selemangrace346
JF-Expert Member
- Sep 26, 2018
- 450
- 613
Wasalaamu wakuu!
Imenilazimu kuja na uzi huu baada ya kuona Hali inazidi kuwa Tete
Mwaka 2017 nilibahatika kukutana na Mrembo fulani shombeshombe Mkoani Pwani(home), Ambaye nlimpambania kwa nguvu zote ili mwisho wa siku aje kuwa mke wangu. Inshallah Nlifanikiwa kumnasa Binti huyo na Tukaanza uhusiano. Baada ya muda nlimtambulisha kwa familia yangu na kiukweli walimkubali sana na mama alinisisitiza nimuoe na nlifanya hivo kiukweli maana sikuona cha kusubiri
Mwaka 2018 nilifanikiwa kupata Ajira rasmi Serikalini kama Engineer Mkoani Tanga, nilikwenda kuripoti kazini na kuweka mambo sawa ya kimakazi, Nlipokuwa kule nlikutana na Dada mmoja ambaye ni Engineer pia alitokea kuwa mwenyeji wangu na kuonekana kunijali sana yaani muda mwingi alitaka tuwe pamoja, unfortunatelly nikajikuta navunja amri ya saba na haikuchukua muda yule dada akapata ujauzito
Mimba ikafikia miezi 8 hivyo ikabidi arudi nyumbani kwao kwenda kujifungua huko Arusha , kipindi yupo kule nimekaa kama mwezi mmoja hivi ndipo tena nikawa nimekutana na Binti mwingine ambaye ni kabila langu naye alikuwa ni mfanyakazi( Askari), akatokea kunipenda sana na kunijali nikajikuta nimeanzisha uhusiano na yeye tena yaani ilikuwa sijui shetani gani yule alinipitia kipindi hicho.
As time goes yule dada nae akapata ujauzito na movie ikaanzia hapo maana kiukweli hawa wote sikuwa nimewakubali na wao ndiyo kama walinitongoza, akili yangu yote ilikuwa kwa mke wangu, But wote sikuwa nimewaweka wazi kuwa nina mke nyumbani
Haikuchukua muda mke wangu naye akataka aje tuishi pamoja huku nilipo, nikamkatalia kwanza maana nilijua huku ni pa moto sana asubiri niweke mambo kwanza kama itawezekana na nilikuwa mkali sana kwake. Kiukwel akili yake sijui ilimtuma vipi , Baada ya siku kadhaa ananiambia yupo stand niende nikampokee ilibidi nifanye hivyo, kiukwel nilitamani ardhi ipasuke.
Wakuu ilikuwa bonge ya movie, maana yule Askari aliposikia kuwa nimepata mgeni( mke ) alikuja usiku huo huo na kufanya fujo pale nyumbani, Mke wangu alipata kujua kuhusu hiyo situation kwa majirani na ikabidi nimweke wazi kuwa nimeteleza kuna watu wawili wana ujauzito wangu.
Mazungumzo yalikuwa si mazuri maana alilia sana aliposikia hizo taarifa kiukwel,but finally mke wangu alinisamehe na akakubali kuendelea kuishi hii ulikuwa ni zaidi ya upendo maana nilitegemea asingekubali kuendelea kuishi na mimi,
As time goes wakuu maisha kidogo yamekuwa magumu sana kelele haziishi kwa hawa wanawake hadi inafikia stage natamani kuachana na mke wangu japo ninampenda sana ili tu nchukue Mwanamke mmoja wapo kati ya hao wenye watoto na ni wafanyakazi kidogo nahisi nitapata ahueni ya maisha maana hata jamii inanchukulia kuwa ni mtu mbaya sana yaani sina amani japo kiukweli nampenda sana mke wangu.
Naomba ushauri wakuu je niendelee tu na mke wangu ambaye amekubali kuishi na mm licha ya mazingira hayo magumu au niachane nae nichukue mmoja kati ya hao wenye watoto?
Imenilazimu kuja na uzi huu baada ya kuona Hali inazidi kuwa Tete
Mwaka 2017 nilibahatika kukutana na Mrembo fulani shombeshombe Mkoani Pwani(home), Ambaye nlimpambania kwa nguvu zote ili mwisho wa siku aje kuwa mke wangu. Inshallah Nlifanikiwa kumnasa Binti huyo na Tukaanza uhusiano. Baada ya muda nlimtambulisha kwa familia yangu na kiukweli walimkubali sana na mama alinisisitiza nimuoe na nlifanya hivo kiukweli maana sikuona cha kusubiri
Mwaka 2018 nilifanikiwa kupata Ajira rasmi Serikalini kama Engineer Mkoani Tanga, nilikwenda kuripoti kazini na kuweka mambo sawa ya kimakazi, Nlipokuwa kule nlikutana na Dada mmoja ambaye ni Engineer pia alitokea kuwa mwenyeji wangu na kuonekana kunijali sana yaani muda mwingi alitaka tuwe pamoja, unfortunatelly nikajikuta navunja amri ya saba na haikuchukua muda yule dada akapata ujauzito
Mimba ikafikia miezi 8 hivyo ikabidi arudi nyumbani kwao kwenda kujifungua huko Arusha , kipindi yupo kule nimekaa kama mwezi mmoja hivi ndipo tena nikawa nimekutana na Binti mwingine ambaye ni kabila langu naye alikuwa ni mfanyakazi( Askari), akatokea kunipenda sana na kunijali nikajikuta nimeanzisha uhusiano na yeye tena yaani ilikuwa sijui shetani gani yule alinipitia kipindi hicho.
As time goes yule dada nae akapata ujauzito na movie ikaanzia hapo maana kiukweli hawa wote sikuwa nimewakubali na wao ndiyo kama walinitongoza, akili yangu yote ilikuwa kwa mke wangu, But wote sikuwa nimewaweka wazi kuwa nina mke nyumbani
Haikuchukua muda mke wangu naye akataka aje tuishi pamoja huku nilipo, nikamkatalia kwanza maana nilijua huku ni pa moto sana asubiri niweke mambo kwanza kama itawezekana na nilikuwa mkali sana kwake. Kiukwel akili yake sijui ilimtuma vipi , Baada ya siku kadhaa ananiambia yupo stand niende nikampokee ilibidi nifanye hivyo, kiukwel nilitamani ardhi ipasuke.
Wakuu ilikuwa bonge ya movie, maana yule Askari aliposikia kuwa nimepata mgeni( mke ) alikuja usiku huo huo na kufanya fujo pale nyumbani, Mke wangu alipata kujua kuhusu hiyo situation kwa majirani na ikabidi nimweke wazi kuwa nimeteleza kuna watu wawili wana ujauzito wangu.
Mazungumzo yalikuwa si mazuri maana alilia sana aliposikia hizo taarifa kiukwel,but finally mke wangu alinisamehe na akakubali kuendelea kuishi hii ulikuwa ni zaidi ya upendo maana nilitegemea asingekubali kuendelea kuishi na mimi,
As time goes wakuu maisha kidogo yamekuwa magumu sana kelele haziishi kwa hawa wanawake hadi inafikia stage natamani kuachana na mke wangu japo ninampenda sana ili tu nchukue Mwanamke mmoja wapo kati ya hao wenye watoto na ni wafanyakazi kidogo nahisi nitapata ahueni ya maisha maana hata jamii inanchukulia kuwa ni mtu mbaya sana yaani sina amani japo kiukweli nampenda sana mke wangu.
Naomba ushauri wakuu je niendelee tu na mke wangu ambaye amekubali kuishi na mm licha ya mazingira hayo magumu au niachane nae nichukue mmoja kati ya hao wenye watoto?