Mapishi ya Mlenda wa bamia na nyanya chungu

FirstLady1

JF-Expert Member
Jul 29, 2009
16,792
5,375
Karibuni kwa Bibi yangu Singida>.

[h=3]Mapishi ya Mlenda wa bamia na nyanya chungu[/h]
Mahitaji
Bamia (okra) 20
Nyanya chungu (garden eggs) 5
Magadi soda (Bicabonate soda) 1/4 ya kijiko cha chai
Nyanya (fresh tomato) 1
Chumvi (salt) kidogo
Pilipili 1/4

Matayarisho
Osha bamia, nyanya chungu na nyanya kisha vikatekate katika vipande vidogovidogo. Baada ya hapo vitie kwenye sufuria na vitu vyote vilivyobakia na kisha tia maji kidogo.Chemsha mpaka bamia na nyanya chungu ziive na vimaji vibakie kidogo sana. Baada ya hapo ziponde na mwiko kidogo kisha zikoroge na uipue na mlenda utakuwa tayari kwa kuliwa na ugali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom