Ukitaka kujua barabara inatengenezwa na wa tz ni rahisi sana, kwa mfano wanafanya marekebisho, watachimba sehemu zilizoharibika ili kuweka lami, wakishachimba wataacha mashimo kwa miezi miwili au zaidi, hakuna alama zozote. Baada ya miezi miwili au zaidi, watakuja na mashine zao wataweka mabango mekundu kila mahali na kusababisha foleni kubwaaa kwa wiki nzima au zaidi, ndio kazi ikamilike. Kazi ndogo kero kubwa, kama ni mchina hiyo kazi yote angemaliza kwa siku mbili tu.
Arusha kuna barabara nyingi za magari lakini hizi barabara ni mbovu kupita maelezo, watu wengi wanang'ang'ania kupita barabara kuu ingawa na yenyewe ni nyembamba sana. Hakuna vituo vya daladala, vipanya vinapenya pembezoni mwa barabara na kusimama popote, wewe unayefuata sheria za barabara unakuwa kama mshamba, kulia kwako msururu wa pikipiki za wajasiria mali, kushoto umebanwa na dadalada kama nne hivi.
OMBI KWA MAGUFULI
Kuna barabara ya vumbi inayotoka NMC hadi mjini, mwisho wa hii barabara kuna Daraja linatengenezwa, limeshachukua zaidi ya miezi minne hatuoni kinachoendelea, kuna mabango yamerembwa yanasema kuna ujenzi unaendelea. Muheshimiwa Pombe Magufuli naomba uwaamshe wajenzi wa hili daraja wamalize kazi, pia wachonge hiyo barabara kidogo ili iweze kupitika. Nahakika ni ule usingizi wetu wa kawaida tu, embu waamshe wamalize kazi. Au wape tenda wachina ili mambo yaende. Hii barabara ni muhimu sana kwa wakazi wa Arusha kwa sababu itapunguza msongamano. Magari mengi ya private yatapita kwenye hii barabara na itapunguza msongamano kwa kiasi kikubwa.
Arusha kuna barabara nyingi za magari lakini hizi barabara ni mbovu kupita maelezo, watu wengi wanang'ang'ania kupita barabara kuu ingawa na yenyewe ni nyembamba sana. Hakuna vituo vya daladala, vipanya vinapenya pembezoni mwa barabara na kusimama popote, wewe unayefuata sheria za barabara unakuwa kama mshamba, kulia kwako msururu wa pikipiki za wajasiria mali, kushoto umebanwa na dadalada kama nne hivi.
OMBI KWA MAGUFULI
Kuna barabara ya vumbi inayotoka NMC hadi mjini, mwisho wa hii barabara kuna Daraja linatengenezwa, limeshachukua zaidi ya miezi minne hatuoni kinachoendelea, kuna mabango yamerembwa yanasema kuna ujenzi unaendelea. Muheshimiwa Pombe Magufuli naomba uwaamshe wajenzi wa hili daraja wamalize kazi, pia wachonge hiyo barabara kidogo ili iweze kupitika. Nahakika ni ule usingizi wetu wa kawaida tu, embu waamshe wamalize kazi. Au wape tenda wachina ili mambo yaende. Hii barabara ni muhimu sana kwa wakazi wa Arusha kwa sababu itapunguza msongamano. Magari mengi ya private yatapita kwenye hii barabara na itapunguza msongamano kwa kiasi kikubwa.