Borakufa
JF-Expert Member
- May 26, 2011
- 1,503
- 390
Heshima kwenu wakuu!
Tido Muhando alipofanyiwa zengwe TBC wengine tulijua nini kinafuata! Shirika hili ambalo ni mali yetu sisi wananchi lilisimama katika kutoa haki japo lilikuwa likibanywa kwa njia moja au nyingine wakati wa ukurugenzi wa Tido Muhando. Kweli alikuwa na mapungufu yake kama binadamu, lakini kwa kiasi kikubwa wananchi wengi waliridhika na utendaji wake.
Ni wiki mbili tu tangu kuteuliwa mkurugenzi mpya huwezi kuamini sifa za TBC kwisha kabisa! wanaripoti uongo mtupu na habari za upande mmoja tu. Hivi ndivyo ilikuwa asili ya TBC. Ilitumika kuwadanganya wananchi huko nyuma ili tutawaliwe wanavyotaka watawala kandamizi.
Ninachotaka kusema hapa namshauri yule ambaye bado anafikiria kuwa eti bado anaweza kulitumia shirika la habari ambalo linaendeshwa kwa fedha zetu sisi wananchi eti kutudanganya kwa faida ya tumbo lake kama ilivyokuwa RTD na TVT. zama za zidumu fikra sahihi zilishapitwa na wakati.
Wito kwa mkurugenzi mpya wa TBC namsihi kuachana na mpango wake wa kutuchakachulia habari kwani kufanya hivyo atakuwa analipwa fedha zetu kwa njia haramu.
Tafakari chukua hatua!
Tido Muhando alipofanyiwa zengwe TBC wengine tulijua nini kinafuata! Shirika hili ambalo ni mali yetu sisi wananchi lilisimama katika kutoa haki japo lilikuwa likibanywa kwa njia moja au nyingine wakati wa ukurugenzi wa Tido Muhando. Kweli alikuwa na mapungufu yake kama binadamu, lakini kwa kiasi kikubwa wananchi wengi waliridhika na utendaji wake.
Ni wiki mbili tu tangu kuteuliwa mkurugenzi mpya huwezi kuamini sifa za TBC kwisha kabisa! wanaripoti uongo mtupu na habari za upande mmoja tu. Hivi ndivyo ilikuwa asili ya TBC. Ilitumika kuwadanganya wananchi huko nyuma ili tutawaliwe wanavyotaka watawala kandamizi.
Ninachotaka kusema hapa namshauri yule ambaye bado anafikiria kuwa eti bado anaweza kulitumia shirika la habari ambalo linaendeshwa kwa fedha zetu sisi wananchi eti kutudanganya kwa faida ya tumbo lake kama ilivyokuwa RTD na TVT. zama za zidumu fikra sahihi zilishapitwa na wakati.
Wito kwa mkurugenzi mpya wa TBC namsihi kuachana na mpango wake wa kutuchakachulia habari kwani kufanya hivyo atakuwa analipwa fedha zetu kwa njia haramu.
Tafakari chukua hatua!