Magufuli: Hakuna haja ya hivi vyama vya siasa

Nimesikiliza hiyo hotuba na ni kweli ametamka kuwa kinachohitajika sio haya mavyama ya siasa bali maendeleo! Nilichokiona kutoka katika hotuba yake ikiwa ni pamoja na lugha ya maneno na ya mwili (body language), ni kweli JPM anayosema anayesama kwa dhati, ana nia nzuri lakini HANA uelewa wa kutosha kutambua na kukubali kuwa chama chake, CCM, ndicho kilisababisha hayo anayoyaita 'mambo ya hovyo kabisa' aliyoyakuta na kwamba bila vyama vya upinzani kupaza sauti kali leo hii tungekuwa na Maembe na hayo anayoyaita ya hovyo yangekuwa business as usual! JPM anahitaji mshauri makini wa siasa au niseme sayansi ya siasa na anayemwamini na kumheshimu ili ampige msasa kwamba asikandamize wala kubeza upinzani (ninafikiri anaposema hawataki mavyama, anamaanisha upinzani) kwani ndio unampa nafasi aliye madarakani kujua wapi amejikwaa ama ameteleza katika juhudi zake za kutaka kuwaletea wananchi maendeleo.
Amekiri kwa uwazi kuwa amekuwa serikali kwa muda wa miaka 20 na anaposema kuna uozo anajua anachosema. Sasa kama aliuona huo uozo, kwa nini asijiulize kwa nini hakuthubutu hata kutoa pendekezo ya kuuondoa? Ni kwa sababu kwa utamaduni wa utawala wetu, ukiwa sehemu ya utawala huwezi kumkosoa mkubwa wako hata kama unaona anayofanya hayafai. JPM anakiri utawala wa awamu ya nne ulifanya mengi ya hovyo lakini asingeweza kufanya lolote. Ni mpinzani tu ambaye ana nafasi ya kumnyooshea mtawala kidole, tena hii imehalalishwa kikatiba. JPM anahitaji kasemina-elekezi ka faraghani ili aache kuwa anajishusha kiasi anachofanya linapokuja suala na siasa za upinzani. Siasa za upinzani (mavyama ya siasa) ni NGUZO kuu ya kuwaletea wananchi maendeleo, Mr President!

Correct mkuu, uelewa mdogo sana
 
Anasema kinachohitajika ni maendeleo ya wananchi. Km kuna wengine bado wanategemea democracy Tz labda waombe wawepo baada ya miaka 200 ijayo. Vinginevyo tafuteni njia nyingine, inawezekana tuna laana au kuna makosa ya evolution kwa waafrika


HATA MIMI NADHANI HAKUNA HAJA NA HASA HIKI KINACHOITWA CHA CCM
 
Kabla ya kuchangia zaidi ningependa kumsikia akiongea alicho ongea. Kama kuna mwenye kideo tafadhali atuwekee.
 
Siwezi Kusema Lolote Kabla sijaona Video ya Magufuli akisema haya. Maana Nitakayosema Ni Mazito sitaki Kumsingizia Mtu, Mwenye Video aiweke hapa!
 
hata mimi naona hivyo. watutsi waroho wa madaraka sana.
tatizo umelimaliza mkuu,wale wasiompenda kagame wamtarajie kwa karibu kabisa kwenye nchi yetu
Tukisema system zetu zina matatizo tunatukanwa.uchu uchu
 
Alikuwa na maana ni pamoja na CCM au anataka ibaki CCM peke yake? Tusipoangalia utawala huu utaturudisha kwenye ujima na utawala wa chama kimoja. Dalili zimeshaanza kuonekana.
 
Yupo sahihi kabisaaa!!!

Afrika hakuna Demokrasia

Hakuna demokrasia,kwasababu demokrasia haiwezi kutekelezwa na watu au vyama vyenye uchu wa madaraka kama CCM.

Heri wakoloni waje,si kututawala tena

Bali waje kutufundisha demokrasia kwa vitendo,

Hata dhahabu tutawapa.

Waafrika hatuna laana,tuna ujinga wa kurithi.

Ujinga mpaka kwenye damu.
 
Umuhimu wa Vyama vingi Tanzania ni mkubwa sana kama wangekuwa wanafanya yanayopaswa lakini Uoinzani kwao wametafsiri kupinga kila kitu. Agrrrrr

Mkuu, kama wanapinga kila kitu, si uwaambie ni nini wanachopaswa kupinga?
 
Atusaidie kuvifuta kwenye katiba, ili pia vimrahisishie kazi yake ya kuwatumia polisi kuzuia shughuli za vyama vya siasa, kama anavyofanya sasa. Kumbe naanza kuamini, ile marufuku ya PM ilikuwa na baraka zote kutoka kwake. Nchi yetu hii bado ina safari ndefu sana.
 
Hakuna jambo limewakera CCM kama kukataliwa na watu wa jiji la Dar. Sasa CCM inatapatapa na wameamua liwalo na liwe, ni heri waonekane madikteta kuliko kuwaachia Ukawa halmashauri ya jiji la Dar es salaam.
 
Msimfanye rais zoba kiasi hicho, simuungi mkono lakini hawezi kuwa wa kiasi cha chini kiasi cha kufikiria hayo
maazimisho ya ccm kule singida alisema nchi haiwez kuongozwa na vyama vya hovyo hovyo ina maana upinzan
 
Maendeleo hayana chama, hayo ni maneno ambayo rais Magufuli anapenda kuyasema. Siasa za vyama vingi zimeua kabisa hata ule uwezo wa kuyaangalia mambo katika mtazamo chanya. Watu wanatazama katika hali ya chuki, wanatamani kuwekeana sumu, wanaombeana mabaya. Lakini maendeleo ya kweli wala hayana uhusiano na itikadi za kisiasa.

Balozi wa Japan enzi za awamu ya nne, wakati anatoa msaada wa vyandarua kule pemba, aliwahi kusema mbu anapomuuma mtu anakuwa hajui kama ni mwanachama wa CCM au CUF, na malaria atakayoipata yule aliyeng'atwa na mbu, itabidi itibiwe kwa kutumia matibabu ambayo wala hayajali kama aliyeumwa ni mwanachama wa chama fulani au sio mwanachama.

Watanzania tunapoteza utu na upendo kwa sababu tu ya huu mtego wa siasa za vyama vingi, mtego tulioletewa na wazungu.
 
Siwezi Kusema Lolote Kabla sijaona Video ya Magufuli akisema haya. Maana Nitakayosema Ni Mazito sitaki Kumsingizia Mtu, Mwenye Video aiweke hapa!

Uzinduzi, road, Arusha, Taarifa ya ITV saa 2 usiku, March 3, 2016.
 
Maendeleo hayana chama, hayo ni maneno ambayo rais Magufuli anapenda kuyasema. Siasa za vyama vingi zimeua kabisa hata ule uwezo wa kuyaangalia mambo katika mtazamo chanya. Watu wanatazama katika hali ya chuki, wanatamani kuwekeana sumu, wanaombeana mabaya. Lakini maendeleo ya kweli wala hayana uhusiano na itikadi za kisiasa.

Balozi wa Japan enzi za awamu ya nne, wakati anatoa msaada wa vyandarua kule pemba, aliwahi kusema mbu anapomuuma mtu anakuwa hajui kama ni mwanachama wa CCM au CUF, na malaria atakayoipata yule aliyeng'atwa na mbu, itabidi itibiwe kwa kutumia matibabu ambayo wala hayajali kama aliyeumwa ni mwanachama wa chama fulani au sio mwanachama.

Watanzania tunapoteza utu na upendo kwa sababu tu ya huu mtego wa siasa za vyama vingi, mtego tulioletewa na wazungu.

Hata hii ICT unayotumia imeletwa na wazungu, mwaafrika jpm amewahi kuleta nini, nenda kalipwi kwa kupotosha
 
Afrika aihitqji vyama bali inahitaji.maendeleo....Jpm
Kama hahutqji vyama basi afute sisiemu kwani chama hicho pamoja na baba na mama yyao TANU/ ASP wamekuwepo madarakani kwa zaidi.ya miongo mitano. Hivyo kukosa maendeleo,uzembe,rushwa na ufisadi vimelelewa na kukomazwa na wao hivyo wafutwe kabisa
 
Mtoa mada wewe ni popompo

alichosema sio hakuna haja ya vyama Bali amesema sasa ni muda wa kutafuta maendeleo sio kujizuuka kwenye mambo ya vyama tuungane kuhakikisha afrika tunajikwamua Na umasikini
pia akasema lengo lake yeye ni kuhakikisha anapambana Na wachache wanaomiliki Mali nyingi huku wakisababisha wananchi walio wengi wa Hali ya chini kupata shida.

naona ni mwongo tu...kwanini asianze na suala la umeya wa dar es salaam...kwanini asikubali kwamba chama chake kimezidiwa idadi na waruhusu ukawa waliendeshe jiji....yeye ndo kakumbatia uchama...penye ukweli lazima tuseme
 
Back
Top Bottom