Mahakama Kuu yatupilia mbali kesi ya kupinga Ndugai kujiuzulu Uspika. Yasema hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa

sajo

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
3,034
5,268
1643368941960.png

Leo tarehe 28.01.2022 Mahakama Kuu ya Tanzania chini ya majaji watatu wakiongozwa na Jaji Mgeta, imetupilia mbali kesi ya kikatiba Na 2 ya 2022 iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, Francis Mbatia dhidi ya aliyekuwa Spika wa bunge, Job Ndugai.

Mahakama imeeleza kuwa kesi hiyo haina mashiko kwa kuwa hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa. Mahakama imetambua barua iliyotolewa mahakamani na Wakili mkuu wa Serikali kuonesha kuwa Ndugai aliandika barua ya kujiuzulu kwenda kwa Katibu wa Bunge na nakala kwa Katibu Mkuu wa CCM ni halali na hivyo alifuata taratibu zote.

Nakala ya barua iliyotambuliwa na Mahakama ni hii hapa.


Pia soma

Barua ya Ndugai_1.jpg
 
Kikubwa hapa ni kuangalia namna ya kuinarisha katiba ili mteule asilate nafasi ya kujiuzulu ili kupunguza gharama na usimbufi na kuongeza mzoo who wastaqfu. Otherwise ukijiuzulu yafaaa kupoteza haki zote stahili.
 
Leo tarehe 28.01.2022 Mahakama Kuu ya Tanzania chini ya majaji watatu wakiongozwa na Jaji Mgeta, imetupilia mbali kesi ya kikatiba Na 2 ya 2022 iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, Francis Mbatia dhidi ya aliyekuwa Spika wa bunge, Job Ndugai.

Mahakama imeeleza kuwa kesi hiyo haina mashiko kwa kuwa hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa. Mahakama imetambua barua iliyotolewa mahakamani na Wakili mkuu wa Serikali kuonesha kuwa Ndugai aliandika barua ya kujiuzulu kwenda kwa Katibu wa Bunge na nakala kwa Katibu Mkuu wa CCM ni halali na hivyo alifuata taratibu zote.

Pia soma
hii nchi inanipa burudani
 
Bush Lawyers njooni na uamuzi wenu.Uzushi ndio umechukua nafasi kubwa JF kuliko facts.
 
Leo tarehe 28.01.2022 Mahakama Kuu ya Tanzania chini ya majaji watatu wakiongozwa na Jaji Mgeta, imetupilia mbali kesi ya kikatiba Na 2 ya 2022 iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, Francis Mbatia dhidi ya aliyekuwa Spika wa bunge, Job Ndugai.

Mahakama imeeleza kuwa kesi hiyo haina mashiko kwa kuwa hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa. Mahakama imetambua barua iliyotolewa mahakamani na Wakili mkuu wa Serikali kuonesha kuwa Ndugai aliandika barua ya kujiuzulu kwenda kwa Katibu wa Bunge na nakala kwa Katibu Mkuu wa CCM ni halali na hivyo alifuata taratibu zote.

Pia soma
Hiyo barua ilifichwa wapi? Tulioonyeshwa ni barua kutoka kwa Ndugai kwenda kwa katibu mkuu wa CCM nakala kwa katibu wa Bunge!
 
Hiyo barua ilifichwa wapi? Tulioonyeshwa ni barua kutoka kwa Ndugai kwenda kwa katibu mkuu wa CCM nakala kwa katibu wa Bunge!
Hata mimi nimeishangaa hii barua. Au walibadili gia angani ili kunlfunika kombe mwanaharam apite?

Katibu wa bunge alipohojiwa alisema yeye hajaandikiwa barua bali amepata nakala ya barua ya spika kwenda kwa katibu mkuu wa chama chake kwa ajili ya kujiengua katika nafasi hiyo.
 
Hata mimi nimeishangaa hii barua. Au walibadili gia angani ili kunlfunika kombe mwanaharam apite?

Katibu wa bunge alipohojiwa alisema yeye hajaandikiwa barua bali amepata nakala ya barua ya spika kwenda kwa katibu mkuu wa chama chake kwa ajili ya kujiengua katika nafasi hiyo.
Mahakama yetu imelaanika!
 
Tulimwambia Mbatia akatuona hatufai, Hakuna kesi ya kikatiba ambayo ilishawahi kupenya - Angechungulia kesi zote za kikatiba za Maheremu Mtikila kama zilishawahi kupenya.

CCM ishachagua Spika tayari afu eti mtu agomeshe Jobo kuachia ngazi wakati kashasema ati nchi itapigwa mnada - hiiiii.
 
Tulimwambia Mbatia akatuona hatufai, Hakuna kesi ya kikatiba ambayo ilishawahi kupenya - Angechungulia kesi zote za kikatiba za Maheremu Mtikila kama zilishawahi kupenya.

CCM ishachagua Spika tayari afu eti mtu agomeshe Jobo kuachia ngazi wakati kashasema ati nchi itapigwa mnada - hiiiii.
Mtikila alishinda kesi zake zote, kilichofanywa na serikali ni kukata rufaa na kuweka majaji wa kimagumashi!
 
Tulimwambia Mbatia akatuona hatufai, Hakuna kesi ya kikatiba ambayo ilishawahi kupenya - Angechungulia kesi zote za kikatiba za Maheremu Mtikila kama zilishawahi kupenya.

CCM ishachagua Spika tayari afu eti mtu agomeshe Jobo kuachia ngazi wakati kashasema ati nchi itapigwa mnada - hiiiii.
Ni ngumu kuushinda mhimili uliojichimbia chini, mbatia asingeweza. Hakuna aliyeweza
 
Hiyo barua ilifichwa wapi? Tulioonyeshwa ni barua kutoka kwa Ndugai kwenda kwa katibu mkuu wa CCM nakala kwa katibu wa Bunge!
Kilichotokea sasa ni kuwa bunge limefuta taarifa zote kwa umma zilizokuwa katika tovuti yake parliament.go.tz zikionesha taarifa ya umma kutoka kwa Ndugai na taarifa kwa umma kutoka kwa Katibu wa Bunge zote zikionesha kuwa kilichowasilishwa bungeni ni nakala. Kwa sasa tovuti ya bunge ina barua ya kuwaita wabunge tu ila zile taarifa kwa umma wamezifuta. Pia kwenye ukurasa wao wa twitter wamefuta tweets hizo zilizokua na taarifa kwa umma.🤣🤣
 
Back
Top Bottom