Manchester City bado itatawala sana

Sella turcica

Senior Member
Oct 13, 2020
104
193
Kila jambo huwa na zama zake. Kwenye mpira ni hivyo hivyo, clubs hutamba na kupotea. Zama za Man U na Chelsea zimekwisha. Tangu SAF aondoke man u haijafanikiwa kushinda taji la EPL. Usinambie shida ni budget, maana wamiliki wanatoa mpunga wa kutosha tu. Hali kadhalika ndugu yao Chelsea nae yuko hoi. Wametumia pesa nyingi sana kufanya usajili lakini hamna kinachoonekana.

Njoo kwa Man city. Tangu Sheikh Mansour aichukue timu mwaka 2008 wamekuwa wakipiga hatua kwenda mbele. Walitamba kwenye EPL ila kipengele ilikuwa kutamba kwenye UEFA. Wamemvumilia Pep kwa miaka 7 ndipo wakafanikiwa kupata taji la kwanza la UEFA.

Siwezi kuisifia zaidi ila ukweli usemwe kwa sasa man city ni team ambayo inaendeshwa kisasa na kwa weledi. Angalia sajili zao, wachache sana ndo wanashindwa kuonyesha makali kama kina Kalvin Philips. Wengi wao wanafanikiwa kuonyesha potential zao. Fikiria mtu kama Akanji au Alvarez; ni watu walionuniliwa kwa pesa ndogo sana, less than 20 M euros, lakini shughuli zao uwanjani zinaonekana.

Kuna huyu bwana mdogo Doku, amenunuliwa kwa euros 55 M lakini mziki wake mjana mmeuona. Grealish huko aliko anaogopa. Sasa njoo angalia man u walimchukua Anthony kwa euros 85 M lakini anachofanya ni kupiga watu mabuti. Chelsea walimchukua Mudryk kwa 100M euros ila hajaweza kudeliver. Kwa sasa mchezaji kukataa kwenda man city ni sawa na kupishana na gari la mshahara. Harry Kane anaelewa vizuri hili. Nina uhakika city wangempata Kane basi huenda jamaa angetwaa Ballon D’or.

Mchezaji anaweza kuwa mzuri ila akienda Chelsea au man U mnamkataa kabisa. Zile timu ni kama zina gundu hivi.
Arsenal japo wanajitahidi ila bado, hawajafika kwenye levels za kushindania makombe. Mpinzani wa Man city ni Liverpool. Na timu zisipokaa vizuri Pep anabeba tena ile ndoo. Pep anaufanya mpira uonekane rahisi sana. Wapinzani wake wanajaribu kusema anapewa hela za waarabu, wakikumbuka timu zao nazo zimesajili wanaamua kunyamaza. Kama wewe kweli ni mpenzi wa soka safi huwezi kukosa kuangalia game za man city. Tuenjoy zama hizi kabla hazijapita.
 
Kila jambo huwa na zama zake. Kwenye mpira ni hivyo hivyo, clubs hutamba na kupotea. Zama za Man U na Chelsea zimekwisha. Tangu SAF aondoke man u haijafanikiwa kushinda taji la EPL. Usinambie shida ni budget, maana wamiliki wanatoa mpunga wa kutosha tu. Hali kadhalika ndugu yao Chelsea nae yuko hoi. Wametumia pesa nyingi sana kufanya usajili lakini hamna kinachoonekana.

Njoo kwa Man city. Tangu Sheikh Mansour aichukue timu mwaka 2008 wamekuwa wakipiga hatua kwenda mbele. Walitamba kwenye EPL ila kipengele ilikuwa kutamba kwenye UEFA. Wamemvumilia Pep kwa miaka 7 ndipo wakafanikiwa kupata taji la kwanza la UEFA.

Siwezi kuisifia zaidi ila ukweli usemwe kwa sasa man city ni team ambayo inaendeshwa kisasa na kwa weledi. Angalia sajili zao, wachache sana ndo wanashindwa kuonyesha makali kama kina Kalvin Philips. Wengi wao wanafanikiwa kuonyesha potential zao. Fikiria mtu kama Akanji au Alvarez; ni watu walionuniliwa kwa pesa ndogo sana, less than 20 M euros, lakini shughuli zao uwanjani zinaonekana.

Kuna huyu bwana mdogo Doku, amenunuliwa kwa euros 55 M lakini mziki wake mjana mmeuona. Grealish huko aliko anaogopa. Sasa njoo angalia man u walimchukua Anthony kwa euros 85 M lakini anachofanya ni kupiga watu mabuti. Chelsea walimchukua Mudryk kwa 100M euros ila hajaweza kudeliver. Kwa sasa mchezaji kukataa kwenda man city ni sawa na kupishana na gari la mshahara. Harry Kane anaelewa vizuri hili. Nina uhakika city wangempata Kane basi huenda jamaa angetwaa Ballon D’or.

Mchezaji anaweza kuwa mzuri ila akienda Chelsea au man U mnamkataa kabisa. Zile timu ni kama zina gundu hivi.
Arsenal japo wanajitahidi ila bado, hawajafika kwenye levels za kushindania makombe. Mpinzani wa Man city ni Liverpool. Na timu zisipokaa vizuri Pep anabeba tena ile ndoo. Pep anaufanya mpira uonekane rahisi sana. Wapinzani wake wanajaribu kusema anapewa hela za waarabu, wakikumbuka timu zao nazo zimesajili wanaamua kunyamaza. Kama wewe kweli ni mpenzi wa soka safi huwezi kukosa kuangalia game za man city. Tuenjoy zama hizi kabla hazijapita.
Wachache wenye akili watakuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu,kwahiyo hapa umemsifu mmiliki wa team Sheikh Mansoor au Kocha Pep Guardiola? coz umekubali kua Chelsea na Man united nao pia wanapewa hela za kutosha na wamiliki wao,

Nakubaliana na wewe kua Man city atatawala sana pale EPL na pengine hata UEFA.
 
Mkuu,kwahiyo hapa umemsifu mmiliki wa team Sheikh Mansoor au Kocha Pep Guardiola? coz umekubali kua Chelsea na Man united nao pia wanapewa hela za kutosha na wamiliki wao,

Nakubaliana na wewe kua Man city atatawala sana pale EPL na pengine hata UEFA.
City anakuja vizuri sana, ila UEFA kimsingi ni uwanja wa nyumbani wa Liverpool, hata sasa naamini UEFA haijanoga bila Liverpool. City amejaribu jaribu ila Liverpool anakua na uhakika sana UEFA.
VAR isingetuonea ile game na Spurs hata sasa tungekuwa tunaongoza ligi, ila bado hatujachelewa, leo tunarudi nafasi ya pili na baadae tutarudi kileleni.

Ila kweli kwa sasa pale Uingereza washindani ni Liverpool na Man City tu.
 
Mkuu,kwahiyo hapa umemsifu mmiliki wa team Sheikh Mansoor au Kocha Pep Guardiola? coz umekubali kua Chelsea na Man united nao pia wanapewa hela za kutosha na wamiliki wao,

Nakubaliana na wewe kua Man city atatawala sana pale EPL na pengine hata UEFA.

Wote, mmiliki, kocha na sporting director. Mmiliki anajua kuwa hajui mambo ya mpira akahire watu wanaoujua. Akawapa pesa then akakaa pembeni kuvuna matunda ya uwekezaji.
 
City anakuja vizuri sana, ila UEFA kimsingi ni uwanja wa nyumbani wa Liverpool, hata sasa naamini UEFA haijanoga bila Liverpool. City amejaribu jaribu ila Liverpool anakua na uhakika sana UEFA.
VAR isingetuonea ile game na Spurs hata sasa tungekuwa tunaongoza ligi, ila bado hatujachelewa, leo tunarudi nafasi ya pili na baadae tutarudi kileleni.

Ila kweli kwa sasa pale Uingereza washindani ni Liverpool na Man City tu.

Mkuu hadi leo Liverpool hajaweza kufuta uteja kwa Madrid, unalizungumziaje hilo?
 
Mkuu hadi leo Liverpool hajaweza kufuta uteja kwa Madrid, unalizungumziaje hilo?
Mkuu, unajua ni kama vile Liverpool asivyoogopa mechi za UEFA huku kwenye ligi kunamsumbua sumbua. Madrid when it comes to UEFA ni kama utamaduni vile, watafanya kila wawezavyo kulibeba. Wanatuzidi kwa uzoefu.

Hata historia inawabeba mzee, wamebeba mara 13 sijui.. lile ni kama kombe lao hivi..

Ila uteja ni tukikutana nao kuanzia nusu fainali, ikiwa ni hatua za makundi huku tunawapiga tu
 
Mkuu, unajua ni kama vile Liverpool asivyoogopa mechi za UEFA huku kwenye ligi kunamsumbua sumbua. Madrid when it comes to UEFA ni kama utamaduni vile, watafanya kila wawezavyo kulibeba. Wanatuzidi kwa uzoefu.

Hata historia inawabeba mzee, wamebeba mara 13 sijui.. lile ni kama kombe lao hivi..

Ila uteja ni tukikutana nao kuanzia nusu fainali, ikiwa ni hatua za makundi huku tunawapiga tu

Sasa ili uweze kujiestablish kama mbabe lazima uweze kumbutua Madrid. Jamaa wamewafanya Liverpool wateja wao wa kudumu. Usipoweza kumtoa Real Madrid basi sahau kuhusu UEFA. Ila nina uhakika EUROPA inaenda Liverpool
 
Game ya Bournemouth isikutoe Kwenye reli... Msimu uliopita away Bournemouth walipigwa 9-0 na Liverpool kwao vipigo vikubwa washavizoea....

Doku ni mchezaji Jana alipaform vizuri sana lakini kusema atamuweka Jack benchi moja Kwa moja ni ngumu japo naamini ni mzuri kuliko Jack.

Kumpa ubingwa City moja Kwa moja bado ni mapema Sana. Japo ana asilimia nyingi za kushinda kulingana na timu inavocheza na wachezaji wengi wenye talents iliyonayo.

Kitu pekee city anachoweza kujivunia ni wapinzani dhaifu alionao. Arsenal ni ngoma ya watoto, man U ndo kama unavowaona, Chelsea ipo ICU... Tottenham Hotspur ni Moto wa makaratasi. Walau Liverpool ndo mpinzani sahihi tatizo Naye hua anakumbwa na majeruhi anapoteana mazima.

Tusubiri mechi 18 Kwanza tutajua mbivu na mbichi.
 
Game ya Bournemouth isikutoe Kwenye reli... Msimu uliopita away Bournemouth walipigwa 9-0 na Liverpool kwao vipigo vikubwa washavizoea....

Doku ni mchezaji Jana alioaform vizuri sana lakini kusema atamueka Jack benchi moja Kwa moja ni ngumu japo naamini ni mzuri kuliko Jack.

Kumpa ubingwa City moja Kwa moja bado ni mapema Sana. Japo ana asilimia nyingi za kushindi kulingana na timu inavocheza na wachezaji wengi wenye talents iliyonayo.

Kitu pekee city anachoweza kujivunia ni wapinzani dhaifu alionao. Arsenal ni ngoma ya watoto, man U ndo kama unavowaona, Chelsea ipo ICU... Tottenham Hotspur ni Moto wa makaratasi. Walau Liverpool ndo mpinzani sahihi tatizo Naye hua anakumbwa na majeruhi anapoteana mazima.

Tusubiri mechi 18 Kwanza tutajua mbivu na mbichi.

Sio game ya Bournemouth pekee mkuu. City amekuwa dominant kwa misimu nenda rudi, amekuwa consistent. Tangu ameanza kuingia big 4 hajawahi kutoka. Wamefanikiwa kufanya transition ya wachezaji bila kupoteza ubora wa timu. Hivi ndo vitu vitafanya aendelee kutawala. Nasubiri game na Liverpool tarehe 25 mwezi huu pale Etihad.
 
Sio game ya Bournemouth pekee mkuu. City amekuwa dominant kwa misimu nenda rudi, amekuwa consistent. Tangu ameanza kuingia big 4 hajawahi kutoka. Wamefanikiwa kufanya transition ya wachezaji bila kupoteza ubora wa timu. Hivi ndo vitu vitafanya aendelee kutawala. Nasubiri game na Liverpool tarehe 25 mwezi huu pale Etihad.
Mi nazungumzia msimu huu..
Naamini hata huu Uzi umeufungua baada ya game ya Jana City kutoa kichapo heavy Kwa Bournemouth. Tunajua city kawa mzuri tangu enzi za Robert Mancini na Balotelli wake, lakini hoja yangu kubwa ni kua bado ni mapema kumpa ubingwa..
Kumbuka 2016 Leicester aliibuka na kubeba ubingwa Katika mazingira tatanishi na city alimaliza akiwa namba 4, hivo siwezi kumpa guarantee kua atakua bingwa Hadi dakika ya mwisho.

Lakini pia msimu wa 2018/19 City alishinda kombe Kwa mbinde ambapo alimzidi Liverpool point moja Tu... Alikua na point 98 huku liver akiwa na point 97!!..... Msimu uliofata liver alichukua kombe Kwa points 99...

Kwahiyo bado ni mapema Sana Mzee ndo Kwanza tupo game week ya 11...
 
Sasa ili uweze kujiestablish kama mbabe lazima uweze kumbutua Madrid. Jamaa wamewafanya Liverpool wateja wao wa kudumu. Usipoweza kumtoa Real Madrid basi sahau kuhusu UEFA. Ila nina uhakika EUROPA inaenda Liverpool
Vile tunavibutua vitimu kule magoli 5 nk Sevilla mwenye kombe lake Euro hayupo, tuna imani tutabeba. Tuna hasira sana na UEFA msimu ujao, tushiriki kwa kuwa mabingwa wa EUROPA na pia kwa kuwa Top 4 EPL

Madrid ile game ya 2018 hatutaisahau...ilikuwa tumpige goli za kutosha, kabla ya Ramos kumuumiza Salah
 
Umesema kweli kabisa
Pia umewataja man city na Liverpool
Lakini kumbuka Tottenham now means business
 
Sana ni muda gani ?

Kuna sustainable way ya kuendesha Clup; Kuna kutegemea Pesa (ingawa sio guarantee ya kushinda) kuna chemistry na feel good factor katika sehemu husika..., Man United ilitawala kwa muda wa Sir Alex sio sababu ya Pesa pekee au Ujuzi wa Sir Alex bali ilikuwa na bahati ya kupata crop ya wachezaji wengi kwa wakati mmoja kutoka academy jambo ambalo lilikuwa a backbone...

Ila ukiniuliza sana nadhani EPL timu nyingi ni unsustainable bora hata Liverpool na Fan base yake na Foundation naweza kusema ina misingi imara..., ila ukiniuliza jinsi bora ya kuendesha Timu nitakujibu....

 
Vile tunavibutua vitimu kule magoli 5 nk Sevilla mwenye kombe lake Euro hayupo, tuna imani tutabeba. Tuna hasira sana na UEFA msimu ujao, tushiriki kwa kuwa mabingwa wa EUROPA na pia kwa kuwa Top 4 EPL

Madrid ile game ya 2018 hatutaisahau...ilikuwa tumpige goli za kutosha, kabla ya Ramos kumuumiza Salah

Game ya 2022 jamaa walifika golini kwenu mara mbili na zote zilikuwa kamba sema moja ilikuwa offside. Ukiweka na kipigo cha 5-2 Anfield, mna deni kubwa sana na hawa jamaa.
 
Umesema kweli kabisa
Pia umewataja man city na Liverpool
Lakini kumbuka Tottenham now means business

Toti ni ile ile, ipo kuvuruga mipango ya watu na sio kushinda makombe. Ni suala la muda kabla hajashuka. Usishangae kesho akadondosha points kwa Chelsea.
 
Mi nazungumzia msimu huu..
Naamini hata huu Uzi umeufungua baada ya game ya Jana City kutoa kichapo heavy Kwa Bournemouth. Tunajua city kawa mzuri tangu enzi za Robert Mancini na Balotelli wake, lakini hoja yangu kubwa ni kua bado ni mapema kumpa ubingwa..
Kumbuka 2006 Leicester aliibuka na kubeba ubingwa Katika mazingira tatanishi na city alimaliza akiwa namba 4, hivo siwezi kumpa guarantee kua atakua bingwa Hadi dakika ya mwisho.

Lakini pia msimu wa 2018/19 City alishinda kombe Kwa mbinde ambapo alimzidi Liverpool point moja Tu... Alikua na point 98 huku liver akiwa na point 97!!..... Msimu uliofata liver alichukua kombe Kwa points 99...

Kwahiyo bado ni mapema Sana Mzee ndo Kwanza tupo game week ya 11...
Kumbe Leicester alichukua ubingwa 2006🤷
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom