Maelezo binafsi ya Mhe. Zitto Zuberi Kabwe dhidi ya tuhuma za rushwa kwa Umma

mkiandika ZZK nakumbuka Zana Za Kilimo... kumbe mnamaanisha Zitto Zuberi Kabwe.... kwa sasa sina la kusema nasubiri nichanganye na zangu then nifanye conclusion..
 
1. Re: Zitto: Sijahongwa, ni siasa za urais na hasira za posho!

Hekima inanikumbusha katika historia ya wana wa Israeli na kisa cha wao kuingia na kukaa nchini Misri. Alikuwa ni nabii Yusuph juu yake iwe rehema na amani aliyechukiwa na ndugu zake. Wakafanya fitina kubwa ya kukamia na kutaka kumuua. Azma yao ilipotimia Mwenyezi Mungu akamuokoa. Ikaja suala la kutaka kubakwa na mke wa bwana wake kwa sababu ya uzuri wake usiomithilika. Akakimbia nje na mwanamke akamchana kanzu yake kwa nyuma. Ghafla bwana mwenye nyumba akawa anaingia na kukutana na sekeseke hilo. Mara yule mwanamke akamsingizia Yusuph uongo na kusema; "Hakuna malipo ya mtu anayetaka kumbaka mkeo isipokuwa jela". kitoto kidogo kikamsafisha Yusuph na kusema; ikiwa kanzu ya yusuph imechanwa mbele basi yusuph ana makosa, na ikiwa imechanwa nyuma basi yusuph ni msafi na mwanamke ana makosa".
Mzee akaona kuzima soo bora ampeleke jamaa jela.
Huko jela akawabashiria waota ndoto juu ya yatakayowatokea na ikaja kuwa kweli. Yule jamaa aliyepandisha cheo akaombwa amkumbuke katika ufalme lakini kama ilivyokawaida ya binadamu - kuhukumu mtu kwa ubaya na kusahau mema yake yote, yule jamaa kampotezea. Uzalendo wake wote, ukweli wake wote na uadilifu wake wote ukawa sio kitu bali na kejeli juu.
Zama zikapita na Ikaja wakati mfalme wa wakati huo akaota ndoto iliyoashiria miaka ya neema na tabu. waganga na makuhani wakaitwa na wote wakashindwa kukokotoa ndoto ile. Wakasema hizo ni ndoto zilizoparaganyika. Mshikaji kakumbuka yule jamaa wa gerezani aliyemsaidia kupata cheo.
Nabii Yusuph akaitwa na kukokotoa ndoto ile na a asema ni YEYE PEKEE AMBAYE ANAWEZA KUSIMAMIA ILE KAZI YA KUKUSANYA MAVUNO KWA MIAKA SABA ili iwafae kipindi cha miaka saba ya shida. Mfalme AKAMKABIDHI KAZI ILE NA AKAIFANYA KWA USTADI. Mfalme hakuangalia UMRI wa kijana Yusuph bali AZMA na Uwezo wa kiakili.
Sharti la kwanza aliloweka Yusuph ili kukubali kazi ya uweka hazina ni kuwa aletwe yule mama aliyetaka kumbaka ili athibitishe ni nani aliyekuwa mkosaji. Yule mama (mzee sasa na aliyepoteza nuru ya macho) akakiri kuwa alimpenda sana yusuph kinyume na matakwa yake kiasi cha kushindwa kujizuia.
Baada ya hapo Mwenyezi Mungu akamrudishia nuru na macho yule mama na akamfanya mzuri (KIGORI) na akaja kuwa ndiye MKEWE YUSUPH.

HALELUYA!!!!!!!!!!!

My stance: HEKIMA HUPEWA WACHACHE.


Nimeingia leo JF kwa ajili ya post yako maridhawa, umemeliza kila kitu, salaam kwa Matola na wale wote walo ktk upofu, Zito hana wa kumfikia CDM.
 
Hivi Zitto mbona anaandika vitu kama mtoto wa darasa la kwanza? Sasa hii sentensi ina maana gani ". Naamini katika nchi yetu tunazo rasilimali za kutosha mahitaji/haja ya kila mmoja wetu lakini si ‘tamaa/ulafi' wa baadhi ya watanzania wenzetu;"

Hii ka-plagiarize kwa Mahatma Gandhi aliyepata kusema; "[h=1]"Earth provides enough to satisfy every man's need, but not every man's greed"[/h]
 
  1. Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
  2. Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa
hapo red sijaelewa zzk....mmmh

ZZK=Zitto Zuberi Kabwe, wewe Smile vipi kaaaaaah
 
kola chane

nadhani ukituhumiwa na ukajibu kama ulivyofanya, unawafanya waliokutuhumu kukukimbia kwa aibu.
katika biblia inaelezwa hivi, adui zako watakuja kwa njia moja lakini watasambaratika mbele yako kwa njia saba

hivyo walioungana na tungo za uzushi na uongo watagombana wao kwa wao!
 
Hata kama amecopy basi amecopy vibaya mpaka maana imepotea! Kwanza kabisa sijawahi kuona sentensi ambayo inamalizwa kwa semicolon! Pia ukisoma hiyo sentensi unaona kabisa kuna kitu kinamiss especially baada ya neno lakini. Mbaya zaidi, ameibold hii senstensi kuonyesha msisitizo, wakati that sentence doesn't have legs.
 
Nimeingia leo JF kwa ajili ya post yako maridhawa, umemeliza kila kitu, salaam kwa Matola na wale wote walo ktk upofu, Zito hana wa kumfikia CDM.
Pole sana, Naona unaweweseka na Matola bure, kwa taarifa yako Matola is no body ni Mwananchi wa kawaida ambaye hata bado sijafikiria kuwa Mwanachama wa Chadema licha ya kuisaidia Chadema kwa hali na mali.

Ningewaona ninyi Wanachama wa Chadema wa maana zaidi zaidi kama kipindi hiki mngejikita katika kuimarisha mtandao wenu wa Chama chenu ili mnapoingia kwenye Uchaguzi Mkuu watu kama mimi Matola tunapoongezea nguvu zetu basi mambo yanakuwa Super, sasa naweza kuungana na Pasco kwamba ni miujiza tu ndiyo itakayomnyima Lowasa Urais, kwani upande wa CCM yeye ameshamaliza kazi. nyinyi endeleeni kugombea maji tu kama vyura yangu yangu yangu yangu na hakuna atakayeyanywa.
Andika maneno haya kwenye note book yako. sijawahi kuwa na kadi ya Chadema.
 
Last edited by a moderator:
kwa maneno yako naanza kupata picha kuwa kuna kitu kinaendelea juu yako,pigana for the sake of our nation naamin ww ni mpambanaji ila nazan kashfa nyingi zinakuandama kutokana na ww kutangaza nia ya kuutaka urais fanya kazi kwanza achana na kasumba za urais sasa hivi "time will tell"na watu watakuona kama ni kweli huusiki ukweli utajulikana..usiofu kaka tuko pamoja katika harakati za ukombozi ingawa maadui ni wengi ndani na nje ya chama
 
kama kweli tuna vyombo makini vya uchunguzi...basi kweli itajulikana.

by the way, kwa kuwa magamba wanahusika...sidhani kama kuna la maana tutalipata, nadhani itakuwa ni biashara ya MEREMETA(kwa usalama wa taifa, hatuwezi kuiweka ripoti hiyo hadharani.)
 
Nimemskia leo Zitto kwenye Radio Clouds anasema eti yeye ndio kafanikisha ishu ya stika kwenye kazi za wasanii,wakati watu wanajua hii ishu aliyoifanikisha ni nani!!kutoka mwanzo hadi mwisho.
Ameidandia na kuifanya yake..

Akasema anampango sasa wa kuunganisha nguvu na Januari Makamba ili wazunguke nchi nzima na wasanii wote kupiga show za Tanzania All Stars baada ya Kigoma All Stars(nadhani hii ndio M4C yake).

Yani nimegundua uyu jamaa yuko tayari kukanyaga ata kichwa cha mwenzie ili afikie dhamira yake...yani ni nyoka wa kuogopwa.

Bado ajanishawishi kuhusu mlungula.
 
Mh.Zitto,
Shukran sana kwa taarifa hii na hakika umeweka ukweli wazi kwa wale wanaotaka kuusikia. Binafsi nilikuwa na imani na wewe toka mwanzo kwa sababu najua ukweli ulipo na najua kinachoendelea dhidi yako. Nina hakika sasa watatafuta kitu kingine kwa sababu vita bado kabisa haijaisha, huu ni mwanzo tu wakitumia majeshi ya miguu - infantry..

Mashaka ya watu wote hapa ni kwamba Umechukua RUSHWA sasa ni kazi yao kuthibitisha na ingekuwa vizuri sana kama watu hawa wataitwa bungeni kuja kuthibitisha kauli au madai yao. Halafu nashangaa sana watu wanataka wewe ujieleze ktk tuhuma hizi lakini hakuna kiongozi, mwandishi wa habari au mwananchi aliyediriki kwenda kwa Muhongo ama Maswi na kuwauliza kuhusu tuhuma hizi kama zina ukweli maana ndio source ya habari inayodaiwa - HAKUNA, sasa nabakia kujiuliza wanachoamini haswa kinatoka wapi?

Sasa mathlan tunachukua maneno haya na kuyageuza kuwa na ukweli Je, Muhongo na Maswi waksema hatujawahi kusema hivyo sisi Wanabodi tutabakia na lipi na kujitetea. NI wapi tumepata habari hizi kuhusu Zitto kuchukua Rushwa ikiwa Muhongo na Maswi hawakumtaja Zitto?. Na kwa nini watu wote wameondoka kabisa fikra zao kwa kamati iliyotajwa mbele ya Bunge hadi Spika akavunja bunge. Au tuseme hawa ni majeruhi tu wa vita baina ya Zitto na wizara ya nishati na Madini?..

Kuna Ufisadi mkubwa sana umefanyika Wizara ya nishati na Madini ambao unatakiwa kuwekwa wazi na Tanesco ni sehemu kubwa ya Ufiisadi huo japokuwa Zitto anasema Tanesco ni kati ya mashirika 259 ya umma ambayo wanayasimamia lakini Tanesco ni muhimu sana na ndiko Mafisadi wamejipanga zaidi kuitafuna nchi na inahitaji moyo kupambana nao...

Shukran tena kwa ukakamavu wako na hakika hukutuangusha..
 

Mwisho

Kumejengeka tabia hivi sasa ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo. Kumeanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitna zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari na nguvu ya fedha. Naamini mbinu hizi chafu, kama nyingine nyingi zilizojaribiwa kwangu huko nyuma nazo zitashindwa.

Naamini katika kweli na kweli daima huniweka huru. Naamini kuwa mwale mdogo wa mwanga wa mshumaa hufukuza kiza. Kwa imani hiyo, sitasalimu amri mbele ya dhamira zao ovu hata nitakapobaki peke yangu katika mapambano hayo ya kulinda na kutetea rasilimali za taifa zinufaishe watanzania wote.

Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, ‘Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga”.

Ahsanteni sana.

Kwa kawaida mwisho au hitimisho hutumika kuileta mada inayoongelewa kwa muhtasari. Kwa kuwa mada ilipewa kichwa MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI. Nilitaraji hapa angewaondolea shaka wanaomtuhumu kwa kutamka kuwa hakuwa na maslahi binafsi alipokuwa anamtetea Mhando. Angeainisha sababu zenye maslahi ya kitaifa za kumtetea Mhando japo kwa ufupi. Watu wengi wasiopenda kufuatilia maelezo marefu husoma tu hitimisho na kujua kile kilichokuwa kinaongelewa. Mtu anayesoma hitimisho pekee atachukulia kuwa maelezo yako yalihusu tu watu wanaotaka kukudhoofisha na jinsi ulvyojiandaa kukabiliana nao. Umetunyima uhondo wa usomi hapo
 
Hizo mbinu werevu tulishazijua.piga kazi zito,hauko mwenyewe utashinda tu.MUNGU MKUBWA
 
ZZK mie nahisi hiyo tuhuma ni mapito wangapi wamezushiwa na wanazidi kula maisha. Wewe weka mpira kati tutafute magoli uchaguzi ujao. Hawana jipya wanadhofisha juhudi yako ndugu. Hapa hatupo kukukandamiza maana wewe ni kijana mwenzetu. Hata ukiongea bungeni wadau tunajua Jembe limesimama. Linatoa pointi. Na wanaokupinga ni wangese 2. Hawana jipya umewabania sana mie kwa uelewa wangu. Hata unge tulia kimya hyo tuhuma imewafanya watanzania wengi wakujue hata na wale ambao walikuwa hawakufahamu wamekufahamu. Ambapo wao wametoa doa lakini kitu chochote kinacho ongeza umaarufu wake ni doa,na endapo doa lika toweka kamwe huyo mtu umaarufu wake haupotei. Wanakuongezea jina baba wewe Jembe. Kama umekula mlungula au kama hujala poa tu yote maisha, mbona wao wametafuna hadi mpini wa jembe na kubakiza vumbi kama Mchwa. Ningekuwa raisi mimi mafisadi yote ningeya nyon*elea mbali. Wewe jembe ninge kupa last warning!
 
hoja yako ni dhaifu!
Mkuki kwa nguruwe huo kwani mara ngapi Zitto naye aliweza kukemea tabia ya viongozi wa CC0 na magazeti wanamchonganisha yy na chama chake CDM?
Je ni ara ngapi Zitto aliwahi kukanusha propaganda za udini, Ukabila, na ukanda zinazoelekezwa kwa chama chake?

THINK BIG

Vipi atakanusha wakati yeye mwenyewe yanamkuta? watu si watamuona mwehu! Jamani tuseme ukweli hakuna chama chenye nguvu kama cdm kwa zama hii au nakosea kusema hivi? ila hizi propaganda za ukanda zinaweza kudhihirika kwa jinsi chama kinavyo handle issues za ZZK na Shibuda.

Hivi tuchukulie mfano ile kauli ya Nassari ya Arusha wajitenge angeitoa Zitto ingekuwaje?

Ifike wakati kurekebishwe hizi errors kwani hatuna chama mbadala kwa sasa ila cdm msifanye watu wenye akili zao timamu wakawatia lakini lakini.
 
Not convinced... Ni yale yale anayoyasema kila siku.. Tuhuma tofauti, utetezi ule ule... kuonewa, kuhujumiwa na siasa chafu. Why wewe tu? Utasema posho na Urais! Ila binafsi nitakuwa wa mwisho kukubaliana na wewe

zzk ni mlevi na mchu mkubwa wa madaraka! wasiomjua vizuri kwa matendo yake yanayoakisiwa na kauli zake tata nawasikitikia sana, kwani nyie member wa jf (great thinkers) tunarudia kule kule kwa nyinyiemu kwenye siasa za kishabiki. UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU! Viva cdm! Viva Tanzania! Viva Nyerere!
 
  • Thanks
Reactions: SG8
zito mimi ni mwana chama wa chadema nanina ipenda sana chadema tena mapenz ya dhati kabisa ya kutoka moyoni lakini kwa taarifa nilizopewa na mtu wa karibu sana na muhando kuwa umekuwa ukionekana nyumbani kwa muhando mikocheni mara kwa mara je huwa unakwenda kufanya nini na hiyo mara ya mwisho kuonekana ni kabla ya habari ya gazeti la RAI kutoka na matokeo yake ndo hilo gazeti likatoa habari ya katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini na hata kabla ya hapo mtu aliyekuwa karibu sana wewe alikuwa akikusikia ukizungumza na simu kutoa maagizo juu ya taarifa itakayo andikwa kwenye gazeti na mengine mengi tu ambayo nikiyaa ndika hapa waweza juta kujiingiza kwenye mambo ya ajabu pasipo kujali kuwa chama chako saizi kina nafasi kubwa sana ya kutwaa dola ushauri wangu kwa zito umejisahau sana umebweteka unahitaji kukaa chini ukaangalia mstakabali wako nin ufanye kujisafisha ni mengi tuna jua kuhusu ww zito ila aitusaidi kuyaweka hapa adhalani tunachokuomba jirekebishe ili wananchi waendelee kuwa na imani na wewe.

Sikio la kufa halisikii dawa!
 
Well said,

Ila kama ulivyosema tuiachie kamati ya kinga na maadili ya Bunge ichunguze kila kitu na wale walio wasafi na wachafu pumba na mchele utaonekana.

Mapambano yapo Mhe Zitto na sio madogo ila unapokuwa mpambanaji kubali yote.

Kuna kuanikwa mpaka siri zako za ndani ili kuwadhoofisha wale ambao wanapambana ili tuu kukuvunja moyo usipambane ila kama unaamini katika Mungu yote ni mapito wanasema utashinda na mnafiki mwishowe atajionyesha

Mi naona anajaribu kujinasua tu lakini ukweli unabaki pale pale kwamba amehusika, ingawa inaweza kuwa ngumu sana kuthibitisha.

Ila mimi nimuulize swali moja tu: mbona hakuchukua hatua kama hizi wakati bosi wa TBS alivyosimamishwa na Kigoda? si TBS nalo ni shirika la Umma (kama Tanesco) mbona hakumwandikia spika kumwomba aridhie waite bodi, CAG na PPRA?
 
Back
Top Bottom