Mujumba
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 853
- 306
Zifuatazo ni juhudi zimezofanywa na serikali hii ya awamu ya nne chini ya Rais shupavu Mh.Jakaya Kikwete katika kuleta mapinduzi ya kilimo Tanzania.
Lengo la kwanza: Kuweka misingi ya mapinduzi ya kilimo (Ibara ya 30-33)
UTEKELEZAJI: Kwa kutambua nafasi maalumu ya kimkakati ya sekta ya kilimo katika kukuza uchumi na kupunguza umasikini ,serikali iliyo chini ya chama cha mapinduzi imefanya yafuatayo:
1) Kutayarisha na kuanza utekelezaji wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo (ASDP). Programu hii sasa imehuishwa na kufanyiwa marekebisho na kuiwezesha Nchi yetu kutia saini makubaliano ya programu kabambe ya kuendeleza sekta ya kilimo barani Afrika (COMPREHENCIVE AFRICAN AGRICULTURE DEVELOPMENT PROGRAMME (CAADP)
2) Kutayarisha azma ya kilimo kwanza ambayo kwa sasa imekuwa ni ya mfano duniani.
3) Kuanzisha dirisha la mikopo ya kilimo katika benki ya rasilimali (TIB)
4) Kuanzisha mchakato wa kuanzisha benki ya kilimo.
5) Kuanzisha mfumo wa kutoa ruzuku ya pembejeo kwa kutumia vocha
6) Kufanyika kwa mikutano minne kati ya waziri mkuu na wadau wa sekta ya kilimo kuhusu mifugo, uvuvi na utafiti.
LENGO LA PILI: KUBUNI MPANGO KABAMBE WA KUENEZA MATUMIZI YA PLAU NA ZANA ZA KISASA ZA KILIMO.(Ibara ya 31(b)
UTEKELEZAJI:
1. Matumizi ya majembe ya kukokotwa na ng'ombe yameongezeka kutoka 585240 mwaka 2005/2006 hadi kufikia 819360 mwa ka 2009/2010.
2. Jumla ya matrekta 1737 yaliingizwa nchini yakiwemo makubwa 362 na madogo (power tillers)1379 kwa kipindi cha kuanzia 2006 hadi 2009.
3. Mfuko wa pembejeo za kilimo umeongeza utoaji wa mikopo ya pembejeo za kilimo kutoka shilingi 4.9 mwaka 2005/2006 hadi shilingi bilioni 8.0 mwaka 2009/2010. Kwa wale wenye akili timamu naamini tumeona kuwa ni kwa kiasi gani serikali hii imefanya kazi juu ya suala hili.
Karibuni tujadili bila jazba, matusi wala kejeli
Lengo la kwanza: Kuweka misingi ya mapinduzi ya kilimo (Ibara ya 30-33)
UTEKELEZAJI: Kwa kutambua nafasi maalumu ya kimkakati ya sekta ya kilimo katika kukuza uchumi na kupunguza umasikini ,serikali iliyo chini ya chama cha mapinduzi imefanya yafuatayo:
1) Kutayarisha na kuanza utekelezaji wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo (ASDP). Programu hii sasa imehuishwa na kufanyiwa marekebisho na kuiwezesha Nchi yetu kutia saini makubaliano ya programu kabambe ya kuendeleza sekta ya kilimo barani Afrika (COMPREHENCIVE AFRICAN AGRICULTURE DEVELOPMENT PROGRAMME (CAADP)
2) Kutayarisha azma ya kilimo kwanza ambayo kwa sasa imekuwa ni ya mfano duniani.
3) Kuanzisha dirisha la mikopo ya kilimo katika benki ya rasilimali (TIB)
4) Kuanzisha mchakato wa kuanzisha benki ya kilimo.
5) Kuanzisha mfumo wa kutoa ruzuku ya pembejeo kwa kutumia vocha
6) Kufanyika kwa mikutano minne kati ya waziri mkuu na wadau wa sekta ya kilimo kuhusu mifugo, uvuvi na utafiti.
LENGO LA PILI: KUBUNI MPANGO KABAMBE WA KUENEZA MATUMIZI YA PLAU NA ZANA ZA KISASA ZA KILIMO.(Ibara ya 31(b)
UTEKELEZAJI:
1. Matumizi ya majembe ya kukokotwa na ng'ombe yameongezeka kutoka 585240 mwaka 2005/2006 hadi kufikia 819360 mwa ka 2009/2010.
2. Jumla ya matrekta 1737 yaliingizwa nchini yakiwemo makubwa 362 na madogo (power tillers)1379 kwa kipindi cha kuanzia 2006 hadi 2009.
3. Mfuko wa pembejeo za kilimo umeongeza utoaji wa mikopo ya pembejeo za kilimo kutoka shilingi 4.9 mwaka 2005/2006 hadi shilingi bilioni 8.0 mwaka 2009/2010. Kwa wale wenye akili timamu naamini tumeona kuwa ni kwa kiasi gani serikali hii imefanya kazi juu ya suala hili.
Karibuni tujadili bila jazba, matusi wala kejeli