Mbunge: Heri tufe kuliko Muungano kuvunjika

Baadhi ya Wazenji wapinga-muungano wanadhani wabara wanaulilia saaana Muungano eti tu kwa sababu JK na wenzake hawajawawekea mazingira ya kuuvunja kwa haraka. Ngoja niwaambie ninachokiona Bara:-Majority ya wabara ni wakarimu na wasiopenda mizozo. Kwao hawa Zanzibar inawekera inapolalamika saana kuonewa na Bara wakati inajulikana wazi kuna mambo mengi sana Wazanzibar wanapendelewa katika Muungano huu (pengine hii inafanywa maksudi ili wasilalamike zaidi). Wazanzibar ni watanzania wanapokuwa huku Bara wakati ambapo sisi ni Wabara tunapoenda Zanzibar.Aina nyingine ya Wabara ni ile ya wanaotaka Zanzibar iache kudekezwa ili wanaopenda purukushani za mara kwa mara kama UAMSHO (Wapenzi wa CUF) wajue maisha ya sasa ni kufanya kazi kwa juhudi na si kulalamikia kukosa misaada ya OIC na FIFA kila unaposikia njaa. Mfano wa hawa ni Mimi, Mh. Tundu Lissu nk.Nisiwafiche ndugu zangu wa "nchi ya visiwa jirani". Katika hali practical huwezi kuwa na Muungano wenye usawa kati ya Tanganyika na Zanzibar hata siku moja. Sababu ni hizi zifuatazo:-1. Kuna tofauti kubwa sana zitakuja katika kuchangia gharama za Muungano huo. Can these Brothers contribute equally?2. Imagine nani atakubali kuwa soko la mitumba inayotoka Jpn, Dubai, England na kupitia kwa mwingine kama inavyotokea kwa sasa wakati wote tuna bandari zetu?3. Kama nafasi za kazi katika vyombo vya Muungano kama jeshi la ulinzi, polisi nk zitatolewa kwa idadi sawa kila upande, Zanzibar itaweza kulipia gharama za watumishi hao? Ununuzi wa vifaa vya kijeshi, kulipia mkonga wa taifa, nk je?Nikipata nafasi nitaandika thread kuelezea umaana wa serikali mbili (japo hata mimi sizitaki) pamoja na kwamba watu wanamponda mwalimu kwa muundo wa Muungano.
 
MMMhhh ndoto za mchana za maslahi binafsi... Tusiwaseemee marehemu...maana maslahi ya nchi si ya waliotutangulia kwenye haki baali wale wanaoendelea kuitafuta haki amani na usawa hapa duniani....Wajenge Hoja ipitie taratibu tujadili wote .. kama katiba inavyotaka...
 
Kwa masikio yangu nimesikia Baraza la Mapinduzi wanaomba Muungano uwe wa Mkataba
Km kweli hawa Mawaziri wafanyabiashara/Bahresa hatuwataki
 
Huyo jamaa bunge likiisha mpeni salamu ,mwambie akodi au anunue nyumba hukohuko DODOMA , WaChwaka hatakiwi hata kuonekana sura yake ,labda avae buibui na viatu vya kisigino.
 
Leo mh mbunge yahya khasim wa jimbo lachwaka zanzibar, Bungeni kasema kuwa hakuna mzanzibar yoyote ambae hautaki muungano.

Wanaoupinga muungano ni wale ambao siyo wazawa wa Zanzibar bali ni wale walio hamia Dubai tangu mwaka 1964 ndio wanaoupinga muungano.

Si ajabu ukakuta hata wale wanaojifanya kuwa hawautaki muungano huenda tayari wameshavuta kitu kidogo ndio maana wanalalama kila siku kuwa hatuutaki muungano; kumbee.....?

WaZanzibari wapinga muungano hao
we unaonaje hizo picha hao ni WaZanzibari halisi au wageni kutoka Oman??
542174_196699820445053_1931741280_n.jpg
531393_10150673060866176_222099803_n.jpg

392398_10150805906961176_750015797_n.jpg
 
Aiseee Tukundane ka laptop angu kananipa tabuu kadogo nimeona kapicha kengine kumbe hata wale chokoraa kule zenji wanapinga muungano bwana wee jameeni mm nasema nataka Tanganyika yangu kama walivyoishi mababu na bibi zangu,
542162_241500322631669_1422734381_n.jpg
 
MZIMU wa Muungano umeibuka tena bungeni jana baada ya mbunge wa Micheweni, Haji Khatibu Kai (CUF), kudai kuwa Wazanzibari wako tayari kufa njaa kuliko kuendelea na Muungano aliodai hauna tija.

Mbunge huyo alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Waziri Mkuu, alidai kuwa wananchi wa Zanzibar hawanufaiki na Muungano wakati wanaonufaika ni watu wa upande wa Tanzania Bara.

Mbunge huyo alisema muungano huo umeiondoa Zanzibar katika ramani ya dunia, hivyo ni bora ukavunjwa na kila upande ukaendelea kuwa nchi inayojitegemea.

Hata hivyo, Mbunge wa Magomeni, Muhammad Amour Chomboh (CCM) alitoa taarifa kwa Spika akidai kuwa kinachosemwa na mbunge huyo wa CUF ni mawazo yake.

“Nataka kumpa taarifa mbunge mwenzangu kuwa Wazanzibari ambao ni wazawa na wazalendo wa Zanzibar siyo kweli kuwa wanaukataa Muungano na wala hawako tayari kufa kwa njaa kwa ajili ya kuukataa,” alisema Chomboh.
 
HUYO MBUNGE WA MICHEWENI ANAHITAJI KUPELEKWA MIREMBE WAKAPIME AKILI YAKE WAKATI ANGALI YUPO DODOMA.


UCHAGUZI WA MIJITU ISIYO AKILI NI UPUMBAVU WA IGNORANCE YA WAPIGA KURA


KULE PEMBA KUNA KAULI WALIITOA WAKISEMA

'Aje Mtume Muhammad akagombee Jimbo kwa Kupitia CCM na Liwekwe Jiwe kugombea Jimbo Kupitia CUF; Wallahiladhimu Sie twachagua Jiwe'

Sasa ndio Kachaguliwa KICHAA.

Na matatizo kama haya yako maeneo yenye ushabiki wa CHADEMA.

Watu wanapiga kura za hasira.

It is a hight time ikatolewa Civic Education Nchi Hii
 
NITAUTETEA MUUNGANO

img-4684-1.jpg


RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dkt Ali Mohamed
Shein amesema ataendelea
kuutetea Muungano na hakuna
atakaemlaghai wala kumchezea katika uongozi
wake. Kauli hiyo ameitowa
jana katika mkutano wa
Jumuiya ya Wastaafu wa
Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania uliofanyika Bwawani mjini
Unguja.

Dk Shein amesema kwamba
yeye ndie rais wa Zanzibar na
ndie mwenye mamlaka na
hatomuogopa mtu wala kusita
kuwachukulia hatua kwa wale
wote ambao watakwenda kinyume na matakwa ya
kikatiba.

Alisema kuwa dhamana ya
nchi hii pamoja na ile ya
Jamhuri ya Muungano imo
mikononi mwao kati yake na
Rais Jakaya Kikwete na ndio
maana wakawa wanashirikiana na
kushauriana kwa yale yote
ambayo yana maslahi na nchi.

“katika kuiongoza Zanzibar
mimi ndie rais simuogopi mtu
yeyote”, alisema kwa
kujiamini Dk Shein.

Dk Shein alisema Zanzibar ni
nchi ya kidemokrasia inayotoa
uhuru wa maoni kwa kila mtu,
lakini kwa upande wake
pia yeyé ndio mwenye
dhamana kubwa ya kuendesha nchi kwa
mujibu wa katiba iliyopo.
“Mimi ndio rais siogopi mtu
katika kuendesha nchi, siko
tayari kuirudisha nchi katika
misukosuko na kuirejesha Zanzibar kule ilipotoka wakati
iko katika hali ya amani hivi
sasa,” alisema katika mkutano
huo.

Hata hivyo alisema kuwa
Muungano upo na utaendelea
kuwepo na kwani yeye ndiye
rais ambaye anatokana na
chama cha mapinduzi na pia
ameingia madarakani chini ya ilani ya chama chake hivyo
lazima afuate ilani ya chama
chake ambapo alisema
changamoto zilizomo
zinahitaji kujadiliwa ili
kuweza kuziondoa na sio kuvunja muungano.

“Hakuna mtu asiyejua kuwa
kuna kero za Muungano hivyo
ni vizuri tukajitokeza kwa
wingi katika kutoa maoni yetu
juu ya katiba na sio kukaa
pembeni yanazungumzwa mengi kuhusu mimi lakini yote
nimeyapokea kwa kuwa
ukubwa ni jaa”, alisema Dk
Shein bila ya kutaja jina lakini
alikuwa akijibu hoja
zilizokuwa zimeibuka kuwa hana uwezo wa kuchukua
maamuzi magumu katika
suala la uongozi.

Aliwaeleza wastaafu hao
kwamba Muungano una kero,
zinazojadiliwa na ndio maana
njia nyingi, ikiwemo ya
mawasiliano baina ya Rais wa
Zanzibar na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
zimeanzishwa ili kuzitafutia
ufumbuzi ambapo alisema njia
hizo zitaendelea kutatua
mambo ya muungano.

Aidha Dk Shein alisema kazi
hiyo anaifanya kwa umakini
ili kuhakikisha kuwa
Muungano upo na unazidi
kuwepo na kwamba
wasioutaka wasubiri tume ikija ndio watoe maoni yao na
sio kuanza kutoa maoni hivi
sasa kabla ya wakati hufika.

“Hakuna asiyejua katika
Muungano kuna kero,…
wananchi wazijadili kupitia
tume ya mabadiliko ya katiba,
na kwa nini tunaanza kusema
sema… subirini tume mkatoe maoni yenu” alisema. Katika hatua nyengine Dk
Shein alisema kwa sababu
hiyo anaagiza kutokufanyika
kwa maandamano ya aina
yoyote kuhusiana na suala hilo
na kuwataka wazanzibari kutoshiriki hadi
pale wanaotaka kufanya hivyo
wanaporuhusiwa kuandamana
na jeshi la polisi kwa kufuata
taratibu za kisheria.

“Naagiza
maandamano yasifanyike,…
wakiruhusiwa kufanya basi
msiende kushiriki,” alisisitiza
Dk Dk Shein alikuwa
akizungumza na zaidi ya watu 500, waliohudhuria katika
mkutano huo, ambao ni
wastaafu wa taasisi za
Muungano waliopo Zanzibar.

Katika waliohudhuria katika
mkutano huo ni taasisi mbali
mbali pamoja na Bunge, Ulinzi
na Uslama, Mambo ya Nje,
Mamlaka ya hali ya hewa
(TMA), Mamlaka ya Kodi na mapato (TRA), Mamlaka ya
Usafiri wa Anga (TCAA), Idara
ya Uhamiaji, Shirika la Posta
na Simu, na taasisi za masuala
ya elimu na ufundi.

Sambamba na hayo aliwataka
vijana kuthami ni jitihada,
michango na maelekezo ya
wastaafu kwa kutambua
kuwa uzoefu wao katika
maisha ni sehemu muhimu kwa maendeleo yao. “Sote hatuna budi kuelewa
kuwa iko siku tutakuwa
wastaafu hivyo ni muhimu
kujitayarisha hasa kwa
kujenga tabia ya kujiwekea
akiba na matayarisho mengine ya lazima kwa maisha ya
wastaafu”, alisema.

Akizungumza katika mkutano
huo Mwenyekiti wa jumuiya
hiyo , Mohamed Ali Maalim,
alisema miongoni mwa
majukumu ya jumuiya hiyo ni
kudumisha Muungano kwa sababhu unalinda maslahi ya
wastaafu wote nchini. Katika risala yao wastaafu hao
wamesema kwamba
wanakabiliwa na changamoto
mbali mbali ndani ya Jumuiya
yao ikiwemo uwezo mdogo
wa uendeshaji na usimamizi wa ofisi ikiwemo ukosefu wa
ofisi ya kutosheleza mahitaji.

Katibu mkuu wa Jumuiya hiyo
Rashid Ali alitaja changamoto
nyengine ni kukosekana kwa
wataalamu na waratibu wa
kusimamia utekelezaji wa
mipango ya Jumuiya, ukosefu wa vitendea kazi, ukkatika
kutekeleza malengo yao. Jumuiya ya wastaafu Zanzibar
imeanzishwa mwaka 2009 ina
wanachama 537 ambapo 486
kati ya hao ni wastaafu wa
Jeshi la Wananchi wa
Tanzania.

SOURCE: Zanzibaryetu.blogspot.com
 
Kama ni muungano baina yake na mke wake ataulinda usivunjike. Lakini kama ni muungano wa nchi mbili, wananchi wenyewe ndio wenye uwezo wa kuamua kama uvunjike au la.
 
Yeye ni nani?? Labda wake na mkewe, zaidi ye si ni mtetezi wa magamba tu?? Aondoe ushamba wake wa uko mchambawima na mfereji maringo
 
Hakuna Kuvunjika kwa Muungano. Ni upepo tu Utapita. Si mnataka Zanzibar Iwe nchi ya Kiislam. Hakuna kitu kama Hicho. Muuanze Kufuga Magaidi na Kufukuza Watanganyika na Wakristo. NEVER GONNA HAPPEN
 
Safi sana mheshimiwa rais na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi.

Lazima tuenzi makubaliano yaliyoongozwa na mwalimu jk nyerere na sheikh aa karume

tanzania tanzania jina lako ni tamu sana
 
Hapa Dr. Shein atakuwa amewaudhi UAMUSHO kupita kiasi.

Vipi Dr. Shein makanisa yaliyochomwa moto utayafidia kwa kutumia kodi za Wazanzibari?
 
HUYO MBUNGE WA MICHEWENI ANAHITAJI KUPELEKWA MIREMBE WAKAPIME AKILI YAKE WAKATI ANGALI YUPO DODOMA.


UCHAGUZI WA MIJITU ISIYO AKILI NI UPUMBAVU WA IGNORANCE YA WAPIGA KURA


KULE PEMBA KUNA KAULI WALIITOA WAKISEMA

'Aje Mtume Muhammad akagombee Jimbo kwa Kupitia CCM na Liwekwe Jiwe kugombea Jimbo Kupitia CUF; Wallahiladhimu Sie twachagua Jiwe'

Sasa ndio Kachaguliwa KICHAA.

Na matatizo kama haya yako maeneo yenye ushabiki wa CHADEMA.

Watu wanapiga kura za hasira.

It is a hight time ikatolewa Civic Education Nchi Hii
Na wewe mbona unaongea kama kichaa,sasa CHADEMA hapo inahusikaje!!
 
Pale wananchi wanapokuwa brainwashed na kuambiwa hata likisimamishwa jiwe, ikiwa chadema lazima lipigiwe kura


huku ni kupotosha jamii


dhambi za cuf na chadema zinafanana

na wewe mbona unaongea kama kichaa,sasa chadema hapo inahusikaje!!
 
huyu naye bana..kuongea kwenyewe tu hajui ..urais kapewa afu anajitunisha kifua ...aghhh
 
Pale wananchi wanapokuwa brainwashed na kuambiwa hata likisimamishwa jiwe, ikiwa chadema lazima lipigiwe kura


huku ni kupotosha jamii


dhambi za cuf na chadema zinafanana
Na dhambi za ccm za kudiriki kuwatoa roho wale wanaotofautiana nao kimawazo unaziweka kundi gani?
 
Back
Top Bottom