Maswali yangu kadhaa kwa wataalam wa mambo ya ulinzi na diplomasia kuhusu kinachoendelea huko Haiti

6 Pack

JF-Expert Member
Apr 17, 2022
1,826
4,076
Niaje waungwana,

Leo ningependa kupata majibu kutoka kwa wajuzi wa mambo ya kidiplomasia, kuhusu kile kinachoendelea huko kwa ndugu zetu wa Haiti.

Kwanza nafahamu kwamba baada ya uhuru, kila nchi huwa na uongozi (serikali) ambayo chini yake kuna vyombo mbali mbali vya ulinzi na usalama kwa ajili ya kuilinda serikali, nchi na wananchi wanaoongozwa na hiyo serikali. Vyombo hivyo huwa katika mpangilio wa:

1. Jeshi ambalo mamlaka yake ni kulinda nchi, wananchi, na raisi wa nchi ambae ndie "serikali".

2. Polisi ambao kazi yao ni kulinda mali za raia, pia kuwalinda raia, na pia kuhakikisha usalama wa ndani ya nchi wakishirikiana na vyombo vingine vya usalama.

3. Uhamiaji ambao kazi yao ni kuhakikisha ni nani anaeingia na kutoka ndani na nje ya nchi.

4. Askari magereza ambao kazi yao ni kuwalinda wafungwa na watuhumiwa mbali mbali.

5. Vyombo mbali mbali vya usalama wa taifa nk.

Kwa maana hiyo mimi naamini au nafikiri kuwa hata Haiti baada ya kupata uhuru ilifanikiwa kuwa na vyombo hivyo ambavyo kila nchi huwa navyo.
Sasa maswali yangu ni manne tu..

1. Je, Haiti bado inavyo hivyo vyombo vya ulinzi na usalama kama vile jeshi na vyombo vingine vya usalama nk mpaka leo?

2. Kama wanavyo ni kwanini jeshi limeshindwa kuingilia ndani kuilinda nchi, kuwalinda wananchi na kulinda viongozi waliowekwa na wananchi hadi kupelekea nchi hiyo kuomba msaada wa kiulinzi kutoka katika nchi zingine?

3. Inamaana jeshi na vyombo vya usalama vyote vya nchi hiyo vimezidiwa nguvu na magenge ya vijana wasiokuwa na mafunzo yoyote ya kijeshi? Tena wanaotumia salaha za kawaida, nikiwa na maana ni bunduki tu za kawaida, hawana kifaru wala ndege ya jeshi?

4. Je, inamaana jeshi la nchi hiyo ni dhaifu na linashindwa hata na Burundi au Congo ambazo zimekuwa zikitumia majeshi yao kupambana na waasi miaka na miaka bila waasi hao kuziangusha serikali zao?
 
Nchi kama hizo zinashindwa kujiendesha zenyewe Zipo nyingi zinaitwa failed state

Kuna nchi kama Somalia ,Congo,Yemen ,Sudan Sasa hivi nk Hivyo huhotaji tu jumuiya za kimataifa zihurumie raia na kwenda kuingilia kati kupitia kutuma majeshi ya kimataifa

Haiti ni failed state
 
Inasemekana aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo; ndio aliyepanga mauaji kwa rais; kwa hiyo machafuko lazima yataendelea kuwepo kutokana na makundi
 
Nchi kama hizo zinashindwa kujiendesha zenyewe Zipo nyingi zinaitwa failed state

Kuna nchi kama Somalia ,Congo,Yemen ,Sudan Sasa hivi nk Hivyo huhotaji tu jumuiya za kimataifa zihurumie raia na kwenda kuingilia kati kupitia kutuma majeshi ya kimataifa

Haiti ni failed state
Kuna nchi za kivita ambazo waasi wanaishi misituni, hivyo ni ngumu kidogo kwa jeshi la nchi na sometimes hata la nje kushindwa kupambana na watu wanaopambana wakiwa kisituni kama vile kule Congo, Sudan, Msumbiji nk.

Lakini kule Haiti na makundi tu ya wahuni wa mitaani kama vile panya road au wahalifu wengine wa kawaida. Sasa inashangaza jeshi linashindwaje kupambana na vijana wanaofanya matukio yao wakiwa mijini sio misituni ambapo ni ngumu kidogo kufikika?

Alafu bora Congo, Sudan, Msumbiji nk ambapo tunasikia jeshi likipambana na waasi, lakini Haiti hatukuwahi kusikia jeshi limepambana na hao wahuni, mara zote utasikia vyombo tu vya usalama kama vile polisi, usalama wa taifa nk. Je wanajeshi kweli au wana polisi tu peke yao?

Maana hata msaada wa nje wameomba polisi tu peke yao na sio jeshi.
 
Ndio maana ya neno failed state.
Kama wame fail kujiongoza kwa kipindi cha miaka takriban 200 toka wapate uhuru, basi kuna umuhimu wa kutafuta kuungana na taifa lingine lenye nguvu kama vile Marekani ili iwe sehem ya nchi hiyo (mkoa) na usalama wa mkoa (Haiti) uwe chini ya serikali ya Muungano kama ilivyo sisi kwa Zanzibar.
 
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."
Pieter W. Botha, a former President of South Africa during that Apartheid era.

Nchi ya Haiti ina watu weusi wengi wenye asili ya Afrika, kwa hiyo kinachoendelea huko siyo kitu cha ajabu, ni Yale Yale mambo ya Waafrika.
Ulichoandika nakikubali kwa asilimia karibu zote. Watu weusi kujitawala tumeshindwa, tena waliotawaliwa na Ufaransa ndio wanaoongoza kwa kushindwa kujitawala. Angalau kidogo zilizotawaliwa na waingereza wana kamuanga fulani machoni.
 
Kama wame fail kujiongoza kwa kipindi cha miaka takriban 200 toka wapate uhuru, basi kuna umuhimu wa kutafuta kuungana na taifa lingine lenye nguvu kama vile Marekani ili iwe sehem ya nchi hiyo (mkoa) na usalama wa mkoa (Haiti) uwe chini ya serikali ya Muungano kama ilivyo sisi kwa Zanzibar.
Maamuzi hayo ya kuungana atayafanya nani wakati nchi Haina serikali wala bunge
 
Maamuzi hayo ya kuungana atayafanya nani wakati nchi Haina serikali wala bunge
Hapo ndo shida ilipo. Alaf magenge yatapinga kuungana, maana huo ndio utakuwa mwisho wa kuendesha mambo yao kupitia magenge yao.
 
Kuna jamaa anaitwa Jimmy Berbecue Kiongozi wa hao wahuni unashangaa anatamba tu mtaani na anatizimwa tu bila kuguswa.
huyu hapa,Jimmy Cherizier a.k.a Berbecue.wahuni wote wanamtii yeye.

images (5).jpeg
 
Ulichoandika nakikubali kwa asilimia karibu zote. Watu weusi kujitawala tumeshindwa, tena waliotawaliwa na Ufaransa ndio wanaoongoza kwa kushindwa kujitawala. Angalau kidogo zilizotawaliwa na waingereza wana kamuanga fulani machoni.
Kwanini waliotawaliwa na Mfaransa ndio ngumu zaidi kujitawala kuliko waliotawaliwa na Muingereza?

HIVI MZUNGU mwenye teknolojia na silaha bora, anamvamia Muafrika[mwenye teknolojia na silaha duni] ambaye was just minding his own business, anajaribu kupambana lakini anashindwa, anataliwa for about 100 years na mzungu, ambaye anatengeneza mfumo wa dunia ambao ni ngumu kujinasua, then Mzungu huyo adai kuwa mwafrika huyo eti hawezi jitawala. Ni sawa na CCM wanavyodai kuwa CDM hawana uwezo wa kuongoza nchi wakati huo huo wameweka mifumo ya kuwazuia wasiwe huru.
 
Kwanini waliotawaliwa na Mfaransa ndio ngumu zaidi kujitawala kuliko waliotawaliwa na Muingereza?

HIVI MZUNGU mwenye teknolojia na silaha bora, anamvamia Muafrika[mwenye teknolojia na silaha duni] ambaye was just minding his own business, anajaribu kupambana lakini anashindwa, anataliwa for about 100 years na mzungu, ambaye anatengeneza mfumo wa dunia ambao ni ngumu kujinasua, then Mzungu huyo adai kuwa mwafrika huyo eti hawezi jitawala. Ni sawa na CCM wanavyodai kuwa CDM hawana uwezo wa kuongoza nchi wakati huo huo wameweka mifumo ya kuwazuia wasiwe huru.
Kuna tofauti kubwa ya system za kiutawala kati ya makoloni ya waingereza na wafaransa. Ndiomaana 95% ya nchi za kiafrika ambazo zimetawaliwa na wafaransa zipo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Na wafaransa wanatumia mwanya huo wa vita kuuza silaha kimya kimya kwa pande zote mbili yani wanaiuzia serikali, na kwa upande mungine wanawauzia waasi.

Wakati serikali inatoa hela keshi kununua silaha kwa wafaransa, waasi wao mara nyingi huwa hawana keshi, hivyo hubadilishana silaha kwa rasilimali za nchi wanazoiba katika maeneo wanayoyakalia mfano dhahabu, diamond, gesi nk.

Waingereza wao hawakujikita sana kwenye kuleta vita, bali wanatumia zaidi ubovu wa mikataba kati yake na serikali husika. Japo baadhi zina vita kutokana na tamaa ya baadhi ya watu wanaotaka kutawala nk.
 
Back
Top Bottom