Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,681
- 46,362
Eneo la Somaliland liliojitenga kutoka Somalia tangu mwaka 1991 limekuwa likijiendesha kama taifa bila kutambuliwia rasmi na nchi yoyote duniani.
Hali hii ya kutotambulika sasa inaonekana kuelekea mwisho baada ya kuingia katika makubaliano ya awali na Ethiopia yalipo makao makuu ya AU kuipatia Ethiopia sehemu ya bandari yake kwa miaka 50 kwa mashariti ya Ethiopia kuitambua Somaliland kama nchi rasmi.
Ethiopia ni taifa kubwa zaidi duniani lisilo na bandari tangu Eritrea kujitenga na taifa hilo miaka 30 iliyopita. Tangu waziri mkuu Abiy Ahmed kuingia madarakani amekuwa akitoa kauli za mara kwa mara kwamba Ethiopia itafanya lolote linalowezekana chini ya utawala wake kujipatia bandari na kuwa na jeshi la majini.
Hali hii ya kutotambulika sasa inaonekana kuelekea mwisho baada ya kuingia katika makubaliano ya awali na Ethiopia yalipo makao makuu ya AU kuipatia Ethiopia sehemu ya bandari yake kwa miaka 50 kwa mashariti ya Ethiopia kuitambua Somaliland kama nchi rasmi.
Ethiopia ni taifa kubwa zaidi duniani lisilo na bandari tangu Eritrea kujitenga na taifa hilo miaka 30 iliyopita. Tangu waziri mkuu Abiy Ahmed kuingia madarakani amekuwa akitoa kauli za mara kwa mara kwamba Ethiopia itafanya lolote linalowezekana chini ya utawala wake kujipatia bandari na kuwa na jeshi la majini.