Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
MADIWANI saba kati ya 11 wa Chadema jijini hapa wamegoma kujiuzulu nyadhifa zao au kuomba msamaha kama walivyotakiwa kufanya na uongozi wa juu wa chama hicho.
Miongoni mwa waliogoma ni pamoja na Naibu Meya wa Jiji la Arusha, Estomih Mallah ambaye jana aliongoza vikao vya Halmashauri ya Jiji.
Hata hivyo, madiwani wanne waliomba msamaha kutokana na kukubali mwafaka na madiwani wa CCM wiki tatu zilizopita.
Madiwani waliogoma walisisitiza, kwamba hawatatetereka hadi uongozi wa juu wa chama hicho utakapowasafisha kutokana na kuwatuhumu kuhongwa na CCM ili waridhie mwafaka wa CCM kuishika Halmashauri ya Jiji la Arusha.
Madiwani walioomba msamaha ni Ephata Nanyaro wa Kata ya Levolosi, Isaya Doita, wa Ngarenaro na wawili wa viti maalumu, Viola Lazaro na Sabina Francis.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Mallah alisema hakulazimishwa wala kushurutishwa na mtu au kiongozi yeyote kufikia mwafaka na CCM, bali ni utashi na mawazo yake ni namna gani anaweza kuwatumikia wananchi wa Kata yake ya Kimandolu.
Alisema kila diwani alikuwa na kila sababu ya kutaka mwafaka kwa maslahi ya wakazi wa kata waliyochaguliwa juu ya maendeleo, lakini kwa sababu watu wanataka migogoro ya mara kwa mara ili waweze kufaidika, hilo kwao kama madiwani halina sababu ya msingi.
Mimi niko tayari sasa kwa lolote, kwani sioni sababu ya kuomba msamaha kwa kitu ambacho naona natenda haki kwa maslahi ya wakazi wa Kata yangu, alisema Mallah.
Akizungumzia kushiriki kikao cha Baraza la Madiwani jana, Mallah alisema yeye kama Naibu Meya ameshiriki kikamilifu na madiwani wengine `wasio na woga katika kikao hicho.
Mallah alisema katika kikao chao cha jana, mambo mengi ya msingi yamezungumzwa katika kuleta maendeleo katika Jiji la Arusha, hiyo ndio kazi ya diwani na si kuzusha mgogoro.
Wakati hayo yakiendelea Arusha, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa alisema amepokea barua kuhusu sakata la madiwani wa Arusha.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa alisema alipokea barua (hakutaja idadi) saa tatu asubuhi na kuahidi kutoa taarifa baada ya kuzifanyia kazi.
Alisema kwa kuwa suala hilo linahitaji umakini wa hali ya juu, anahitaji muda wa kutosha bila kuingilia ratiba yake ya mikutano ya hadhara ambayo anatarajiwa kuifanya leo na kesho.
Tafadhali naomba mnipe muda, kwani suala lenyewe ni zito na linahitaji muda wa kutosha kulijadili na kutoa uamuzi nitatoa taarifa kamili baada ya kuifanyia kazi barua niliyopokea, alisema Dk. Slaa ambaye chama chake awali kilipinga kumtambua Meya wa Jiji la Arusha kutoka CCM, Gaudence Lyimo.
Chadema ilimkataa kwa madai kuwa uchaguzi wake haukufuata utaratibu na misingi ya haki.
Pamoja na madai ya Lema ya usaliti kutokana na mwafaka kutokuwa na baraka za viongozi wa juu wa chama, madiwani hao waliendelea kudai kuwa uamuzi wa kumkubali Lyimo ulizingatia maslahi ya wananchi wa kata zao na Jiji la Arusha na si vyama.
Miongoni mwa waliogoma ni pamoja na Naibu Meya wa Jiji la Arusha, Estomih Mallah ambaye jana aliongoza vikao vya Halmashauri ya Jiji.
Hata hivyo, madiwani wanne waliomba msamaha kutokana na kukubali mwafaka na madiwani wa CCM wiki tatu zilizopita.
Madiwani waliogoma walisisitiza, kwamba hawatatetereka hadi uongozi wa juu wa chama hicho utakapowasafisha kutokana na kuwatuhumu kuhongwa na CCM ili waridhie mwafaka wa CCM kuishika Halmashauri ya Jiji la Arusha.
Madiwani walioomba msamaha ni Ephata Nanyaro wa Kata ya Levolosi, Isaya Doita, wa Ngarenaro na wawili wa viti maalumu, Viola Lazaro na Sabina Francis.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Mallah alisema hakulazimishwa wala kushurutishwa na mtu au kiongozi yeyote kufikia mwafaka na CCM, bali ni utashi na mawazo yake ni namna gani anaweza kuwatumikia wananchi wa Kata yake ya Kimandolu.
Alisema kila diwani alikuwa na kila sababu ya kutaka mwafaka kwa maslahi ya wakazi wa kata waliyochaguliwa juu ya maendeleo, lakini kwa sababu watu wanataka migogoro ya mara kwa mara ili waweze kufaidika, hilo kwao kama madiwani halina sababu ya msingi.
Mimi niko tayari sasa kwa lolote, kwani sioni sababu ya kuomba msamaha kwa kitu ambacho naona natenda haki kwa maslahi ya wakazi wa Kata yangu, alisema Mallah.
Akizungumzia kushiriki kikao cha Baraza la Madiwani jana, Mallah alisema yeye kama Naibu Meya ameshiriki kikamilifu na madiwani wengine `wasio na woga katika kikao hicho.
Mallah alisema katika kikao chao cha jana, mambo mengi ya msingi yamezungumzwa katika kuleta maendeleo katika Jiji la Arusha, hiyo ndio kazi ya diwani na si kuzusha mgogoro.
Wakati hayo yakiendelea Arusha, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa alisema amepokea barua kuhusu sakata la madiwani wa Arusha.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa alisema alipokea barua (hakutaja idadi) saa tatu asubuhi na kuahidi kutoa taarifa baada ya kuzifanyia kazi.
Alisema kwa kuwa suala hilo linahitaji umakini wa hali ya juu, anahitaji muda wa kutosha bila kuingilia ratiba yake ya mikutano ya hadhara ambayo anatarajiwa kuifanya leo na kesho.
Tafadhali naomba mnipe muda, kwani suala lenyewe ni zito na linahitaji muda wa kutosha kulijadili na kutoa uamuzi nitatoa taarifa kamili baada ya kuifanyia kazi barua niliyopokea, alisema Dk. Slaa ambaye chama chake awali kilipinga kumtambua Meya wa Jiji la Arusha kutoka CCM, Gaudence Lyimo.
Chadema ilimkataa kwa madai kuwa uchaguzi wake haukufuata utaratibu na misingi ya haki.
Pamoja na madai ya Lema ya usaliti kutokana na mwafaka kutokuwa na baraka za viongozi wa juu wa chama, madiwani hao waliendelea kudai kuwa uamuzi wa kumkubali Lyimo ulizingatia maslahi ya wananchi wa kata zao na Jiji la Arusha na si vyama.