Magufuli aponda dhana ya polisi jamii dhidi ya majambazi : Waziri Masha na Mwema mpo!

Umar Farouk Abdulmuttalab.

Nilidhani huyo kijana aligundulika baada ya suruali yake kuanza kuwaka moto na kuunguza ukuta wa ndege. Mwenyewe alijipindua kama Mpakistan wa Times Square). Au wewe hebu tueleze polisi jamii ilifanikiwa vipi kumnasa Umar?

Dhana ya polisi jamii haina maana kuwa suala la kukamata wahalifu wanaachiwa wananchi. Hata huko kwa wenzetu, kazi ya kukamata na kufanya uchunguzi bado ni ya polisi. Kinachofanyika ni kuwa jamii inashiriki katika kutoa taarifa n.k. Jamii isiyokuwa na imani na polisi ni mara chache wanakuwa tayari kutoa taarifa zinazoweza kusaidia uchunguzi wa matukio ya uhalifu. Unachanganya polisi jamii na sungusungu. Sungusungu ndiyo walitegemewa kufanya kazi ya polisi. Katika polisi jamii, mamlaka na wajibu wa kukamata wahalifu unabaki wa polisi
[FONT=Verdana, sans-serif]
Jibu hili swala, usizunguke mibuyu: Nani ana jukumu, na nani awajibike, na nani anaweza kuwa na taarifa zaidi, idara ambayo kazi yao ni uchunguzi wa ujambazi au raia ambae hana nyenzo, ujuzi, muda wala malipo? Jibu.[/FONT]

Mafanikio si kutokomeza uhalifu. Hata nchi zenye sheria kali bado zina uhalifu. Mafanikio ni kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa. Na huko kwa wenzenu, katika maeneo mengi uhalifu wa kipuuzi umepungua sana. Lakini bado kuna sehemu ambako uhalifu bado uko juu. Mara nyingi katika maeneo haya polisi anachukuliwa kama adui na hamna kitu kibaya kama kuwa "snitch".
Wewe mwenyewe umesema uhalifu huko kwa wenzetu upo kwa viwango kama vya kwetu “... Kitu kingine usichojua ni kuwa pamoja na wao kuendelea lakini kero za uhalifu ni kama kwetu, mauaji, vibaka, uuzaji wa madawa ya kulevya n.k” Hukudai hivyo? Huishi kujifunga funga. Na usiite ujambazi “uhalifu wa kipuuzi.” Labda kama unaishi kwenye ahera-salama huko kwa wenzenu ndio unaweza kuwa na moyo mkavu kiasi cha kuita ujambazi hapa kwetu ni upuuzi. Ni janga linalotuua kila siku! Usiwe nje ya mguso.

Na si kweli kwamba sehemu zilizojaa uhalifu huko kwa wenzenu kuna uhusiano na wambea kuchukiwa. Viwango vya uhalifu huko vinaendana na milinganyo ya hali ya uchumi wa miji na maeneo, elimu na ajira. Si kwa sababu ya mafanikio ya polisi jamii. Usipotoshe.


Kwa wenzenu wapi ulikoenda? Dhana ya polisi kufanya patrol kwa kutembea iko uingereza.
Wewe mwanzoni ulipoongelea kwa wenzenu ulianisha ni Uingereza? Kumbe Uingereza ndio polisi wanatembea mitaani kusogoa na Wananchi wakisakanya dodoso za majambazi? Basi Magharibi niliyoiona mimi hilo hakuna! Askari akichoka doria anaenda kula mandazi sukari yenye matobo, ndo sifa waliyonayo, haendi kuvinjari na porojo katini mwa wananchi. Wananchi hawana muda huo barabarani.

Si wananchi wote wana ari na kasi katika maisha yao. Kuna watoto wadogo, vikongwe, wenye biashara ndogo ndogo, watalii n.k. Wote hawa wanapokuwa na shida ndogo ndogo kimbilio lao ni polisi...
Watoto na Wafanya biashara wana kazi pia, hawana mda wa kusogoa na polisi kwenye “beats.”! Watalii hawajui majambazi ya jamii, wengi wao ni watembezi wageni. Vikongwe huko kwa wenzenu vingi vinafungiwa ndani ya nyumba za wakunga na si kuzurura kwenye polisi jamii.

...Wanaofanya uchunguzi wa matukio ya uhalifu mara nyingi si askari wanaokuwa kwenye beats. Uchunguzi unafanywa na askari kanzu (CID).
Kwa hiyo “beats” hawakusanyi taarifa za majambazi. Na ulisema “beats” wanasimama kuongea na wananchi. Kumbe maongezi haya ya nini, matokeo ya Azam FC na Yanga? Nini maana ya hizi “beats” na polisi jamii kama hazitusaidii kiuchunguzi? Kwenye kurasa za nyaraka ya polisi uliotubandikia hapa wamesema msingi mmoja wa polisi jamii ni uchunguzi wa siri kung'amua matatizo kwenye jamii, “Intelligence-led identification of community concerns...” Sasa kama hizo “beats” hazikusanyi taarifa zozote basi usizipigiea chapuo kama kielelezo cha polisi jamii.

...e hiyo Witness Protection Program ... si ndiyo sehemu ya polisi jamii?

Na ni kielelezo cha utisho wa jambazi kwa raia. Raia anaogopa jambazi ndo maana akimshuhudia yabidi alindwe. Sisi mnatuambia tukashuhudie kichwa kichwa eti majambazi wanatuogopa, tafadhali!


... Sisi wakati tunakuwa uhalifu wa kipuuzi ulikuwa chini. Na sababu kubwa ilikuwa ukionekana unaiba embe basi utacharazwa bakora na ukishitaki kwa mzazi wako atakuongezea. Kulikuwa na zero tolerance na upuuzi kama huo. Leo ukijaribu kumsema tu mtoto wa jirani ...
Fundi Mchundo, umefanya utafiti kung'amua kwamba wakati wenu “uhalifu wa kipuuzi” ulikuwa chini? Umefanya uchunguzi kugundua kwamba sababu ya tofauti hizo za enzi ni kwa vile mlikuwa mnanyukwa viboko na jirani? Na kama hayo ni kweli, basi inawezekana ni kwa sababu ya kuiga hayo mambo ya “kwa wenzetu.” Maana hatuishi kuchambua jambo bila kuiga ya “kwa wenzetu.” Halafu “uhalifu wa kipuuzi” ni upi? Tunaongelea ujambazi hapa. Usidogoeshe uzito wa janga la wananchi tafadhali.

Na huko kwa wenzenu sehemu kama hizo zipo.
Sehemu gani, huku kwa wenzetu wapi kaka? Nilidhani ni wenzenu wewe, unanichenjia kibao? Usiwateme wenzenu bana... hahahaaaaaa.

Marekani kuna sheria za State na sheria za nchi nzima. FBI wanashughulikia uvunjaji wa sheria za nchi. Kwa mfano, ukikamatwa unauza bangi, utashitakiwa na kushughlikiwa na mamlaka za state. Lakini ukikamatwa unasafirisha bangi kutoka State moja kwenda Nyingine, utashughulikiwa na FBI pamoja na polisi wa state husika.
Hili somo la mtapanyiko wa ufuatiliaji wa sheria baina ya majimbo na shirikisho la Marekani apa linatusaidia nini? Nilipoongelea FBI ukasema uhalifu mwingi unashughuliwa na “local police.” Nikwambia hata FBI nao wanahusika kwa kiasi kikubwa tu. Sasa unasema FBI wanahusika na usafirishaji bangi majimboni, kwani huo sio uhalifu? Kwa nini ulisema nisiwaongelee FBI?

...Sasa kama mzazi wa polisi yuko Magu au Tarime wakati yeye mwenye anafanya kazi vingunguti itasaidia nini katika kuwakamata wahalifu wa vingunguti?
Kama anafanya kazi kitengo cha uhalifu wa silaha Vingunguti anatakiwa aelewe hali na mandhari nzima ya Vingunguti. Atasemaje yeye mgeni wazazi wake wanatoka Magu? Arudi akafanye kazi Magu basi, anakokuelewa. Eti polisi ni wageni, sisi ndio tunajua wezi wa maeneo yetu, nyinyi ndio mnalipwa, mnafundishwa, mna muda, mna nyenzo za kusakanya majambazi, fanyeni kazi yenu.


Hamna kitu ambacho jambazi wanaogopa kama jamii kuwageuka. ... Polisi jamii itasaidia kuwa hata kabla ya tukio jambazi atajua kuwa hakubaliki na jamii itamtosa akifanya upuuzi wake.
He! Kwa hiyo Fundi Mchundo unatuambia kwamba majambazi yameshamiri kwa sababu yanakubalika na jamii? Msikieni huyu mja. Kuwageuka? Wanaogopa jamii kuwageuka, ina maana kwa sasa wana jamii wako upande wa majambazi? Tukiwageuka wataacha! Jambazi halitegemei raia awe upande wake, ndo maana linamuua!


]Polisi posti zinafanya polisi kuwa karani na kungojea aletewe taarifa na mwananchi...Vituo vya polisi vitakuwepo.
Nini tofauti ya polisi posti na vituo vya polisi?


...Akitoa taarifa kwenye kituo cha polisi kwa simu basi wao ndio watamuagiza polisi aliyekaribu na tukio kwenda kutoa msaada.

Hilo la simu ni kwetu au la “kwa wenzetu”? Tanzania hakuna namba ya polisi ya dharura itakayoleta askari papo hapo. Tulikamata mwizi mtaani miezi michache iliyopita nikapiga simu, polisi walipofika jamaa keshafika kuzima kitambo. Wakaanza kutuhoji sisi kuhusu anaejua ubini wa marehemu. Nikawaambia kwa nini hamkuwahi kuja kumhoji mwenyewe? Zamani tulikuwa na 999, siku hizi tunapewa namba ya mkononi ya Kamanda Kova. Usiwe nje ya mguso.


Kama mwananchi atakuwa na swala la kawaida linalomuhitaji polisi basi atamsubiri mtaani maana ni lazima atapita.
Na akipita atatugongea mlangoni? Kila mtu ana zake mtaani, hakuna mwenye mda kukaa gengeni kusubiri askari apite amweleze matatizo yake. Au kilabuni? Na tunaongelea ujambazi hapa, sio “swala la kawaida” la kusubiri askari apite.

Mfano huu nimetumia kukujibu ulipodai kuwa wananchi wanogopa majambazi kwa sababu wanabeba SMG. Hakuna mahali nilipotetea uchukuaji wa sheria mikokoni

Kama wananchi hawaogopi SMG majambazi yanawezaje kuweka kitongoji kizima chini ya ulinzi? Umati wa watu wenye mawe unafua dafu kwenye shaba za m-gobole? Sasa unataka kujifanya Kinjekitile mamboleo.


Hiyo nyaraka inakuonya kwenye dibaji kwamba usiisome kama kilelezo cha ufanisi wa polisi jamii. Kwa sababu, kwanza, inasema ni picha ya haraka ya mpango majaribio wa awali, na yabidi tusubiri mpango mzima ukamilike ndani ya miaka mitatu; “ The report provides a snapshot of the evidence as it stood after the first year of national implementation, and should not be read as a definitive account of whether neighbourhood policing ‘works’. Such an assessment can only be made after the end of the three-year programme, when neighbourhood policing should be implemented in full.” Moja, la pili, ripoti inaongelea aina za uhalifu wa huko kwa wenzenu, ambao ni tofauti kabisa na halifu za hapa kwetu. Huwezi niwekea ki-ripoti cha kwa wenzenu wa Liverpool ukadai kitusaidie kuelewa umuhimu wa polisi jamii Vingunguti. Tatu, nipe vielelezo vilivyoandikwa na watafiti huru, sio dondoo ya askari hukusu mafinikio ya mpango wa askari, iliyoandikwa na idara ya askari!

Polisi jamii ni ukingu unaowapa polisi kisingizio wanapolegalega kwenye majukumu yao kulinda raia.


Ni kweli upeo wako wa kufikiri ni mdogo. Hii haikuondolei haki yako ya kutokubaliana na chochote nitakachokisema.
Wewe ndo ulisema ni bora ninyamaze, ufikiri wangu mfupi. Sasa unanipa ruhsa ya kusema. Basi ngoja nimalizie kwa kusema “Zidumu Fikra za Fundi Mchundo... Ziduuum”!
 
Hii ni mara ya mwisho kujibishana na wewe. Unanipotezea muda.

Nilidhani huyo kijana aligundulika baada ya suruali yake kuanza kuwaka moto na kuunguza ukuta wa ndege. Mwenyewe alijipindua kama Mpakistan wa Times Square). Au wewe hebu tueleze polisi jamii ilifanikiwa vipi kumnasa Umar?



Kumbe una habari za Umar! Waliomkamata huko hewani walikuwa polisi? Na lawama kubwa zilizoelekezwa kwa hao unaodai ni jukumu lao si kwa sababu wangeweza kumkamata mapema kwa vile baba yake Umar aliisha waeleza kuhusu wasiwasi wake kuhusu mwanae? Polisi jamii maana yake ni kuongeza ushirikiano kati ya jamii na polisi. Na kuanzia huko kutoa taarifa na hatua ya abiria mwenzake Jasper Schuringa kumrukia hadi wahudumu walipozima moto. Kutokana na dhana yako, Jasper na wenzake wangemwangalia tuu na kusubiri hadi washuke Detroit ambapo wenye jukumu la kumkamata wangemkamata!

Jibu hili swala, usizunguke mibuyu: Nani ana jukumu, na nani awajibike, na nani anaweza kuwa na taarifa zaidi, idara ambayo kazi yao ni uchunguzi wa ujambazi au raia ambae hana nyenzo, ujuzi, muda wala malipo? Jibu.

Maswali kama haya ndiyo yanayoniimanisha kuwa uwezo wako wa kufikiri au kuelewa ni mdogo. Kwenye mabano umeweka nilivyokujibu kuhusu jukumu la kukamata wahalifu lakini bado unangania swali hilo hilo. Soma tena nilivyokujibu.

Katika polisi jamii, mamlaka na wajibu wa kukamata wahalifu unabaki wa polisi


Hakuna mahali niliposema kuwa kazi ya kuchunguza matukio ni ya raia. Nilichokisema ni kuwa wananchi mara nyingi wanakuwa na taarifa za uhalifu kuliko hata polisi. Wananchi wanaweza kuwa wameshuhudia tukio, wamemtambua anayehusika n.k. wakati polisi ni lazima afanye uchunguzi kwanza kama hakuwasili wakati tukio linatendeka. Wananchi wanakuwa na taarifa za vificho vya wahalifu kabla hata ya polisi kuchungua. Katika polisi jamii kinachosisitizwa ni kwa jamii kutoa taarifa zao na ufahamu wao kwa polisi. Polisi ndiyo wana jukumu la kuchunguza, ambao utasaidiwa kwa kiasi kikubwa na taarifa na ufahamu wa wananchi hadi mhusika atakapojulikana. Akijulikana , polisi ni wajibu wao kumkamata, kumfungulia mashtaka na kumpeleka mahakamani. Katika hatua hii, ushiriki wa jamii ni katika kutoa ushahidi tu.
Wewe mwenyewe umesema uhalifu huko kwa wenzetu upo kwa viwango kama vya kwetu "... Kitu kingine usichojua ni kuwa pamoja na wao kuendelea lakini kero za uhalifu ni kama kwetu, mauaji, vibaka, uuzaji wa madawa ya kulevya n.k" Hukudai hivyo? Huishi kujifunga funga. Na usiite ujambazi "uhalifu wa kipuuzi." Labda kama unaishi kwenye ahera-salama huko kwa wenzenu ndio unaweza kuwa na moyo mkavu kiasi cha kuita ujambazi hapa kwetu ni upuuzi. Ni janga linalotuua kila siku! Usiwe nje ya mguso.

Na si kweli kwamba sehemu zilizojaa uhalifu huko kwa wenzenu kuna uhusiano na wambea kuchukiwa. Viwango vya uhalifu huko vinaendana na milinganyo ya hali ya uchumi wa miji na maeneo, elimu na ajira. Si kwa sababu ya mafanikio ya polisi jamii. Usipotoshe.

Kusema kuwepo kwa uhalifu katika nchi za magharibi hakuna maana kuwa upo kwa kiwango kama chetu! Hata humu humu nchini viwango vya uhalifu vinatofautiana kutoka sehemu hadi sehemu, sasa itakuwaje nifananishe na ujumla wa nchi za magharibi?

Sijawahi kusema kuwa ujambazi ni uhalifu wa kipuuzi. Hivi ni vitu viwili tofauti. Polisi hawashughulikii ujambazi peke yake bali kila aina ya uvunjaji sheria. Wizi wa kuku kwa kunyemelea kwenye kibanda kwangu mimi si ujambazi. Kulewa na kupiga kelele kupita kiasi kwangu mimi si ujambazi. Kupigana kwa sababu mmelewa kwangu mimi si ujambazi. Kumpiga mtu sachi wakati anapanda daladala kwangu mimi si ujambazi. Kukaa kijiweni na kuvuta bangi kwangu mimi si ujambazi. Kupika gongo kwangu mimi si ujambazi. Kuiba nguo zilizoanikwa kwangu mimi si ujambazi. Kumvizia mwanamke na kumvua hereni kwangu mimi si ujambazi. Kwangu mimi vyote hivi ni uhalifu wa kipuuzi. Na uhalifu wa aina hii kuliko wa majambazi kuvamia benki wakiwa wamebeba smg ndiyo kero kubwa kwa sehemu kubwa ya wananchi. Na hawa vibaka, wauza gongo, walevi mbwa wote tunaishi nao na ni rahisi kutoa taarifa kwa polisi kuhusu vitendo vyao. Lakini mara nyingi hatufanyi hivyo ama kwa sababu hatuwaamini polisi au kwa vile ni ndugu na jamaa zetu. Polisi jamii inalenga huko kutoaminiana kati ya polisi na jamii.

Unazidi kudhihirisha ufinyu wa uelewa wako. Hakuna mahali nimedai kuwa polisi jamii peke yake itadhibiti uhalifu. Au kuwa mahali ambapo uhalifu umepungua ni kwa sababu ya polisi jamii peke yake. Vitu vinachangia kiwango cha uhalifu katika eneo husika. Polisi jamii ni moja ya mikakati ya kujaribu kupunguza matukio ya uhalifu. Polisi jamii haitafanikiwa kama maeneo kama polisi kuhakikisha kuwa uchunguzi dhabiti unafanyika ili wahalifu wanaokamatwa wanapewa hukumu zinazostahili. Polisi jamii haitafanikiwa kama polisi wataonekana wanafanya upendeleo katika utekelezaji wa majukumu yao. Polisi jamii haitafanikiwa kama itaonekana kuwa polisi wanaitumia kuwasukumizia mzigo jamii. Haya yalifanyika katika zoezi zima la sungu sungu ambapo wananchi walitegemewa wafanye doria na kukamata wahalifu! Hii sio kazi yao. Ni kazi ya polisi. Polisi jamii si uvigilante.

Wewe mwanzoni ulipoongelea kwa wenzenu ulianisha ni Uingereza? Kumbe Uingereza ndio polisi wanatembea mitaani kusogoa na Wananchi wakisakanya dodoso za majambazi? Basi Magharibi niliyoiona mimi hilo hakuna! Askari akichoka doria anaenda kula mandazi sukari yenye matobo, ndo sifa waliyonayo, haendi kuvinjari na porojo katini mwa wananchi. Wananchi hawana muda huo barabarani.



Ala, kwa hiyo mwenzetu kwa sababu ulitembelea sehemu moja au mbili za magharibi basi zimekufanya mtaalamu wa utendaji kazi wa polisi katika magharibi nzima? Hata marekani kuna sehemu polisi wanaongea na wananchi. Kuna sehemu ambapo hawaongei na wananchi. Katika State ya Arizona kuna polisi wawili ambao wameshtaki State yao wakipinga sheria mpya dhidi ya wahamiaji haramu, wakisema kuwa itaondoa imani na ushirikiano ambao imewachukua muda mrefu kujenga kati yao na jamii ya kilatino. Hii ni sehemu ya polisi jamii.

Watoto na Wafanya biashara wana kazi pia, hawana mda wa kusogoa na polisi kwenye "beats."! Watalii hawajui majambazi ya jamii, wengi wao ni watembezi wageni. Vikongwe huko kwa wenzenu vingi vinafungiwa ndani ya nyumba za wakunga na si kuzurura kwenye polisi jamii.

Hivi kweli unataka kuniambia huko ulikoenda wananchi wa kawaida hawaongei na polisi? Hawatakiani hali asubuhi. Polisi wanapoenda kununua donats hawaongei na muuzaji wa hizo donats. Na huko hauoni kikongwe mtaani kwa sababu wote wako kwenye nursing homes? Basi badala ya kujificha kwenye euphemisms basi bora utuambia ni wapi huko ulikoona yote hayo ili kama kuna wengine nao waliotembelea huko watueleze kuwa huko watoto hawachezi, wafanya biashara hawaongei na wateja wao na hakuna vikongwe mitaani!
Kwa hiyo "beats" hawakusanyi taarifa za majambazi. Na ulisema "beats" wanasimama kuongea na wananchi. Kumbe maongezi haya ya nini, matokeo ya Azam FC na Yanga? Nini maana ya hizi "beats" na polisi jamii kama hazitusaidii kiuchunguzi? Kwenye kurasa za nyaraka ya polisi uliotubandikia hapa wamesema msingi mmoja wa polisi jamii ni uchunguzi wa siri kung'amua matatizo kwenye jamii, "Intelligence-led identification of community concerns..." Sasa kama hizo "beats" hazikusanyi taarifa zozote basi usizipigiea chapuo kama kielelezo cha polisi jamii.

Sijasema kuwa kazi pekee ya polisi waliokuwa kwenye beat ni kuongea na wananchi. Lakini kwa vile hiyo ni sehemu yake ya kazi na kila siku anakutana na hao wanachi basi bila shaka watatakiana heri na kuongea kidogo kuhusu mechi ya jana. Lakini kama kazi yake ni kuongea tu, hiyo beat yake ataikamilisha vipi? Au watakuwa wanaongea wakati anatembea?

Wigo wa polisi jamii ni mkubwa na unajumuisha polisi walio kwenye beats, polisi walio kwenye vituo, polisi wanaosoma matangazo kwenye redio n.k. Na ndiyo, ni lazima wafanye uchunguzi wao kuhakikisha kuwa taarifa wanazozipata ni za uhakika. Hao askari wa kwenye beats wanaweza kusaidia kupata huo uhakika.

Uchunguzi wa siri au discreet unaweza kufanywa na hao askari walio kwenye beats. Si lazima ufanywe na mashushu. Zote hizi ksudi lake ni kumfanya mwananchi na mali zake wawe salama.

Na ni kielelezo cha utisho wa jambazi kwa raia. Raia anaogopa jambazi ndo maana akimshuhudia yabidi alindwe. Sisi mnatuambia tukashuhudie kichwa kichwa eti majambazi wanatuogopa, tafadhali!

Mimi nazungumzia uhalifu. Si uhalifu wote unafanywa na majambazi. Hata huko Marekani si mashahidi wote ambao wanawekwa kwenye hiyo Witness Protection Program. Jambazi haogopi jamii iliyogawanyika. Vile vile mtu unaweza kushuhudia tukio bila kukusudia, si lazima uingie kichwa kichwa.

Fundi Mchundo, umefanya utafiti kung'amua kwamba wakati wenu "uhalifu wa kipuuzi" ulikuwa chini? Umefanya uchunguzi kugundua kwamba sababu ya tofauti hizo za enzi ni kwa vile mlikuwa mnanyukwa viboko na jirani? Na kama hayo ni kweli, basi inawezekana ni kwa sababu ya kuiga hayo mambo ya "kwa wenzetu." Maana hatuishi kuchambua jambo bila kuiga ya "kwa wenzetu." Halafu "uhalifu wa kipuuzi" ni upi? Tunaongelea ujambazi hapa. Usidogoeshe uzito wa janga la wananchi tafadhali.

Mimi sijasema mabadiliko ni kutokana na kuiga mambo kutoka kwa wenzetu. Hayo ni ya kwako. Mimi nazungumzia uhalifu kwa ujumla wake. Dhana ya polisi jamii inalenga uhalifu wa aina zote na si ujambazi peke yake. Au kwako wewe kazi ya polisi ni kushughulikia ujambazi peke yake?

Sehemu gani, huku kwa wenzetu wapi kaka? Nilidhani ni wenzenu wewe, unanichenjia kibao? Usiwateme wenzenu bana... hahahaaaaaa.

Na hii nayo imetokea wapi? Natumia neno kwa wenzenu kumaanisha nchi za magharibi! Ulitaka nisemaje? Huko kwa wenzangu wakati mimi si mtu wa nchi za magharibi?

Hili somo la mtapanyiko wa ufuatiliaji wa sheria baina ya majimbo na shirikisho la Marekani apa linatusaidia nini? Nilipoongelea FBI ukasema uhalifu mwingi unashughuliwa na "local police." Nikwambia hata FBI nao wanahusika kwa kiasi kikubwa tu. Sasa unasema FBI wanahusika na usafirishaji bangi majimboni, kwani huo sio uhalifu? Kwa nini ulisema nisiwaongelee FBI?

Kwa vile unataka kulazimisha FBI katika mjadala huu basi niambie kama hao FBI wanafanya doria katika maeneo wanayoishi wananchi? Uhalifu unaomgusa mwananchi moja kwa moja mara nyingi unashughulikiwa na local police na sio FBI. Sisi hatuna mfumo wa majimbo kama Marekani kwa hiyo kuingiza mifano ya FBI hapa si mahali pake. Polisi wanaofanana na polisi wetu ni hao local police kama NYPD, LAPD n.k. Hatuna chombo kinachofanana na FBI.

Kama anafanya kazi kitengo cha uhalifu wa silaha Vingunguti anatakiwa aelewe hali na mandhari nzima ya Vingunguti. Atasemaje yeye mgeni wazazi wake wanatoka Magu? Arudi akafanye kazi Magu basi, anakokuelewa. Eti polisi ni wageni, sisi ndio tunajua wezi wa maeneo yetu, nyinyi ndio mnalipwa, mnafundishwa, mna muda, mna nyenzo za kusakanya majambazi, fanyeni kazi yenu.

Huyo polisi unayemzungumzia hata afanye nini hawezi kuijua vingunguti kama mzawa wa vingunguti au mtu aliyekulia au hata yule anayeishi vingunguti. Ndiyo maana anahitaji ushirika wa hawa wote ili aweze kufanya kazi yake kikamilifu.

Kwani daktari anapokuuliza umueleze wapi panapokusumbua ni kuwa hajui kazi yake? Kwa nini basi unapoenda kumuona unamweleza matatizo yako na yeye anakusikiliza na baada ya hapo ndipo anaanza kufanya uchunguzi wake na kukupatia tiba. Daktari yeyote anaujua mwili wa binadamu lakini si kama yule ambaye anasumbuliwa. Vile vile kwa mapolisi. Wanajua nadharia lakini mwananchi aishie mahali husika ndiye anayejua hali halisi. Kuomba ushirikiano wako si kusema kuwa polisi hajui kazi yake! Bila ushirikiano wenu basi tutabaki kuwa wageni. Na mshindi katika hili atakuwa mhalifu.

He! Kwa hiyo Fundi Mchundo unatuambia kwamba majambazi yameshamiri kwa sababu yanakubalika na jamii? Msikieni huyu mja. Kuwageuka? Wanaogopa jamii kuwageuka, ina maana kwa sasa wana jamii wako upande wa majambazi? Tukiwageuka wataacha! Jambazi halitegemei raia awe upande wake, ndo maana linamuua!

Jamii inawasaidia wahalifu kwa kuwafungia macho. Sasa hivi Kingston kunawaka moto kwa vile wananchi hawataki jambazi wao akamatwe.Wakina Escobar waliweza kutamba kwa muda mrefu si kwa sababu walikuwa wakatili bali kwa vile jamii iliwaona kama wafadhili. Hapa kwetu, mganga wa kienyeji anamficha mhalifu kwa vile ni mteja wake. Mzazi anammezea kibaka kwa vile ni mtoto wake n.k. Hawa wote wakiacha tabia ya uvumilivu wahalifu watakosa pa kukimbilia.

Nini tofauti ya polisi posti na vituo vya polisi?

Polisi posti ni kituo kidogo ambacho hakina uwezo wa kumweka mtuhumiwa usiku kucha. Hivi mara nyingi vinajengwa na wananchi kwa kujitolea. Kituo cha polisi ni kituo ambacho kina mahabusu inayoeleweka na polisi wa kutosha kufanya kazi za utawala, doria, uchunguzi n.k. Hivi mara zote vinajengwa na serikali.

Hilo la simu ni kwetu au la "kwa wenzetu"? Tanzania hakuna namba ya polisi ya dharura itakayoleta askari papo hapo. Tulikamata mwizi mtaani miezi michache iliyopita nikapiga simu, polisi walipofika jamaa keshafika kuzima kitambo. Wakaanza kutuhoji sisi kuhusu anaejua ubini wa marehemu. Nikawaambia kwa nini hamkuwahi kuja kumhoji mwenyewe? Zamani tulikuwa na 999, siku hizi tunapewa namba ya mkononi ya Kamanda Kova. Usiwe nje ya mguso.

Wewe unazungumzia hali ilivyo wakati nina zungumzia hali inavyotakiwa kuwa. Mara ngapi mtu umeenda polisi posti kutoa taarifa kuhusu mtu aliyekupiga, polisi akakwambia nenda kamkamate umlete hapa! Ni mara ngapi wananchi wamepiga simu polisi wakaambiwa hawana usafiri, kama wana usafiri basi wawafuate! Yote haya ni mapungufu. Na naamini kinachochangia ni kuwa polisi wamekuwa mamangi meza wakitaka wananchi wawafanyie kazi. Dhana ya polisi jamii ni kuwaweka karibu na wananchi ili wawajibike zaidi. Ili ifanikiwe itatakiwa 999 ifufuliwe na kukarabatiwe. Itabidi wawekeza kwenye kuwekeza kwenye nyenzo zitakazoweza kuwafikisha polisi mapema iwezekanavyo kwenye tukio la uhalifu. Hii itasaidia kupunguza uwezekano wa ushahidi kuharibiwa na wananchi wenye nia njema. Bila kuwekeza hivyo, hiyo polisi jamii itakuwa ndoto tu.

Na akipita atatugongea mlangoni? Kila mtu ana zake mtaani, hakuna mwenye mda kukaa gengeni kusubiri askari apite amweleze matatizo yake. Au kilabuni? Na tunaongelea ujambazi hapa, sio "swala la kawaida" la kusubiri askari apite.

Kwa hiyo kwako wewe polisi kazi yake ni kukabiliana na hicho unachoita ujambazi tu? Akugongee kwa sababu gani wakati wewe ndiye mwenye tatizo? Kama ni majambazi wamekuzingira utapiga simu ili waje wakupe msaada maana hauwezi kutoka nje ukimbilie polisi posti kutoa taarifa ambako unaweza kuwakuta tayari wamekiteka nyara au polisi wa zamu ameenda kwenye nyumba ndogo! Au unataka polisi wanuse na wajue kila panapotaka kutokea ujambazi basi wao watangulie kufika na kuwashughulikia? Uko siriasi kweli?

Kama wananchi hawaogopi SMG majambazi yanawezaje kuweka kitongoji kizima chini ya ulinzi? Umati wa watu wenye mawe unafua dafu kwenye shaba za m-gobole? Sasa unataka kujifanya Kinjekitile mamboleo.

Sijasema wananchi hawaogopi SMG. Nilichosema ni kuwa wakishirikiana na wakichukia vya kutosha hiyo SMG haiwi tishio tena. Bahati mbaya si kila wakati wanashirikiana. Ndiyo maana vibaka wenye visu wanaweza kuzuia njia na kumpora kila apitaye.
Hiyo nyaraka inakuonya kwenye dibaji kwamba usiisome kama kilelezo cha ufanisi wa polisi jamii. Kwa sababu, kwanza, inasema ni picha ya haraka ya mpango majaribio wa awali, na yabidi tusubiri mpango mzima ukamilike ndani ya miaka mitatu; " The report provides a snapshot of the evidence as it stood after the first year of national implementation, and should not be read as a definitive account of whether neighbourhood policing ‘works'. Such an assessment can only be made after the end of the three-year programme, when neighbourhood policing should be implemented in full." Moja, la pili, ripoti inaongelea aina za uhalifu wa huko kwa wenzenu, ambao ni tofauti kabisa na halifu za hapa kwetu. Huwezi niwekea ki-ripoti cha kwa wenzenu wa Liverpool ukadai kitusaidie kuelewa umuhimu wa polisi jamii Vingunguti. Tatu, nipe vielelezo vilivyoandikwa na watafiti huru, sio dondoo ya askari hukusu mafinikio ya mpango wa askari, iliyoandikwa na idara ya askari!

Polisi jamii ni ukingu unaowapa polisi kisingizio wanapolegalega kwenye majukumu yao kulinda raia.

Nilisema kama unataka kujifahamisha zaidi soma. Huu ni mfano mmoja, kuna mingi. Muda wa kukuwekea unachoita kielelezo ambacho hauna uwezo wa kuthibitisha kama ni kweli au sio sina. Kama hujaridhika na yaliyoandikwa hilo ni juu yako. Siwezi kukubadilisha. Na wala sina haja.

Wewe ndo ulisema ni bora ninyamaze, ufikiri wangu mfupi. Sasa unanipa ruhsa ya kusema. Basi ngoja nimalizie kwa kusema "Zidumu Fikra za Fundi Mchundo... Ziduuum"!

Nilisema na bado ninasema kuwa heri unyamaze maana ufinyu wa fikra zako unazidi kuudhiirisha. Sikukukataza kusema. Uhuru huo ulikuwa nao siku zote na sina uwezo wa kuuzia. Nilichotoa ni ushauri tu ambao ni hiari yako kuusikikiliza au kuupuuza. Na kama ufinyu huo wa kufikiri unakufanya useme Zidumu Fikra Sahihi za Fundi Mchundo... basi na iwe hivyo.

Amandla......







 
Hapa Magufuli amnichanganya kabisa na Dhana iliyokuwa Kichwani ya Polisi jamii mpaka nikafikiri sielewi nini maana ya Polisi jamii lakini mwishwe nimegundua kama Ndicho alichosema Basi yeye ndiyo hajui dhana ya Polisi Jamii
 
Hii ni mara ya mwisho kujibishana na wewe. Unanipotezea muda.

Kumbe ulikuwa unabishana? Kweli umepoteza muda, maana mimi naingia hapa muda wangu wa ziada. Ukitaka kuondoka mjadalani huna haja ya kuaga, usije kuwa kama Shy ukenda rudi...
Kumbe una habari za Umar!

Hukutaja unaemzungumzia, ukisema "kijana aliyeficha nanii kwenye nanihii" nani atakuelewa? Vichwa vya habari vya kwa wenzenu huwa si vyote vinakumbukwa kwetu bila ufafanuzi.

Waliomkamata huko hewani walikuwa polisi?...

Kesi ya Umar sio hali halisi ya polisi jamii, hakuna aliyetoa taarifa za siri kuhusu ugaidi kabla ya tukio na kusaidia kuepusha janga. Ukitoa mfano tafuta kesi timilifu inayokusaidia kutushawishi ufanisi wa polisi jamii!

...Wananchi wanakuwa na taarifa za vificho vya wahalifu kabla hata ya polisi kuchungua.
Hilo umelijuaje? Umejuaje wananchi wana taarifa za jambazi ambazo polisi hawana? Usitoe kauli jumla jumla bila msingi. Hicho ndicho kisingizio kinachowapa askari upenyo wa kutupia mzigo wa uwajibikaji kwa wananchi. Sijui kama umewahi kusikiliza mkutano wa waandishi wa habari ya Kova na makamanda wengine wa polisi nchini, kitu cha kwanza na cha mwisho wanachosisitiza ni "wananchi ni jukumu lenu... wananchi ni jukumu lenu..." lakini wao hakuna anaewakalia kooni kudai uwajibikaji wao. Dhana ya polisi jamii sio mtaa wa mwelekeo mmoja, unaenda kote kote. Bahati mbaya unaliangalia swala hili kimgando.

Kusema kuwepo kwa uhalifu katika nchi za magharibi hakuna maana kuwa upo kwa kiwango kama chetu! .. sasa itakuwaje nifananishe na ujumla wa nchi za magharibi?

Hukufananisha?

Mabishano ya "kitaa" ndio yanaishia na ulisema-sikusema, hapa kuna rekodi. Hukusema hivi: "...Kitu kingine usichojua ni kuwa pamoja na wao kuendelea lakini kero za uhalifu ni kama kwetu, mauaji, vibaka, uuzaji wa madawa ya kulevya n.k." Tena kama kawaida ya utashi wako unaanza na "kingine usichokijua..." Unadhani unajua...


...Na uhalifu wa aina hii kuliko wa majambazi kuvamia benki wakiwa wamebeba smg ndiyo kero kubwa kwa sehemu kubwa ya wananchi.

Unaona ulivyo nje ya mguso, unaishi wapi we ndugu? Uhalifu wa kusachiwa ukipanda daladala na upikaji gongo ndio kero kubwa kuliko ujambazi wa kumwaga damu? Kituko mkubwa wewe! Ujambazi wewe unaosoma kwenye tarakishi, wengine unatugongea hodi.Ukikaa hapo unachapisha vituko kama hivyo nakushangaa kama Mtanzania mwenzangu. Kama una ahera-salama "kwa wenzenu" pilipili ya mbali hii haitishii usalama wako, inakuwashia nini?

Hakuna mahali nimedai kuwa polisi jamii peke yake itadhibiti uhalifu. Au kuwa mahali ambapo uhalifu umepungua ni kwa sababu ya polisi jamii peke yake...

Acha kujiruka. Umesema maeneo ambayo polisi anachukiwa na umbea na udadisi wa wengine ni marufuku uhalifu umezidi" Na huko kwa wenzenu, katika maeneo mengi uhalifu wa kipuuzi umepungua sana. Lakini bado kuna sehemu ambako uhalifu bado uko juu. Mara nyingi katika maeneo haya polisi anachukuliwa kama adui na hamna kitu kibaya kama kuwa "snitch". Sasa unaambiwa unyooshe kauli zako unajiruka.

Ala, kwa hiyo mwenzetu kwa sababu ulitembelea sehemu moja au mbili za magharibi basi zimekufanya mtaalamu wa utendaji kazi wa polisi katika magharibi nzima?

Ulijenga hoja kwamba "kwa wenzetu" polisi jamii wanasogoa barabarani na hili na lile, na mpango umefanikiwa. Mimi nikasema Magharibi niliyotembelea mimi hicho kitu hakuna. Wewe hukutaja "kwa wenzenu" ni wapi. Kwa hiyo popote ulipo wewe, na popote nilipotembelea mimi, mwisho wa siku kuna mahala ambapo huo mpango jamii hautumiki, hata kama ni nchi moja. Hivyo inawezekana na kwetu haujitajiki. Upo? Na wewe uliposema "kwa wenzenu" ulimaanisha Uingereza na kwingine wapi?

...Katika State ya Arizona kuna polisi wawili ambao wameshtaki State yao wakipinga sheria mpya dhidi ya wahamiaji haramu, wakisema kuwa itaondoa imani na ushirikiano ambao imewachukua muda mrefu kujenga kati yao na jamii ya kilatino. Hii ni sehemu ya polisi jamii. [/FONT]

Hii ni kesi yenye sura ya siasa za uhamiaji. Hao askari wana uzao wa kigeni, wala lao jambo pia, wakitetea wa Chicano wenzao. Hilo la polisi jamii ni hoja sindikizi. Na hata kama sio, bado hilo dai halijathibithishwa na kukubaliwa na mahakama. Huwezi kutuletea kigecho cha dai la mtu mahakamani. Kwani nikidai hapa kwa kilio kwamba Fundi Mchundo kanitukana fikra zangu fupi ndo inamaanisha ni kweli za kwake ndefu?


Hivi kweli unataka kuniambia huko ulikoenda wananchi wa kawaida hawaongei na polisi? Hawatakiani hali asubuhi. Polisi wanapoenda kununua donats hawaongei na muuzaji wa hizo donats.

Huko polisi aliyevaa sare watamshangaa akionekana kwenye mijumuiko ya soga kitaa. Akisimama kununua andazi sukari hawezi kuanza sogoa na mchuuzi maana mchuuzi hana muda wa kuuza kahawa, mandazi na kusogoa. Huko watu ni wachapa kazi kwa ari, kasi na nguvu. Hawaongezi na simu wala hawasomi Mwanahalisi wakiwa kwenye saa ya bosi. Kwanza ukionekana unasogoa na polisi eneo la kazi bosi atataka kujua kulikoni. Bado hujashawishi ni modeli gani ya polisi jamii ya "kwa wenzenu" ungetaka tugeze.


...Basi badala ya kujificha kwenye euphemisms basi bora utuambia ni wapi huko ulikoona yote hayo ili kama kuna wengine nao waliotembelea huko watueleze kuwa huko watoto hawachezi, wafanya biashara hawaongei na wateja wao na hakuna vikongwe mitaani!

Watoto wanacheza, lakini hawapo barabarani kusogoa na polisi bila walezi karibu, wanafungiwa ndani. Watu wazima wakiongelea uhalifu na polisi hawakutani migahawani, bali ofisi za mchunguzi. Modeli yako bado haieleweki.

... Lakini kama kazi yake ni kuongea tu, hiyo beat yake ataikamilisha vipi? Au watakuwa wanaongea wakati anatembea?

Naam, sasa umeelewa. Huwezi kuwa kwenye "beat" unaongea, na unalinda doria, na unatembea, na unakusanya taarifa. Ukilinda doria unakunja ndita. Ukikusanya taarifa unakaa chini na karatasi. Ukitembea "beat" unaangaza macho. Sasa huyu "beat" huyu kazi yake nini hasa? Ha ahahaaaaa

Wigo wa polisi jamii ni mkubwa na unajumuisha polisi walio kwenye beats, polisi walio kwenye vituo, polisi wanaosoma matangazo kwenye redio n.k..

Hao wanaobaki kwenye vituo huko na wanaokaa pembeni ya redio tulishasema hawako karibu na jamii, si uliwaita mangimeza? Kuna mkanganyiko hapa na hii modeli yako ya polisi jamii. Kipi ni lipi?


Uchunguzi wa siri au discreet unaweza kufanywa na hao askari walio kwenye beats. Si lazima ufanywe na mashushu. Zote hizi ksudi lake ni kumfanya mwananchi na mali zake wawe salama.

Bado modeli yako imechanganyikiwa. Ulisema hawa wa beats hawaweki kipaumbele kwenye uchunguzi: "Wanaofanya uchunguzi wa matukio ya uhalifu mara nyingi si askari wanaokuwa kwenye beats. Uchunguzi unafanywa na askari kanzu (CID)." Unaona unavyochanga sumu?

Mimi sijasema mabadiliko ni kutokana na kuiga mambo kutoka kwa wenzetu. Hayo ni ya kwako. Mimi nazungumzia uhalifu kwa ujumla...

Nilimaanisha hili: Uliongelea utamaduni wa malezi huria ambayo mtoto wa jirani mtukutu siku hizi humgusi. Ukasema hili linaongeza uhalifu. Lakini tamaduni hii imeboboe zaidi huko kwa wenzenu. Huko mtoto mfalme. Kwa hiyo ningedhani kwamba huko ndiko uhalifu ungepita kifani. Lakini unatuambia huko heri. Sasa inakuaje hapo mkuu na hiyo hoja, huoni imepinda?

Natumia neno kwa wenzenu kumaanisha nchi za magharibi! Ulitaka nisemaje? Huko kwa wenzangu wakati mimi si mtu wa nchi za magharibi?

Kwa wenzenu wewe na nani? Mi nitoe, sijui kama hao wa Magharibi ni wenzangu. Wewe ndio umewaita wenzako halafu sasa unawaruka. "Kwa wenzetu wanaita "neighbourhood policing". Hata siku moja si dhana ya kuwakumbatia majambazi." Si wewe huyo? Na kingine, Wa Kambodia au Wahindi si wenzenu? Ningejuaje una maanisha wa Magharibi? Eleweka.


Uhalifu unaomgusa mwananchi moja kwa moja mara nyingi unashughulikiwa na local police na sio FBI.

Unachemsha! Ugaidi haumgusi raia moja kwa moja? Na mara nyingi unashughulikiwa na nani, "local police"? Nani anashughulikia makosa ya sheria la shirikisho la Marekani?

Sisi hatuna mfumo wa majimbo kama Marekani kwa hiyo kuingiza mifano ya FBI hapa si mahali pake. Polisi wanaofanana na polisi wetu ni hao local police kama NYPD, LAPD n.k. Hatuna chombo kinachofanana na FBI.

FBI ni polisi wa Taifa zima, wanatamba nchi zima, wakipulikiza sheria za nchi nzima. TPF ni polisi wa Taifa zima, wanatamba nchi zima, wakipulikiza sheria za nchi nzima. Katika upana, wajibu na mamlaka ya utekelezaji kwa nini nisitumie mfano wa FBI nikiongelea TPF?

Huyo polisi unayemzungumzia hata afanye nini hawezi kuijua vingunguti kama mzawa wa vingunguti au mtu aliyekulia au hata yule anayeishi vingunguti. Ndiyo maana anahitaji ushirika wa hawa wote ili aweze kufanya kazi yake kikamilifu.

Si lazima. Kuna idara za usalama za nchi zilizoendelea kwa kutumia teknolojia, ujasusi na usomi wanafahamu hali, mandhari, watu, ardhi na mali ya Tanzania kuliko wengi wa Watanzania. Wakina Livingston walitoka Ulaya wakaja kutuchorea ramani za vijiji vyetu nasi tumo mumo humo. Na polisi nae afanye ujasusi wake aibue majambazi kwenye mapango yao. Wawe na mafunzo na wajibu wa kuijua jamii yao kinyume nyume, wasitupie mzigo raia.

]...Wanajua nadharia lakini mwananchi aishie mahali husika ndiye anayejua hali halisi. Kuomba ushirikiano wako si kusema kuwa polisi hajui kazi yake! Bila ushirikiano wenu basi tutabaki kuwa wageni. Na mshindi katika hili atakuwa mhalifu.

"Bila ushirikiano wenu," kwani we haumo? Unasikika kama wakimbizi wa "kwa wenzenu" aliye nje ya mguso. Polisi hatakiwi kujua nadharia, anatakiwa ajue hali halisi ya jamii anayofanya kazi. Usimtupie mpira raia.

.. Hapa kwetu, mganga wa kienyeji anamficha mhalifu kwa vile ni mteja wake. Mzazi anammezea kibaka kwa vile ni mtoto wake n.k. Hawa wote wakiacha tabia ya uvumilivu wahalifu watakosa pa kukimbilia.
Ya Kingston na Escobar hayatusaidii hapa wala hayasaidii kujenga hoja yako kwa vile hawa wote wanajulikana na serikali husika. Walioshindwa kushughulika hapa ni serikali, hakuna siri ambayo wananchi wanayo vyombo vya dola havina. Kusema wazazi waripoti watoto wao wote ujambazi utaisha ni mawazo njozi, ya kufikirika. Tusisubiri kila Mama aripoti mtoto wake jambazi, polisi wakamuibue, na kama mzazi anamficha na yeye achukuliwe hatua. Kama mganga wa kienyeji anaeficha jambazi. Usitegemee msaada wa huyo mganga wa kienyeji, na yeye ni sehemu ya jambazi.

Polisi posti ni kituo kidogo ambacho hakina uwezo wa kumweka mtuhumiwa usiku kucha...

Naam, kwa hiyo, kimsingi, hakuna tofauti kati ya kituo kidogo na Kituo cha Polisi inapokuja kwenye polisi jamii, maana hata kituo kikubwa askari anaweza kufanya umangimeza. Mwanzoni ulisema hutaki vituo vidogo unataka vikubwa, wakati mimi naona hivi vidogo navyo vinasogeza askari kwenye jamii, kama ndio polisi jamii. Unaona unavyochanganya habari unapochora modeli ya polisi jamii?

Wewe unazungumzia hali ilivyo wakati nina zungumzia hali inavyotakiwa kuwa. Mara ngapi mtu umeenda polisi posti kutoa taarifa kuhusu mtu aliyekupiga, polisi akakwambia nenda kamkamate umlete hapa! Ni mara ngapi wananchi wamepiga simu polisi wakaambiwa hawana usafiri, kama wana usafiri basi wawafuate! Yote haya ni mapungufu. Na naamini kinachochangia ni kuwa polisi wamekuwa mamangi meza wakitaka wananchi wawafanyie kazi. Dhana ya polisi jamii ni kuwaweka karibu na wananchi ili wawajibike zaidi...

Unakosea tena. Dhana ya polisi jamii - kama inavyotekelezwa kwa sasa - si kuwafanya polisi wawajibike zaidi. Hapana, hapana, hapana. Dhana hii inaweka uzito zaidi katika upande wa utendaji wa mwananchi. Mwananchi atoe taarifa, atoe ushahidi, apige kura za majambazi, afanye hili afanye lile. Ni upolisi wa jamii ya wananchi. Askari wanakwepa uwajibikaji.

Kwa hiyo kwako wewe polisi kazi yake ni kukabiliana na hicho unachoita ujambazi tu? Akugongee kwa sababu gani wakati wewe ndiye mwenye tatizo?

Ujambazi ndio tishio nambari moja la usalama wa raia siku hizi, kama ulikuwa hujui. Unataka tuongelee kupokonywa hereni tu? Na kwa nini asigonge, si umesema "beat" wanatembea tembea mitaani. Hawana mwelekeo maalum, wako "beat."

...Nilichosema ni kuwa wakishirikiana na wakichukia vya kutosha hiyo SMG haiwi tishio tena....

Ukisema wananchi hawachukii SMG vya kutosha unatukana maisha ya raia wanaomwaga damu na ndugu zao waliowaacha. Huo moyo mkavu au nje ya mguso. Binadamu gani hachukii kuonyeshwa mtutu wa Submachine Gun? Kusema wananchi wapambane na ujambazi wa SMG ni kulilinda jeshi la polisi lililolegalega. Polisi wawajibike na ujambazi, sio raia wasio mafunzo, nyenzo, rasilimali wala muda. Polisi wawajibike.


Nilisema kama unataka kujifahamisha zaidi soma. Huu ni mfano mmoja, kuna mingi. Muda wa kukuwekea unachoita kielelezo ambacho hauna uwezo wa kuthibitisha kama ni kweli au sio sina. Kama hujaridhika na yaliyoandikwa hilo ni juu yako. Siwezi kukubadilisha. Na wala sina haja.
Huo "mfano mmoja" ni mbovu! Sikusema uniletee mingi, lakini kama iko mingi, lete mmoja usopinda. Na kama huna haja ya kunibadilisha na, au, huwezi, kwa nini ulijaribu "kubishana"? Kushindwa kunishawishi isiwe sababu ya kusema "sikuwa na haja" kama sungura wa sizitaki mbichi hizi. Mtu mzima unashindwa kuwa na adibu ya kutofautiana?

... Na kama ufinyu huo wa kufikiri unakufanya useme Zidumu Fikra Sahihi za Fundi Mchundo... basi na iwe hivyo.

Wewe si mkweli. Sikusema fikra zako sahihi zidumu. Nilitumia salata kukuonyesha wewe ni nduli wa mawazo unaeshtuka kusikia unatofautiwa na kuishia kushambulia mtu badala ya kudahili yaliyomo. Ndio maana tunasimama wima tukiimbia:

Zidumu Fikra za Fundi Mchundo..... Ziduuum!
 
Wewe si mkweli. Sikusema fikra zako sahihi zidumu. Nilitumia salata kukuonyesha wewe ni nduli wa mawazo unaeshtuka kusikia unatofautiwa na kuishia kushambulia mtu badala ya kudahili yaliyomo. Ndio maana tunasimama wima tukiimbia:

Zidumu Fikra za Fundi Mchundo..... Ziduuum!

Nimeshajieleza vya kutosha na wewe umeeleza unachotaka kueleza. Hata tuendelee kujibishana vipi hatutakubaliana Kwa hiyo kama ulivyosema:

Naam. Zidumu kweli fikra za Fundi Mchundo hata kama sio sahihi!

Nilikuwepo.

Amandla.........
 
Mimi nashangaa kwa nini huyu bwana hachukui fomu ya kuwa rais. Hapa nina maana ya kwamba huyu bwana anatakiwa awe rais wa Tanzania na hapo ndo tunaweza at least kuwa na ndoto ya maisha bora. Namshangaa kikwete kumpa wizara za ajabu ajabu lakini bado twaona mambo anayofanya. Sijui ni kwa nini anaogopa kumpa hata uwaziri mkuu!
 
Back
Top Bottom