Mahojiano na aliyenusurika katika shambulio lililoua askari wanne

Siku zote tunajifunza kutokana na makosa.
Ni wakati wa jeshi la polisi kufanya kazi yake kwa weledi bila kuonekana kutumika na upande fulani dhidi ya upande mwingine.
Mazoezi ya hadharani ya siku mbili zilizopita yameonesha dhahiri jeshi la polisi lipo kwa ajili ya kupambana na upinzani. Hali hii inaleta uhasama kati ya polisi na upinzani ambao sio wachache kwa mujibu wa uchaguzi uliopita.

Kwa sasa ni vigumu mno kwa raia mwema kuweza kusaidia jeshi la polisi kwa sababu ni kama wameshatengeneza uhasama wa kudumu kutokana na kauli tata za viongozi zinazowasisitiza wananchi kuwaogopa polisi.
RIP polisi wetu. Mmetutangulia hata kabla ya 1 sept.

Mwigulu anasema hiki sio kibiriti cha njiti ni gesi, hizi kauli hazifai kabisa sote ni dhaifu, viongozi wanatengeneza mazingira ya chuki kama vile wako usingizini. wanafikiri hao askari ni robot?
 
Hiyo gari ya polis si nzuri kwa kaz hiyo ya kupeleka polis lindo..wabadilishe..
 
Utoaji taarifa ndani ya jf nao ni shida, mleta Uzi hajasema tukio limetokea wapi na lini, hivyo kama member hajapitia media nyingine hawezi pata taarifa kamili
 
Pole kwa wafiwa, hao majambazi watakua na mafunzo ya hali ya juu, kuua polisi sio jambo dogo, you must be trained very well.
 
Naona mbagala sasa ni eneo hatari zaidi kwa matukio ya uvamizi wa kutumia silaha,jeshi la polisi limulike eneo hilo na kutumia Raia kuwapa habari za watu wabaya wenye silaha za moto.
 
Utoaji taarifa ndani ya jf nao ni shida, mleta Uzi hajasema tukio limetokea wapi na lini, hivyo kama member hajapitia media nyingine hawezi pata taarifa kamili

Limetokea Temeke -Mbagala Karibu na CRDB Bank
 
Mkuu kumbuka risasi/silaha aliyopigwanayo SHEKH PONDA MOROGORO na Mwandishi wa Habari MWANGOSI ziliibwa wapi? hao sio Watu

Tatizo haliwezi kuisha tu huku POLISI wakiwakandamiza RAIA
Lakini kumbuka pia tatizo halimalizi tatizo. Bali suluhisho huja baada ya kujua kiini cha tatizo!
 
Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba anasema tukio limeondoa maisha ya askari wanne na kujeruhi raia wawili.

Majeruhi mmoja anaitwa Ally Chionda ambaye ni mfanyabiashara wa duka la vifaa vya ujenzi karibu na benki ya CRDB ambayo pilisi wamepoteza maisha.

Anadai walikuja majambazi kwenye muda kama wa saa 1:15 usiku wakiwa na pikipiki kama tano na kila pikipiki ilikuwa na watu wawili.

Kulikuwa na watu sita au saba ambao walikuwa wamebeba bunduki.

Walipofika walianza kupiga risasi upande wa eneo la benki na upande wa duka lake.

Bahati mbaya risasi moja ilimpata kwenye mguu wa kushoto ikatokeza na kwenda tena kwenye mguu wa kulia.

Majeruhi anaendelea vizuri na anategemea kufanyiwa x-ray kwa uchunguzi zaidi.

VIDEO.




ANGALIZO:
Kuna baadhi ya watu wanaleta kejeli kuhusiana na tukio hili ambalo linasikitisha sana kwa watu wanaofahamu misingi ya kibinadamu.

Ni kweli binadamu tunatofautiana katika mitazamo lakini mizania ya kibinadamu huwa inapimwa wakati wa majonzi.

Hizo silaha walizopora inawezekana kesho zikatumika katika mwili wako au ndugu yako. Kama hujabahatika kutembelewa na majambazi huwezi kuelewa maana na uzito wa maneno yangu.

Tuombe uzima na Mungu awape faraja ndugu wa askari waliopoteza maisha wakiwa katika kazi ya kulinda maisha na mali za watanzania.

Amin.
 
Police nao waache kutumika vibaya na wanasiasa...Haiwezekani inteligensia za Police ziwe zinaona mikutano na maandamano ya vyama vya upinzani tu lakini ujambazi haiuoni ...Iwe fundisho kwao wafanye kazi za kupambana na ujambazi sio kupambana na raia wasiokuwa hata na fimbo
Acha Siasa kwenye mambo ya msingi sio kila sehemu ulete Siasa haina haja ya Comment kama kila kitu utoe mtazamo wa kisiasa. Watu wamepoteza ndugu na jamaa hapo sio kutoa kejeli Mkuu
 
Police nao waache kutumika vibaya na wanasiasa...Haiwezekani inteligensia za Police ziwe zinaona mikutano na maandamano ya vyama vya upinzani tu lakini ujambazi haiuoni ...Iwe fundisho kwao wafanye kazi za kupambana na ujambazi sio kupambana na raia wasiokuwa hata na fimbo
Wewe ni wa kupuuzwa maana hujawahi kuongea jambo la akili.
 
Hivi kwanini Jambazi akikamatwa anapelekwa mahakamani?. Ndiyo maana kila siku matukio kama haya hayataisha.
Mi nashangaa jambazi ameuwa akikamatwa anapelekwa mahakamani wakati ameuwa Hawa majambazi iwepo sheria ya kuwanyonga tu majambazi ni watu wabaya sana.
 
Majeshi yaliyooneshwa hivi karbuni kwenye TV ninaimani yatatosha kuzima ukuta, ujambazi na democrasia. Mbona walimu na madaktari walishika adabu! Umeshaona walimu wanagoma tena? Hata kama hawapewi nauri kwa wakati, hawapandishwi vyeo/madaraja, hawapati nyongeza ya mishahara wameshika adabu yao! Hivi kwa akili ya kawaida walimu wakipewa mishahara inayokidhi mahitaji ya familia zao, wabunge watagawana shilingi ngapi mwisho wa kuvunja bunge? Au viongozi wa juu watapiga wapi pesa ya ziada mbali na mishahara yao ya million 40? Ni bora walimu wakafahamu kuwa Dunia haina usawa! Kama huamini subiri uone majeshi yanayolinda serikali yatakavyo fanya hapo trh moja septemba!!!!?
 
Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba anasema tukio limeondoa maisha ya askari wanne na kujeruhi raia wawili.

Majeruhi mmoja anaitwa Ally Chionda ambaye ni mfanyabiashara wa duka la vifaa vya ujenzi karibu na benki ya CRDB ambayo pilisi wamepoteza maisha.

Anadai walikuja majambazi kwenye muda kama wa saa 1:15 usiku wakiwa na pikipiki kama tano na kila pikipiki ilikuwa na watu wawili.

Kulikuwa na watu sita au saba ambao walikuwa wamebeba bunduki.

Walipofika walianza kupiga risasi upande wa eneo la benki na upande wa duka lake.

Bahati mbaya risasi moja ilimpata kwenye mguu wa kushoto ikatokeza na kwenda tena kwenye mguu wa kulia.

Majeruhi anaendelea vizuri na anategemea kufanyiwa x-ray kwa uchunguzi zaidi.

VIDEO.




ANGALIZO:
Kuna baadhi ya watu wanaleta kejeli kuhusiana na tukio hili ambalo linasikitisha sana kwa watu wanaofahamu misingi ya kibinadamu.

Ni kweli binadamu tunatofautiana katika mitazamo lakini mizania ya kibinadamu huwa inapimwa wakati wa majonzi.

Hizo silaha walizopora inawezekana kesho zikatumika katika mwili wako au ndugu yako. Kama hujabahatika kutembelewa na majambazi huwezi kuelewa maana na uzito wa maneno yangu.

Tuombe uzima na Mungu awape faraja ndugu wa askari waliopoteza maisha wakiwa katika kazi ya kulinda maisha na mali za watanzania.

Angalizo lako sijalipenda! Hakuna anayeleta kejeli, wanatoa mawazo yao kuhusiana na tukio hili. Matokeo kama haya yanatoa nafasi ya kufanya reflection ya maneno yetu, matendo yetu etc. "Kiberiti hiki si cha njiti ni cha gesi kitalipuka," ni maneno hayapashwi kusemwa na kiongozi. Leo kimelipuka kwa wizara yake. Anafurahi kulipuka hivyo? Hapana, basi futa kauli ya kiberiti kulipuka. Mazoezi ya kuwatisha wananchi barabarani hayawezi jenga mahusiano mazuri na raia! Watu wataogopa kutoa hata taarifa wakihisi jambo la uhalifu kutaka kutokea, maana mnawatisha!
Tumeumia sote kufa vijana wetu. hakuna anyefanya kejeli kwa tukio baya kama hili.
 
Shukran kwa taarifa hii na kauli nzuri za maelekezo. Inasikitisha kuona mwanadamu anamkasifu mlinda usalama badala ya kulaani majambazi. Wao ni walinda usalama popote pale hata ktk mikutano hiyo kwakuwa haijaruhusiwa kutokana na sababu za kiusalama kwakuwa kauli nyingi zinaashiria uvunjifu wa amani na kuingilia kati utendaji Serikalini. Hiyo mikutano si ifanyike kule ilikoruhusiwa?
Eti 'kauli zinaashiria uvunjifu wa amani' unaongea kama Babu wa enzi za ujamaa,Tumia akili zako kufikiri acha kukaririshwa upuuzi.
 
Wapumzike kwa amani, Siasa wawaachie wanasiasa, wao wafanye kazi yao tu.
 
Mungu akusaidie sana na akusamehe hujui ulicho comment
sijaiba sijaua so sijamkosea Mungu na nakifahamu pia maaskari hawa wanaotumika na wanasiasa kila siku kupiga na kutia huku wengine wanashangilia kuona watz kapigwa

Leo kwa kua ni askari eeehhh!!basi mka mkijua huku mitaani tumechoka na udhalimu wanaofanya maaskari wenu wa kila aina,kuanzia rushwa na kusingiziwa kesi kibao!
Tena hakuna kituo chenye rushwa na udhalimu kama kizuiani mbagala almaarufu'maturubai'

Wananchi wamechoka wamechoka wamechokaaaaa!!!
 
Back
Top Bottom