1. Anajaribu kutuaminisha udini upo - kati ya Wakristo na Waislamu - na anajenga hoja kuwa makundi haya mawili yalipiga kura kidini. Ana data au anafikiria hivyo?
2. Anajenga hoja pia Waislamu waliamua kutumia udini baada ya kuona Wakristo wakitumia makanisa kuwanadi wagombea wao (Wakristo). Ana data pia kwa hili? Mfano, Kanisa gani, lini na yaliyosemwa kuhusu hao wagombea yalikuwa yapi? Vinginevyo M.M. Mwanakijiji naye anaanza kuwa mpiga debe wa udini.
3. Nijuavyo mimi udini ni wakati mtu anapopata haki zake za msingi kama ajira, elimu, afya na huduma nyingine za jamii hadi hapo tu anapoonesha ni wa dini fulani.
4. M.M. Mwanakijiji amesahau mchango wa vyombo vya habari katika kuwajengea wananchi wa kawaida dhana ya kile anachokiita 'udini wa kijinga...'
5. Binafsi naamini Tanzania hakuna udini ila kunajengeka imani ya uadui wa kidini (religious conflict) kati ya Uislamu na Ukristo... target likiwa hasa dhidi ya Kanisa Katoliki. Nasema hili maana mihadhara mingi ambayo nimepata bahati kuhudhuria maudhui yake ni hayo. Pia kuna mabishano ya kidini Kariakoo karibu kila siku kati ya vijana Wailsamu na Wakristo - Waislamu wakiwatuhumu Wakristo kuwa walimpigia kura Dr Slaa na Wakristo, kwamba wamekuwa wakipendelewa kiajira na kielimu na huduma nyingine za jamii. Mawazo ya M.M. Mwanakijiji yanashabihiana na hayo.
2. Anajenga hoja pia Waislamu waliamua kutumia udini baada ya kuona Wakristo wakitumia makanisa kuwanadi wagombea wao (Wakristo). Ana data pia kwa hili? Mfano, Kanisa gani, lini na yaliyosemwa kuhusu hao wagombea yalikuwa yapi? Vinginevyo M.M. Mwanakijiji naye anaanza kuwa mpiga debe wa udini.
3. Nijuavyo mimi udini ni wakati mtu anapopata haki zake za msingi kama ajira, elimu, afya na huduma nyingine za jamii hadi hapo tu anapoonesha ni wa dini fulani.
4. M.M. Mwanakijiji amesahau mchango wa vyombo vya habari katika kuwajengea wananchi wa kawaida dhana ya kile anachokiita 'udini wa kijinga...'
5. Binafsi naamini Tanzania hakuna udini ila kunajengeka imani ya uadui wa kidini (religious conflict) kati ya Uislamu na Ukristo... target likiwa hasa dhidi ya Kanisa Katoliki. Nasema hili maana mihadhara mingi ambayo nimepata bahati kuhudhuria maudhui yake ni hayo. Pia kuna mabishano ya kidini Kariakoo karibu kila siku kati ya vijana Wailsamu na Wakristo - Waislamu wakiwatuhumu Wakristo kuwa walimpigia kura Dr Slaa na Wakristo, kwamba wamekuwa wakipendelewa kiajira na kielimu na huduma nyingine za jamii. Mawazo ya M.M. Mwanakijiji yanashabihiana na hayo.