Mafanikio kimaisha

Mi inaonekana siridhiki, na sitakaa nifanikiwe kimaisha (sijui wenzangu), maana;

Mwaka 1995 (form 1); niliamini siku nikiweza kusoma hadi nikafika chuo kikuu cha SUA nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

Mwaka 1998 (form 4); wakati wa kombe la dunia, niliamini siku na mimi nikwa nakaa kwenye nyumba yangu (hata chumba cha kupanga), huku nikiwa na TV yangu naangalia kombe la dunia, nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

Mwaka 2000 (form 6, bado sijafika SUA, sina TV), nikaongeza 'hitaji', kuwa siku nipate kazi, niwe najitegemea nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2002 (first year SUA); niliamini siku nikifanikiwa kuajiriwa kama mwalimu wa chuo kikuu nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2006 (4th yr, SUA); niliamini siku nikiwa na ajira inayonilipa kama laki nne hivi nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2007 (graduating SUA), niliamini siku nikiwa na ajira, nikaoa mke ninayempenda, nikawa na gari aina ya chaser, nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha

Mwaka 2008 (nimeshaajiriwa, nimeshaoa), niliamini siku nikiwa na mtoto, nikiwa na Masters, nikiwa na ajira nzuri zaidi... nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

Mwaka 2010; ninaamini siku nikiwa na nyumba yangu mwenyewe (ghorofa), kipato cha kutosha niende ninapopenda wakati wowotena mke wangu, nitakuwa nimefanikiwa sana kimaisha...

2011; ???

2012; ???

n.k ...

Conclusion; Asilimia 99 ya vitu nilivyokuwa natamani hadi 2008 nimeshavipata, lakini kwa sasa najiona niko duni sana kimaisha, natamani, natamani natamani, na natamani niibadilishe Tanzania ifanane na Netherlands (can you imagine?!!)

Nikiwaza watu 'waliofanikiwa' kimaisha (kifedha), wanavyoendelea kufight kutafuta pesa, nikiangalia watu waliofanikiwa kijamii na kisiasa wanavyoendlea kutafuta kufanikiwa zaidi, inabidi niamini hakuna siku nitakokaa 'nifanikiwe kimaisha'

Decision; Nimeamua kuwa nitatumia 60% ya kipato changu 'kuifurahisha nafsi yangu na ya familia yangu na 40% kuwekeza kwa ajili ya baadae, maana nimeshaona kuwa hakuna siku nitakayorizika eti nimeshavuna sasa nianze kula...

...ni kama vile ulikuwa mawazoni mwangu wakati naitengeneza thread hii...

mwanzoni, nilifikiria kuipa title life starts at 40....kisha nikafikiria mitazamo tofauti ya watu itakinzana na ninachokitafuta.
kiukweli, hayo yote uliyoyaorodhesha hapo juu ni sahihi kabisa....
  • inaonekana mtazamo wako kwa kiwangi kikubwa unalingana na mimi. Nitakupa mfano;
  • kwa umri wangu (40) tayari nishaonja matamu na machungu ya mapenzi, ndoa na talaka
  • kwa umri wangu, tayari watoto wote weshamaliza GCSE wote wapo college na universities
  • kwa umri wangu, "i live my dream"...my dream job na maisha overseas
  • kwa umri wangu, na freedom ya movement popote pale ulimwenguni (nikitaka!)
  • kwa umri wangu, na SWOT analysis...am secured kimaisha sababu ya investments za hapa na pale iwapo nitazi manage vizuri.
tatizo linakuja, bado najihisi kuna kitu muhimu kinakosekana maishani mwangu...kiasi najiuliza mafanikio ni kitu gani hasa!
who said life starts at 40?
 
Mhhh mkuu Mbu
Safari ya maisha bado ndefu sana na haina mahali utasema hapa nimefikia mwisho.
Hata safari yangu ya maisha japo nina vitu basic ambavyo ni vya muhimu kwa maisha bado natamani hiki na kile
Bado natamani niwe na kile na kile na hiki na hiki
Kweli maisha ni safari na sidhani kama nitafikia sehem ambako nitasema hapa nimefikia kilele cha mafanikio.
 

...ahsante sana gaijin kwa ufafanuzi wako...dahhh,....angalau nakuangalia kwa jicho la afadhali yako unayejua dira ya maisha yako..hongera sana...

Mbu

kujua dira na kuweza kuifuata ni vitu viwili tofauti. Sometimes unakuwa influenced na vitu vyengine na kukutoa kwenye njia uliyojiwekea
 
nadhani definition ya "mafanikio kimaisha" inatofautiana mtu na mtu kwa sababu inakuwa influenced na vitu vingi sana ikiwemo malezi, mazingira mtu aliyokulia, utamaduni wa eneo husika, pamoja na elimu

...umesema vyema.

sasa utawezaje kuyachanganya hayo yote kuweza kufanikisha maisha yako?
 
It is a whole list, that changes from time to time... but the core ideas are to be happy, to give happiness to people around me and to satisfy the material needs so I can focus on the inner ones. wewe je?
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Naungana mkono na wengi walofatia, amani na furaha ya moyo ndio mafanikio makubwa ingawa samtaimu tunatamani vile ambavyo tunahisi vitalutuletea amani kumbe badala yake vinatuongezea migogoro.

Hapa nitoe mfano wa maselebriti ambao kikawaida wanaufurahia uselebriti wao mwanzoni kwa kuona wamefanikiwa, lakini skendo zikiwaandama wanaanza kuuchukia huo huo uselebriti wao walioudefine kama ni mafanikio earlier.

Mimi mafanikio yangu ni amani ya moyo na amani yangu mara nyingi inaletwa na kukubalika kwangu kwa jamii ilionizunguka.

Mkuu Mbu nimeandika haraka haraka aisee nawahi kumshuhudia Manu anavyosulubiwa.
 
I learned this from my boss,leaving my 2nd job for the 3rd. 'Money will never be enough,I'm still having financial issues', wakati huo salary yake ni 10x wa kwangu. I ddnt blv him then,bt I almost am. The more the money,the more the needs.it is nt worth loosing what is worth for money
m

Huwa inasikitisha sometimes mtu yuko radhi kuvunja mahusiano kwa ajili ya pesa 'ndogo' kwake... Kwa mfano mtu ana kipato cha zaidi ya laki nne kwa mwezi, lakini yuko radhi agombane hata na mtaa mzima kwa kukataa kuchangia 3000 za kufanya lets say ukarabati kwenye mtaro wa maji machafu hapo mtaani!
 
Mkuu Mbu kingine zaidi ya material things ni amani ndani ya moyo na kwa familia yangu. Nikae nikiwa na amani na furaha katika maisha hata kama sina chochote ila nina amani
Hilo ndo la muhimu maana ukiwa na amani haya mengine yanakuja taratibu and kama tulivyo wapambanaji naamini furaha ya moyo itanipa kile ninachokitaka
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
...umesema vyema.

sasa utawezaje kuyachanganya hayo yote kuweza kufanikisha maisha yako?

nadhani Mbu ni suala la kuangalia nini zaidi kimeku influence katika kudefine mafanikio yako kimaisha na iwapo hicho kilicho ku-influence kinajitosheleza, kinahitaji kurekebishwa au kinahitaji kufutwa na kuchukuliwa chengine, au kuchanganya kuwa mix fulani

Mfano unaweza kukuta mtu kwa jamii yake kufanikiwa ni kuwa na wake wanne, na kula chakula marosti kila siku, na yeye akaamini vile, lakini asiwe na furaha akipata mafanikio yale.

Au mtu mwengine ameambiwa na kuamini kuwa kufanikiwa ni kuishi Ulaya lakini anapofika kule akajikuta hana furaha na akajiongeza stress zaidi kwa kujishangaa kwa nini haridhiki.


kwa hiyo nadhani ni kuzichanganya influence ukatafuta a right balance for you
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
MbuKusema ukweli, kufanikiwa kimaisha (being successful) is a very subjective term ambayo mara nyingi huwa pia inategemea na society’s standards. Kwa wengine mafanikio au kufanikiwa inamaanisha kuwa responsible, you make more than enough to pay your bills, you're married with children, you have a college degree and you have a prestigious job. Sure, kila mtu atakuangalia na kukudefine kama mtu mwenye mafanikio. Mara nyingi wengi wetu tunaishi kwa jinsi jamii inavyotumould na kujikuta mtu unajihesabu umefanikiwa kwa kuangalia acknowledgement ya wengine kwako kuwa umefanikiwa. Kwamba kwa wewe kujiita mtu aliyefanikiwa ni lazima kuwe na a general acknowledgement kutoka katika jamii, mfano watu wengi tunamwona Mzee Mengi kama mtu mwenye mafanikio sana

Lakini kama alivyosema Gaijin hapo juu……nani alishawahiuliza kama hawa tunaowaona wana mafanikio kama wana furaha, upendo na amani ndani ya mioyo, familia na nyumba zao?


So to me, being successful ni kuweza kuishi maisha yako to the fullest, ukiwa happy, umezungukwa na amani na upendo no matter una pesa kiasi gani, elimu kiasi gani au materials gani.
Uwe na amani, upendo na furaha kiasi cha kuweza kufulfil malengo yako uliyojiwekea maishani.

...umezungumza mambo ya msingi sana mwj1...

mzee wangu bw mengi namjua mapungufu yake maskini,...acheni tu ajifaidie pesa zake mzee wa watu...ametokea mbali,
bahati mbaya ndio hivyo tena, maisha sio kama vile tunataka yawe...

nisingependa kumjadili mtu, ila nitagusia tu kwamba pamoja na mafanikio yote, failed marriage, losing a dear son,
na mengineo ya hapa na pale pia ni disappointments ambazo kwa kiwango kikubwa zina athari kwenye
mafanikio ya mtu... au?

hilo la amani na upendo kiasi cha kufulfil malengo uliyojiwekea inapingana na ile hoja ya mafanikio ya mtu kwenye jamii zetu yanatokana na muonekano wako wa nje.

hudhani hilo litakupelekea kuwa "a slave" of your own success?..mfano; Michael Jackson pamoja na kutufurahisha mamilioni ya watu tangu miaka ya 70's kwa cheza kwa stepu...kumbe mwenzetu alikuwa hawezi kulala bila chloroform, like wise kwa kina Elvis Presley, nk...
 
Hii thread inanisaidia sana kupanua wigo wa uwezo wangu wa kufikiri. Aksante Mbu kwa kuileta na aksante Gaijin na wachangiaji wengine.

Gaiji umezungumzia aspect ya mahusiano. Nadhani happiness inafall pia kwenye hiyo aspect na vile vile success kwenye angle hiyo inatofautiana kwa mtu na mtu.

Kwa upande wangu, mafanikio kwa upande huu ni kuwa na mahusiano mazuri (nikimaanisha kimapenzi zaidi) kwani naelewa hii huchukua sehemu kubwa ya maisha ya binadamu. Pamoja na kuwa na mwenza anayekuthamini, kujali na kukupenda but awe pia ni mwenza niliyempenda for who he is and not what he can give or make me..............na mwenza huyo akalitambua hilo na kulithamini. Si kuwa na mtu anayehisi kuwa you are after something from him, kitu ambacho kinawezasababisha akaabuse love yako. Na itakapotookea kuwa sijabahatika kumpata mtu wa aina hii haimaanishi sitojihesabu myself as successful kwa sababu nitajiaminisha kuwa at least I tried. I will sit down na kumshukuru MUNGU kuwa haya ndio maisha alonipangia so yasi-get into my way ya kujiona mwenye mafanikio.
 
Mhhh mkuu Mbu
Safari ya maisha bado ndefu sana na haina mahali utasema hapa nimefikia mwisho.
Hata safari yangu ya maisha japo nina vitu basic ambavyo ni vya muhimu kwa maisha bado natamani hiki na kile
Bado natamani niwe na kile na kile na hiki na hiki
Kweli maisha ni safari na sidhani kama nitafikia sehem ambako nitasema hapa nimefikia kilele cha mafanikio.



Rocky are you saying kua mpaka hapo ulipo bado kabisa hujapata hata kijihisia kua kitu fulani ama mahala fulani ndo utaona umefanikiwa??
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
peace of mind is everything to me

Mkuu Mbu mie nakubaliana na Aminata9, unaweza kujaliwa kuwa na material things za kila aina ikiwemo pesa, nyumba ya haja, kazi nzuri unayoipenda na yenye mshahara na marupurupu mazuri na gari/ magari ya haja lakini bado ukakosa raha moyoni kwa sababu moja au nyingine.

Angalia kule Hollywood ambako watu wengi wa kule wamejaliwa kila kitu lakini asilimia kubwa unakuta maisha yao wengi wao yamejaa migogoro ya aina mbali mbali na hivyo kusababisha hata ndoa za nyingi zisiwe za muda mrefu na mafanikio.

 
Last edited by a moderator:


Angalia kule Hollywood ambako watu wengi wa kule wamejaliwa kila kitu lakini asilimia kubwa unakuta maisha yao wengi wao yamejaa migogoro ya aina mbali mbali na hivyo kusababisha hata ndoa za nyingi zisiwe za muda mrefu na mafanikio.

BAK suala moja la kujiuliza, ndoa za kwetu Tanzania ni za mafanikio kwa sababu wote wawili wako happy kwenye ndoa au kwa kuwa watu wanauvumilivu tu?

Sidhani kama takwimu za talaka pekee zinaweza kuonyesha mafanikio au uwepo wa peace of mind
 
Tuko,good analysis. Kuna ndoto tumeota tukiwa watoto,some of them tumezipata tukagundua it was nt such a big deal. Mwisho wa siku u lead ur heart and follow through. Nakubaliana na mwl pia.kuwa na amani na upendo ndo mafanikio muhimu kuliko yote kwangu,japo kuna basic materials ambazo zisipokuwepo amani inatetereka.hata kama itabidi mie kushuka ama kupunguza priority zangu ili amani iwepo nitajisikia kufanikiwa

king'asti umesema la maana sana...the higher we climb the harder we fall...!
unajua, nikiwa nje ya jiji hasa dar....huwa nawa admire furaha yao hawa wenzetu wanaoishi
maisha ya kijijini...

wakishajitosheleza kwa mazao na mifugo tu...wanaonekana 'hawana' presha nyingine za maisha.


tanz+village+to+dar.jpg
...correct me if am wrong, otherwise i bet am going nutter huh!
 

...umezungumza mambo ya msingi sana mwj1...

mzee wangu bw mengi namjua mapungufu yake maskini,...acheni tu ajifaidie pesa zake mzee wa watu...ametokea mbali,
bahati mbaya ndio hivyo tena, maisha sio kama vile tunataka yawe...

nisingependa kumjadili mtu, ila nitagusia tu kwamba pamoja na mafanikio yote, failed marriage, losing a dear son,
na mengineo ya hapa na pale pia ni disappointments ambazo kwa kiwango kikubwa zina athari kwenye
mafanikio ya mtu... au?

hilo la amani na upendo kiasi cha kufulfil malengo uliyojiwekea inapingana na ile hoja ya mafanikio ya mtu kwenye jamii zetu yanatokana na muonekano wako wa nje.

hudhani hilo litakupelekea kuwa "a slave" of your own success?..mfano; Michael Jackson pamoja na kutufurahisha mamilioni ya watu tangu miaka ya 70's kwa cheza kwa stepu...kumbe mwenzetu alikuwa hawezi kulala bila chloroform, like wise kwa kina Elvis Presley, nk...

Ni kweli kabisa Mbu kuwa Mengi wengi hatumjui na kama alivyosema Gaijin inaezekana sie tukamwona ni mtu mwenye mafanikio kumbe yeye kwake bado anajiona ndo kwanza hajafika kwenye Main road, bado yuko kwenye feeder road.

Kiwango cha malengo mtu ajiwekeayo hutokana na SWORT analysis yake mwenyewe. Iwapo unajiona uko katika hali ya kai basi huweziweka malengo ya mtu aliye katika kiwango cha juu. So ujipangie malengo kwa kadri. Mimi Furaha, amani na upendo ndivyo vinavyoniguide maishani.....I dont care Mzee ananicategorise vipi (Inauma but sitokuwa na jinsi) sucessiful au looser ilimradi am happy, nina amani na upendo (haijalishi unatokea upande gani) but naamini anayewezanipatia upendo ni mtu yoyote si lazima awe ndugu.

Ni ngumu nakubali but inabidi tufike sehemu tukubali kudifferentiate malengo ya mtu binafsi na yale anayotazamiwa ayafanye na jamii yake. Ninaamini katika mazishi yangu hakuna atakayenikumbuka kama Marehemu alokuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa nilikuwa na kampuni au kiwanda but nitakumbukwa kwa namna ntakavyokuwa na uwezo wa kuigusa mioyo yao kwa upendo, ucheshi na huruma nilizojaaliwa.
 
The whole trick is in balancing. Don't chew more than u can bite,no matter how tempting it looks

The thing is sometimes you don't know your strength.

Labda nikijipangia mafanikio ni lazima niwe na kampuni yangu yenye kutoa ajira kwa watu walau 50 ninaweza kufika huko lakini kama sijajiwekea hayo malengo naweza wala nisihangaike kufika. Kwa hiyo kuwa too cautious nayo inaweza kukuondolea fursa za kufanya makubwa zaidi (kupata mafanikio makubwa?!?)
 
Hii thread inanisaidia sana kupanua wigo wa uwezo wangu wa kufikiri. Aksante Mbu kwa kuileta na aksante Gaijin na wachangiaji wengine.

Gaiji umezungumzia aspect ya mahusiano. Nadhani happiness inafall pia kwenye hiyo aspect na vile vile success kwenye angle hiyo inatofautiana kwa mtu na mtu.

Kwa upande wangu, mafanikio kwa upande huu ni kuwa na mahusiano mazuri (nikimaanisha kimapenzi zaidi) kwani naelewa hii huchukua sehemu kubwa ya maisha ya binadamu. Pamoja na kuwa na mwenza anayekuthamini, kujali na kukupenda but awe pia ni mwenza niliyempenda for who he is and not what he can give or make me..............na mwenza huyo akalitambua hilo na kulithamini. Si kuwa na mtu anayehisi kuwa you are after something from him, kitu ambacho kinawezasababisha akaabuse love yako. Na itakapotookea kuwa sijabahatika kumpata mtu wa aina hii haimaanishi sitojihesabu myself as successful kwa sababu nitajiaminisha kuwa at least I tried. I will sit down na kumshukuru MUNGU kuwa haya ndio maisha alonipangia so yasi-get into my way ya kujiona mwenye mafanikio.

...umenigusa kwenye jambo la muhimu sana maishani mwangu.
nadhani binafsi katika kitu muhimu kinachokosekana maishani mwangu kuweza ku justify
mafanikio ya maisha yangu ni mwenza wa aina hiyo....pheewww!

mwj1 tuoane basi, nipo tayari kukuombea talaka kwa mumeo...lol!
 

...umenigusa kwenye jambo la muhimu sana maishani mwangu.
nadhani binafsi katika kitu muhimu kinachokosekana maishani mwangu kuweza ku justify
mafanikio ya maisha yangu ni mwenza wa aina hiyo....pheewww!

mwj1 tuoane basi, nipo tayari kukuombea talaka kwa mumeo...lol!

Kwani Mbu uliweka kwenye mafanikio yako parameter hiyo? lol

Kama hujaweka si haihusu? au ndio ile unakuwa umejiwekea lakini hujijui :[
 
Back
Top Bottom