Majina ya wauza Madawa ya Kulevya: Kikwete anayo!

same reply as well

The following errors occurred when this message was submitted:
Mzee Es has exceeded their stored private messages quota and can not accept further messages until they clear some space.


futa basi hizo email zilizo jaa humo basi
 
huo ni uwongo na chuki mbaya sana ,sasa mnataka tuamini huyo amina aliyeleta hii hoja wanaajenda ya kuwapakazia watu wasiowapenda...maana nashangaa wanakamaiwa masikini tu...

anyway kama unapiga mahesabu ya haraka mama rwakatare ana wanafunzi 15,000 kwenye shule zake na ada inakaribia 1million /year sasa kweli hapo akitajirika mnashangaa nini? labda mngemsingizia ananufaika na misaada ya yatima kutoka marekani kidogo tungefikiria lakini hii kumpakazia huyu mama ni chuki, hata kama siabudu kwake namtetea kwa hili...tuache majungu

kAKOBE sina taarifa za miradi yake ila sadaka anayokusanya inamtosha...walishawahi kumpakazia analamba cheni za waumini ,sijui iliishia wapi...

mzee ES naomba upost hayo majina tuyaone isijekuwa ndio kama haya yanayopandikizwa kwa chuki...polisi wafanywe upelelezi makini na culprits wa unga washtakiwe
 
Nimesoama hiyo post nadhani ni cyberfabrications ya DHW ambayo wake wachangiaji wengi hawako serious kabisa.
 
Naona sasa watu wamechoka kusubili list ya Kikwete na Kamanda Tibaigana. Kila mtu sasa anatoka na Orodha yake.

Kwa mtazamo wangu hii mada ya madawa ya kulevya imeanzishwa na watu wa serikali, hili kupoteza lengo wananchi waache kuhoji utendaji wa serikali wa awamu ya nne na matatizo yake kama Masuala ya mikataba mibovu ya madini, Kikwete kuchindwa kutimiza ahadi zake za kupanua ajira,safari zisizoisha za JK; Masuala ya umeme na kampuni hewa kama Richmond.Watanzania sasa wako busy kusikilizia majina ya wauza unga, siku zinapita na wanasahau mambo ya maana na msingi, kama issue ya wauza UNGA ipo serious? mbona majina wanayaficha, au wanachangua nani wa kumkamata na nani wa kumuacha?. Tusisawau walianzisha issue ya kukamata majambazi-wakawakamata wafanyabiashara kibao na kuwataja majina lakini mpaka leo hatujui kesi zao zimeishia wapi?

Naomba tuwe makini na michezo hii ya kisiasa,hawa jamaa wa serikali wanawazuga tuu wananchi.
 
Kikwete na wasaidizi wake hawapo straight forward kama Ben Mkapa kuwaeleza wananchi ukweli kipi kinawezekana na kipi akiwezekanani(angalau nae alikua na udhaifu wake).Msanii Kikwete anachofanya ni kucheza na akili za wabongo kila siku anawaanzishia mada ambayo inagusa watu,hili kusahaulisha wananchi udhahifu wake, matokeo yake siku zinaenda itafika 2010 na atashinda kwa kishindo,lakini alichofanya kwenye uongozi wake sifuri. Tujitaidi kuwasaidia watanzania wenzetu home kufahamu huu usanii wa JK. Inasikitisha sana watu wapo busy na mada ya hewa ya madawa ya kulevya, huku jamaa wanaendelea kuifirisi nchi yetu.
 
PREACHER MAN

The president got the names and decided to advertise to the whole world (what did he expect us to do?) keep quite and wait for the miracle?

Well there isn't one at least for the moment, he should come clean and let them be convicted without all this spin.

If they're clean they will be released by the courts. There isn't any point for him to do the police work.

If this isn't the case, then there is no point to blame Richmond for the delay in their promises on generators; two weeks given to buyers of cashew-nuts; two weeks given to eradicate cholera in DSM etc. We should just wait for manna from heaven.

Well this time the manna will be there, the rain season has started and very soon the dams will lessen MGAWOOOOO and our friends (Richmond and others) will disappear in thin-air – BRAVO!!!!!! BRAVO!!!!! BRAVO!!!!!!! Job well done.
 
Mzee Dua,

You got it right, wazungu wamemjia juu Mzee JK, kuwa lazima awaseme or else, sasa watu wazima wametumwa London kutuliza wazungu, aibuu tupu na gharama za bure kwa walipa kodi!

Robo tatu ya majina kumi ni MTANDAO!
 
Mambo yaiva, vinara hawa hapa

2006-12-02 18:06:24
Na Mwandishi Wetu


Harakati zinazoendelea kufanywa chinichini na maafisa mbalimbali wa vyombo vya usalama nchini katika kuwachunguza, kuwabaini na hatimaye kuwanasa vinara wa biashara ’kichaa’ ya madawa ya kulevya imeanza kulipa.

Vinara wa biashara hiyo ’kichaa’ wameshaanza kudakwa na hadi sasa, kwa maelezo yaliyothibitishwa jana na kauli ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, Kamishna Robert Manumba, vinara 10 kati ya wale wanaotajwa kuwa wamebobea katika kucheza dili za ’unga’ wameshanaswa na wangali wakihojiwa mmoja baada ya mwingine.

Habari ambazo Alasiri imezinasa toka kwenye chanzo ’spesho’, zinasema kuwa mambo yameiva na kadiri siku zinavyokwenda, wahusika wakuu wa biashara hizo ambao wengi hujivika ngozi ya kondoo kwa kujifanya wema mbele ya jamii wataumbuka mmoja baada ya mwingine.

Chanzo chetu kinasema kati ya watu hao kumi ’hatari’ miongoni mwa wale ambao mpaka sasa polisi ilishawanasa na kuendelea kushughulika nao, ni watu wenye fedha za kutosha na baadhi ya sifa zao ni hizi:

Kwanza, mambo yao ni ya ’unyatu-unyatu’ wa paka. Kamwe biashara zao haziko wazi na tena, si watu wa kupenda ’kujichoresha’ kuwa mambo yao ni safi.

Pili, magari yao ni ya kisasa, ya bei mbaya sana na hupenda kuweka ’tinted’ katika vioo vya magari yao hayo ambayo kwa hakika, hayaendani na vipato vya biashara wanazoonekana kuwa nazo machoni mwa watu.

Tatu, miongoni mwa hao kumi, wengine hawaishiwi vijisafari vya mamtoni.

Hazipiti siku nyingi kabla hawajafanya safari ya nje ya nchi na kisha kurejea na baadhi ya bidhaa ambazo zinaelezwa kuwa ni za kuzugia tu, biashara halisi wanazofanya NI UNGA.

Nne, wapo katika hao 10 ’hatari’ ambao wao, wana urafiki mkubwa, lakini wa siri, na baadhi ya maafisa wa juu katika Jeshi la Polisi.

Tano, katika hao 10, wapo baadhi ambao licha ya kutopenda kujichanganya na watu wengine huku majumbani kwao wageni tofauti tofauti wakiwa hawaishi, ni mabuzi wazuri mno mbele ya vimwana wanaowabadili kama nguo.

Sita, wengine hujifanya ni watu wa Mungu.
Saba, wana mafanikio ya haraka katika biashara zisizotambulika.

Nane, wapo wenye wapambe kibao katika kuhakikisha kuwa biashara zao zinaenda vyema huku wao wakiwa kando kabisa, wasijihusishe moja kwa moja na biashara za kuonekana.

Tisa, wana mitandao yao iliyosambaa sehemu nyingi duniani, hasa katika nchi za Pakistan, Brazil, Afrika Kusini na zile za falme za kiarabu.

Mbali na baadhi ya sifa hizo, kubwa inayoelezewa kuwa inawagusa wote ni ile ya kutomuamini mtu. Wanapenda kutanguliza ’bastola’ katika ufanyaji wao biashara huku pia, wengine wakisapotiwa biashara yao hiyo kichaa na nguvu za giza washirikina mno!

’’Tuipe muda tume... ifanye kazi yake ya upelelezi kwa sababu waliomo ni wazoefu katika kazi hiyo na makosa ya dawa za kulevya ni ya kuvuka mipaka, na tunashirikiana na vyombo vya ulinzi wa Kimataifa (Interpol),’’ amesema Kamishna Manumba wakati akizungumzia harakati zinazoendelea katika kukomesha biashara hiyo.

* SOURCE: Alasiri

Magazeti yetu haya....natamani kuwatukana.
 
Five months later JK is NOT capable of releasing the names ? Whom should we trust ? I gues the first name is Jakaya Kikwete.
 
Shukrani mzee wangu, na ubarikiwe nimeitafuta sana, maana rais alisema kama tuna ushahidi tuseme na tuwataje, wakati ni huuu sasa!

na pia nimegundua kuwa 75% ya issues mpya hapa huwa zipo lakini kwa haraka hazikusemwa vizuri kwa hiyo ninataka kuanza hako katabia kakufukua tuliyoyaachia nusu nusu!
 
kwa hiyo kama kweli jk anayo majina ya hao drug dealers, na yeye anafahamu hilo wazi, na KAMA ni kweli walimsaidia katika kampeni kwa njia moja ama nyingine katika uchaguzi uliopita kwa kutumia hizo pesa walizopata kutokana na hizo drugs, basi naye rais ni drug dealer and needs to face charges in the second degree with dealing of illegal drugs indirectly ! na ndio maana hawezi if not "kurelease majina" then "kuwafikisha mbele ya haki hawa jamaa zake". consequences will follow. jamani sasa msione jk hataki kutoa majina anajua nini kitakachofuata baadae either yeye a-face charges (kitu ambacho sio rahisi kwa nchi yetu tz kutokea) au/na kutofadhiliwa katika kampeni zijazo !!
 
Jamani kwanza kabisa ningependa kui-dedicate hii thread kwa marehemu Amina Chifupa ( M/Mungu amrehemu ). Kutokana na quotes ambazo marehemu mbunge Chifupa alizowahi kutoa zikiwemo na "Nafahamu ninapambana na watu hatari, lakini kesho (leo) namuomba Mwenyezi Mungu aniamshe salama, ili niweze kuliweka bayana suala hili mbele ya waandishi wa habari MAELEZO. Nimekusudia kusema ukweli wote kuhusu suala langu," alisema Amina.

&

"Daima nasimamia ukweli na sababu ya dhamira yangu. Nipo tayari kufungwa au kuchukuliwa hatua yoyote iwapo nitaonekana sina nidhamu... hata ikibidi kupoteza ubunge na uanachama wangu wa CCM. Mimi si mwanasiasa wa 'ndiyo mzee'," alisema Amina baada ya kuulizwa iwapo ukweli anaotaka kusema hautamgharimu."

Inaashiria kabisa kwamba huyu mtu alikuwa anaandamwa na kundi la watu fulani, na kuna kipindi ( angalau siwezi kuthibitisha kwa sasa ) ilidaiwa kwamba, marehemu alipokuwa ndani ya bunge, alitoa hoja kuhusiana na madawa ya kulevya, alitumiwa ujumbe wa text kwenye simu yake na kuambiwa kwamba (sio exact words ) bora akae chini kabla vijana hawajamshughulikia. kwa kweli haya maneno nina hakika yameweza kutimizwa na hao watu, na isitoshe pia baba mzazi wa marehemu nae aliambiwa amkanye mwanae au atampoteza, ( damn ), yaani familia inaonewa vivi hivi, siwezi amini kwa kweli.

Sasa basi, najua kuna watu waliokuwa wanasema afya yake ina migogoro ( sijui kuhusu hilo ) lakini hata kama ingekuwa hivyo, yule ni mheshimiwa na isitoshe this is 2007, yaani mnataka kuniambia hakuna madawa ya kurefusha maisha ? sitaki inawezekana akawa amefariki kwa ugonjwa huo ( ambao sio mgeni kwetu kwani yeye sio wa kwanza na yeye sio wa mwisho kufa nao i.e kama kweli alikuwa nao ) Lakini still, sitoweza kuamini hicho tu pekee bali umafia nao uli-play a role !

Hivyo being said, wanaJF naomba tupeane mawazo kadha wa kadha kuhusu shughuli za madawa ya kulevya, nani na nani wanahusika, wanaendesha vipi shughuli zao, wadhamini, wanapata wapi bidhaa ( drugs ), wanaingizaje nchini, nini kifanyike, n.k.

itakuwa vizuri tumwage "potential mchele" aliotaka kuumwaga marehemu dada yetu hapa, ikiwa pamoja na kuwaanika wahusika wote hapa kwenye mwanga. asanteni, Mungu amrehemu Amina Chifupa. Lets not worry cause there's nothing wrong when God, Allah, Jah does something to his creatures. na ndio maana wote tunamuamini. leteni data ndugu.
 
UNGA.....UNGA....UNGA......madawa ya kulevya!


Akizungumzia msiba huo nje ya ukumi wa Bunge, Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alisema kifo hicho kimeacha pengo na kinasikitisha.

Lowassa alipoulizwa kama serikali itaendelea kuchunguza mambo aliyowahi kusema marehemu kuhusu vigogo wauza dawa za kulevya, alikwepa swali na kujibu kwa kifupi tu, dawa za kulevya ni moja ya jambo alililozungumza, lakini alikuwa akizungumza mengi.

Sisi Wakristo tunaamini, Bwana alitoa na bwana alitwaa, alijibu Lowassa na kuondoka.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Mtera, John Malecela, aliliambia gazeti hili kwamba, hakuna mtu atakayetokea bungeni kuwa kama Chifupa.

Malecela ambaye alionekana kujawa na huzuni, alisema atamkumbuka marehemu kwa mambo mawili, kwanza ujasiri wake wa kuzungumzia biashara haramu ya dawa za kulevya bila woga na jinsi alivyotetea maslahi ya vijana.
Alisema Chifupa alikuwa ni nyota miongoni mwa wabunge wanawake chipukizi, lakini imezimika ghafla pia kama ua lililoyeyushwa na moto ghafla.

Mimi siamini kama tutapata Amina mwingine katika Bunge, hii ilikuwa ni nyota na taa ambayo imezimika ghafla, Amina alikuwa jasiri hasa alipouzungumzia dawa za kulevya, hakuogopa, alisema.

Mbunge wa Viti maalumu (Chadema), Muhonga Said, alisema marehemu Chifupa alikuwa muwazi, na kwamba alipoona kitu hakifurahii hakusita kusema. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Dk Hussein Mwinyi, alisema Chifupa alikuwa ni mbunge ambaye ni rafiki wa kila mtu na aliyetetea vijana bila kujali itikadi zao.

Magareth Sitta, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, alisema marehemu Chifupa, alikuwa ni mtetezi wa vijana wakiwemo wanafunzi na watoto yatima. Chifupa ambaye alizaliwa mwaka 1981 na kuingia bungeni mwaka juzi, pamoja na mambo mengine, katika kikao cha mwisho cha Bunge cha Aprili, alitoa maelezo mazito akisema yuko tayari kushirikiana na Jeshi la Polisi kutaja wauza dawa za kulevya.

...Watanzania waomboleza


WATANZANIA wengi wameelezea masikitiko yao kuhusiana na kifo cha Mbunge wa Viti maalum (UVCCM), Amina Chifupa Mpakanjia kilichotokea usiku wa kuamkia jana. Wamesema kifo chake ni pigo kubwa kwa wanatanzania wote kutokana na mchango wake mkubwa wa kupigania haki na kupambana na maovu.

Kutoka Moshi, Ally Sonda anaripoti kuwa Moshi na vitongoji vyake jana ulikuwa ni uwanja wa simanzi na majonzi karibu kila kona kufuatia msiba wa mbunge huyo kilichotokea usiku wa kuamkia jana.

Pamoja na wakazi wengi wa mji huo kuonekana wenye masikitiko makubwa kufuatia msiba huo, baadhi yao wamemwomba, Rais Jakaya Kikwete kutumia mamlaka aliyopewa na Watanzania kuamuru watuhumiwa wa dawa za kulevya wafikishwe mahakamani.

Kauli zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo maafisa wa Jeshi la Polisi wakidai majina ya wauza dawa za kulevya yapo hazitakuwa na maana endapo majina ya wahusika yataendelea kukumbatiwa, alisema mmoja wa wakazi wa mjini Moshi.

Baadhi ya wanawake wanaofanya kazi kwenye saloon za kike licha ya kuupokea msiba wa mbunge huyo kwa huzuni kubwa, wamedai kuwa Amina amekufa akiwa shujaa na mpiganaji wa kutetea afya na uchumi wa Watanzania maskini.

Amina Chifupa hakuwa mnafki katika vita dhidi ya dawa za kulevya, aliwahi kuwataka maafisa wa Jeshi la Polisi wamfuate awape majina ya wauza unga kwa kuwa anawafahamu, yeye mtoto wa miaka 25 ameweza, huyu amekufa shujaa, alisema Ester Nkwezu.

Baadhi ya maafisa wa serikali, wasomi na wananchi wengine waliohojiwa walisema hakuna njia ya mkato ya kumuenzi mbunge huyo isipokuwa kuwataja hadharani watu wanaofanya biashara ya dawa za kulevya na kisha kuwafikisha mahakamani.

Naye Mwandishi Wetu, anaripoti kuwa Chama cha Wananchi (CUF) kimetoa salaam za rambi rambi kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete na Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samwel Sitta kufuatia kifo cha Amina Chifupa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum-Vijana kupitia cha hicho.
Amina Chifupa alifariki dunia juzi usiku katika Hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na maradhi mchanganyiko ikiwamo malaria, shinikizo la damu pamoja na kisukari.

Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad, alisema mbunge huyo alikuwa jasiri na mtetezi wa jamii katika kupigania haki zao na kwamba CUF imesikitishwa na kushtushwa na kifo hicho. ?Marehemu Amina Chifupa alikuwa ni mmoja wa wabunge vijana katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alikuwa mtetezi wa jamii. Hivyo basi Watanzania tumempoteza kiongozi shupavu,? ilieleza sehemu ya taarifa ya Maalim Seif. Mbali ya kutoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Maalim Seif pia alitoa pole kwa wabunge wote, ndugu na jamaa wa marehemu akisema chama chake kinaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na maombolezo.

Maalimu Seif baadaye akizungumza na waandishi wa habari alimlinganisha Chifupa na mshumaa uliozimika ghafla, akisema alisimamia mambo ambayo yalikuwa yakigusa jamii kama vile vita dhidi ya dawa za kulevya.

Michael Uledi,anaripoti kutoka Dodoma kuwa Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi,Luteni Mstaafu,Yusuf Makamba amesema kuwa Marehemu Amina Chifupa alikuwa jino la dhahabu na kwamba kifo chake ni pengo kubwa sana kwa chama chakle.

Makamba aliimbia Mwananchi Ofisini kwake mjini Dodoma kuwa pamoja na kujua kuwa pengo lililoachwa na Amina Chifupa litazibwa lakini pengo hilo ni sawa na pengo la jino la dhahabu ambalo haliwezi kuzibwa na jino la fedha.
Kabla ya kifo chake alisema alipenda kugombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa,nasikitika ametutoka wakati tukiwa katika mchakato.Najua pengo lake litazibwa lakini pengo lake ni la jino la dhahabu ambalo haliwezi kuzibwa na jino la fedha lakini litazibwa?Alisema Katibu Mkuu kwa masikitiko makubwa.

Makamba alisema kuwa ili kuweza kuendeleza mapambano ana imani kuwa pengo lake litazibwa na jino la dhahabu.Alisema kuwa alimfahamu Amina Chifupa kama kiongozi kijana aliyekuwa na mapenzi na chama chake. Moja ya sifa ya amina ambayo nitaendelea kumkumbuka ni kuwa alikuwa anakipenda sana chama cha mapinduzi, alikuwa mchangiaji mzuri wa fedha mali na vifaa vyake kwa ajili ya chama cha mapinduzi. Katika uhai wake amejitolea kukisaidia chama na kila mara alitoa bila kusita, alisema Katibu Mkuu huyo.

Alisema Mbunge huyo kijana alikuwa anakerwa sana na matatizo yanayowakabili wanachama na kwamba alikuwa kimbilio la watu walipokuwa na matatizo na kwamba Chama cha mapionduzi kimepoteza mbunge na mwanachama mwaminifu na kitaendelea kumuenzi.
 
Nashangaa kwa nini Lowassa alishindwa kujibu hilo la madawa ya kulevy directly wakati ni jambo linaloeleweka. Je ana interest zozote kwenye biashara hiyo au naye anawaogopa vibosile wa unga?
 
2006-11-15 08:47:13
By Guardian Reporter



The Police Force is prepared to provide security to CCM Special Seats MP Amina Chifupa, who has told the on-going Parliament session that she has told the police time and again that she is prepared to reveal names of drug barons.

The MP’s public utterance has provoked fears among sections of the population that she deserves police protection; otherwise she might be exposed to danger.

Apart from being prepared to show the places where drug peddling is rampant, Chifupa also called for the exposure of all drug dealers, ”be it a Speaker of the National Assembly, an MP or a minister, or even my husband”

Impeccable sources had informed The Guardian that the Police Force is taking the MP’s offer seriously and is prepared to offer her some protection.

The chairman of the Tanzania Labour Party, Augustino Mrema, has commended Chifupa’s move, and also called for the MP to be protected.

”She needs all our support in her drive to ensure that all those who are involved are dealt with,” Mrema said yesterday, adding that Chifupa had manifested that she was a courageous individual.

Amina Chifupa made the remarks when she was contributing to the Money Laundering Bill, which was tabled by Deputy Minister of Finance Abdisalaam Issa Khatib on Monday.

She said the government was keen to enforce law and order when it came to demolishing vendors’ stalls but it dragged its feet when called to arrest drug kingpins.

Another MP, Hamza Mwenegoha, advised MPs and politicians to put their own houses in order.

”Before going outside, let us begin with our own homes.

Some members of this House are undertaking fishy business but they remain untouched.

Other politicians have got such huge money-loads that they are unable to cart them anywhere,” Mwenegoha said.

Another MP, Anne Komu (Chadema), urged the government to take action against well-to-do individuals who were using resources well beyond their means to finance political campaigns.
 
....its a tall order my friend.

....hebu tupe mwanga kwanza,kwa weye kutoa ka-intro ka hii deal.

....baada ya hapo flow inaweza kupatikana!
 
Kada; hii ni dangerous path kwelikweli; kwa mfano, ni habari za kuaminika kuwa wengi wa vijana wasafirishaji huwa wanapitia VIP lounge watokapo huko kuzimuni na hayo madawa; hii yatosha kukuonyesha namna mtandao wake ulivyo. Tizama yule jamaa jirani yake marehemu Amina alokufa majuzi akiwa na madawa tumboni, na wenzie wakamfanyia upasuaji wa kikatili; hao sio watu wa kawaida; kutoa mtu roho kwao si kazi, na mtandao wao ni bab kubwa!
 
Wote humu mnajua ni mmoja kati ya hao wauza unga ambao majina yao yako kwa rais. Sasa mindhali alishaachana na Amina na huyo Amina sasa ni marehemu, mnaonaje tukasema yale ambayo wengi wenu humu mnaogopa kuyasema kwa hofu zenu za kinafiki ? (including mimi mpaka nilipochokan na unafiki wa nyumba hii)
 
lakini hata hivyo, kwani hatuwezi kuja na mawazo ya kuwazidi kete, i cant agree kwamba wao ni bab kubwa zaidi ikiwa hata hatujajaribu chochote. Step moja nadhani ingekuwa vizuri kama tungekuwa na majina ya hao viongozi inasemekana ikiwa na haya majina nayo yamo

- MEDI MPKAKANJIA
- MADIWANI WATANO ( 5 )TOKA MKOA WA DAR
- LIST GOES ON...........
- WAHINDI ( AKINA RAJ PATEL )
 
Back
Top Bottom