Mafanikio kimaisha

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,845
Nini tafsiri yako ya mafanikio (yako) kimaisha kiasi kwamba unaamini kwa kufikia hayo utakuwa umefanikiwa!


crossroads.jpg
 
furaha, amani na upendo...ndio maneno makuu mliyoyagusia Gaijin na JouneGwalu...
mmewahi kufikiria ili kufikia hiyo furaha, amani na upendo mnahitajika kupitia njia gani
ambayo/ambazo unaweza kumbana na vikwazo vya aina kwa aina?

je, mnakabiliana vipi na changamoto hizo...!
 
furaha, amani na upendo...ndio maneno makuu mliyoyagusia Gaijin na JouneGwalu...
mmewahi kufikiria ili kufikia hiyo furaha, amani na upendo mnahitajika kupitia njia gani
ambayo/ambazo unaweza kumbana na vikwazo vya aina kwa aina?

je, mnakabiliana vipi na changamoto hizo...!

Furaha kwangu binafsi inahusisha vitu vinavyogawanyika kwenye mafungu mawili.

1) Nikiwa kwenye uhusiano mzuri na watu ninaowapenda nakuwa na furaha. Na ili niwe kwenye uhusiano mzuri na watu natumia kanuni ya kuwa mkweli ( to be me), kutoingilia maisha ya watu wengine, kuwa mcheshi kwa watu (though sometimes hii huibua tatizo)

2) Huwa na furaha nikiweza kufanya yale yanayonivutia na kunipendeza (hobbies) pamoja na kusambaza furaha kwa wengine (charities and presents). Ili niweze kufika hapo, nahitaji pesa.

Kikwazo kikubwa nafikiri kinakuja kwenye means za kutafuta pesa yenyewe. Mimi nakwenda na kanuni kuwa kazi si kazi unless iwe nafurahia kuifanya hata iwe na mshahara kiasi gani.
 
Ah Mkuu sasa hii imekuwa kama interogation, nldhani tunapeana xperience kwamba na wewe utuambie maono yako!

Ila ok! Kufikia hayo mafanikio kwa kweli ni kuna changamoto sababu ile kuishi na kukutana watu tu ni changamoto tosha sana.
Hivyo mbinu mama ni kujielewa na kujitambua malengo yako, hii itakufanya usipoteze focus.
Kwa mbinu hyo itakufanya uweze kuelewa watu wa aina zote na namna ya kuishi nao, hii itakufanya kupata amani katika mapito unayopitia na vilevile upendo!
Amani na Upendo huzaa furaha ambayo huchochea nguvu ya kupambana
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mi inaonekana siridhiki, na sitakaa nifanikiwe kimaisha (sijui wenzangu), maana;

Mwaka 1995 (form 1); niliamini siku nikiweza kusoma hadi nikafika chuo kikuu cha SUA nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

Mwaka 1998 (form 4); wakati wa kombe la dunia, niliamini siku na mimi nikwa nakaa kwenye nyumba yangu (hata chumba cha kupanga), huku nikiwa na TV yangu naangalia kombe la dunia, nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

Mwaka 2000 (form 6, bado sijafika SUA, sina TV), nikaongeza 'hitaji', kuwa siku nipate kazi, niwe najitegemea nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2002 (first year SUA); niliamini siku nikifanikiwa kuajiriwa kama mwalimu wa chuo kikuu nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2006 (4th yr, SUA); niliamini siku nikiwa na ajira inayonilipa kama laki nne hivi nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2007 (graduating SUA), niliamini siku nikiwa na ajira, nikaoa mke ninayempenda, nikawa na gari aina ya chaser, nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2008 (nimeshaajiriwa, nimeshaoa), niliamini siku nikiwa na mtoto, nikiwa na Masters, nikiwa na ajira nzuri zaidi... nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

Mwaka 2010; ninaamini siku nikiwa na nyumba yangu mwenyewe (ghorofa), kipato cha kutosha niende ninapopenda wakati wowotena mke wangu, nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

2011; ???

2012; ???

n.k ...

Conclusion; Asilimia 99 ya vitu nilivyokuwa natamani hadi 2008 nimeshavipata, lakini kwa sasa najiona niko duni sana kimaisha, natamani, natamani natamani, na natamani niibadilishe Tanzania ifanane na Netherlands (can you imagine?!!)

Nikiwaza watu 'waliofanikiwa' kimaisha (kifedha), wanavyoendelea kufight kutafuta pesa, nikiangalia watu waliofanikiwa kijamii na kisiasa wanavyoendlea kutafuta kufanikiwa zaidi, inabidi niamini hakuna siku nitakokaa 'nifanikiwe kimaisha'

Decision; Nimeamua kuwa nitatumia 60% ya kipato changu 'kuifurahisha nafsi yangu na ya familia yangu na 40% kuwekeza kwa ajili ya baadae, maana nimeshaona kuwa hakuna siku nitakayorizika eti nimeshavuna sasa nianze kula...
 
nadhani definition ya "mafanikio kimaisha" inatofautiana mtu na mtu kwa sababu inakuwa influenced na vitu vingi sana ikiwemo malezi, mazingira mtu aliyokulia, utamaduni wa eneo husika, pamoja na elimu
 
Furaha kwangu binafsi inahusisha vitu vinavyogawanyika kwenye mafungu mawili.

1) Nikiwa kwenye uhusiano mzuri na watu ninaowapenda nakuwa na furaha. Na ili niwe kwenye uhusiano mzuri na watu natumia kanuni ya kuwa mkweli ( to be me), kutoingilia maisha ya watu wengine, kuwa mcheshi kwa watu (though sometimes hii huibua tatizo)

2) Huwa na furaha nikiweza kufanya yale yanayonivutia na kunipendeza (hobbies) pamoja na kusambaza furaha kwa wengine (charities and presents). Ili niweze kufika hapo, nahitaji pesa.

Kikwazo kikubwa nafikiri kinakuja kwenye means za kutafuta pesa yenyewe. Mimi nakwenda na kanuni kuwa kazi si kazi unless iwe nafurahia kuifanya hata iwe na mshahara kiasi gani.

Hayo mawili yanahusiana sana...

Unapotafuta pesa, kuna na mwingine anazitafuta na kuna wakati inabidi m-compete kuzipata na hapo mahusiano yanakuwa compromised. Kwa haraka haraka, zaidi ya 50% ya magomvi kwenye jamii yanahusiana na pesa kwa namna moja au nyingine.... (challenge)...
 
nadhani definition ya "mafanikio kimaisha" inatofautiana mtu na mtu kwa sababu inakuwa influenced na vitu vingi sana ikiwemo malezi, mazingira mtu aliyokulia, utamaduni wa eneo husika, pamoja na elimu

True...
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Hayo mawili yanahusiana sana...

Unapotafuta pesa, kuna na mwingine anazitafuta na kuna wakati inabidi m-compete kuzipata na hapo mahusiano yanakuwa compromised. Kwa haraka haraka, zaidi ya 50% ya magomvi kwenye jamii yanahusiana na pesa kwa namna moja au nyingine.... (challenge)...


Unachoongea kipo, lakini kwangu hadi sasa hakijawahi nikuta....labda ndo kwanza mapema kwenye haya masuala ya kuzisaka faranga
 
MbuKusema ukweli, kufanikiwa kimaisha (being successful) is a very subjective term ambayo mara nyingi huwa pia inategemea na society's standards. Kwa wengine mafanikio au kufanikiwa inamaanisha kuwa responsible, you make more than enough to pay your bills, you're married with children, you have a college degree and you have a prestigious job. Sure, kila mtu atakuangalia na kukudefine kama mtu mwenye mafanikio. Mara nyingi wengi wetu tunaishi kwa jinsi jamii inavyotumould na kujikuta mtu unajihesabu umefanikiwa kwa kuangalia acknowledgement ya wengine kwako kuwa umefanikiwa. Kwamba kwa wewe kujiita mtu aliyefanikiwa ni lazima kuwe na a general acknowledgement kutoka katika jamii, mfano watu wengi tunamwona Mzee Mengi kama mtu mwenye mafanikio sana

Lakini kama alivyosema Gaijin hapo juu……nani alishawahiuliza kama hawa tunaowaona wana mafanikio kama wana furaha, upendo na amani ndani ya mioyo, familia na nyumba zao?


So to me, being successful ni kuweza kuishi maisha yako to the fullest, ukiwa happy, umezungukwa na amani na upendo no matter una pesa kiasi gani, elimu kiasi gani au materials gani. Uwe na amani, upendo na furaha kiasi cha kuweza kufulfil malengo yako uliyojiwekea maishani.

 
m
Unachoongea kipo, lakini kwangu hadi sasa hakijawahi nikuta....labda ndo kwanza mapema kwenye haya masuala ya kuzisaka faranga

Huwa inasikitisha sometimes mtu yuko radhi kuvunja mahusiano kwa ajili ya pesa 'ndogo' kwake... Kwa mfano mtu ana kipato cha zaidi ya laki nne kwa mwezi, lakini yuko radhi agombane hata na mtaa mzima kwa kukataa kuchangia 3000 za kufanya lets say ukarabati kwenye mtaro wa maji machafu hapo mtaani!
 
MbuKusema ukweli, kufanikiwa kimaisha (being successful) is a very subjective term ambayo mara nyingi huwa pia inategemea na society's standards. Kwa wengine mafanikio au kufanikiwa inamaanisha kuwa responsible, you make more than enough to pay your bills, you're married with children, you have a college degree and you have a prestigious job. Sure, kila mtu atakuangalia na kukudefine kama mtu mwenye mafanikio. Mara nyingi wengi wetu tunaishi kwa jinsi jamii inavyotumould na kujikuta mtu unajihesabu umefanikiwa kwa kuangalia acknowledgement ya wengine kwako kuwa umefanikiwa. Kwamba kwa wewe kujiita mtu aliyefanikiwa ni lazima kuwe na a general acknowledgement kutoka katika jamii, mfano watu wengi tunamwona Mzee Mengi kama mtu mwenye mafanikio sana

Lakini kama alivyosema Gaijin hapo juu……nani alishawahiuliza kama hawa tunaowaona wana mafanikio kama wana furaha, upendo na amani ndani ya mioyo, familia na nyumba zao?


So to me, being successful ni kuweza kuishi maisha yako to the fullest, ukiwa happy, umezungukwa na amani na upendo no matter una pesa kiasi gani, elimu kiasi gani au materials gani. Uwe na amani, upendo na furaha kiasi cha kuweza kufulfil malengo yako uliyojiwekea maishani.


Mwanajamii

Si hayo tu, tunaweza kumuona Mengi amefanikiwa kwa standards zetu sisi lakini yeye mwenyewe akadhani hajafanikiwa hata kidogo, na ndo kwnza anasaka mafanikio (hatujui targets zake ni nini)
 
Tuko,good analysis. Kuna ndoto tumeota tukiwa watoto,some of them tumezipata tukagundua it was nt such a big deal. Mwisho wa siku u lead ur heart and follow through. Nakubaliana na mwl pia.kuwa na amani na upendo ndo mafanikio muhimu kuliko yote kwangu,japo kuna basic materials ambazo zisipokuwepo amani inatetereka.hata kama itabidi mie kushuka ama kupunguza priority zangu ili amani iwepo nitajisikia kufanikiwa
 
Furaha kwangu binafsi inahusisha vitu vinavyogawanyika kwenye mafungu mawili.

1) Nikiwa kwenye uhusiano mzuri na watu ninaowapenda nakuwa na furaha. Na ili niwe kwenye uhusiano mzuri na watu natumia kanuni ya kuwa mkweli ( to be me), kutoingilia maisha ya watu wengine, kuwa mcheshi kwa watu (though sometimes hii huibua tatizo)

2) Huwa na furaha nikiweza kufanya yale yanayonivutia na kunipendeza (hobbies) pamoja na kusambaza furaha kwa wengine (charities and presents). Ili niweze kufika hapo, nahitaji pesa.

Kikwazo kikubwa nafikiri kinakuja kwenye means za kutafuta pesa yenyewe. Mimi nakwenda na kanuni kuwa kazi si kazi unless iwe nafurahia kuifanya hata iwe na mshahara kiasi gani.

...ahsante sana gaijin kwa ufafanuzi wako...dahhh,....angalau nakuangalia kwa jicho la afadhali yako unayejua dira ya maisha yako..hongera sana...
 
Ah Mkuu sasa hii imekuwa kama interogation, nldhani tunapeana xperience kwamba na wewe utuambie maono yako!

Ila ok! Kufikia hayo mafanikio kwa kweli ni kuna changamoto sababu ile kuishi na kukutana watu tu ni changamoto tosha sana.
Hivyo mbinu mama ni kujielewa na kujitambua malengo yako, hii itakufanya usipoteze focus.
Kwa mbinu hyo itakufanya uweze kuelewa watu wa aina zote na namna ya kuishi nao, hii itakufanya kupata amani katika mapito unayopitia na vilevile upendo!
Amani na Upendo huzaa furaha ambayo huchochea nguvu ya kupambana

hapana kaka, usikwazike ni katika kusaidiana kupanua wigo wa ufahamu...
ahsante kwa majibu yako ya nyongeza...nitaweka mtazamo wangu kwa post inayofatia..
 
Mbu kila mmoja anaishi maisha yake.. na yaweza onekana kama ni swali rahisi saana. But kimsingi ukifikiria kwa mapana saaana waweza kuta one akashindwa kabisa kujua hasa kitu gani chaweza define mafanikio yake... Nakubaliana na Tuko... Yale ambayo twapenda yana vary saaana tokana na wakati na Umri pia... Lakini ningependa nisisiteze kua kuna wakati ukifika kile ambacho ungependa upate ili uonekane una mafanikio husimama unapo fika ukubwani hasa utu uzima....

Enways naamini kua Mafanikio ambayo mtu mzima hutaka saana ama kutarajia yapo consistent kwa mda mrefu. IMO Upendo tena upendo wa kweli na dhati ndani ya familia yangu, kati ya familia za wanandugu na watu wanizungukao i.e jamaa na marafiki - Upendo ni moja ya kitu ya msingi saana kwani mara nyingi saana huzaa Amani. Na sehemu yoyote ile yenye Amani kuna furaha....

Mafanikio yangu naamini kabisa yatakua fullfilled pale watoto wangu watapokua watu wazima na good people in the society... Ndio kuna vimakosa vya kibinadamu lakini yalo msingi wazingatie, Wawe na elimu nzuri, wawe na upendo, wawe watu wema katika jamii... Kwamba hata niwe proud kusimama mbele za watu na kusema "Yule ni Mwanangu" wawe na ubinadamu - for jamii imeharibika saana and i am so scared for them and what the future holds for them... Namuomba Mungu kila siku ili at the end wawe wanadamu wanaofaa kua wanadamu... Ikifika hapo i believe nitajiona mwenye mafanikio saana.

However mimi kwangu Pesa nayo ni muhimu saana katika kuwezesha furaha na Amani... Nimeona saana tena the hard way kua familia/ndugu na jamaa waweza kua na Upendo But pesa ndo ikawa chanzo cha kufutika hayo yoote. Napenda kua hata kama wakaribu yangu hana pesa ndefu, ana pesa yakuweza mtosheleza mambo na shughuli zooote za msingi bila kukwama.... Naweza onekana kama sifai na pesa sio muhimu... Lakini mie siamini hilo....
 
QUOTE=Mbu;2691525]
hapana kaka, usikwazike ni katika kusaidiana kupanua wigo wa ufahamu...
ahsante kwa majibu yako ya nyongeza...nitaweka mtazamo wangu kwa post inayofatia..
[/QUOTE]

Pamoja mkuu, nlikuwa nakuchombeza tu nipate neno lako!

Nimependa sana Tuko alivyodadavua akianzia toka primary hadi sasa.
Kwa mtu mzima yeyote uliye na fikra ni lazima ujiwekee malengo toka hatua hadi hatua na ukijilinganisha na mazingira, hyo kweli inakufanya kila hatua unayokanyaga upate hamu ya kukanyaga na kukunjua hatua nyingine.
Hivyo tena ni kweli swali la "mafanikio" linakuwa tata sababu jibu lake lazima liwe "ndiyo" na "hapana". Sababu hata kuwa hai tu ni sehemu ya mafanikio
 
Back
Top Bottom