Madaktari wamuweka JK kikaangoni! Ni kuhusu uamuzi wa kumfukuza kazi Dr Mponda

Status
Not open for further replies.
Cha uongo kipi alichosema hapo, je si kweli mtoto wa mkulima aiwahadaa ma dr? Na sasa wamemkalia kooni sijui atatokaje, hii ni faida ya serikali isiyo sikivu, wanalazimishwa kufanya maamuzi kwa lazima
 
Asiishie hapo kuna makopo mengi tu ya kutupa pale, yameshaisha muda wake
mama Nagu
Kawambwa
Mwakyembe (Mgonjwa)
Mwandosya (mgonjwa)
Ngeleja (hayuko serious)
Malima (boza)
Mponda (zero)
Nkya (conflict of interest, useless)
nk

Aha ha ha ha! hii kali.Kuna watu mna matusi ya rejareja..lakn ukweli huwa unauma mara nyingi
 
We are praying for you guys!! Ni mwanzo mzuri, hope the teachers will also stop working for CCM during election!! Walimu wanatucost sana, ukiona mtoto wako anafeli feli darasani siyo kwa sababu hana akili ila walimu hawako motivated!! Madaktari tutawatunukia nishani ya ushujaa huku mbele ya safari kwa kulikoboa hili taifa!! msilegee, hawa viongozi wetu hawana huruma na hii nchi!! They travel everywhere, but for nothing! they use money to win their desire! they are ready to kill anyone who go against their will even when is not a public interests. In short, these leaders are not ours but they are puppets.
 
Serikali inayoamani katik propaganda katika mambo ya wazi ni kijinga na haina maisha.
 
Blackmailing a president,! chantaje!
sasa mgomo wa madaktari utakua meaningless sabab madai na vitisho vyao sasa vinaboa, mi nawaungamkono katika kudai mishahara na mazingira mazuri ya kazi, wakishapata hivyo tu wafanye kazi watulie, ila wakianzakusema sijui wataachia watanzania wafe kisa tu eti rais hajabadili waziri, it's nonsense! na sio maadili ya kazi alio tuachia Esculapio
 
mtaishia kuwatetea mpmda na nkya kwa sababu hamna taarifa,hilo siyo kosa lenu. Mnakumbuka mponda ndo alisema intern ni mwaka wa nne muhimbili? Utakuwaje mtendaji huwajui wafanyakazi wako wana elimu gani? Hata kuuliza huwezi? Yeye mwenyewe akalidanganya bunge kwamba hali inaendelea vizuri huku mnh wamesitirha huduma,ile taarifa aliitoa kwa manufaa ya nani? Mama nkya naye ndiye aliyeanza kuwakimbia madaktari na kwenda kwenye vyombo vya habari kuwatisha,kama wewe ni msafi kwa nini umwogope mtumishi wako? Na sasa hivi hayo makubaliano yanatakiwa kusimamiwa na wizara ya afya,unadhani hawa maadui wakiwepo yatatekelezwa? Kwa nini tusimalize kila kitu sasa hivi? Kama wafanyakazi waliochini yako hawana imani na wewe,ukiachia madaraka utauawa? Kwani hiyo ni ajira ya kudumu? Mbona nyoni na mtasiwa wameondolewa,hawa kinashindikana nini?
 
UFAFANUZI SAHIHI

Kuna watu hawaelewi ni Kwa nini drs wanataka waziri wa afya aondoke kabla mazungumzo hayajaenda mbali.
Madai ya drs yapo yanayohitaji muda mfupi, wa Kati na muda mrefu kuyatekeza.
Kamati iliyoundwa ni chombo cha muda muda mfupi na isitoshe mtekelezaji mkubwa wa hayo madai ni Wizara ya afya.
Mfano dai la kwanza la drs huduma bora za afya Kwa wa tz wote mfano ukosefu wa dawa na wagonjwa kulala sakafuni au wawili wawili kitanda kimoja. Dai Kama hili linahitaji muda wa Kati na muda mrefu kulitekeleza, na mtekelezaji mkuu ni Wizara ya afya wakati huo kamati itakuwa haipo tena ukizingatia yenyewe ni chombo cha muda.
Ikumbukwe kuwa watendaji walioko Wizara ya afya wameonyesha uwezo mdogo sana wa utendaji mfano waziri hajui hata tofauti Kati ya medical student na medical doctor.
Ikumbukwe Kwa uzalendo wa drs wameona ni vema waweke uzalendo mbele yaani kuwapigania wagonjwa kwanza kabla ya kuongelea mambo ya mishahara Yao Kama baadhi ya watu wanavyotaka hapa jf.
Aidha drs wameonyesha uwezo mkubwa sana wa negotiation Kwa kuepuka mitego mbalimbali ambayo serikali imekuwa ikiweka pamoja na kufikiria mbali zaidi kuliko hata wataalam wa negotiation wa serikali.
Mimi binafsi napenda kuwapongeza drs wote Kwa Moyo wa uzalendo wa kukataa kukimbilia vihela vya serikali badala yake kuweka maslahi ya wa tz mbele.

MUNGU IBARIKI TZ.
 
CWT, it is now or never!
Join force

Nurses, it is now or never!
Join forces

rise up and fight for ur rights!
Saa ya ukombozi ni sasa,
know that right is never given in a silver plate, you got to fight hard and firmly for it,
those who will die in this cause will be remembered as our true heroes, including the patients who will loose life in the period of medical staff boycot.

Right is bought for blood,lukcy for the nation whose sons and daughters have got blood.
 
Tatizo rais wetu usanii mwingi,hayupo serious na kila analofanya,timua tu hao sasa hapo nae sioni kazi anayofanya kama anashindwa kumfukuza mtu ambae analega mgogoro katika sekta ya afya....be serious kikwete
 
Du hii serikali yetu kwa kweli inasikitisha, kwa wiki nzima sasa kila chombo cha habari kinahabarisha jinsi walimu wapya wanavyoteseka kwa kukosa stahiki zao. Inafikia mwalimu anakosa mahali pa kula na kulala ataweza vipi kufundisha watoto wetu. Madaktari wagome kabisa wasifanye mchezo na serikali ya mazezeta, yamechoka hayana tena jipya isipokuwa kuliangamiza taifa hili la Mungu.

Karibu JF!! na nyie ungana walimu wote mgome muwasapoti Madaktari kuiadabisha Goverment!! kenya nako ma dr wamegomo:juggle:
 
the media report from PM's office was a ''lie and incitement.the gov. is playing propaganda in this issue'', one wonders what's going on in our 'rulers' minds.what did the govt expect from doctors? Anyway lets hope for good!
 
Serikali isitudanganye hawana pesa mbona za kuwahonga wapiga kura wanayo? Lakini za kulipa malipo halali kama ya madaktari na walimu wanaoanza kazi hawana, kama siyo kupuuza huduma muhimu za jamii na kuthamini uhalifu nini?
 
We are praying for you guys!! Ni mwanzo mzuri, hope the teachers will also stop working for CCM during election!! Walimu wanatucost sana, ukiona mtoto wako anafeli feli darasani siyo kwa sababu hana akili ila walimu hawako motivated!! Madaktari tutawatunukia nishani ya ushujaa huku mbele ya safari kwa kulikoboa hili taifa!! msilegee, hawa viongozi wetu hawana huruma na hii nchi!! They travel everywhere, but for nothing! they use money to win their desire! they are ready to kill anyone who go against their will even when is not a public interests. In short, these leaders are not ours but they are puppets.

Puppets indeedd of the Freemasons.
 
Imenisikitisha sana niliposikia tamko la madaktari kupitia ITV habari mpasuka kuwa wataendelea na mgomo ikiwa wabaya wao Dr Haji Mponda na Dr Nkya wataendelea kuwepo wizara ya afya kama mawaziri, kwa mjibu wa ITV, madaktari hao wameipa Serikali siku nne hadi Jumatano ijayo saa 2;00 asbh iwe imewaondoa wabaya wao lasivyo mgomo utaendelea. Kwa kauli hii ya madaktari namuomba JAKAYA atumie busara kuchagua kuendelea kumkubatia huyo waziri na naibu wake na watanzania wasio na hatia waendelee kufa kwa vifo visivyo vya lazima ama awatimue ili kuondokana na janga hilo.

Dah!kweli ****** ni sikio lisilosikia dawa
 
Hawa wana-usalama walikuwa wapi siku zote? Nadhani kama wangekuwa wanafanya lazi zao vizuri, kwanza hata huu mgomo usingetokea, na hata baada ya kutokea na kufikia muafaka, walikuwa wapi kufahamu kuwa haya maamuzi ya madaktari lazima yangefika hapa ikiwa kama mambo kama ya kuwawajibisha hao mawaziri hayakufanyika? Napata shida sana na hao wanaoitwa wana usalama, na ninaona pia kuna uwezekano mkubwa kabisa nao wakawa wameingia ktk vita hii ya makundi ndio maana mambo hayaendi.

Kwa vile Serikali imeonekana kulegea kabisa, basi hakuna ujanja ni lazima ipate shinikizo kama hilo ili itoe maamuzi, na kila siku bila mashinikizo Serikali nyingi za Africa zinakuwa hazieleweki. Na kama madaktari watakuja na mashinikizo mengine, sawa tu, ili mradi yana manufaa kwa watanzania.

Pili, ktk kila historia ya mabadiliko, huwa kunakuwa na Agent of Change, na kwa Tanzania, kutokana na historia yetu ya kimaisha na jinsi Mwalimu Nyerere alivyotukuza na kutufunza, sisi wananchi kuwa change agent ni kazi kidogo.

Kwa nchi kama yetu, professions can be agent of change, na hapa nazungumzia fani kama hawa madoctor wetu, walimu na kadharika. Kwa hapa tulipofika, naona kabisa, madaktari wanaweza kuwa agent of change kwa Tanzania.

Mimi nilisema mwanzo na naendelea kusema, nawaunga mkono, nawaomba wabebe jukumu hili la kuwa Agent of change kwa niaba ya watanzania wote, bila kujali itikadi zao. Nawaomba madaktari, wakisha inyosha serikali kwa masuala yaliyopo ktk sector ya Afya, wahamie na sector nyingine kama Walimu nk. Watusaidie kuleta haya mabadiliko, wanaweza kuja na hoja kuwa wao kama madoctor wamefika hapo walipo kwa ajili ya walimu, sasa kama walimu wasipotekelezewa maslahi yao basi wao wanaitisha mgomo tena.

Wakimaliza hapo waje kwa watumishi wazembe na hasa mafisadi Serikalini, waseme, haiwezekani watu wachache watumie rasilimali za nchi kwa manufaa yao pekee, wakati watanzania wengi wanakufa kwa kukosa dawa na hospitali za kutosha, basi waseme wanataka watu wote waliotuhumiwa kwa ufisadi wafukuzwe kazi na wakamatwe na wafikishwe ktk vyombo vya sheria, na waitishe mgomo kama Serikali haitaka kufanya hivyo.

Wakimaliza hapo waende katika sector nyingine, mpaka wamalize zote. Nadhani Madaktari wanaweza kututoa hapa na kutupeleka mahali pengine bila hata kutumia vyama vya siasa.

Tena wanapotoa hayo mashinikizo watoe na timeframe, kama vile wanavyo-prescribe dawa zao kwa mgonjwa, 2X3 kwa Wiki Moja, au 1x1 for two weeks au etc etc. Basi waipe serikali time frame kama dozi za dawa, kama walivyofanya hili la sasa, kwamba mpaka J5 hao mawaziri wawe wameondoka - dozi safi sana kama ya dawa ya siku tatu.

Hongereeni Madaktari na naomba mlifikirie wazo langu la ninyi kuwa agent of change na watanzania tuwape support hawa. Aluta continua!....

Aluta continua.....
 
wapendwa,

kumbukeni kuwa si kazi ya madaktari wala kada nyingine yoyote kupanga baraza la mawaziri. huko ni kukiuka katiba. watanzania kama jamii ya watu wastaarabu hatupaswi kukiuka katiba yetu wenyewe.

mara nyingi tunawanyooshea vidole viongozi kuwa wamekiuka katiba lakini tunasahau kuwa kila raia anapaswa kuheshimu na kuilinda katiba iliyopo.

hao madaktari wana madai ya msingi, sawa. tena si peke yao. karibu kila kundi nchini mwetu lina madai kadhaa ya msingi kabisa, lakini wasisahau kuwa haki yao ni hayo madai waliyonayo na sio zaidi ya hapo. kumlazimisha mponda , nkya au waziri yoyote atoke kazini ili wao "wafurahi' ni kinyume cha katiba. hao kina mponda ni watanzania kama watanzania wengine na wana haki ya kufanya kazi iwe ni uwaziri au kazi nyingine yoyote, kama walivyo na haki kama hiyo watanzania wengine wote.

mimi binafsi sioni haki wala haja yoyote ya madaktari kugoma kutimiza wajibu wao wa kikazi hadi waone sura wanazozipenda wao kwenye baraza la mawaziri. hiyo si haki ya kikazi kwa kada ya madaktari, labda watuambie wana maslahi gani katika hilo.

hao madaktari wameishaonja "nyama ya mtu", wameishaua wagonjwa waliokwenda kupata huduma yao huku wakiwa wameishakula mishahara na stahili nyingine, iliyotokana na kodi walizotozwa hao hao waliowaua kwa mgomo wao uliopita! na sasa wamezoea harufu ya damu za watanzania wenzao masikini wasioweza kukimbilia india wala hospitali nyingine ghali zaidi za binafsi nchini.

ni wauaji wakubwa na siungi mkono mgomo wao mwingine kwa sababu za eti fulani na fulani bado ni mawaziri au manaibu mawaziri! hiyo si kazi yao, wao wazingatie kazi zao na wapeleke serikalini madai yanayoendana na haki au maslahi yao kama madaktari. hilo la kulazimisha mabadiliko ya baraza la mawaziri ni uhujumu wa kiraia na ukiukwaji wa katiba. imefika wakati sasa katiba na sheria ziseme, raia asiye kiongozi wa umma akikiuka katiba afanyweje.

siungi mkono hoja na nawalaani sana kwa nia na azimio lao hilo (kama ni la kweli)

mbarikiwe sana wapendwa

glory to God!

MUNGU AKUSAMEHE MAANA HUJUI UNENALO!!!!!!. Tanzania tumefikia hapa tulipo sababu ya uzembe wa viongozi wetu. Kama anayesimamia katiba hawezi kuwawajibisha viongozi wazembe, waliompa madaraka ya kuisiomamia katiba wana wajibu wa kumlazimisha kuisimamia katiba. Katiba yetu pamoja ubovu wake hairuhusu uzembe.
 
Blackmailing a president,! chantaje!
sasa mgomo wa madaktari utakua meaningless sabab madai na vitisho vyao sasa vinaboa, mi nawaungamkono katika kudai mishahara na mazingira mazuri ya kazi, wakishapata hivyo tu wafanye kazi watulie, ila wakianzakusema sijui wataachia watanzania wafe kisa tu eti rais hajabadili waziri, it's nonsense! na sio maadili ya kazi alio tuachia Esculapio


Hoovyoooo!
 
Hahaha madokta wanachekesha sana, badala ya kudai mambo yao ya msingi wamekuwa kama chama cha siasa.Rais akiwakubalia madaktari atakuwa ameonesha udhaifu mkubwa sana na next thing watasema pinda hawamtaki naye atoke hakutakuwa na serikali. Ningependa jk aache hao jamaa wagome wakae benchi kwakuwa kimsingi wakigoma wataenda kufanya kazi hospitali binafsi ili wasife njaa.

Hujui ulisemalo, kwa taarifa yako hata vitendea kazi tu havipo kwenye mahospitali mfano Hospitali ya Rufaa ya Bugando mashine ya x-ray imeharibika inabidi wagonjwa waende hospitali ya mkoa Sekou Toure. Je kama Serikali ingekuwa serious suala la vifaa isingekuwa tatizo. We unafikiri hao madaktari wa Appollo wanawazidi sana utaalam madaktari wetu?, tatizo vifaa duni vipaumbele vya serikali ni safari za nje ya nchi na posho za wabunge. Madaktari gomeni hadi kieleweke, tena JK ashukuru wananchi ni wapole mno ingekuwa kwingine hii ni kashfa kubwa kwa serikali makini.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom