Baba yangu alifariki mwaka jana mwezi wa saba, katika harakati za kufuatilia mali zake tukakuta kumbe nyumba moja imeshauzwa kwa Mpangaji anaekaa humo ndani kitambo tu. baada ya kupekua nyaraka za marehemu hatukukuta hata chembe ya "document" kuonyesha kuwa imeuzwa, Lakini katika zile hati za mauzo kati ya Marehemu yaani BABA na Mnunuzi yaani yule (Mpangaji). kuna mashahidi wa3 yaani Mununuzi, Mkewe na mtoto wao, kwa upande wa muuzaji alikuwepo pekee yake pamoja na Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa eneo husika
JE, ni kweli haya yatakuwa mauzo halali kisheria.
JE, ni kweli haya yatakuwa mauzo halali kisheria.