ommy15
JF-Expert Member
- Jan 23, 2011
- 670
- 1,012
Habari zenu wanaJF,nimatumaini yangu wengi ambao niwadau wa hili jukwaa ni wanafunzi wa vyuo,wahitimu na watarajiao kuwa wanavyuo. Ila kuna malumbano ambayo mara nyingi nimeyakuta hasa kwenye jukwaa hili la elimu,hii hasa ni juu ya chuo kipi eti ni bora Tanzania yaani udsm vs mzumbe,udsm vs udom,mzumbe vs sua. Mm binafsi sijawahi vutiwa na mjadala huu na kwa watu wasomi wavyuo vikuu kama nyie mnaoanzisha mjadala na kuchangia,narudia sijawahi vutiwa wala kufurahishwa kwani michango na mada zenyewe zinadharaurisha na kushusha hadhi zenu na za vyuo vyenu.Kwani baadhi yenu mnafikia hadi kuwaona wenzenu mbwa koko! Kweli hii ndio kazi ya wasomi,hii ndio kazi ya JAMIIFORUMS(The home of Great thinkers)? Mfano ni thread yenye kichwa "ubora wa digriiza udom na st.joseph". Hapa nlishindwa kuelewa kuanzia aliyeanzisha mjadala hadi wachangiaji(sio wote) kwamba nini hasa wanajifunza huko kwenye chuo bora Tanzania{UDSM} kwani naona jinsi wasivyokuwa na uelewa wa usomi na kazi ya msomi ktk jamii yake.
Kwa upande wangu msomi ni mtu mwenye uwezo wa kutambu,kuchanganua na kutatua au kupendekeza njia za kumaliza matatizo yaliyopo ktk jamii,na hii ndo iliyokuwa sifa kubwa na ya pekee kwa wasomi wa mlimani kipindi cha nyuma(enzi za kina Prof.Issa Shivj,Tundu Lissu)na wengine ambao hadi leo tunaona mchango wao ktk jamii. Wanafunzi wengi wa mlimani wasasa mnadharau sana vyuo vingine sijui hapo mnaifundisha nini jamii yetu.
kweli matatizo yapo sio udom,st,Joseph,muccobs tu hata hapo kwenu pia,pili mkumbuke waliochaguliwa udom au st.joseph mlisoma nao huko mashuleni na wengi wanauwezo kama wenu na hata kuwashinda baadhi yenu ila hilo hamliangalii kwani mnakiburi cha historia ambayo hamjaijenga nyie bali mnafanya juhudi kubwa kuibomoa.Kama kweli nyie niwanafunzi bora na mmegundua kwamba vyuo hivyo havina ubora mbona sijawahi sikia mmetoa mapendekeza kwa waziri anayehusika au serikali nini kifanywe(kama udsm ya miaka ya nyuma). Acheni ushabiki kwani hamjengi elimu yetu mnabomoa hivyo nategemea siku1 mtagoma kushiniza serikali iwapatie udom,st.joseph,sua,muccobs,tumaini n.k walimu bora kama wenu.
Kwakifupi malumbano yenu hayaoneshi kama kweli nyie mnaweza kupambana na changamoto za maisha ambazo zinahitaji wasomi ambao ni waadilifu,hawana majivuno na dharau,pia kusoma kwenye chuo bora africa au duniani bado wewe binafsi unaweza usiwe bora kwani mifano ipo ni wangapi wamemaliza mzumbe,udsm lakini wanafanya madudu jiulizeni wanaoingia mikataba ya kijinga nchini walisoma wapi? Hivyo basi nadhani ifike sehemu jukwa hili liwe sehemu ya kuheshimika na kuheshimiwa lakini kwa jinsi ilivyo sasa tunajidhalilisha kama wasomi na watanzani coz we dont think of solutions to our problems.
Jiulize ww kama msomi wa chuo bora utasaidia vipi kuleta ubora wa elimu nchini nasio malumbano yasiyo na tija,kuna mambo mengi ya kujadiliana humu mfano jinsi gani wanamzumbe,wanasua,wanaudom,wanudsm etc mnaweza nufaika na jumuia ya afrika mashariki.Remember the life that you are livng u didnt choose but that life choosed u.
Kwa upande wangu msomi ni mtu mwenye uwezo wa kutambu,kuchanganua na kutatua au kupendekeza njia za kumaliza matatizo yaliyopo ktk jamii,na hii ndo iliyokuwa sifa kubwa na ya pekee kwa wasomi wa mlimani kipindi cha nyuma(enzi za kina Prof.Issa Shivj,Tundu Lissu)na wengine ambao hadi leo tunaona mchango wao ktk jamii. Wanafunzi wengi wa mlimani wasasa mnadharau sana vyuo vingine sijui hapo mnaifundisha nini jamii yetu.
kweli matatizo yapo sio udom,st,Joseph,muccobs tu hata hapo kwenu pia,pili mkumbuke waliochaguliwa udom au st.joseph mlisoma nao huko mashuleni na wengi wanauwezo kama wenu na hata kuwashinda baadhi yenu ila hilo hamliangalii kwani mnakiburi cha historia ambayo hamjaijenga nyie bali mnafanya juhudi kubwa kuibomoa.Kama kweli nyie niwanafunzi bora na mmegundua kwamba vyuo hivyo havina ubora mbona sijawahi sikia mmetoa mapendekeza kwa waziri anayehusika au serikali nini kifanywe(kama udsm ya miaka ya nyuma). Acheni ushabiki kwani hamjengi elimu yetu mnabomoa hivyo nategemea siku1 mtagoma kushiniza serikali iwapatie udom,st.joseph,sua,muccobs,tumaini n.k walimu bora kama wenu.
Kwakifupi malumbano yenu hayaoneshi kama kweli nyie mnaweza kupambana na changamoto za maisha ambazo zinahitaji wasomi ambao ni waadilifu,hawana majivuno na dharau,pia kusoma kwenye chuo bora africa au duniani bado wewe binafsi unaweza usiwe bora kwani mifano ipo ni wangapi wamemaliza mzumbe,udsm lakini wanafanya madudu jiulizeni wanaoingia mikataba ya kijinga nchini walisoma wapi? Hivyo basi nadhani ifike sehemu jukwa hili liwe sehemu ya kuheshimika na kuheshimiwa lakini kwa jinsi ilivyo sasa tunajidhalilisha kama wasomi na watanzani coz we dont think of solutions to our problems.
Jiulize ww kama msomi wa chuo bora utasaidia vipi kuleta ubora wa elimu nchini nasio malumbano yasiyo na tija,kuna mambo mengi ya kujadiliana humu mfano jinsi gani wanamzumbe,wanasua,wanaudom,wanudsm etc mnaweza nufaika na jumuia ya afrika mashariki.Remember the life that you are livng u didnt choose but that life choosed u.