Makonda: Sekta ya Ardhi imejaa Dhulma, Unyang'anyi na Hati Feki

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
#UWAJIBIKAJI: Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda amesema katika ziara zake alizofanya katika Mikoa 23 nchini, amebaini matatizo na kero kubwa zinazowakabili Wananchi ikiwemo Watu kudhulumiwa Ardhi na tatizo la Hati Batili.

Amesema Ipo dhulma kubwa kwenye Sekta ya Ardhi, huko imekithiri. Kilio cha Watu kunyang'anywa maeneo yao na Watu wenye nguvu ya Fedha, kupewa Nyaraka au Hati Feki kimetawala. Tulitoa maelekezo kwa Wizara na tunatiwa Moyo na hatua zinazochukuliwa na Waziri wetu wa Ardhi, Jerry Silaa".

Ameongeza kuwa Chama kilimuelekeza Waziri Silaa kuendelea na kazi ya kutatua migogoro ya Ardhi pamoja na kuhakikisha Watu waliodhulumiwa Ardhi wanarejeshewa mali zao pamoja na kuchukua hatua kwa Waliohusika na dhulma hizo wakiwemo Watumisi wa Sekta ya Afya.

==========
 
Kwahio hizo habari amezifisha panapohusika au kama kawaida ya Mwanasiasa kutueleza matatizo tunayoyajua badala ya kutafuta suluhisho ?

By the way Sekta gani ni Safi.....
 
Jerry Slaa anajitahidi kujaribu kutatua haya matatizo ya ardhi lakini peke yake hawezi kwani watendaji wa hiyo wizara wamelelewa kudai rushwa.!!
Hata hivyo kitendo cha kuvunja nyumba huko wilaya ya Kinondoni ni kitendo cha haki ambacho kinataliwa kiendelezwe kuwa fundisho kwa wale wenye fedha kuacha dhuluma.
Ningemsihi waziri Slaa atakapofannya round ya pili wilaya ya Kinondoni aweke kliniki yake hapo JANGWANI beach ili aone jinsi wenye fedha walivyoharibu hilo eneo kwa kufunga barabara kiasi kwamba wakati wa mvua eneo lote la makazi hujaa maji kwa kukosa drainage! Kwa shida hiyo viwanja. Vingi havinaendelezwa!
 
Safi sana comrade Makonda,mimi mwenyewe nina kesi mahakama ya ardhi Geita,mwaka wa nne huu bila mwelekeo,hati kila kitu kipo,mwenyekiti wa baraza amekuwa mtu wa danadana sana .

Bila kuwa na haka kamshahara kangu ningeshakimbia kesi,nauri kula na kulala guest house kila mwezi.

Wapeni wakeup call wenyeviti wamalize kesi zilizokaa muda mrefu wananchi tupate haki zetu


Nakukubali sana comrade Makonda
 
Waziri sio Baraza la Ardhi, mbona hii nchi tinafanya mambo kiholela sana kwa gharama za walipa kodii?

Hii migogoro ya ardhi mingi haiishi sababu ya viongozi hawa hawawa serikali. Hawataki mamlaka sahihi zitatue haya mambo.

Pili wananchi wengi wanapeleka.migogoro ya ardhi polisi kana kwamba ni jinai na kwa bahati mbaya sana baadhi ya askari polisi wetu wasio na weledi wenye tamaa ya fedha na ujuaji wa kijinga wanakamata watu na kuanza kusuluhisha au kutoa amri za hovyo. Wadaiwa wanaenda Mahakamani wanashinda raia wanabaki kulalamika. Wakiona haifai wanaanza migogoro yenye mapigano wanakatana mapanga wanakufa wengine wanatoroka au kuishia magereza.

It's all stupidity!! over stupidity!! Na imekuwa kama vile wanasema we shall continue.
 
Mimi mwenyewe nipo na kesi ya Ardhi mwaka wa tatu sasa mahakama ya mwanzo Dodoma na haijawahi sikilizwa.
Eneo langu lipo Dodoma mjini ,Mtuma lina hekari 3,na Nyumba 2 zenye thamani ya Molino 82 na kisima 1 Thamani yake ni Molion 6.
Pia ni eneo lililo endelezwa kwa kupandwa mikorosho .
Lakini bado TBC na mthamini wa Serikali wanaungana na kuja na hoja ya kututaka tupokee milioni 100 kama fidia na wakati ujenzi wa nyumba kama hizo sasahivi ni una gharimu milion 103.2.
Kweli huu ni uungwana ????
 
Safi sana comrade Makonda,mimi mwenyewe nina kesi mahakama ya ardhi Geita,mwaka wa nne huu bila mwelekeo,hati kila kitu kipo,mwenyekiti wa baraza amekuwa mtu wa danadana sana .

Bila kuwa na haka kamshahara kangu ningeshakimbia kesi,nauri kula na kulala guest house kila mwezi.

Wapeni wakeup call wenyeviti wamalize kesi zilizokaa muda mrefu wananchi tupate haki zetu


Nakukubali sana comrade Makonda
Mimi aridhi nawaogopa kama ukoma, nilimzika Mzee wangu mwezi wa pili, mwezi wa kumi ghafla eti mzee wangu taarifa zake zinaonekana yuko aridhi anahamisha umiliki wake kwenda kwa mtu mwingine!! Tanzania shikamoo!!
 
Back
Top Bottom