Barua ya wazi kwa Mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania

MESAYA

Member
Jan 4, 2012
55
52
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Nianze waraka wangu huu kwa kutanguliza salamu zangu za dhati kwako. Kwa taratibu za mila na desturi za kimasai, napaswa nikusalimie kama baba yangu kwa kusema "Airoroki papa". Tukirudi kwa lugha yetu mama ya taifa napaswa nikusalimu kwa kusema "Shikamoo baba". Vile vile kwa kuwa una wawakilisha watanzania wanaoamini kwa Imani za dini mbalimbali, nisiwanyime nao ladha ya salamu zangu kwako. Nianze kwa salamu za kikristu ambapo napaswa niseme "Bwana Yesu asifiwe Mheshimiwa Rais". Nikisema pia "Asalam Aleikum Warahman tulahi Allah wabarakatu" nafikiri utanielewa nawakilisha kundi lipi.

Mheshimiwa Rais, ama baada ya aya nzima ya salamu zangu kwako, nikupe pole sana kwa maradhi yaliyokupata hivi majuzi na kupelekea mwili wako kufanyiwa upasuaji. Pole sana kwa hilo na Mwenyezi Mungu mwingi warehema muumba wa mbingu na dunia akujalie kheri upone haraka na urudi katika hali yako ya kawaida kiafya ili uendelee kuwatumikia watanzania.

Mheshimiwa Rais, mimi ni kijana wa kimasai niliyebahatika kupata elimu hadi ya chuo kikuu kwa kutegemea ufugaji wetu ule ule wa kuhama hama kutafuta malisho ya mifugo na maji. Aina ya uchumi wetu huu umetusaidia tulio wengi kupata fursa za kusoma ijapokuwa kwasasa tumedhamiria kuwarudisha watu wa jamii hii katika lindi la umasikini tororo kwa kuona umuhimu wa mwekezaji kwenye ardhi yao na kuyapa kisogo matunda wanayoyapata kwa aina hii ya uchumi wanaoendesha kwenye ardhi yao.

Mheshimiwa Rais, nadhani umezunguka na kupita kila kona ya nchi hii. Nadiriki kusema kila hatua uliyopiga ndani ya viunga vya nchi hii, hujawahi kumkuta ama kumwona mtanzania mwenye asili ya umasai ambaye amekaa barabarani akisubiri wapiti njia wamtupie japo chochote kitu ili afanikishe kusonga mbele kwa maisha yake. Bali umekutana na wamasai ambao wamekuwa mstari wa mbele wakichakarika huku na kule ama kwa kuwalinda watanzania wengine ili apate ndarama za kuendeshea maisha yake, ama kwa kusokota na kusuka nywele za dada zetu ili tu mdomo uende kinywani, ama wakizunguku kila kona kutoa huduma za kuponya afya za watanzania kwa kuuza dawa za asili ili mradi tu kuitwe jioni na hatimaye kesho, ama wakisafiri huku na kule na mikokoteni yenye madumu ya maji wakihakikisha kwamba watanzania wote wanapata huduma ya maji kwa malipo yatakayowawezesha kupata mkate wa kila siku. Hiyo ndiyo asili ya mmasai, kamwe haishi kutafuta ili mkono uende kinywani na kamwe hawezi kuwa ombaomba.

Mheshimiwa Rais, Lengo langu kubwa leo si kukupa sifa za kabila hili la wa masai bali nimejaribu tu kukuonyesha ni athari gani tutapata jamii ya wamasai kama sera hii ya taifa itaendelea ya kutunyang'anya ardhi yetu tuliyopewa na Maulana na kumpa mwarabu ama mzungu kwa kisingizio cha uwekezaji.

Mheshimiwa Rais, Nisikuchoshe sana kwa utangulizi mrefu ambao sio lengo kuntu la barua yangu hii kwako. Lengo hasa la Makala hii kwako, ni kufikisha mawazo yangu kama mtanzania wa daraja la mwisho kabisa kwako ambaye sidhani kama ipo hata siku moja nikapata nafasi japo hata ya kukusalimu shikamoo na ukaitikia marahaba.

Mheshimiwa Rais, Mawazo yangu haya ya leo yanaweza yakawa yamezungumzwa na watanzania walio wengi wenye nafasi mbalimbali ndani ya nchi hii ila sidhani kama walizungumza kwa namna hii ambayo mimi leo nimeamua kuwasilisha kwako. Nimekuwa na desturi ya kuandika Makala za kila namna kwa umma kama njia niliyojiwekea kuwalipa fadhila watanzania wenzangu wa Vijiji vya Nadosoito na Mkonoo ambao naamini nimepata elimu na makuzi yaliyo bora kwa busara, hekima na malezi yao.

Mheshimiwa Rais, Kama mtiririko na muendelezo wa karia yangu ya uandishi wa Makala, leo nimeona niwasilishe Makala yangu kwako kwa namna ya barua kama alivyokuwa anafanya mwanamapinduzi wa India Nerhu kwa kijana wake Indra Ghandhi (Glimpses of the World history)

Mheshimiwa Rais, Makala yangu hii ya leo inahusu mustakabali wa muungano wetu kwa vizazi vijavyo. Naamini utavutiwa sana kuona uwepo wa vijana wachache ndani ya taifa hili ambao wanawaza juu ya mustakabali wa nchi hii na vizazi vijavyo.

Mheshimiwa Rais, Nianze kwa kukumbusha japo kidogo juu ya sababu za Tume ya Jaji Nyalali kupendekeza uwepo wa serikali ya Tanganyika. Sina maana kwamba hujui, wala sina maana kwamba umesahau, bali nataka nitengeneze msingi wa hoja yangu ya mustakabali ya muungano wetu kwa vizazi vijavyo.


  1. Kutambua usawa wa nchi mbili ambazo zimejiunga katika Muungano uliozaa Tanzania. Tume ilizingatia hali ya sasa ambapo nchi moja kati ya zile zilizoungana, inatambuliwa wakati nchi nyingine imefutika katika utambulisho wa serikali ya Muungano.
  2. Kwa kuipa Tanganyika serikali yake, unaondoa ile hofu ambayo imeelezwa mara kwa mara kwamba Zanzibar itamezwa na Tanganyika, hasa kwa kutambua ukweli kwamba masuala ya Tanganyika na yale ya Muungano yanashughulikiwa pamoja, jambo ambalo linawapa watendaji wa serikali ya muungano fursa ya kuingilia mambo ya Zanzibar bila sababu.
  3. Kuondoa hisia za watu wa Tanganyika kwamba wananyonywa na wazanzibari katika kuchangia gharama za uendeshaji na katika kugawana madaraka, hasa kwa kuzingatia hali ya sasa ambapo nafasi za Tanganyika ziko wazi kwa Wazanzibari wakati za Wazanzibari haziguswi na Mtanganyika.
  4. Kuondoa hali isiyoeleweka na isiyoingia akilini, ya kuwa na Muungano ambao unabaki ni kitendawili daima. Nchi mbili zinajiunga halafu moja inakuwa na serikali yake lakini ya pili serikali yake inaipata mumo humo ndani ya Muungano

Mheshimiwa Rais, Kung'ang'ania kusema kwamba Tanzania lazima itakufa kama serikali ya Tanganyika ikundwa ni jambo ambalo haliishi kushangaza walio wengi. Kwanza tunasahau kwamba ili kuunda Tanzania ilibidi kwanza iwepo Tanganyika. Kama kuwepo kwa Tanganyika 1964 hakukuzuia Tanzania kuzaliwa, kwanini leo kuwapo kwa Tanganyika LAZIMA kupelekea kufa kwa Tanzania? Hii ni mantiki ya wapi?

Mheshimiwa Rais, Kwa kuwa hoja ya msingi inayosimamiwa na wabunge wa CCM katika kupinga serikali tatu ni idadi ya watu ya watu waliotoa mapendekezo hayo kuwa walikuwa wachache, kwanini usifunguliwe mjadala utakaoongozwa na hasasi mbalimbali za kiraia juu ya hili ili ukweli upatikane?

Mheshimiwa Rais, Kama tunavyosema mwamba ngozi haishi kuvutia upande wake, chukulia mfano kukatokea ubishi kati ya serikali ya Zanzibar na ile ya Tanzania na ikabidi timu mbili zikutane kupata suluhisho, na upande mmoja ukiwakilishwa na wazanzibari watupu na upande mwingine ukawakilishwa na nusu wazanzibari na nusu watanganyika, huo utakuwa mjadala wa aina gani?

Mheshimiwa Rais, Kwa hakika, huu ni muundo ambao kudumu kwake kunategemea kutokuwepo na migongano ambayo inahitaji mjadala wa pande mbili, kila upande ukisisitize maslahi yake, jambo ambalo ni upuuzi kuliamini katika dunia hii ya nipe nikupe.

Mheshimiwa Rais, Aina hii ya Muungano wa serikali mbili uliyopendekezwa na "Bunge maalumu la Katiba la CCM" kwenye katiba pendekezwa ni bomu na manowari za kuuwa Muungano huku tukiimba wimbo wa "Tudumishe Muungano"

Mheshimiwa Rais, Rai yangu katika hili ni kwamba iwapo tunataka kudumisha Muungano, hatuna budi tuchague moja, ama tunaunda Muungano wa serikali moja ama tunaunda Muungano wa serikali tatu.

Mheshimiwa Rais, Ili kuendelea kuwa na Muungano ulio imara na unaokubalika na wananchi wa pande zote:

a) Hatuna budi kutambua kwamba wananchi hawawezi wakaupenda Muungano kwasababu tu viongozi wa pande mbili wanaalikana, hawa kwenda kule na wale kuja huku, wakastarehe na kufurahi basi. Ni lazima kuhakikisha kwamba wananchi wa kawaida wananufaika kutokana na manufaa yanayotokana na Muungano.

b) Hatuna budi kuachana na dhana potofu za kudhani kwamba Muungano uliopo ndio huo huo na wala hauruhusiwi kufanyiwa marekebisho

c) Viongozi na wananchi wanaowaongoza hawana budi kujenga utamaduni wa kujadili waziwazi matatizo yao badala ya kujiingiza katika manung'uniko ya chini chini, ambayo ni dalili ya unafiki na chanzo cha vurugu katika nchi. Kama uwazi na ukweli havitathaminiwa, kuvumiliwa na kuheshimiwa, matokeo yake yatakuwa ni chuki dhidi ya Muungano na dhidi ya viongozi na pia Tanganyika dhidi ya Zanzibar na Zanzibar dhidi ya Tanganyika.

d) Hatuna budi kuamini pia kwamba, jambo lingine linaloweza kuamsha hisia za chuki lile la upande mmoja kuona kwamba upande mwingine unaingilia mambo yake ya ndani huku hauna uwezo wala haki ya kuingilia mambo ya ndani ya upande ule mwingine.

e) Hatuna budi kuelewa kwamba hali ilivyo sasa wabunge wa Zanzibar wa kuchaguliwa wapo watano (5) Kwenye bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Maana yake kila mbunge anawakilisha wananchi wapatao laki mbili na sitini (260,000) wakati baadhi ya wabunge wa bara wanawakilisha wananchi zaidi ya laki tatu na thelathini (330,000). Pamoja na kuwepo kwa idadi hii ya wabunge watano kutoka Zanzibar kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bado Zanzibar ina Baraza la wawakilishi ambalo lipo kwa ajili ya kutunga sheria zinazohusu Zanzibar pekee. Ilihali hawa wa Tanganyika wapo kutunga sheria za Tanganyika na Zanzibar kwa wakati mmoja kwani Bunge la Tanzania ndio hili hilo Bunge la Jamhuri. Ili kulinda muungano hatuna budi kutafuta na kuweka utaratibu ili wabunge wa Zanzibar wawe na idadi inayowiana na wingi wa wananchi wanaowawakilisha.

f) Ni lazima tutambue kwamba kuendelea na mtindo uliopo sasa, ni kuwanyima baadhi ya wananchi haki ya kuwa na uwakilishi unaofanana na mazingira yao. Kama haifai kuwa na serikali ya Tanganyika ambayo maana yake inakuwa na Bunge au Baraza la Tanganyika, itabidi tutafute njia nyingine ya kuhakikisha kwamba uwakilishi wa walio wengi haufutwi kwa nguvu ya wachache. Ninachosema ni kwamba, kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania mabadiliko ya kikatiba hayawezi kupitishwa bungeni ila tu kwa kupata theluthi mbili ya wabunge wa Zanzibar. Hii ina maana iwapo wabunge wa Zanzibar hawataki jambo lipite, wanaweza kuliua kwa kukubaliana miongoni mwao, hata kama jambo lenyewe ni kipengele kinachohusu bara katika katiba.

g) Ni lazima yawepo mabaraza matatu, moja la Zanzibar, moja la Tanganyika na moja la Muungano. Katika Baraza la Muungano ambalo litakuwa kama Seneti, uwakilishi uwe sawa sawa kwa bara na visiwani, kwa kutambua usawa wa dola mbili zilizoungana. Yale mabaraza mengine mawili yafanye kazi kwa uhuru unaotambuliwa na katiba na yakubali kuelekezwa na Baraza la Muungano. La sivyo, kama serikali ya Tanganyika ni haramu kwa hiyo baraza lake pia ni haramu, tukubali kutekeleza mantiki ya uwiano wa wingi wa watu. Tanganyika ambayo ina watu wapatao milioni 43 iwe na wabunge 300 na Zanzibar yenye watu milioni 1.3 iwe na wabunge 5

Mheshimiwa Rais, nisikuchoshe sana kwa siku ya leo ila uapatapo barua yangu hii aitha moja kwa moja ama kupitia kwa vyombo vyako vya usalama, tafadhali legeza moyo wako na tafakari juu ya mustakabali wa Muungano wetu kwa vizazi vijavyo ili lisijebaki kama historia kama ilivyokuwa kwa Muungano wa Nchi za Kisoviet.

Mheshimiwa Rais, Nashukuru sana kwa kunipa muda wako kwa kupitia maandiko haya ya kijana wa kitanzania mwenye ndoto za kuvunjika kwa Muungano kama tutaendelea na mfumo huu wa serikali mbili. Mwisho kabisa nimalizie na usemi wetu wa Kimasai unaosema "Tanzania tamelono nimunyanu kanaa naishi oo kule"

Asante

Ni mimi wako katika harakati za ukombozi wa fikra,
Ole Mesaya
+255 712 814 285
 
Ugumuwa Kumshauri rais Kikwete [na ombwe la uongozi Tanzania]
Gazeti la Raiamwema September 16, 2009

Sasa kuna malalamiko ya watu wengi kuwa washauri wa Raiswanampotosha. Wengine wanasema Rais hana washauri kabisa. Ukiwauliza washauriwenyewe, katika mazungumzo yasiyo rasmi wanasema, "wao wanasema"lakini hawawezi kumlazimisha Rais kukubali ushauri wao.

Baadhi yao nadhani wanajisikia vibaya wanaposikia lawama za watuwengi juu ya wajibu wao wa kushauri, na wamefikia siku za karibuni kuanzakusema, "Rais hashauriki", "haambiliki", "nimbishi" n.k.

Haya si maneno mazuri kusemwa na washauri wa Rais, na ikiwawanayoyasemani kweli, itakuwa heshima kubwa kwao kujiuzulu warudi katikavibarua vyao vya zamani. Kuendelea kumshauri rais asiyeshaurika, asiyeambilikana mbishi ni kosa kwa mshauri, si kwa mshauriwa.

Ukiendelea kushauri bila kusikilizwa, basi ujue umekubali kuwasehemu ya tatizo. Wakati ni kosa la kimaadili kwa rais kutowasikiliza washauriwake, lakini ni kosa zaidi kwa washauri kuendelea kutoa ushauri usiosikilizwa.
Kama wanabaki ili baadaye waje kuunda asasi za kutuambiayaliyotokea Ikulu wakati wa utumishi wao, wajue hatutawasikiliza. Twawezakuwasikiliza sasa na kuwaheshimu ikiwa watajiheshimu na kuacha kushauri bilakusikilizwa.

Kundi la kwanza la washauri
Rais wetu ana makundi sita ya kumshauri na ambayo kwa haliilivyo yameshindwa kumshauri kama nitakavyobainisha kwa kila kundi. Kundi lakwanza ni la wazee wastaafu, wengi wao ni wanasiasa. Kundi hili linajumuishamajeruhi wa mheshimiwa Rais katika mbio zake za kuingia Ikulu.
Tangu mwaka 1995, Jakaya Kikwete alijichimbia katika mikakati yakuingia Ikulu, na si siri kuwa baadhi ya mikakati ilijaa fitna na vikumbovilivyowajeruhi baadhi ya wazee hawa.

Ili kuwashinda, ilibidi timu yake itumie mbinu za medani ambazohata sasa, miaka minne baadaye, zinamfanya ashindwe kufungua moyo wake nakuzungumza na wazee hawa au kuteta nao bila kujisikia kusutwa.
Kutokana na hali hii, wazee hawa hawawezi kumshauri, akapokeaushauri wao bila kuutilia shaka hata kama wakifanya kwa moyo mweupe. Halikadhalika, wazee hawa, kibinadamu, hawawezi pasipo shaka kusema wanasikitika palewanapoona mambo hayaendi sawa.

Kwao, yasipokwenda sawa ni rahisi kusema, "tulijua hayayatatokea". Kwa bahati mbaya, Mheshimiwa Rais katika siku za karibuni,ameshindwa kuwadhibiti mashabiki wake na wana habari wake pale walipoanza tenakuwashambulia wazee hawa kwa kejeli na vijembe katika magazeti kadhaa yenyekulenga kumsifia lakini yakiendelea kuwachafua wazee hawa.
Laiti kama yangemsifia bila kulazimika kuwachafua wazee hawa,Rais angejipatia fursa murua ya kushauriana na wazee hawa. Hili limeongeza ufakati ya Rais na wazee wastaafu na kwa hiyo niseme, hawawezi kumshauri kwalolote.

Kinachotawala ni unafiki na usanii wa kupiga picha katikamatukio maalumu.
Kwa upande wao, wazee baada ya kushambuliwa magazetini, wamekaakimya kwa sababu pia sehemu ya fadhila zao za kikatiba zimo mikononi mwa Ikulu,kama vile pensheni, matibabu, ulinzi, na matunzo mengine.
Unahitajika ujasiri wa ajabu kumsema mtu anayekutunza kwa mambohaya hata kama ni haki yako kikatiba.

Kundi la pili la washauri
Kundi la pili la washauri ni la wanaoitwa "WanaMtandao". Hiki ni kikosi-kazi kilichomwingiza Rais Ikulu. Kilijaa wababena kuongozwa zaidi na maslahi binafsi badala ya uzalendo. Kutokana na mbinuchafu zilizotumika kufikia lengo, kikosi hiki kilijeruhi na kujeruhiwa, nahapajakuwapo na nafasi ya kutibu majeraha haya kwa pande zote.
Falsafa ya Rais wetu juu ya majeraha haya ni kutegemea mudauyaponye, lakini baadhi ya vidonda vinanuka na uvundo wake unasikika kitaifa.Kwa juu juu Mtandao umesambaratika, lakini kivuli na mwangwi wake vinamtishaRais na kumnyima raha kila wakati. Anahitaji ushauri nasaha kuishi na hali hiiasiyoweza kuibadili.
Kinachotisha kuhusu Mtandao ni ukweli kuwa kwa macho yakealishuhudia wana Mtandao wakiwararua washindani wake bila huruma, na kwa hiyoanawajua jinsi wanavyorarua. Ujuzi huu ukigeuziwa kwake hapatatosha, kwa sababuwana mtandao walitanda kila mahali – majeshi yote, serikalini, chamani, kwenyemadhehebu ya dini, asasi za kiraia, vyuo vikuu na hata katika balozi zetu.

Kundi hili lingeweza kumshauri Rais lakini sasa haliwezi kwasababu kwanza linaogopana lenyewe; pili, Rais analiogopa pia na tatu, haliwezikukutana kwa uhuru kama ilivyokuwa zamani.
Hivi sasa linakutana kwa kujificha kana kwamba linapanga ujasusiau ugaidi. Mara nyingi ushauri unahitaji kuaminiana kila upande na wakati woteushauri unaojenga haufichwi.

Kundi la tatu la washauri
Kundi la tatu ambalo humshauri Rais kwa masuala mazito ni Idaraya Usalama wa Taifa. Tangu Rais Kikwete aingie Ikulu idara hii imekumbwa namatatizo makubwa mawili. Kwanza, historia yake na Rais huyu ni ya shaka, kwasababu inadaiwa kuwa idara hii "haikumtaka" kuwa kati ya wagombea.
Kuna madai kwamba taarifa maalumu iliyoandaliwa na Idara kuhusumgombea ambaye ni Rais wa sasa, haikuwa "nzuri" japo haikufuatwa navikao vya chama.

Wengine wamedai kuwa hayo madai si chochote bali ni uzushi tu,lakini wengine wanahoji kuwa kama ni uzushi, basi hiyo ni hatari zaidi kamaIdara hii haikuandika taarifa hiyo kwa jinsi ambavyo wana Mtandao walikuwawanafanya rafu za awali katika mchakato.
Kama hoja ya kwanza ni kweli, basi hilo linatosha kuwanyima wanaIdara hiyo fursa ya kumshauri Rais waliyemkataa katika "taarifa yaomaalumu" kwa Mwenyekiti aliyepita. Kumtumikia Rais, au mtu mwingineyeyote, uliyemkataa au kumwandika vibaya, kunahitaji ujasiri wa pekee.

Pili, Idara hiyo imekumbwa na mgongano wa maslahi paleinapolazimika kutumikia Taifa au kutumikia fedha. Matokeo ya mgongano huo niwatumishi wa Idara kujikuta wakitumikia wana Mtandao wenye fedha au kumtumikiaRais na Taifa bila kujali kama wanalipwa vizuri au la.
Hali hii haiwezi kuwapa fursa ya kumshauri vyema Rais katikamasuala makubwa ya kitaifa kwa sababu Rais anashawishika, wakati mwingine,kuwaangalia usoni kujiridhisha kama hawakutumwa na watu fulani.
Katika hali ya sasa, ambamo chama tawala kimegawanyika katikamakundi ya kimaslahi, kwa maumbile ya binadamu, Idara itavutika zaidi kuelekeakundi lenye dau kubwa. Dalili ya mgongano huu ni uvujaji wa taarifa nyeti zavikao vya chama na Serikali, ufisadi wa kidola unaowezeshwa na idara hii naukuwadi wa idara kwa chama tawala.

Enzi ya Mwalimu Nyerere Idara hii ilikuwa kioo. Tuliopitwa nawakati, tunaangalia hali hii na kutoa machozi. Kimsingi, Idara hii imebakikujikomba kwa watawala na si kushauri tena.

Kundi la nne la washauri
Kundi la nne ambalo lingemshauri Rais ni chama chake. Tumekwishakuona jinsi CCM ilivyosambaratika katika makundi ya kimaslahi katikati ya ombwela kiuongozi na kiitikadi.
Rais hutoka katika chama na wakati wote chama huwa ndichokimbilio lake mambo yanapokwenda mrama. Hata kama rais ni wa watu wote, lakinimchango wa ushauri kutoka chama chake husaidia kuboresha afya ya rais katikakuliongoza taifa.

Hali si hivyo kwetu. Rais Kikwete ni Mwenyekiti wa chama chake,lakini ndani ya chama kuna wenyeviti wengi wa makundi yaliyomo. Ni kama yeye niMwenyekiti kwa nje ya chama lakini ndani ya chama wamo wengine, tena wenyenguvu na ushawishi kuliko yeye.
Watendaji wa kazi za chama wanawasikiliza wenyeviti wa ndanikuliko wanavyomsikiliza Mwenyekiti yeye ambaye ni Rais wa nchi. Lazima katikahali hii, pale chama kinapojaribu kumshauri Rais, atashuku ushauri huo naanaweza kuupuuza akiuita kuwa ni fitna au majungu.
Kwa ujumla, fursa hii imepotezwa na haiwezi kupatikana kwasababu makundi ya ndani yamekidhoofisha chama na hakuna jitihada za wazikurejesha mshikamano. Kwa upande mwingine hii ni fursa kwa Taifa kufikiriamaisha bila CCM!

Kundi la tano la washauri
Kundi la tano ni la watendaji wateule serikalini; yaanimawaziri, makatibu wakuu, makamishna, wakurugenzi na wateule wengine wa Rais.Chini ya Katibu Mkuu Kiongozi, timu hii ndiyo hujenga hoja kwa njia yamadokezo, taarifa na hata mikakati ya kushughulikia masuala muhimu ya kila sikukatika Taifa.
Enzi za Mwalimu Nyerere, kundi hili lilimsaidia sana Baba waTaifa na lilikuwa na uhuru wa kumwona, kumshauri na hata kumwandaa kwa ajili yakukabiliana na matukio makubwa.

Mwalimu alilipa uhuru wa kubishana naye nje ya jukwaa ilimradiajenda ilikuwa na maslahi ya Taifa, na si maslahi ya kundi au mtu. Kwa haliilivyo sasa, kundi hili la wataalamu ni kama halipo au liko katika vipandevipande vya kimaslahi pia.

Kashfa nzito kama EPA, Deep Green, Richmond, TRL, IPTL n.kzimeliacha kundi hili likiwa hoi bin taabani. Haliwezi kumshauri Rais kwasababu ama linanuka rushwa nzito au lenyewe linahofia lisije kuwajibishwabaadaye endapo ufisadi utakuja kujitokeza katika ushauri lililoutoa kwa Rais.
Hata pale Rais anapolitaka kama kundi au mtu binafsi, kumpa ushaurikatika masuala nyeti, kigugumizi kinatawala na hakuna uwazi wa kweli uliojengwakatika utii utokao moyoni. Balaa zaidi katika kundi hili ni pale uteuzi wakeulivyogubikwa na maslahi ya kundi fulani.

Inapotokea kuwa uteuzi wa Rais kwa mtu unatanguliwa na michakatoisiyo rasmi nje ya mamlaka ya Rais, mteuliwa hujikuta ana mgongano wa utii katiya anayeteua na aliyefanya ukuwadi kwa manufaa ya mteuliwa.
Si siri sasa kuwa wateuliwa wa Rais wanasogezwa mezani kwa Raisna watu wenye historia zinazotia shaka juu ya uadilifu wao na uzalendo kwaTaifa.
Mgongano huu hauwezi kumpa ujasiri mtoa ushauri na wala hauwezikumpa ujasiri Rais kupokea ushauri huo kwa moyo mweupe. Mifano iko mingi yamaamuzi yaliyofanywa na Serikali au na Rais mwenyewe na baadaye yakaja kubatilishwakwa kushindwa kutekelezeka kutokana na ukweli kuwa hapakuwa na uwazi na ukwelikatika kuyaandaa.

Tukubali ukweli – kundi hili liko taabani na ndiyo maana maamuzimengi yanachukua muda mrefu sana kwa sababu watendaji wanakwepa kufanyamaamuzi.

Kundi la sita la washauri
Kundi la sita ni la viongozi wa dini. Rais wetu ni Mwislamulakini pia amekuwa karibu na viongozi wa madhehebu kadhaa ya Kikristo.Nimemshuhudia mwenyewe kwa mazungumzo ya ana kwa ana akihangaika na kulalamikajuu ya mnyukano wa dini mbili kubwa nchini (Uislamu na Ukiristo), na kwelihaumpi raha hata kidogo.
Anajua jinsi dini hizi mbili zinavyotuhumiana juu ya maamuzi yaRais na Serikali yanayozigusa.
Wakristo wanadai kwa wazi na sirini kuwa Rais anawapendeleaWaislamu, wakati Waislamu nao wakidai Wakristo wanapendelewa sana na Serikaliya Rais wetu.

Matokeo yake ni Rais kukosa msimamo na kubaki kulalamika nakutilia shaka kila ushauri anaopewa na watu watokao pande hizo mbili za dini.Katika harakati za kuwasikiliza, Rais amejikuta njia panda katika maamuzimbalimbali.
Panapo majaliwa, mada hii itafikia mwisho wiki ijayotutakapochambua ugumu wa kumshauri Rais katika mazingira ya sasa.






Lakini pia kama tulivyoona, fursa ya makundi mbalimbalikumshauri imeteleza upesi na kutokomea kutokana na sababu za kihistoria naki-haiba (personality) ya Mheshimiwa Rais mwenyewe. Kana kwamba hiyo haitoshi,ziko sababu nyingine kadhaa zinazofanya mazingira ya kumshauri Rais yawemagumu. Nitataja chache katika makala hii.

Baada ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kustaafu urais nakubakia kuwa mwenyekiti wa chama, nilipata bahati ya kutumwa naye na wenzanguwawili, kwenda kumjulia hali rafiki yake mmoja aliyekuwa anaumwa, lakini wakatihuo akiendelea kuongoza chombo muhimu cha dola katika taifa moja la Afrika.
Tulipofika, tulikuta ugomvi ambao hata mkuu wa nchi ile alikuwaamejaribu kusuluhisha bila mafanikio.
Ugomvi ulihusu nafasi ya waganga wa kienyeji katika kumshaurimkubwa yule juu ya afya yake. Mara mbili alipelekwa hospitalini Ulaya naMarekani, na madaktari walishauri afanyiwe upasuaji lakini kila alipoandaliwakwa ajili hiyo, alibadili mawazo dakika za mwisho na madaktari waliheshimuuamuzi wake.

Kisa cha kubadili kilikuwa ni ushauri wa waganga wa kienyejikuwa wazungu wanataka kumuua kupitia upasuaji huo. Mkubwa yule aliendeleakudhoofu kwa kuchelewa kufanyiwa upasuaji kwa sababu tu waganga wa kienyejiwametoa ushauri na ukaheshimika.
Hatimaye waganga hao walihamia nyumbani kwa mkubwa yule,wakapewa gari lao maalumu katika misafara ya mkubwa yule. Washauri na wasaidiziwakapuuzwa na hata ushauri wa marafiki kama Mwalimu Nyerere haukufua dafu.

Nalisema hili kusisitiza jambo moja muhimu kuwa, viongozi wengiwa Kiafrika wanajiweka katika mazingira magumu ya kushauriwa pale hofuinapowatawala na hatimaye kujisalimisha kwa washauri wasio rasmi kama hawa.
Tulipomweleza Baba wa Taifa juu ya yaliyotukuta alicheka sana nakutukumbusha kuwa "Waswahili" hawaachani na jadi yao. Akatukumbusha kuwa hatayeye alipokutana na wazee, lilikuwa halianzi jambo mpaka tambiko lifanyike!Siamini kwamba katika hofu iliyogubika makundi ndani ya chama na serikali kamakweli hatujafika huko.

Hofu ya namna hiyo, haiwezi kuruhusu Rais apate ushauri usio nashaka.
Siku moja nilifuatana na mtu mmoja kwenda Ikulu kuomba kuonanana Mheshimiwa Rais ili amshauri Rais juu ya jambo ambalo mpaka wakati huuhakupata kuniambia.
Nilikubali kumsindikiza baada ya yeye kuzungumza na maofisa waIkulu na kuwaambia kuwa angekwenda na mtu mwingine ambaye ni mimi.
Kwanza nilishangaa kuona kuwa hata kuweka miadi ya kuonana naRais ni lazima mtu aende mwenyewe kuonana na maofisa. Nilidhani kwa ujingawangu, angepewa siku au kunyimwa bila kulazimika kuambiwa aende kwanza Ikulu.
Tukiwa ofisini kwa ofisa wa kutoa miadi hiyo, alifika ofisamwingine na baada ya kuambiwa kuwa ndugu yangu niliyefuatana naye alihitajikuonana na Rais ili ampe ushauri fulani, aliulizwa swali "Wewe unatakakumshauri Mheshimiwa Rais, lakini wewe umejishauri"?

Swali hilo lilinitesa sana siku hiyo. Nikahisi kuwa mazingira yakumshauri Rais ni magumu ikiwa wasaidizi wake wanafanya mizaha katika wajibuwao kiasi hicho. Linapofika suala la mwananchi kupenda kumpa ushauri mkuu wanchi, mizaha na kejeli vingewekwa pembeni na kuwa makini kusikiliza watoaushauri. Mpaka leo naamini, kumshauri Rais Kikwete inabidi ujishauri mara mbilikwa sababu zifuatazo:


Rais Kikwete


Kwanza, Rais Kikwete anaongea sana kuliko kusikiliza. Tabia hiipia ilionekana siku alipozungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari kwakujibu maswali ya papo kwa papo.

Ilibidi wakati fulani, Tido Mhando ajaribu kuingiliakumsimamisha au kumshtua lakini akafanya kwa woga na Rais hakushtuka.
Rais mwongeaji sana kama yeye anapoteza fursa nyingi zakushauriwa kwa sababu badala ya kushauriwa, yeye ndiye anatoa ushauri. Tabiahii pia anaiendeleza anapoongoza vikao vya chama na hata baraza la mawaziri.
Baadhi ya mawaziri wake wamesikika wakilalamika kuwa vikao vyabaraza haviishi wala kumaliza agenda kwa sababu Rais anazungumza muda wote nawao wanalazimika kurudi wizarani kwao na madokezo kutoka kwa makatibu wakuuwao.

Wengine wamedai Rais ana mawaziri vipenzi wake ambao anakuwaamekwisha kuzungumza nao na wakifika kwenye baraza wao husimama na kusema"Mheshimiwa Rais kama niliyokwishakudokeza".
Hali hii huwafanya mawaziri ambao ni washauri wakuu wa Raiswabakie kumskiliza Rais awaambie kile alichodokezwa na waziri wake kipenzi.Matokeo yake, mawaziri hurudi wizarani kwao na ushauri wao kwa sababu tu, Raisanaongea sana kuliko kusikiliza.

Pili, Rais hasomi ripoti au hana muda kabisa wa kuzisoma.Washauri wengi wa Rais hutoa ushauri wao kwa njia ya maandishi (ripoti maalumuau madokezo).

Ni wachache wanaofanya kwa kutumia maneno matupu (umbeya naudaku).
Kwa hiyo Rais hana budi kuwa msomaji mzuri wa ripoti. Raisasiyesoma hutegemea "briefings" au "executive summaries" na hii ni hatari sanakwani si ukweli wote waweza kuwekwa katika briefings. Ukitilia maanani kuwaRais wetu ni msafiri na imeonekana wazi akiwa safarini pia hasomi kazi zaofisini, basi anakatisha tamaa washauri wanaotumia muda mwingi kuandaa ripotihizo.

Uwezekano wa kukasimu madaraka ya kusoma na kufanyia kazi ripotihizo ni mgumu kwa sababu kinga ya maofisa hao si za uhakika endapo utekelezajiwake utaleta mgogoro au kashfa baadaye.
Tatu, timu ya washauri wa Rais katika masuala mengi yaliyo nyetiimejaa watu ambao uwezo wao unatia shaka (mediocres).

Hii ni kwa sababu ama Rais hakuwa makini katika uteuzi auwashauri hao walisukumizwa kwake na marafiki kama njia ya kulipa fadhila.

Tumewaona hawa washauri na wasaidizi wa Rais katika matukiomengi ya kimataifa na kitaifa na utendaji wao unazua maswali.
Kuna wakati tumemwona Rais mwenyewe akilazimika kuingilia hatamasuala mengine hasa ya kiitifaki kwa lengo la kuepusha aibu na fedheha kwanchi.

Tabia moja kubwa ya "mediocre" huwa ni kushauri kwa kuigizamambo waliyoyaona sehemu nyingine, na mara nyingi hupenda fitna ili Raisasishawishiwe na ukweli aliousikia kwa watu wengine.
Mifano halisi ya maamuzi ya Rais na Serikali yanayotokana naushauri usiotokana na weredi wa washauri ni kama vile uamuzi wa kupitia upyamikataba ya madini, ufutaji wa misamaha ya kodi kwa taasisi zisizo zakiserikali, kubadilika badilika kwa taratibu za utoaji mikopo ya elimu, ugawajiwa mamilioni ya JK, umeme wa dharura la kashfa ya Richmond, n.k.

Nne, Rais wetu ana marafiki wengi wa sasa na wa zamani. Marafikiwengi huongeza ugumu wa kumshauri rais yeyote kwa sababu ya ugumu wa kubainimambo binafsi ya kiofisi. Hali hii ikitokea humchanganya rais na washauri wake.
Inapotokea kuwa rais mwenyewe hapendi kuwahudhi marafiki zake,basi marafiki hao hugeuka kuwa marafiki wa taifa badala ya kuwa marafikibinafsi wa rais.

Najua na nimemwona Rais akikana na kuwaonya wote wanaotumia jilalake kwa maslahi binafsi, lakini anapofanya hivyo hata yeye mwenyewe haaminikama anafanya kweli.
Anapokuwa mikoani hujiatahidi sana kukumbuka kila mtu aliyewahikukutana naye, na pia marafiki zake wa zamani huingilia ratiba ili kuonana naRais.

Madhara ya tabia hii si tu yanawachanganya washauri, bali piayanamweka Rais mwenyewe katika wakati mgumu anapolazimika kutoa ahadi zilizonje ya utaratibu kama vile kusaidia gharama za matibabu, kurejesha kaziniwaliofukuzwa kazi zamani, kutoa ajira, kurudi kutembelea eneo hilo tena na hatakualika watu waje kumwona.

Kwa ufupi, marafiki wamekuwa wachafuzi wa kwanza wa Serikali yaAwamu ya Nne.
Rais anaposhauriwa juu ya tatizo hili, yeye husema "marafikiwanaochafua kazi yake waache wajipoteze wenyewe". Hayuko tayari kuachana naojapo yuko tayari wao ndio wamwache kama wamekata tamaa naye.
Katika kuhakikisha hili linafanyika, Rais huwajengea mazingiramagumu marafiki zake ili wasikate tamaa haraka.

Njia anayotumia ni kuuma na kupuliza na wakati mwinginekuwatumia mawasiliano yanayopingana na alichokisema hadharani.
Baadhi ya marafiki zake wanatukuza mawasiliano hayo na kuyaenzikama alama ya urafiki wa kudumu na Rais.
Katika mnyukano wa makundi unaoendelea bungeni, baadhi yawabunge wanaokerwa na tabia ya marafiki wa Rais, wamekuwa wakilalamika kuwamarafiki hao wa Rais wanawatambia kuwa watakufa na umasikini wao kwa sababu tuwamezubaa na ndiyo maana sasa wanawaonea wivu wenzao waliofanikiwa.
Siku Mwadhama Kardinali Policarp Pengo aliposema wanaopigakelele za ufisadi wanaweza kuwa wanafanya hivyo kwa wivu wa wao kukosakufisadi, marafiki wa Rais walifanya sherehe na kushangilia kuwa hatimaye haowabunge wenye roho ya "korosho" wamepata vipande vyao.

Nihitimishe sehemu hii kwa kusisitiza tu kuwa marafiki wa Raiskwa idadi yao na tabia yao, ni kikwazo cha kumshauri Rais Kikwete.
Tano, ili kumshauri Rais ni vema ikafahamika kwa washauri wakewalio rasmi kuwa anasimamia mambo gani ya msingi katika utawala wake.

Ni vigumu sana kumshauri rais ambaye kwake kila kitu ni chamuhimu, yaani hana vipa umbele na hajajipambanua kikweli kweli kuwa anasimamiamambo fulani. Kutofahamika kwa rais huitwa "kutotabirika".
Lakini hili kwa Rais wetu ni dogo, kubwa zaidi ni kutoaminikakwa mambo ya msingi na kuaminika sana kwa mambo madogo ya kawaida.

Mathalani Rais huyu anaweza kuchelewesha kuamua jambo zito lenyemaslahi kwa Taifa, lakini hawezi kuchelewesha kutimiza ahadi ya kutoa tiketi yandege ya rafiki yake kwenda India kwa matibabu.
Hili atalikumbuka na hata usiku litamuamusha kuwaagizawasaidizi.

Hata kama unaoshughulikiwa ni uhai wa mtu, lakini pia inatiashaka mkuu wa nchi anapomsahau mshauri wake anayemsubiri sebuleni tayari kwakumpa "briefing" ya maslahi ya taifa lakini rais huyo huyo akasimamisha msafaraau kuchelewesha msafara ili atoe pongezi kwa mtoto wa rafiki yake aliyehitimukidato cha sita.
Baadhi ya wasaidizi na washauri wa Rais Kikwete wanakatishwatamaa wanapofika Ikulu kutoa ushauri au ripoti lakini wakaambiwa Rais hananafasi, warudi siku nyingine, lakini wakaja kumwona Rais akitoa nafasi kwamarafiki au marafiki wa marafiki zake wamwone kwa mambo ya binafsi.

Baadhi ya marafiki zake hivi sasa wanatumia mwanya huo vibaya.Rais asiyetabirika wala kuaminika, huwaweka washauri wake katika mazingiramagumu sana ya kazi yao.

Sita, taifa changa kama la kwetu linamhitaji rais aliyeivakatika itikadi fulani ili awe dira ya watu na taasisi zake.
Naelewa hili ni suala tata kwa sasa lakini utata wake haupunguziumuhimu wake.
Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere alijaribu kujenga Ujamaa naKujitegemea. Waliofuata wakabomoa lakini hawakujenga kipya bali wakawawajasiriamali na makuwadi wa soko huria.
Kipekee Rais Benjamin Mkapa alizungukwa na washauri waliouoneaaibu Ujamaa na kuuonea fahari Ubepari wa soko huria.

Kwa hiyo, walimshauri rais waliyejua kwa hakika kuwa ameongokeaUbepari na kuachana na Ujamaa, na yeye hakuona aibu kusema na kutetea misingiya dini yake mpya.
Mkapa atalaumiwa kwa mengine, si kwa kukosa msimamo katikamasuala anayoyaamini na kuyatetea.
Rais Kikwete hajulikani kama ni mjamaa au ni bepari. Alifanyakampeini kwa lugha ya kijamaa, akitangaza ana nyumba moja, tena ya mkopo.

Walio karibu naye kuliko mimi wanasema siku ya kutangazakugombea Urais alikuwa na hazina ya shilingi milioni mbili na nusu.Kilichotokea ni mabepari kuteka kampeini zake na hatimaye kumfanya abakinjiapanda ya itikadi.
Washauri wake wote wako njia panda maana hawajui Rais waoanapenda nini.
Amesikika mara kadhaa akisema nchi haiwezi kurudi katika enzi zamgawo wa colgate na sukari lakini wakati huo amesikika mara kadhaa akiombolezajuu ya umasikini wa Watanzania.

Rais anayeomboleza kwa kuwaona masikini wanaoongezeka wakatiakiogelea katika utajiri usio na maelezo, anawajengea mazingira magumu washauriwake.
Yeye akiwa mchumi anapaswa ajue kuwa sehemu kubwa ya majibu yaumasikini wa Watanzania, yamo katika utajiri wa marafiki zake waliomzunguka.

Kukosekana kwa itikadi ya Rais kumezua mitafaruku mingi katikachama na Serikali anayoiongoza. Mpaka sasa Rais haaminiki na kundi lolote, liwela mlengo wa kijamaa au kibepari, bali anakubalika na kuaminiwa na watu binafsikatika makundi hayo mawili. Kundi kama kundi halimwamini lakini watu binafsiwanaendelea kumwamini kwa shaka isiyotamkwa wazi.

Nilikuwa Dodoma usiku ule wa kumpata mgombea Urais kupitia CCM.Kila mtu anaweza kueleza kwa urefu mambo yaliyojiri huko Dodoma. Ni usiku wakukumbukwa kwa mengi.
Baadhi ya wagombea urais, hawapendi kukumbushwa matukio ya jumalile na hasa usiku huo. Rais wetu hupenda sana kuyakumbuka na kuyazungumziawakati anapokuwa anaongea na watu katika mazungumzo yasiyo rasmi. Yeye huitahayo kuwa ni "mchezo wa siasa".
Nadhani haelewi jinsi mchezo huo ulivyoumiza wengi na kuiwekaSerikali yake katika mazingira magumu sana kiushauri.

Walipobakia wagombea watatu wa mwisho – Salim Ahmed Salim,Kikwete na Profesa Mark Mwandosya na kisha wakapewa dakika chache za kuombakura kwa mara ya mwisho, Profesa Mwandosya alisema maneno yaliyovutia usikivupale aliposema, Rais atakayechaguliwa ni mtu wa muhimu sana.
Ni huyo anayeweza kuamua nchi iende vitani, ikaenda. Ni yeyeanayeweka sahihi mtu anyongwe, akanyongwa.
Akawataka wajumbe wafanye uchaguzi wenye busara kwa sababuanayechaguliwa ana dhamana ya uhai wa Taifa na uhai wa watu.

Jirani yangu alininong'oneza kwa kusema, "nitampigia Kikwete,lakini naona maneno ya Mwandosya yamenigusa sana."
Wako watu wengi pia walioguswa na maneno ya Salim na niliwashuhudiawakitoa machozi ya uchungu. Kilichofanyika Dodoma usiku ule, ndicho kwa mantikiya makala zangu tatu, kimeleta linaloitwa ombwe la uongozi kitaifa, ndichokinachomnyima Rais washauri wazuri, na ndicho kinachozidi kuharibu mazingira yaRais kushaurika. Tufanye nini?

Rais ni alama ya mshikamano wa taifa. Rais ni msingi wa mwelekeowa taifa. Rais ni afya ya taifa, ndiyo maana ugonjwa wa rais kimsingi niugonjwa wa taifa. Hii ni dhamana kubwa kupewa mtu mmoja aliyezaliwa namwanamke.
Ni vema Watanzania wakatambua na kama wanaweza wakachukua hatuaza haraka.
Chini ya utaratibu wa sasa, akitokea kichaa akakaa katika nafasiya Urais, taifa letu litaangamia.
Mimi ni mwana CCM halisia, mzalendo kwa kujihukumu nakuhukumiwa.
Nawiwa kutoa tamko la gharama kwa sasa, kwamba, ili kukinusuruchama chetu kiweze kuongoza Taifa hili siku zijazo, ni sharti tukinyime kura.

Kuinyima kura CCM kwa sasa ni kujenga nchi na chama chenyewe.Chama imara katika wingi wa vyama tulio nao, sharti kiwe na wanachama wachachewaaminifu kuliko utitiri wa mamluki tulio nao kwa sasa.
Najua msimamo huu haupendwi ndani ya chama chetu, na wakatiunakaribia tutauweka hadharani ili hatima ya kila mmoja wetu ijulikane.

Katika TANU na CCM aliyoienzi Baba wa Taifa, chama kingeweza kutoamwongozo na kuwajibisha watendaji.
Chama chetu kimekuwa chama cha viongozi na si cha wanachama.
Ukiona Rais mwenyewe anatilia shaka Ilani ya chama iliyomwekamadarakani, ujue jahazi linaenda mrama.
Alianza Mkapa akasema Ilani haitekelezeki, tukakaa kimya.Amekuja Kikwete akasema Ilani alipewa Jangwani na hajui iliandaliwaje,waungwana tumekaa kimya.

Ni wajibu wa kila mwanachama kuona umuhimu wa kutilia shakauongozi wa sasa wa chama chetu, na kama hawatatusikia, hatutahama chama balitutawanyima kura tukiwa ndani ya chama chetu kilicholeta uhuru. Rais wetuambaye ni Mwenyekiti wa chama afike mahali achague kati ya kutumikia marafikiau Taifa.
Mwisho niwashukuru sana wote walionitumia ujumbe kwa njia yasimu, barua pepe, na hata kupiga simu kutoa maoni yao kuhusu mada hizi.

Nimezingatia yote mliyonieleza na panapo majaliwa nitafikishabaadhi ya maoni yenu katika nafasi zake. Mimi si mwandishi wa habari, lakininapenda kusoma habari na vitabu.
Waliochukizwa na maoni yangu, nawashauri waandike tusome nakuudhika kama walivyoudhika. Mwisho wa siku, Tanzania ni yetu sote na waliomadarakani twawangoja huku uraiani. Hakuna aliye na hati-miliki ya kutawala.Tukubali kukosolewa, na Serikali isiyopenda kukosolewa, haina haki ya kukusanyakodi zetu.

Mwandishiwa makala hii amejitambulisha kuwa ni msomaji mzuri wa Raia Mwema. Barua Pepe:msomajiraia@yahoo.co.uk, Simu: 0712881704
 
Hii message ilikuwa inafaa sana kama ingelikuwa inalenga kwa kiongozi mwenye uchungu na taifa na anayejali maslahi ya nchi ya leo na kesho. Kwa huyu jamaa na ccm yake.... Sijui?
 
Kwa ufupi sisi wazaliwa wa Tanganyika tunauona huu muungano mapenzi ya chuna buzi.
 
TAFAKURI YANGU
Ndugu vijana wenzangu na watanzania wote, mustakabali wa taifa letu upo mikononi mwetu, mustakabali wa vizazi vijavyo ndani ya taifa letu upo kwenye maamuzi yetu ya leo, mustakabali wa rasilimali zetu upo kwenye sheria, kanuni na taratibu tunazoziweka kwa sasa, mustakabali wa kuendelea kuwepo kwa nchi yetu upo kwenye tafasiri tunazozifanya kwasasa.
Hapa tulipofika tunahitaji hatua ya mwisho kiutawala ili kunusuru existence and furtherance of our nation and natural resources for our sons and daughters as well as the coming generation.
Hatua ya kwanza katika kufikia maamuzi kiutawala ni kwa kufanya MAJADILIANO miongoni mwa makundi mbalimbali yanayokinzana(Table negotiation). Majadiliano haya katika ngazi ya taifa hufanywa na kuratibiwa na hasasi mbalimbali za kijamii, kiraia na serikali. Njia hii ndani ya taifa letu la Tanzania zimefanyika mara nyingi sana na zilionekana kuzaa matunda tu enzi za uhai wa baba wa taifa Hayati Mwl. J.K Nyerere. Vilevile njia hii imeonekana kutoheshimiwa kabisa na kupuuzwa hasa kwenye awamu ya nne ya uongozi wa taifa hili.
Hatua ya pili kwa kawaida hufuata baada ya hatua ya kwanza kuonekana kukwama na mara nyingi hutumiwa ili kuhuisha na kufufua njia ya kwanza ya maamuzi ya kiutawala. Njia hii tunaita SHINIKIZO/VITISHO (Gumboot). Njia hii hufanywa ili kuitahadharisha kundi la utawala juu ya maamuzi yao kulipuuza jambo lililoko kwenye hatua ya kwanza ya maamuzi. Hili nalo limekuwa likifanywa sana na hasasi za kiraia, wanaharakati na vyama vya siasa ndani ya nchi yetu lakini wahusika waliishia kung'olewa meno na kufanyiwa vitendo vya kikatili ikiwa ni pamoja na kuuwawa. Hivyo kwa mara nyingine hatua hii imeshindwa ndani ya taifa letu.
Hatua ya tatu ni KUCHUKUA HATUA (TAKING ACTION). Hatua hii ni kuyatekeleza yale ya hatua ya pili kama kundi la utawala litagoma kurudi hatua ya kwanza ya maamuzi. Hatua hii ni pamoja na kuandamana nchi nzima pasipo kujali itikadi za vyama vyetu na mrengo wetu wa kisiasa bali tu maslahi ya taifa, kulipinga jambo ambalo linaonekana kuwa na madhara hasi kwa taifa letu ama linaonekana kuliumiza jamii.
Ndugu zangu vijana na watanzania wote, ukombozi wa kweli siku zote una gharama na sacrifice kubwa ila udumu milele na kuheshimiwa daima. Katika ukombozi wa mwanadamu, manabii na wafalme wote walijaribu kadri wawezavyo ila hawakufanikiwa kwasababu hawakukubali gharama za maisha yao ili ukombozi huo udumu daima. Nabii Issah/Bwana Yesu alileta ukombozi kwa mwanadamu na ambao ulikuwa ni ukombozi wa kudumu kwa kukubali yeye bila hatia yoyote kutoa maisha yake kama gharama ya kumkomboa mwanadamu. Ukombozi huo hadi leo umedumu na utaendelea kudumu daima.
Nchi za South Rhodesia (Zimbabwe), South Africa, Kenya, France, USA na zingine nyingi sana zilipata ukombozi wao kwa gharama ya watu baadhi kukubali kutoa maisha yao kwa ajili ya vizazi vijavyo. Hadi sasa ndani ya nchi hizi kuna heshima kwa utawala katika kufikia maamuzi kwani aina ile ya ukombozi ulijenga na kuotesha mzizi kwa vizazi na vizazi.
Hoja yangu kwa Tanzania, Ili tuweze kulinda na kuhifadhi rasilimali zetu kwa ajili ya maslahi ya nchi yetu na vizazi vijavyo, hatuna budi sasa kuchukua hatua ngumu ya tatu ya maamuzi. Vyombo vyote vya usalama nawaomba wawe mstari wa mbele katika hili kwa kuwalinda watanzania kwani nasisitiza kama alivyowahi kutamka Wilstone Churchil kwenye hotuba yake kwa wanajeshi kwamba, wao sio mashine kuamuriwa na mtu yeyete ili kulinda maslahi yake hata kwa kudhulumu umma. They have to think and act upon their thinking because they are not machines to be controlled by some people and worse enough is failing to have a free mind for the furtherance of their nation.
Hayo yaliyotokea Misri, Tunisia, Libya, Syria, Ukraine na Cote de avoire ni lazima yatokee kwetu ili maamuzi ya wananchi yaheshimiwe, ili rasilimali za nchi ziheshimiwe, na ili uongozi wa nchi uwaheshimu wananchi na sio kulindana katika masuala nyeti yanayohusu uhujumu uchumi.
Najua waliowengi watanipinga kwa hili kwasababu ya kuogopa gharama hii ya ukombozi lakini niwaonye tu kwamba kuna dalili ya nyota hiyo nyekundu kuanza kuchomoza hapa Tanzania na kama haitaangaza leo basi siku sio nyingi mwangaza wake utaonekana. Hii inatokana na vitendo vya kidhalimu na kiudhalilishaji yanayofanywa na serikali yetu kwa kujisahau kwamba wameajiriwa na watanzania wawaongoze ila wao wana-act like wao ndio wamewaajiri watanzania.
Mungu Ibariki Tanzania.
Comred Ole
 
Back
Top Bottom