa na asali.

Hayo maziwa na asali labda labda uyafuate kwa wafugaji na msituni kwenye nyuki.
 
Mkuu, mbona kwenye maelezo yake hakuna mahala ambapo amesema kuwa alifukuzwa? Kinachoonekana ni kwamba mauzo ya kazi zake za kisanaa ya,eshika kutokana na kuegemea upande mmoja wa kisiasa. Kama mwimbaji wa nyimbo za injili, alipaswa kutambua kuwa wateja wake wapo ccm na upinzani. Kitendo cha kuikashifu ccm ambayo ina wateja wake wengi ni kujiua kisanii. Hivyo akaona bora akajaribu soko lake Kenya ambako mambo yanaendelea kumuwia vigumu. Wasanii mjifunze
Mungu aendelee kuwapiga upofu,muendelee kutoona tanayojiri
 
Back
Top Bottom