Tanzania tunaweza tukalisha Robo ya Dunia kama yatafanyika Mapinduzi kwenye Kilimo

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
2,161
1,493
Tanzania ni moja ya Nchi Duniani ambayo imebarikiwa na kila kitu.

Tanzania imebarikiwa Madini ya kila aina, pongezi kubwa kwa Serikali na Wizara ya Madini kwa kuendelea kuwekeza fedha nyingi kwenye utafiti na sasa Madini adimu kabisa ya Lithium yamegunduliwa na utafiti unaendelea.

Tanzania tumebarikiwa ardhi ya kutosha, tumebarikiwa mito ya kutosha, maziwa, Chemchem za kutosha na bahari pia.

Kama yakifanyika mapinduzi ya Kilimo, zao gani ambalo halistawi Tanzania? . Mipango mikubwa ya Kilimo ipelekwe Njombe, Mbeya, Rukwa, Kigoma, etc, ili Kilimo cha kisasa chenye uhakika cha kutokutegemea mvua kikafanyike..

Pengine ni muda sahihi wa kuanza Mipango ya baada ya miaka 20 ijayo kutumia bahari yetu kwa Kilimo. Yes inawezekana, maji ya bahari ikawa chanzo cha maji ya kutumia majumbani, viwandani na mashambani. Kama imewezekana kufanya miradi mikubwa ya SGR, inawezekana kutoa maji ya Bahari kutoka Tanga kwenda Kigoma.

Mwenyezi Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania.
 
kabisa,hajabu serikali inawekeza pesa ndefu kwenye miradi ambayo kupata return ni zaidi ya miaka 50 au zaidi.

wakati pesa hizo zingeelekezwa kwenye kilimo&mifugo ndani ya miaka mitano tu uchumi wa kweli ungestawi.sio huu uchumi wa janjajanja wa kwenye makablasha.
Mpaka ile laana ya mwaka 1967 inayolia ndani ya ardhi ya Tanzania itoke...ndipo tutaweza kufanikiwa.
 
Mkuu Bujibuji Simba Nyamaume hili linahitaji commitment tu walansio siasa.
Unafahamu siasa ina ushawishi kiasi gani kwenye maisha ya kila siku ya mtu wa kawaida?
Sorry, nitakuuliza swali lililo mbali na mada.

Tangu umezaliwa ni magereza mangapi mapya yamejengwa?

Idadi ya watu inaongezeka, mmomonyoko wa maadili unaongezeka kila kukicha, majizi yanaaiba kuanzia serikalini hadi kwenye majumba ya ibada, lakini magereza hayajengwi, unajua kwanini?
 
Nakulaumu kutoa pongezi kwa Serikali...wewe si mkweli....
Kwa kulisha Dunia nakuunga mkono.
Tulikuwa na kitu kinaitwa NAFCO kama yale mashamba yasingekufa leo tungekuwa mbali sana.....kinacho tukwamisha ni laana ya mwaka 1967....
NAFCO...nakumbuka mashamba haya pia kule Mbeya maeneno ya Chimala, Rujewa, Igurusi ilikuwa chanzo cha ajira kikubwa, Serikali inaweza fufua mashamba haya. Bashe anaweza simamia hili
 
Shida hatuna maarifa Wala uchungu na nchi..viongozi wetu wanaangalia matumbo Yao na acc zao za bank kuliko maslahi ya taifa na vizazi vijavyo.

Ardhi washapewa sana mamilioni ya Heka wageni wazungu waarabu Kwa kigezo Cha uwekezaji huku wao viongozi wakinufaika Kwa asilimia Fulani.migodi wanayopewa wageni sio Kwa maslahi mapana ya taifa Bali ya viongozi wale pia wananufaika.
 
Tanzania ni moja ya Nchi Duniani ambayo imebarikiwa na kila kitu.

Tanzania imebarikiwa Madini ya kila aina, pongezi kubwa kwa Serikali na Wizara ya Madini kwa kuendelea kuwekeza fedha nyingi kwenye utafiti na sasa Madini adimu kabisa ya Lithium yamegunduliwa na utafiti unaendelea.

Tanzania tumebarikiwa ardhi ya kutosha, tumebarikiwa mito ya kutosha, maziwa, Chemchem za kutosha na bahari pia.

Kama yakifanyika mapinduzi ya Kilimo, zao gani ambalo halistawi Tanzania? . Mipango mikubwa ya Kilimo ipelekwe Njombe, Mbeya, Rukwa, Kigoma, etc, ili Kilimo cha kisasa chenye uhakika cha kutokutegemea mvua kikafanyike..

Pengine ni muda sahihi wa kuanza Mipango ya baada ya miaka 20 ijayo kutumia bahari yetu kwa Kilimo. Yes inawezekana, maji ya bahari ikawa chanzo cha maji ya kutumia majumbani, viwandani na mashambani. Kama imewezekana kufanya miradi mikubwa ya SGR, inawezekana kutoa maji ya Bahari kutoka Tanga kwenda Kigoma.

Mwenyezi Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania.
Unaota ndoto za alinacha mchana kweupee.

Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa
 
Shida hatuna maarifa Wala uchungu na nchi..viongozi wetu wanaangalia matumbo Yao na acc zao za bank kuliko maslahi ya taifa na vizazi vijavyo.
Ardhi washapewa sana mamilioni ya Heka wageni wazungu waarabu Kwa kigezo Cha uwekezaji huku wao viongozi wakinufaika Kwa asilimia Fulani.migodi wanayopewa wageni sio Kwa maslahi mapana ya taifa Bali ya viongozi wale pia wananufaika.
Majangili yameikamata system vizuri
 
Unafahamu siasa ina ushawishi kiasi gani kwenye maisha ya kila siku ya mtu wa kawaida?
Sorry, nitakuuliza swali lililo mbali na mada.

Tangu umezaliwa ni magereza mangapi mapya yamejengwa?
Idadi ya watu inaongezeka, mmomonyoko wa maadili unaongezeka kila kukicha, majizi yanaaiba kuanzia serikalini hadi kwenye majumba ya ibada, lakini magereza hayajengwi, unajua kwanini?
Majizi yapo kwenye system
 
1967 kulifanyika nini embu toa ukumbosho kwa faida ya wengi?
Watu walinyang'anywa mali zao nyingi zikihusiana na ardhi hasa nyumba mfano.( msajili wa majumba)..mashamba...migodi...viwanda n.k....watu wakamlilia Mungu na miungu pia wakafanya yao....na Mungu ni Mungu wa haki....kwa hiyo hakuna chochote kitakachofanikiwa kwenye ardhi ya 🇹🇿 mpaka hapo utakapofanyika utaratibu wa kuyashughulikia hayo.
 
Back
Top Bottom