omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 145
Kuna taarifa kuwa maslahi ya Waisrael ndiyo chanzo cha aliyekuwa mhariri mtendaji wa magazeti ya IPP kama The Gurdian, Nipashe, Alasiri na mengineyo mwanadada Sakina Datoo kulazimika kuachia ngazi.
Inasemekana kuwa Mzee Mengi aliamua kumshusha cheo Sakina kwa kumpeleka kuwa mhariri wa gazeti lisilokuwepo la Thisday on Sunday mara baada ya kubanwa na mashushu wa kisrael ambao kwa miaka kadha sasa wamekuwa wakifanikisha michongo mbalimbali ya kibiashara na misaada katika vyombo vyake vya habari kufanya hivyo. Hii ilifuatia kitendo cha Safina kumpokea Balozi Mpya wa Palestina ambaye alimgongea ofisini kwake kumsalimu na pia kumpa makala yake ambayo ilitoka katika gazeti mojawapo la IPP Media.
Inasemekana kuwa wakati Mengi amekuwa akijionyesha kuwa karibu na watu wa Palestina lakini ukweli Mengi amekuwa akitegemea sana misaada mbalimbali ikiwemo ya kiulinzi kutoka kwa "system" na serikali ya Israel.
Baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wamesema kuwa hilo si jambo la ajabu kwa Mengi kuamua kuchagua maslahi ya waisrael zaidi ya misingi ya kibinadamu na kitaifa ambayo amekuwa akijionyesha kuwa yupo mstari wa mbele kuitetea. Wanaendelea kusema kuwa iukiondoa tabia ya binafsi ya mfanyabiashara huyo mahiri inawezekana kuwa Mengi anatambua kuwa mahusiano mazuri na wababe kama Waisrael na Wamarekani ni muhimu sana kwake haswa wakati kama huu ambapo anaelekea kukosa ulinzi wa wenye kuhodhi nguvu za utawala.
Wadau wa karibu wa IPP media wanadai kuwa shinikizo la mashushu na serikali ya israel kupitia njia za kibalozi limekuja wakati mbaya ambapo tayari pia mahusiano kati yake na Sakina yalikuwa yameharibika kutokana na Sakina kukataa kubebeshwa uongozi wa magazeti yake mengine ambayo yalianzishwa maalumu na kuendeshwa kwa minajili ya kupambana na "ufisadi" pamoja na maadui zake wa kibiashara na kisiasa.
Inasemekana tayari Sakina Datoo ameacha kazi. Hii inakuwa mara ya pili kwa mwanadada huyu kuacha kazi kubwa kama hiyo inayompatia malipo makubwa kuzidi waandishi wengine wengi kutokana na mashinikizo yatokayo kwa wamiliki wa vyombo hovyo. Kabla ya Sakina kuajiriwa na Mengi alikuwa amejiuzulu The Citizen/Mwananchi baada ya kubanwa na wamiliki wake kutokana na taarifa aliyotoa iliyokuwa ikimpinga aliyekuwa waziri wa fedha wakati huo Bi Zakia Meghji.
Ukweli ni kuwa ile hali ya kuibuka upya kwa magazeti ya IPP Media mara baada ya Mengi kumuajiri Sakina na kumpa kiasi cha shilingi Bilioni Moja (inasemekana kuwa Waisrael walikuwa na mkono wao katika fedha hizi) kuajiri idadi kubwa ya waandishi mahiri kutoka katika mageziti mengine imeanza kufifia.
Baadhi ya waandishi hao mahiri waliopewa vidau vikubwa kuondoka katika vyombo walivyokuwa walimeanza kukimbia IPP Media na wengine wamekuwa wakihaha mitaani kuomba kazi za ama uandishi ama uafisa habai katika mashirika mbalimbali yakiwemo ya kitaifa na kimataifa.
Hawa ndio masiha wetu ................
Omarilyas
Inasemekana kuwa Mzee Mengi aliamua kumshusha cheo Sakina kwa kumpeleka kuwa mhariri wa gazeti lisilokuwepo la Thisday on Sunday mara baada ya kubanwa na mashushu wa kisrael ambao kwa miaka kadha sasa wamekuwa wakifanikisha michongo mbalimbali ya kibiashara na misaada katika vyombo vyake vya habari kufanya hivyo. Hii ilifuatia kitendo cha Safina kumpokea Balozi Mpya wa Palestina ambaye alimgongea ofisini kwake kumsalimu na pia kumpa makala yake ambayo ilitoka katika gazeti mojawapo la IPP Media.
Inasemekana kuwa wakati Mengi amekuwa akijionyesha kuwa karibu na watu wa Palestina lakini ukweli Mengi amekuwa akitegemea sana misaada mbalimbali ikiwemo ya kiulinzi kutoka kwa "system" na serikali ya Israel.
Baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wamesema kuwa hilo si jambo la ajabu kwa Mengi kuamua kuchagua maslahi ya waisrael zaidi ya misingi ya kibinadamu na kitaifa ambayo amekuwa akijionyesha kuwa yupo mstari wa mbele kuitetea. Wanaendelea kusema kuwa iukiondoa tabia ya binafsi ya mfanyabiashara huyo mahiri inawezekana kuwa Mengi anatambua kuwa mahusiano mazuri na wababe kama Waisrael na Wamarekani ni muhimu sana kwake haswa wakati kama huu ambapo anaelekea kukosa ulinzi wa wenye kuhodhi nguvu za utawala.
Wadau wa karibu wa IPP media wanadai kuwa shinikizo la mashushu na serikali ya israel kupitia njia za kibalozi limekuja wakati mbaya ambapo tayari pia mahusiano kati yake na Sakina yalikuwa yameharibika kutokana na Sakina kukataa kubebeshwa uongozi wa magazeti yake mengine ambayo yalianzishwa maalumu na kuendeshwa kwa minajili ya kupambana na "ufisadi" pamoja na maadui zake wa kibiashara na kisiasa.
Inasemekana tayari Sakina Datoo ameacha kazi. Hii inakuwa mara ya pili kwa mwanadada huyu kuacha kazi kubwa kama hiyo inayompatia malipo makubwa kuzidi waandishi wengine wengi kutokana na mashinikizo yatokayo kwa wamiliki wa vyombo hovyo. Kabla ya Sakina kuajiriwa na Mengi alikuwa amejiuzulu The Citizen/Mwananchi baada ya kubanwa na wamiliki wake kutokana na taarifa aliyotoa iliyokuwa ikimpinga aliyekuwa waziri wa fedha wakati huo Bi Zakia Meghji.
Ukweli ni kuwa ile hali ya kuibuka upya kwa magazeti ya IPP Media mara baada ya Mengi kumuajiri Sakina na kumpa kiasi cha shilingi Bilioni Moja (inasemekana kuwa Waisrael walikuwa na mkono wao katika fedha hizi) kuajiri idadi kubwa ya waandishi mahiri kutoka katika mageziti mengine imeanza kufifia.
Baadhi ya waandishi hao mahiri waliopewa vidau vikubwa kuondoka katika vyombo walivyokuwa walimeanza kukimbia IPP Media na wengine wamekuwa wakihaha mitaani kuomba kazi za ama uandishi ama uafisa habai katika mashirika mbalimbali yakiwemo ya kitaifa na kimataifa.
Hawa ndio masiha wetu ................
Omarilyas