Vaticano hivi kwanini unakuwa na mawazo potofu kiasi hicho kuwa mbunge kwa miaka 15 sio kujinufaisha mwenyewe alitumwa na wananchi wa karatu kuwatumikia hivyo hizo pesa ama mshahara wake huwasaidia wale wasiojiweza na kuleta maendeleo jimboni kwake. Nikuulize swali moja tu Mwl. Nyerere (RIP) alikaa IKULU kwa 25 hakuna kiongozi alie kaa muda mrefu hivyo IKULU hapa Tanzania na alikuja kujengewa nyumba na JWTZ baada ya kungatuka.
Je Mwl hakuweza kujenga hekalu la kuishi kwa muda wote huo hadi aje kujengewa nyumba na jeshi. Alikuwa na uwezo wa kujenga hata nyumba 100 lakini alikuwa na mapenzi ya dhati kwa wananchi aliokuwa anawatumikia hivyo hakuona busara kujilimbikizia mali alikuwa ni mwananchi wakawaida tu. Hivyo basi ni sawa na Dr. Slaa kuishi maisha ya wakaida kama wananchi wengine.
Pili usiingize mambo ya UDINI swala la Mzee wake Dr. Slaa kuishi kwenye nyumba ya matope ni maisha ya kawaida kwa wananchi wa Tanznania. Kila Mtanzania ametokea kwenye nyumba za Matope na Nyasi hii ndi asili yetu.
Huwa sipendi kujibu hoja za kijinga lakini kwa hii acha nivunje mwiko. Kila anayelipwa milioni tano anapaswa kumjengea baba yake nyumba? na wale wasiopata hizo jee? Hoja ya msingi ni ile ya kuhakikisha vifaa vya ujenzi vinaweza kupatikana kwa bei nafuu ili kila mtanzania aweze kujijengea makazi bora kama ilani ya Chadema isemavyo.
TBC wametumia hila ambayo badala ya kumbomoa Slaa imemjenga, kwani anaposema atahakikisha waTZ wanaweza kupata makazi bora hata yeye katika familia yake yanamgusa,sio wale wanaosema zahanati zitakuwa na dawa za kutosha familia zao zinatibiwa nje hata kwa mafua tuu. Slaa ameonyesha kuwa yeye ni mpigania haki za watu wote sii familia tuu na yeye si FISADI.
Kwani katika hayo mahojiano, Baba wa Dr. Slaa amelalamika kuwa mtoto wake hajamjengea nyumba? Amelalamika kuwa nyumba anayokaa si nzuri?
Anahojiwa Baba yake. Anaishi kwenye nyumba ya tope licha ya mwanawe kuwa bunge for 25 years,
Anaepnda sana kujisomea.
Anaongea kiswahili cha shida but ina mashaka na slaa kugombea hasa kutukanana
Dedicated to you http://www.youtube.com/watch?v=vkEHWfj-Dlc:becky:Kwa hiyo tukachague viongozi wenye maradhi na ujinga kwenye familia zao kwa sababu "hata yeye katika familia yake yanamgusa". Bora hata usingevunja huo mwiko ulioudai.
eee! Mungu wa kweli wewe uwawekao wafalme wa dunia nakuomba usikie kilio cha wa tz waliao usiku na mchana, kama ulivyo wapa mfalme daudi watumishi wako baada yakumkataa, sauli tunakuomba umsaidie mwanao dr. Slaa mtumishi wako anaetoa wakati na nafsi yake hata kufa kwa taifa lake tanzania kuwaokoa wanyonge mil.45 ambao wamekuwa wakilia baada ya nchi kutekwa na kikundi kidogo sn ambacho kimeweka pembeni maadili mema yaliyowekwa na mtumishi wako mwalimu na dr. Nyerere, kumbuka hakuna wakusikiliza kio chetu ila wewe mungu wa kweli, tunajua wazi wanauwezo wakila kitu kama vile majeshi yasiyoonekana kwa macho lkn wewe unanguvu zaidi ya hayo, hatutaogopa bali tutakutegemea siku zote, mjalie afya na maono kwa ajli ya watu wako.
Tusome 2nyakati 20.1-26 hatuna sababu yakupigana tunae mungu anaesikiliza kilio cha watu wake.
mungu ibariki tz, mungu mbariki mtumishi wako dr. Slaa
Ni mtanzania kama watanzania wengine..Hayo ndio maisha bora kwa kila mtanzania. Kuishi kwake kwenye nyumba ya udongo nani wa kulaumiwa kama si serikali. Angeishi kwenye nyumba mfano wa hekalu ccm wasingekosa cha kusema 'Dr. Slaa alikuwa mwizi.' Dr. Slaa kaza buti sisi tunakuombea kila la heri waache wenye kuchokonoa mambo hata yasiyo wahusu. TBC mkahoji wazazi wa JK,Lipumba na wengineo mbona Dr. Slaa peke yake kama si uhuni ni nini?
Hata watoto wa Nyerere wakati wanasoma walikuwa wanadandia lifti za watoto wa mawaziri wakati baba yao ni rais. Tena wengine wamesomeshwa na misheni wakati baba yao ni rais. Nyerere nyumba ya maana kajengewa na jeshi wakati ameshang'atuka kwenye urais. Kwa hili CCM wanafikiria kuwa ni kashfa kumbe ndo wamempigia debe Slaa bila wao kujua. Slaa tunakuombea mwaka huu ni mwisho wa kutawaliwa na majingili wa uchumi wetu.