Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,899
Hivi karibuni kituo cha televisheni cha TBC1 kilimnukuu Magufuli akisema: "Ni bora ukafukuzwa wakati unatekeleza sheria na ni bora ukafa wakati unatekeleza sheria, kwa sababu ukienda mbinguni utapewa barabara ya kutengeneza."
Mbali na rais na waziri mkuu, msimamo wa Magufuli pia umewakera viongozi katika maeneo mengine, wakiwamo mameya wote wa manispaa tatu za Dar es Salaam.
KAULI ya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kuwa kwa vyovyote iwavyo lazima abomoe mabango yote ya biashara barabarani akisema kuwa hakuna wa kumzuia kuyaondoa kwa kuwa anatekeleza sheria za nchi, imetuma ujumbe mzito kwa wakubwa wake wa kazi.
Miongoni mwa viongozi walioguswa na kauli hiyo ya Magufuli ni Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambao kwa wakati tofauti walimkemea waziri huyo, wakimzuia kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, kwa masilahi ya kisiasa.
Alipomtembelea wizarani kwake wiki chache zilizopita, Rais Kikwete alimwambia Magufuli, "acha ubabe." Kabla ya hapo, Pinda alimfokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Jimbo la Chato, linalowakilishwa na Magufuli, akimtaka asitishe bomoabomoa mara moja.
Hata juzi wakati akifungua semina elekezi mjini Dodoma, Rais Kikwete alikemea tabia ya ubabe wa mawaziri na kauli za kupingana wenyewe kwa wenyewe kupitia kwenye vyombo vya habari.
Lakini katika wiki hii pekee, Magufuli ametoa kauli zinazoonyesha hayuko tayari kusitisha ubabe wake wala bomoabomoa, kazi ambayo amekuwa akiifanya kwa kuzingatia sheria zilizopo.
Source: Tanzania Daima