Madam Rita, ziko wapi nyimbo za wasanii wa Top 5 ya BSS?

explicity

JF-Expert Member
Oct 9, 2015
207
140
Bongo Star Search ni shindano pekee kwa Tanzania la kusaka vipaji kwa vijana wenye uwezo wa kuimba.

15561906fef112bfd780e15aeeae76db.jpg

Madam Rita kupitia kampuni yake ya Benchmark Production alikuwa na malengo mazuri ya kuanzisha shindano hili ambalo watanzania tulikuwa tunaangalia mashindano kama haya katika nchi za nje tu.

Kwa mara ya kwanza shindano la BSS lilianza mwaka 2007 na lilizalisha vipaji kama, Kala Jeremiah, Baby Madaha, na aliyekuwa mshindi wa shindano hilo Jumanne Iddi ambaye kwa sasa amepotea kwenye ramani ya muziki.
Mashindano ya BSS, msimu wa nane mwaka 2015 yamesaidia kuvitambua vipaji vingi vilivyokuwa vimejificha. Washiriki watano waliofanikiwa kuingia kwenye fainali za shindano hilo ni Kayumba Juma, Nassibu Fonabo, Frida Amani, Angel Mary Kato na Kelvin Gason.

Tunakumbuka kuwa kwenye shindano hilo, Kayumba Juma alifanikiwa kushinda na kufanikiwa kupata mkwanja wa shilingi milioni 50. Moja ya ahadi zilizotoka kwenye mashindano hayo ni kuwa top five yote itakuwa chini ya menejimenti ta Tip Top Connection.
Ni miezi mingi imepita mpaka leo tangu shindano hilo lifanyike, mpaka sasa ni wimbo pekee wa Kayumba Juma ‘Katoto’ ndiyo umeweza kutambulishwa kwa mashabiki wa muziki, je wako wapi hao wasanii wengine walioingia kwenye ile top five?

Tunajua kuwa mkataba na washiriki haona kuwa chini ya menejimenti ya Tip Top Connection ilikuwa ni ya mwaka mmoja tu, mpaka sasa ni miezi mingi imeshapita bado hatujaona chochote kipya na miezi michache tu imebakia mkataba huo uweze kuisha.

Je ndani ya hiyo menejimenti itaweza kusaidia hao vijana kuachia kila mmoja nyimbo mbili ndani ya hii miezi iliyobakia? Sina uhakika na hilo kama litawezeka.

Siku chache zilizopita Babu Tale aliongea kwenye kipindi cha The Chart Show, kinachoruka kupitia Times FM alisema kuwa muda siyo mrefu kuna msanii mmoja kati ya wale wasanii ataachia wimbo wake. Sina shaka kwa lile alilolisema Babu Tale, wasi wasi wangu unabaki kuwa menejimenti ya Tip Top Connection inasimamia wasanii wengi kwa sasa na kila msanii anahitaji msaada kutoka kwenye menejimenti hiyo.

Je hawa wasanii wa BSS wamewekwa kwenye chumba gani kwa sasa ndani ya nyumba ya menejimenti hiyo?
 
Back
Top Bottom