mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,664
- 18,040
Katika gazeti la Raia Mwema toleo no.418 ipo habari ya Mgombea Urais wa CCM kuwa eti atawapatia walimu wote laptops ili kuinua kiwango cha elimu,na labda kwa fikra zake,kuondoa umaskini nchini...
Nikiwa mwalimu,ahadi hii inanikera,hivi anafikiri sisi ni wapuuzi kiasi hicho cha kufikiri kuwa tutaipigia CCM kura kwa ahadi ya laptops?Na OK,ni lini katika madai ya msingi ya walimu kwa serikali kwamba kukosa laptops kumewahi kuwa tatizo?Na hivi katika ilani ya uchaguzi ya CCM kugawa laptop ndicho kipaumbele?Na basi tukubaliane kuwa tunataka laptops,zitasaidia vp kuinua kiwango cha ufundishaji?Iko wapi miundombinu ya ku-support hiyo project?Mradi wa JK wa Tanzania & Beyond uko wapi?
Kwa ufupi,mradi wa laptop umekwama Kenya na ulikwishakwama Nigeria...Mh.Magufuli kama hakujiandaa kugombea urais au kama mafuriko ya UKAWA yanamchanganya basi atangulie tu jehanamu,moto umewaka...waalimu hatuna mpango na CCM na kama haelewi basi aendelee kubwabwaja na mradi wake wa laptop
Huyu hafai kabisa! Lini walimu walidai kuwa wana shida na lap top?
Kura za walimu zishaenda ukawa!