Mapinduzi Cup imeoza, mshindi amepangwa. Rwanda kutoshiriki tena? Simba inatolewa leo kwa Maelekezo?

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,047
20,411
Baada ya APR kunyimwa goli lililoonekana ni halali likifungwa na mchezaji Shiboub aliyewahi kuchezea Simba Sports. Baada ya mechi kocha wa APR alilalamika kubebwa waziwazi kwa timu ya nyumbani Mlandege jambo ambalo si la kiuanamichezo na kwa kuzingatia heshima ya mashindano hayo yanayoshirikisha timu za ndani na nje ya nchi.

Kibaya zaidi hii clip uionayo hapa juu Azam wameiachia kwenye social medias baada ya kusikia malalamiko kwani kwenye live TV interview ilipofikia kocha kutoa lawama na kutishia kutoshiriki tena basi kwa haraka walikatiza interview ya kocha na kuweka tangazo ili tuhuma alizokuwa akitoa zisisikike.

Huku ni kuonyesha udhaifu wa soka na pia vyombo vyetu vya habari hasa kile cha tibisii, asam na wengine wanaoripoti.Imagine huko Rwanda mashabiki wanaoamini timu yao kupokwa ushindi bado tena wanaona kocha wako akizimiwa live interview watajisikiaje?

Yani ung'olewe meno halafu upewe bisi za kutafuna?

Tanzania inawezekana tumekuza matangazo tu ya mipira na viwanja ila soka bado sana kutokana na kubebana. Hayo mafanikio tunayosema Simba na Yanga wamepata kimataifa yamechangiwa na wachezaji wa kulipwa wa kigeni na sio wazawa wanaobebwa na ndiyo maana upande wa Taifa Stars isiyo na professionals wa kigeni bado tunajikongoja.

Ingependeza kiungwana referee wa mechi ya jana apewe adhabu stahili na pia TFF kuiomba radhi club ya APR ya Rwanda na Rais Kagame ambaye pia tunategemea kumfungia yule refa kutokanyaga Rwanda.

Azam TV pia ambao licha ya kutangaza mechi hiyo ni wadhamini pia wa APR wanapaswa kuomba radhi kwa kukatiza interview live katika Televisheni ili malalamiko ya Kocha yasisikike.Azam wamekuwa maduwanzi, hata kurudia lile goli kwenye kila angle wamekataa na ukweli ni kwamba sasa hivi ili kombe ni kama bonanza la CCM ambalo mshndi ni timu ya Mbunge aliyeandaa Bonanza.

Tujitathmini na Tukuze Soka kiuhalisia sio kwa upendeleo wa home team jambo ambalo limeonekana kukua mizizi hata kwenye ligi ya bara hasa kwa timu kubwa na hata ziitwazo ndogo zikiwa viwanja vya nyumbani na kwa matokeo mengi tuliyoshuhudia katika mchezo wa Boxing kutoa ushindi fake kwa mabondia wa nyumbani.

Kisiasa tupore ushindi, kimichezo nako tupore ushindi tunaenda wapi? Kila kitu sisi ni rafu?


Tubadilike.
 
Hata Yanga iliondolewa kwa hila. Mwakani wazanzibari wakatafute washiriki toka Somalia.

Walipanga matokeo ya urais sasa WANAPANGA matokeo ya michezo. Wacha wapeane Hilo kombe tuone Kama watakuza kiwango cha mpira visiwani.

Corruption is eating all sectors in the isles.
 
Simba wali beba Ngao ya Jamii kwakubebwa mechi karibu zote mpaka kwenye matuta.

Mlandege hajabebwa kama alivyo Bebwa Simba Sasa huu ujasiri wa kuwasimanga Mlandege mnautoa wapi?

Mechi zote alizochezesha Tatu Malogo kwenye Ngao zili ibeba Simba na maisha yaliendelea.
 
View attachment 2867048

Baada ya APR kunyimwa goli lililoonekana ni halali likifungwa na mchezaji Shiboub aliyewahi kuchezea Simba Sports.
Baada ya mechi kocha wa APR alilalamika kubebwa waziwazi kwa timu ya nyumbani Mlandege jambo ambalo si la kiuanamichezo na kwa kuzingatia heshima ya mashindano hayo yanayoshirikisha timu za ndani na nje ya nchi.
Kibaya zaidi hii clip uionayo hapa juu Azam wameiachia kwenye social medias baada ya kusikia malalamiko kwani kwenye live TV interview ilipofikia kocha kutoa lawama na kutishia kutoshiriki tena basi kwa haraka walikatiza interview ya kocha na kuweka tangazo ili tuhuma alizokuwa akitoa zisisikike.

Huku ni kuonyesha udhaifu wa soka na pia vyombo vyetu vya habari hasa kile cha tibisii, asam na wengine wanaoripoti.Imagine huko Rwanda mashabiki wanaoamini timu yao kupokwa ushindi bado tena wanaona kocha wako akizimiwa live interview watajisikiaje?

Yaani ung'olewe meno halafu upewe bisi za kutafuna?

Tanzania inawezekana tumekuza matangazo tu ya mipira na viwanja ila soka bado sana kutokana na kubebana.
Hayo mafanikio tunayosema Simba na Yanga wamepata kimataifa yamechangiwa na wachezaji wa kulipwa wa kigeni na sio wazawa wanaobebwa na ndiyo maana upande wa Taifa Stars isiyo na professionals wa kigeni bado tunajikongoja.

Ingependeza kiungwana referee wa mechi ya jana apewe adhabu stahili na pia TFF kuiomba radhi club ya APR ya Rwanda na Rais Kagame ambaye pia tunategemea kumfungia yule refa kutokanyaga Rwanda.

Azam TV pia ambao licha ya kutangaza mechi hiyo ni wadhamini pia wa APR wanapaswa kuomba radhi kwa kukatiza interview live katika Televisheni ili malalamiko ya Kocha yasisikike.Azam wamekuwa maduwanzi, hata kurudia lile goli kwenye kila angle wamekataa na ukweli ni kwamba sasa hivi ili kombe ni kama bonanza la CCM ambalo mshndi ni timu ya Mbunge aliyeandaa Bonanza.

Tujitathmini na Tukuze Soka kiuhalisia sio kwa upendeleo wa home team jambo ambalo limeonekana kukua mizizi hata kwenye ligi ya bara hasa kwa timu kubwa na hata ziitwazo ndogo zikiwa viwanja vya nyumbani na kwa matokeo mengi tuliyoshuhudia katika mchezo wa Boxing kutoa ushindi fake kwa mabondia wa nyumbani.

Kisiasa tupore ushindi,Kimichezo nako tupore ushindi tunaenda wapi? Kila kitu sisi ni rafu?


Tubadikike.
Zanzibar ama Wazanzibari wanapenda mbeleko sana.

Kila nyanja wanataka kubebwa/kupendelewa.

Wanyarwanda sio kama watanganyika waliojaa unafiki na uoga...wanyarwanda na Kagame wao kama ni nyeusi wanasema ni nyeusi na si vinginevyo.
 
Hakuna haja ya kulalamika saana, ningekuona wa maana kama ungesisitiza matumizi ya Assistant Referee Video (ARV) next time kwenye mashindano haya, maana hata lefa ni mwanadamu mwenye macho mawili.

By the way mpira umechezwa dakika 90, kama APR walikuwa bora mbona hawakufunga jingine? pia kama walikuwa bora kwa nini hawakupiga penatI kwa ubora.

Ni kwamba washapigwa,ishaisha hiyo, na wanaolalamika hapa ni UTO na si APR.
 
Simba wali beba Ngao ya Jamii kwakubebwa mechi karibu zote mpaka kwenye matuta.

Mlandege hajabebwa kama alivyo Bebwa Simba Sasa huu ujasiri wa kuwasimanga Mlandege mnautoa wapi?

Mechi zote alizochezesha Tatu Malogo kwenye Ngao zili ibeba Simba na maisha yaliendelea.
Soccar letu kivyetu vyetu.
 
Hata Yanga iliondolewa kwa hila. Mwakani wazanzibari wakatafute washiriki toka Somalia.

Walipanga matokeo ya urais sasa WANAPANGA matokeo ya michezo. Wacha wapeane Hilo kombe tuone Kama watakuza kiwango cha mpira visiwani.

Corruption is eating all sectors in the isles.
Wewe topolo acha upumbavu, mlifunga goli gani likakataliwa? Kocha wenu kasema mlienda kujaribu wachezaji wewe unakuja na utopolo wako hapa.
 
Back
Top Bottom