Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,914
- 6,033
Leo ratiba ya UCL imetoka na Arsenal amepangwa na Bayern Munich. Baada ya kuona ratiba hii, nikawaonea huruma mashabiki wa Arsenal kwani wanaenda kumaliza msimu tena bila taji lolote.
Arsenal ataanzia nyumbani Emirates kisha kwenda Allianz Arena ambapo huko atakufa nyingi si mnajua Harry Kane yupo huko na anaifahamu Arsenal vizuri tangu akiwa EPL amewafunga magoli ya kutosha tu!
Hapo Arsenal atakuwa nje ya Uefa kufikia April 16 na hata akifuzu anaenda kukutana na Man City au Real Madrid bado maisha ni magumu.
Atabaki kwenye ligi, huko nako safari sio rahisi ana safari ngumu.
Kwanza kabisa ana kibarua cha kwenda Etihad kisha baada ya wiki chache atarejea jijini Manchester safari hii akienda Matofali ya Kuchoma. Huko kote atadondosha alama.
Pulia atakuwa na kiporo dhidi ya Chelsea ya Poch.
Wakati hayo yakitokea, Big Ange na Spurs yake watakuwa wanawakaribisha katika North London Derby, Hapa wanaweza wakaambulia sare.
Siwaoni Arsenal wakitwaa ubingwa wa EPL, mechi za karibuni wanacheza na kupata matokeo ya ngekewa sana, ufinyu pia wa kikosi hasa katika idara ya ushambulizi itawagharimu kiaina.
Msisahau FA Cup walishatoka mapema tu!
Kwahyo, nahitimisha kuwa, Arsenal atashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi na kumaliza msimu bila taji lingine licha ya soka bora wanalopiga.
Arsenal ataanzia nyumbani Emirates kisha kwenda Allianz Arena ambapo huko atakufa nyingi si mnajua Harry Kane yupo huko na anaifahamu Arsenal vizuri tangu akiwa EPL amewafunga magoli ya kutosha tu!
Hapo Arsenal atakuwa nje ya Uefa kufikia April 16 na hata akifuzu anaenda kukutana na Man City au Real Madrid bado maisha ni magumu.
Atabaki kwenye ligi, huko nako safari sio rahisi ana safari ngumu.
Kwanza kabisa ana kibarua cha kwenda Etihad kisha baada ya wiki chache atarejea jijini Manchester safari hii akienda Matofali ya Kuchoma. Huko kote atadondosha alama.
Pulia atakuwa na kiporo dhidi ya Chelsea ya Poch.
Wakati hayo yakitokea, Big Ange na Spurs yake watakuwa wanawakaribisha katika North London Derby, Hapa wanaweza wakaambulia sare.
Siwaoni Arsenal wakitwaa ubingwa wa EPL, mechi za karibuni wanacheza na kupata matokeo ya ngekewa sana, ufinyu pia wa kikosi hasa katika idara ya ushambulizi itawagharimu kiaina.
Msisahau FA Cup walishatoka mapema tu!
Kwahyo, nahitimisha kuwa, Arsenal atashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi na kumaliza msimu bila taji lingine licha ya soka bora wanalopiga.