Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 56,528
- 93,103
Huwa namkubali Hussein Mwinyi tu huyu ndiyo naamini anasimama kwa miguu yake na Elimu yake haina walakini. hawa wengine kama kina William Malecela walipaswa kuwa Mameneja wa Ngwasuma.
Wanachama
kadhaa wa CCM wamesikitishwa na majina ya wanachama waliopitishwa
kuwania ubunge wa Afrika Mashariki.Wamesema kwamba kitendo cha chama
chao kupitisha idadi kubwa ya majina ya watoto wa vigogo ni ishara
tosha kwamba chama chao kimegeuka kuwa cha kisultani.Pia wamesema
kitendo hiki kitazidi kuwaweka mbali na wananchi.Baadhi ya watoto wa
vigogo waliopitishwa ni mtoto wa Nyerere,mtoto wa Mwinyi,mtoto wa
Billali na mtoto wa Malecela.SOURCE:TANZANIA DAIMA.
huo ni upotoshaji wa makusudi,walitangaza nafasi hizo na watu wamejitokeza kuchukua fomu na kuomba,kinachofuata ni mchujo wa wale wenye SIFA stahili kupitishwa bila kujali ni mtoto wa kigogo gani....hao ni wateule tu bado hawajachaguliwa,pia hata wakichaguliwa bado ni haki yao kama hakuna wenye SIFA zaidi yao.Mnataka tuwakatae ati kwa sababu ni watoto wa vigogo? basi hata ajira wasipate kwenye taasisi za serikali wala mashirika yoyote? HAPANA huo ni ufinyu wa FIKRA....Acheni TANZANIA DAIMA wafanye SIASA kwa vile ni kazi yao,Lakini Great THINKERS let us go beyond the SKY.....
full nepotism
Wanachama kadhaa wa CCM wamesikitishwa na majina ya wanachama waliopitishwa kuwania ubunge wa Afrika Mashariki.Wamesema kwamba kitendo cha chama chao kupitisha idadi kubwa ya majina ya watoto wa vigogo ni ishara tosha kwamba chama chao kimegeuka kuwa cha kisultani.Pia wamesema kitendo hiki kitazidi kuwaweka mbali na wananchi.Baadhi ya watoto wa vigogo waliopitishwa ni mtoto wa Nyerere,mtoto wa Mwinyi,mtoto wa Billali na mtoto wa Malecela.SOURCE:TANZANIA DAIMA.
Hilo ni kweli sasa kama wameona taizo kinachofuata ni kutafuta dawa!!! hatuwez kuendelea kwa staili hizo!!! wakati ni huu!!!Wanachama kadhaa wa CCM wamesikitishwa na majina ya wanachama waliopitishwa kuwania ubunge wa Afrika Mashariki.Wamesema kwamba kitendo cha chama chao kupitisha idadi kubwa ya majina ya watoto wa vigogo ni ishara tosha kwamba chama chao kimegeuka kuwa cha kisultani.Pia wamesema kitendo hiki kitazidi kuwaweka mbali na wananchi.Baadhi ya watoto wa vigogo waliopitishwa ni mtoto wa Nyerere,mtoto wa Mwinyi,mtoto wa Billali na mtoto wa Malecela.SOURCE:TANZANIA DAIMA.
Dawa ni wewe kuwa na ujasiri wa kuchukua fomu na si kulalamikia kwapani!Hilo ni kweli sasa kama wameona taizo kinachofuata ni kutafuta dawa!!! hatuwez kuendelea kwa staili hizo!!! wakati ni huu!!!
Mzee Makamba alipata kusema ukimkuta panya anakula Biblia Msikitini utashangaa, lakin kama ukimkuta anaila kanisani wala huwezi kushangaa (the same apply kwa Quran na Kanisa). Nadhani hawa vijana watakuwa wanafuata nyayo za wazazi wao, hata hivyo kwangu mimi si tatizo kama watakuwa wanasifa stahiki na wanafuata taratibu zote walizojiwekea bila kubebwa kwani nao wana haki hizo za kuchagua viongozi na kuchaguliwa
Hata hivyo ni vyema ikafahamika kwamba huko kwenye chaguzi zao za ndani, hawapigiwi kura na hao wazazi wao pekee bali wanachama wenzao, hivyo hakuna haja ya kumlaumu mtu mwingine bali wajilaumu wenyewe kwa kuiacha misingi yao ya awali kama watakuwa wamekiuka taratibu
Kumbe na wewe kibaraka umeona hilo eeh?
Cha msingi ni kuwachuja wote na kubakiza raia wa kawaida!
Hivi hakunaga kazi zingine za profession zao?
Kuendelea
kuipenda CCM
yakubidi uwe na
akili ya MAITI!