Mbunge mmoja wa CHADEMA sawa na Wabunge 20 wa CCM

Status
Not open for further replies.

Regia Mtema

R I P
Nov 21, 2009
2,970
864
Wakuu kwanza niombe radhi kwa kutokuwa hewani kwa muda kidogo.Nisingependa nitoe sababu za kutokuwa kwangu hewani. Kwa sasa niko likizo mkoani Tanga.Nikiwa huku Tanga nimepata bahati ya kuhudhuria Operesheni Sangara ya CHADEMA,kwakweli CHADEMA wanajitahidi kuchanja mbuga.Katika speeches nilizovutiwa nazo katika operesheni hii ni hii ya Mbunge Grace Kiwelu,yeye alisema kwamba Mbunge mmoja wa CHADEMA ni sawa na wabunge 20 wa CCM kwa utendaji,akadai kwamba wabunge wengi wa ccm sio watendaji kazi yao ni kupiga makofi tu wanapokuwa bungeni.Nakubalina na kauli ya Mbunge huyu kwamba CHADEMA imejaliwa kuwa na wabun ge vichwa na CCM imejaza makapi.Ila mimi naongeza kwamba mbunge mmoja wa CHADEMA ni sawa na wabunge 50 wa CCM
 
Ni kweli maana wengi wa ccm ni kupiga makofi tuuu bungeni endapo mmoja wao katoa hoja hata kama ni pumba mradi tuu ni ccm na wengi ni wazee wanasinzia tuuu na kuibuka wakisikia makofi na kusapoti bila kujua hoja ni ipi imesemwa.
 
jamani hivi Chadema ina jumla ya wabunge wangapi? na ni akina nani? please
 
Chadema kwa kuajiri wana JF..lol tatizo wengi wao ni blind followers...pole.
 
HIvi hamjachoka na hizi hotuba zao na haya ya Operesheni Sangara na Sato? Hivi Operesheni hii imezaa matunda kiasi gani kule kanda ya ziwa:

Matawi mangapi yameanzishwa?
Wanachama wangapi wamepatikana?
Kiasi gani kimepatikana na michango kwa chama?
 
HIvi hamjachoka na hizi hotuba zao na haya ya Operesheni Sangara na Sato? Hivi Operesheni hii imezaa matunda kiasi gani kule kanda ya ziwa:

Matawi mangapi yameanzishwa?
Wanachama wangapi wamepatikana?
Kiasi gani kimepatikana na michango kwa chama?
Kibaya zaidi wanaongelea agenda moja ufisadi ufisadi??

Elimu vipi? afya vipi? barabara na makazi vipi? mishahara na pension vipi? kilimo vipi?

wanatumia party resources (mikopo) for one agenda for four years? sipati picha wanachama kama wanaelewa na kama kuna justification ya allowances, perdiem kwa viongozi dull kama hawa.
 
Kibaya zaidi wanaongelea agenda moja ufisadi ufisadi??[/quoe]

siyo ajenda mbaya kwani haya mengine yote yamefungamana na mfumo wa kifisadi.

Elimu vipi? afya vipi? barabara na makazi vipi? mishahara na pension vipi? kilimo vipi?

Haya yote hayana maana kama hatushughulikii ufisadi kwanza; vinginevyo utawataka watu wajaribu kufanya kazi na kukamilisha haya mengine wakiuzunguluka kama pia mfumo wa utawala wa kifisadi. NI lazima tuushambulie mfumo huu ili hayo mengine yafanikiwe.


wanatumia party resources (mikopo) for one agenda for four years?

Probably it is the most important agenda of our times

sipati picha wanachama kama wanaelewa na kama kuna justification ya allowances, perdiem kwa viongozi dull kama hawa.

Haya mambo ya wanachama, wakiona hayaendani basi wao washughulikie..
 
Wakuu kwanza niombe radhi kwa kutokuwa hewani kwa muda kidogo.Nisingependa nitoe sababu za kutokuwa kwangu hewani. Kwa sasa niko likizo mkoani Tanga.Nikiwa huku Tanga nimepata bahati ya kuhudhuria Operesheni Sangara ya CHADEMA,kwakweli CHADEMA wanajitahidi kuchanja mbuga.Katika speeches nilizovutiwa nazo katika operesheni hii ni hii ya Mbunge Grace Kiwelu,yeye alisema kwamba Mbunge mmoja wa CHADEMA ni sawa na wabunge 20 wa CCM kwa utendaji,akadai kwamba wabunge wengi wa ccm sio watendaji kazi yao ni kupiga makofi tu wanapokuwa bungeni.Nakubalina na kauli ya Mbunge huyu kwamba CHADEMA imejaliwa kuwa na wabun ge vichwa na CCM imejaza makapi.Ila mimi naongeza kwamba mbunge mmoja wa CHADEMA ni sawa na wabunge 50 wa CCM

- Yale yake ya Yanga na Simba, huku wananchi wanazidi kuwa masikini wakati wabunge wote wa CCM na Chadema, wakikusanya marupurupuya ajabu sana, wakihudhuria vikao Dodoma, na kurudi Dar for the weekend kabla ya kurudi tena Dodoma kuendela na vikao huku wote waki-pollute hewa yetu bigtime na mshangingi mengi ya reconditioned, ambayo kwa majuu ni written off kwa sababu hayako efficient kwenye emissions,

- I mean we can go on and on, kuhusu kufanana kwao huyo Kiwelu si kuna wakati huwa anasafiri na lile kundi la Muungwana, hivi nini cha maana amewahi kufanya kwenye hizo safari na Muungwana kwa taifa hili?

- Ndio maana sometimes huwa ninasema it is about time sasa tuka do away na vyama vyote vya siasa nchini na kuanza upya, maana inaudhi sana!

Respect.


FMEs!
 
Kibaya zaidi wanaongelea agenda moja ufisadi ufisadi??[/quoe]

siyo ajenda mbaya kwani haya mengine yote yamefungamana na mfumo wa kifisadi.



Haya yote hayana maana kama hatushughulikii ufisadi kwanza; vinginevyo utawataka watu wajaribu kufanya kazi na kukamilisha haya mengine wakiuzunguluka kama pia mfumo wa utawala wa kifisadi. NI lazima tuushambulie mfumo huu ili hayo mengine yafanikiwe.




Probably it is the most important agenda of our times



Haya mambo ya wanachama, wakiona hayaendani basi wao washughulikie..
Ufisadi ndio ajenda...pekee lol

hapo ndipo mnaboa wananchi, ufisadi hauondolewi jukwaani ...na nchi haichukuliwi kwa ajenda moja???

Kama wananchi hawatawapa nchi ufisadi utaondokaje?...kama mdau (mwananchi) nahitaji kusikia areas kama afya, elimu, barabara, biashara, zinazungumza vipi? ili niwape kura??

besides si CCM nao wanasema wanapinga ufisadi? na mafisadi? sioni mantiki ya kuongelea miaka minne agenda moja...na wala hakuna tija zaidi ya kupoteza media air time/space, resources (scarce) ...badala kutoa alternatives wanaimba ngojera..lol
 
Hauko Tanzania, kama uko Tanzania chadema wana wabunge wa 5 CUF wanawabunge 19...is 19>5? ushabiki mwingine aibu kuwa great thinker???

Ok, kumbe Chadema ina wabunge 5, 5*20=100

kwa hiyo tunahitaji wabunge 15 zaidi ili tushike nchi!!

Chadema ikiwa na wabunge 20 tu basi imeshamaliza kazi!!
 
Sisiem Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!

Amri mpya kasi mpya nguvu mpya

Watu piiiiiiiiiiiiiiiiiiiippppppppppppppppppooooooooooooooooooooooooooo
 
Mwkjj, nakubaliana nawe kuwa ajenda ya ufisadi ndio kuu, na tatizo la ufisadi ndio sababu ya matatizo mengine yote yanayoikabili nchi!!! Shida nayopata ni kuwa, wanaharakati wengi wanaojiita wapinga ufisadi, wanazungumzia tatizo tu na sio solution ya ufisadi! Kwa wale wachache waliojitahidi wanazungumzia immediate cause lakini sijaona root casue based solution! Hii kama ncni haitusaidii sana japo ina thamani yake!

Kwangu mm wengi naona wamechukulia ajenda ya ufisadi kama mtaji wa kisiasa!

Ama kuhusu mbunge 1 chadema sawasawa na 20 wa CCM, wabunge hao labda Zitto Kabwe au Marehemu Chacha Wangwe!

Waliobaki nao ndio walewale, heshisha, kauli, busara na maamuzi ya muasisi mtei yaheshimiweeee!! Oyeeee. Pengine tofauti tu, wale wa CCM wanafanya dhahir hawa wa Chadema underground!

Wakatabaho!!
 
Chadema kwa kuajiri wana JF..lol tatizo wengi wao ni blind followers...pole.

Juzi Mbowe kasema bila aibu , kuwa JK avunje baraza la mawaziri! atawaweka mawaziri walewale ambao pia ni wabunge, hao wabunge ndio hao wanapimishwa kwenye mizani na wale wa chadema!

so kuanzia mwenyekiti ni blind hajui wajibu wake kama chama!
 
Mwkjj, nakubaliana nawe kuwa ajenda ya ufisadi ndio kuu, na tatizo la ufisadi ndio sababu ya matatizo mengine yote yanayoikabili nchi!!! Shida nayopata ni kuwa, wanaharakati wengi wanaojiita wapinga ufisadi, wanazungumzia tatizo tu na sio solution ya ufisadi! Kwa wale wachache waliojitahidi wanazungumzia immediate cause lakini sijaona root casue based solution! Hii kama ncni haitusaidii sana japo ina thamani yake!

Ndio maana niliuliza kwenye ile makala wapiganaji CCM wanapigania nini? Hadi leo sijapata jibu la kuridhisha.

Kwangu mm wengi naona wamechukulia ajenda ya ufisadi kama mtaji wa kisiasa!

Hili ni kweli.. ndio maana hutasikia wapiganaji wetu wakipigana kuubadilisha mfumo wa utawala wa kifisadi (MUK); wanachotaka wao ni kubadilisha mafisadi wa sasa ili wao waingie na kwa vile mashine ya kukoboa mafisadi inafanya kazi yake bila kukoma basi utaona watakaoingia uadilifu wao utakobolewa na wao wataibuka kama mafisadi wapya.. bila ya kubadili mfumo vita ya ufisadi haina maana ni geresha tu!
 
jamani hivi Chadema ina jumla ya wabunge wangapi? na ni akina nani? please

CHADEMA ina wabunge 5 wa kutoka majimboni na 6 wa viti maalum na wote hawa ni vichwa mtake msitake.Ni wabunge walioko kwenye orodha ya top 50 ya wauliza maswali yawe ya msingi ama ya nyongeza na pia ni vinara wa kuchangia hoja mbalimbali. Wabunge hao ni kamaifuatavyo:

1. Dk Wilibrod Slaa-Karatu
2.Zitto Kabwe- Kigoma Kaskazini
3.Charles Mwera- Tarime
4.Said Amour Arfi-Mpanda Kati
5.Philemon Ndessamburo-Moshi Mjini

Hao ni wa majimbo.
1. Grace Kiwelu
2.Halima Mdee
3.Mhonga Ruhanywa
4.Susan Lyimo
5.Anna Komu
6.Lucy Owenya

Wabunge hawa wamekuwa wakifanya vizuri sana mbishe msibishe.
 
Chadema kwa kuajiri wana JF..lol tatizo wengi wao ni blind followers...pole.

Kama wewe ulivyoajiriwa na CUF.Sidhani kama CHADEMA wanaweza kupoteza resources kwa kuajiri watu kwaajili ya kukaa hapa JF na kujibu hoja au kuanzisha hoja mbalimbli.CHADEMA inawapenzi wengi na credible wanaofanya kazi ya kutetea bila kuambiwa au kupewa posho.Labda huko kwenu CCM na CUF but not CHADEMA. Kwa maelezo yako inelekea wewe umeajiriwa na CUF na baadhi yetu humu jamvini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom