Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,804
- 1,871
Ogaden ni sehemu ya Ethiopia yenye wakazi wenye asili ya Kisomali. Eneo hilo limefungwa na hivyo kutopata mawasiliano na sehemu nyingine yeyote ya Dunia. Si ruhusa kwa waandishi wa habari wa nchi hiyo au kutoka nje kuingia katika Eneo hilo. Suala linakuja, ni nini Serikali ya Ethiopia inakificha?
Inachokificha ni mauaji ya Halaiki yanayoendeshwa na serikali ya MELAZINAWI, waziri mkuu wa Ethiopia kwa wananchi wasio na hatia wa OGADEN. Nia ya mauaji hayo ni kutokomeza kizazi hicho na kuwajaza waethiopia wenye asili nyingine hususan 'AMARA', kabila lililotawala Ethiopia kwa miaka mingi. Na kisa hasa cha kufanya hivyo ni utajiri wa MAFUTA ulioko katika jimbo hilo, hivyo MELAZINAWI anaogopa ikiwa utajiri wa mafuta utakuwa chini ya Waethiopia hao wenye asili ya kisomali wanaweza kutaka kujitenga.
Kinachonishangaza mimi, ni kuwa MELAZINAWI mwenye Asili ya KITIGRINYA toka Eritrea alikuwa mstali wa mbele kupigana na utawala wa MANGISTU (Muamara- Amarinya) aliyeliweka kabila lake kama kabila TEULE, na kudharau na kuendesha mauaji holela hususan Tigrinyi pale wanapodai haki zao. Melazinawi aliahidi kuleta haki sawa kwa makabila yote, lakini anachokifanya kwa wananchi wa OGADEN NI MAUAJI YA HALAIKI. Wakati wa njaa hufunga barabara zote kuhakikisha chakula hakipelekwi OGADEN, na kujipatia maelezo mazuri ya vifo vya wananchi hao.
Mbaya zaidi ni pale ambapo Dunia imekaa kimya, na kinachoniudhi sana ni African Union kutosema lolote kuhusu hili suala. Wamarekani wamefyata mkia kwa sababu MELAZINAWI amewaahidi kuwadaka Magaidi na kuwapeleka Marekani. European Union wamekaa kimya kwa sababu Melazinawi amewaahidi kuwapa mkataba wa kuchimba Mafuta pale atapomaliza kuwaua wananchi wa Jimbo hilo hivyo kupata eneo kubwa lakuchimba mafuta bila mgogoro wa wananchi. Haya yote yananiuma sana Roho.
BBC ilifanikiwa kuingia huko kwa siri na ukiiona hiyo taarifa machozi yatakutoka. Waandishi wa KISWIDI waliojaribu kuingia huko na kupata taarifa za mauaji ya Halaiki, wamekamatwa na Serikali ya Ethiopia na wapo mahakamani wakijibu mashtaka ya kuingia katika eneo hili bila ruhusa na kuhusika na ugaidi. Ndugu zangu waafrika hili ni jukumu letu kuzuia mauaji ya HALAIKI, Tusisubiri Wazungu waje watusemee kana kwamba sisi ni Mabubu. Enough is enough, Ethiopia -STOP MAUAJI YA HALAIKI OGADEN.
Inachokificha ni mauaji ya Halaiki yanayoendeshwa na serikali ya MELAZINAWI, waziri mkuu wa Ethiopia kwa wananchi wasio na hatia wa OGADEN. Nia ya mauaji hayo ni kutokomeza kizazi hicho na kuwajaza waethiopia wenye asili nyingine hususan 'AMARA', kabila lililotawala Ethiopia kwa miaka mingi. Na kisa hasa cha kufanya hivyo ni utajiri wa MAFUTA ulioko katika jimbo hilo, hivyo MELAZINAWI anaogopa ikiwa utajiri wa mafuta utakuwa chini ya Waethiopia hao wenye asili ya kisomali wanaweza kutaka kujitenga.
Kinachonishangaza mimi, ni kuwa MELAZINAWI mwenye Asili ya KITIGRINYA toka Eritrea alikuwa mstali wa mbele kupigana na utawala wa MANGISTU (Muamara- Amarinya) aliyeliweka kabila lake kama kabila TEULE, na kudharau na kuendesha mauaji holela hususan Tigrinyi pale wanapodai haki zao. Melazinawi aliahidi kuleta haki sawa kwa makabila yote, lakini anachokifanya kwa wananchi wa OGADEN NI MAUAJI YA HALAIKI. Wakati wa njaa hufunga barabara zote kuhakikisha chakula hakipelekwi OGADEN, na kujipatia maelezo mazuri ya vifo vya wananchi hao.
Mbaya zaidi ni pale ambapo Dunia imekaa kimya, na kinachoniudhi sana ni African Union kutosema lolote kuhusu hili suala. Wamarekani wamefyata mkia kwa sababu MELAZINAWI amewaahidi kuwadaka Magaidi na kuwapeleka Marekani. European Union wamekaa kimya kwa sababu Melazinawi amewaahidi kuwapa mkataba wa kuchimba Mafuta pale atapomaliza kuwaua wananchi wa Jimbo hilo hivyo kupata eneo kubwa lakuchimba mafuta bila mgogoro wa wananchi. Haya yote yananiuma sana Roho.
BBC ilifanikiwa kuingia huko kwa siri na ukiiona hiyo taarifa machozi yatakutoka. Waandishi wa KISWIDI waliojaribu kuingia huko na kupata taarifa za mauaji ya Halaiki, wamekamatwa na Serikali ya Ethiopia na wapo mahakamani wakijibu mashtaka ya kuingia katika eneo hili bila ruhusa na kuhusika na ugaidi. Ndugu zangu waafrika hili ni jukumu letu kuzuia mauaji ya HALAIKI, Tusisubiri Wazungu waje watusemee kana kwamba sisi ni Mabubu. Enough is enough, Ethiopia -STOP MAUAJI YA HALAIKI OGADEN.