Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Upepo wa Kuondoa viongozi mangi meza wa vyama sasa unaonekana kupamba moto. Ni dhahili kumekua na Udikiteta na Umangi meza wa kutaka kuongoza vyama vya siasa bila kikomo kwa kisingizio eti wao ndio waanzilishi wa vyama hivyo! Mrema mwaka jana amepambana na kumfukuza Katibu wake akikaataa mtu yoyote asiwe na sauti,hali kadhalika Mh Mbowe amekua na utawala wa mabavu kutaka sauti yake iwe ndio sauti ya mwisho kwa maamuzi kisa yeye ndie alie anzisha Chadema! ikumbukwe uchaguzi wa mwenyekiti ndani ya Chadema Mbowe alifanya kila hila ili aendelee kuwa Mwenyekiti wa Chadema kisa yeye ndie mwanzilishi wa Chadema! Hali kama hiyo imehamia sasa NCCR-Mageuzi na CUF ambako nako kuna sumu ile ile ya Udikteta ikiendelea kwa Viongozi hao wa wakuu wa vyama hivyo kuendeleza umimi! Kinacho onekana Chadema ni uvumilivu tu wa watu wenye busara kumvumilia mmliki huyo wa Chadema aendelee kuwa na sauti,lakini muda si mrefu atalazimika kupisha na kuacha kuonesha mabavu ya wazi eti kisa yeye ndie mwazilishi wa Chadema,sitaki kuongea mifano mingi hasa ya mbowe lakini ikumbukwe habari ya kukiuzia Chama magari mabovu kwa milioni 500,na wajumbe wa kamati kuu ya Chadema wataunga mkono hoja hii kuwa Mwenyekiti huyo asome alama za nyakati sasa. Upande wa Mbatia amekua kiongozi alie kosa aibu na hana busara kwani hataki kukosolewa kabisa na mtu yoyote,sababu kubwa yeye ndie mwanzilishi wa Chama. Upande wa CUF chama hicho kimepauka kimtizamo ndani ya Zanzibar na hata Bara kwa kukosa ushawishi,lakini kikubwa ni ndugu Maalim Seif Kuhodhi madaraka! Sababu ni ile ile ya kijinga eti yeye ndie mwanzilishi wa Chama.
My take: ​
Viongozi hawa wa vyama vya siasa ni lazima wajue na waelewe kuwa huu si wa kati wa kuendesha vyama kwa misingi ya kikampuni,ni bora wajue kua kuna wanachama wao ambao wana upeo mkubwa,maono ya mbali,shupavu na wana nia njema ya kuvipa nguvu na mtizamo mpya vyama hivyo,kama mtu anaona ana hati miliki ya chama basi atoe hesabu ya gharama zake ili arudishiwe na chama kisonge mbele na kuwe na demokrasia ndani ya vyama na ustawi mzuri wa vyama.
My take: ​
Viongozi hawa wa vyama vya siasa ni lazima wajue na waelewe kuwa huu si wa kati wa kuendesha vyama kwa misingi ya kikampuni,ni bora wajue kua kuna wanachama wao ambao wana upeo mkubwa,maono ya mbali,shupavu na wana nia njema ya kuvipa nguvu na mtizamo mpya vyama hivyo,kama mtu anaona ana hati miliki ya chama basi atoe hesabu ya gharama zake ili arudishiwe na chama kisonge mbele na kuwe na demokrasia ndani ya vyama na ustawi mzuri wa vyama.