Kongosho
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 35,999
- 24,165
Noamba niweke kisa kinachonitesa kila siku.
Ilikuwa mwaka 1976, nikiwa nimemaliza chuo cha uuguzi na kupangiwa kazi hospitali ya Mbeya.
Baada ya kufika Mbeya na kuanza makazi rasmi niliita wadogo zangu 2 wa kiume na kuanza kuishi nao.
Wakati nafanya kazi, nilitokea kuwa na mahusiano na dada mmoja aliyekuwa anasomea 'nursing', kiukweli nilimpenda sana, sana, sana, huyu alikuwa akiitwa Sophia. Naamini hadi leo hata Sophia alinipenda sana.
Baada ya mahusiano kama miaka 2, Sophia alipata ujauzito na alikuwa tayari kuolewa na mie na mimi nilikuwa tayari kumuoa.
Nikawajulisha ndugu zangu niliokuwa nao kuhusu uamuzi wangu wa kumuoa Sophia kabla ujauzito haujaonekana lakini walinipinga kwa nguvu zote.
Nimetokea kwenye ukoo ambao hatukuruhusiwa asilani kuoa ama kuolewa na mtu wa kabila lingine. Hii ilipelekea kutengwa na ukoo mzima.
Baada ya ndugu woote kukataa na kutishia kunitenga, nilijikuta nimemkataa Sophia kwa hofu ya kutengwa.
Sio siri iliniuma sana na hadi leo inaniuma nikikumbuka uso wa mshangao na kuchanganyikiwa wa Sophia baada ya kumkana simfahamu na wala sijawahi muona mbele ya mama yake. Alikuja na mama yake kutaka kujua msimamo wangu na binti yake. Kweli alilia kiasi cha ajabu sana.
Baada ya kama wiki moja, alinifuata peke yake akanijulisha mama yake ameamua kumpeleka hospitali akatolewe ujauzito, sikuwa na jinsi nilimuacha akatoa ujauzito na kuendelea na masomo yake.
Mwaka 1979, nilirudi nyumbani, nikaoa mwanamke wa kabila langu kwa baraka za ukoo mzima na kuhamia kufanya kazi hospitali moja katika mkoa wa Mwanza.
Mwaka 1981, nilipata mtoto wangu wa kwanza na sasa tuna watoto 4.
Baada ya maisha ya ndoa, ndio nikagundua/hisi machozi ya Sophia yaliniachia laana? Wakati mwingine nashindwa tofautisha nimeoa/nimeolewa.
Nilijikuta, baada ya kuoa nimeanza tabia ya ulevi, ikafikia kipindi nikawa siwezi fanya chochote bila pombe, na mke nae anakunywa pombe vile vile. I was an addict, bila kujua nimeingiaje kwenye alcoholism hii.
Mwaka 1989, nilisafiri kikazi kwenda Morogoro, dah, kweli dunia chungu, nilitaharuki siku moja gari imesimama pembeni yangu, mwanamke akashuka ndani ya gari kwa kufunguliwa mlango, sikuamini alikuwa ni Sophia alinifuata kwa furaha zote na kunisalimu. Alikuwa ameshaolewa na mwanajeshi mmoja mwenye cheo chake, nadhani major general.
Nilijiona kama nyongeza ya wanamme hapa duniani. Tuliongea na kuongea, hakuonekana kuwa na kinyongo, roho iliniuma kama mtu kanipokonya tonge langu mdomoni.
Mwaka 2000, ndipo niliamua kuacha pombe, baada ya kulewa na kuokotwa mtaroni. Walidhani nimepoteza uhai na kunihifadhi kwenye mochwari ya dispensari moja kabla ya kesho yake asubuhi kuhamishiwa hospitali kubwa, niliamka nakujikuta mochwari, kuanzia hapo nilifanyia kazi tatizo langu la pombe na kuacha.
Taztizo linalonisumbua sasa, ni hii ndoa, naishi kama kifungoni. Mke wangu bado mlevi anarudi muda anaotaka. Inanibidi nifanye kazi ya ubaba na umama maana mwenzangu haeleweki kabisa.
Nikikumbuka aliyekuwa chaguo langu, roho inaniuma sana. Nisingekubali kusikiliza ndugu labda ningeishi ndoa ya furaha.
Popote uliko Sophia, jua bado nakukumbuka sana, na huwa najutia sana nilichokifanya. Nimeandika hapa ili kupunguza pressure ndani yangu walimwengu msinisulubu kwa komment zenu, ndoa inanisulubu vya kutosha.
Na kwa ambao hamjaoa wala kuolewa 'follow your heart' nduguzo hawatakuwepo wakati familia yako inaparaganyika.
Asanteni
Ilikuwa mwaka 1976, nikiwa nimemaliza chuo cha uuguzi na kupangiwa kazi hospitali ya Mbeya.
Baada ya kufika Mbeya na kuanza makazi rasmi niliita wadogo zangu 2 wa kiume na kuanza kuishi nao.
Wakati nafanya kazi, nilitokea kuwa na mahusiano na dada mmoja aliyekuwa anasomea 'nursing', kiukweli nilimpenda sana, sana, sana, huyu alikuwa akiitwa Sophia. Naamini hadi leo hata Sophia alinipenda sana.
Baada ya mahusiano kama miaka 2, Sophia alipata ujauzito na alikuwa tayari kuolewa na mie na mimi nilikuwa tayari kumuoa.
Nikawajulisha ndugu zangu niliokuwa nao kuhusu uamuzi wangu wa kumuoa Sophia kabla ujauzito haujaonekana lakini walinipinga kwa nguvu zote.
Nimetokea kwenye ukoo ambao hatukuruhusiwa asilani kuoa ama kuolewa na mtu wa kabila lingine. Hii ilipelekea kutengwa na ukoo mzima.
Baada ya ndugu woote kukataa na kutishia kunitenga, nilijikuta nimemkataa Sophia kwa hofu ya kutengwa.
Sio siri iliniuma sana na hadi leo inaniuma nikikumbuka uso wa mshangao na kuchanganyikiwa wa Sophia baada ya kumkana simfahamu na wala sijawahi muona mbele ya mama yake. Alikuja na mama yake kutaka kujua msimamo wangu na binti yake. Kweli alilia kiasi cha ajabu sana.
Baada ya kama wiki moja, alinifuata peke yake akanijulisha mama yake ameamua kumpeleka hospitali akatolewe ujauzito, sikuwa na jinsi nilimuacha akatoa ujauzito na kuendelea na masomo yake.
Mwaka 1979, nilirudi nyumbani, nikaoa mwanamke wa kabila langu kwa baraka za ukoo mzima na kuhamia kufanya kazi hospitali moja katika mkoa wa Mwanza.
Mwaka 1981, nilipata mtoto wangu wa kwanza na sasa tuna watoto 4.
Baada ya maisha ya ndoa, ndio nikagundua/hisi machozi ya Sophia yaliniachia laana? Wakati mwingine nashindwa tofautisha nimeoa/nimeolewa.
Nilijikuta, baada ya kuoa nimeanza tabia ya ulevi, ikafikia kipindi nikawa siwezi fanya chochote bila pombe, na mke nae anakunywa pombe vile vile. I was an addict, bila kujua nimeingiaje kwenye alcoholism hii.
Mwaka 1989, nilisafiri kikazi kwenda Morogoro, dah, kweli dunia chungu, nilitaharuki siku moja gari imesimama pembeni yangu, mwanamke akashuka ndani ya gari kwa kufunguliwa mlango, sikuamini alikuwa ni Sophia alinifuata kwa furaha zote na kunisalimu. Alikuwa ameshaolewa na mwanajeshi mmoja mwenye cheo chake, nadhani major general.
Nilijiona kama nyongeza ya wanamme hapa duniani. Tuliongea na kuongea, hakuonekana kuwa na kinyongo, roho iliniuma kama mtu kanipokonya tonge langu mdomoni.
Mwaka 2000, ndipo niliamua kuacha pombe, baada ya kulewa na kuokotwa mtaroni. Walidhani nimepoteza uhai na kunihifadhi kwenye mochwari ya dispensari moja kabla ya kesho yake asubuhi kuhamishiwa hospitali kubwa, niliamka nakujikuta mochwari, kuanzia hapo nilifanyia kazi tatizo langu la pombe na kuacha.
Taztizo linalonisumbua sasa, ni hii ndoa, naishi kama kifungoni. Mke wangu bado mlevi anarudi muda anaotaka. Inanibidi nifanye kazi ya ubaba na umama maana mwenzangu haeleweki kabisa.
Nikikumbuka aliyekuwa chaguo langu, roho inaniuma sana. Nisingekubali kusikiliza ndugu labda ningeishi ndoa ya furaha.
Popote uliko Sophia, jua bado nakukumbuka sana, na huwa najutia sana nilichokifanya. Nimeandika hapa ili kupunguza pressure ndani yangu walimwengu msinisulubu kwa komment zenu, ndoa inanisulubu vya kutosha.
Na kwa ambao hamjaoa wala kuolewa 'follow your heart' nduguzo hawatakuwepo wakati familia yako inaparaganyika.
Asanteni