Vancomycin
Senior Member
- Jan 7, 2011
- 171
- 111
Taarifa ambazo zimethibitishwa zinatabanaisha kuwa madaktari walio katika uzoefu kazini, INTERN doctors wameanza kufukuzwa katika hospitali mbalimbali ambapo katika hospitali ya DODOMA madaktari 11 kati ya 33 wamefukuzwa na madaktari wote 70 waliokuwepo hospitali ya rufaa mbeya chini ya ulinzi mkali wa polisi wameambiwa waondoke kufikia saa 11 jioni ya leo wakati huo huo mkurugenzi wa hospitali ya BUGANDO amewafukuza madaktari wote 44 na kuwataka warudi wizarani wakati madaktari waliosajiriwa wameamuriwa kufika kesho wawe kazini au la wanafukuzwa.
Wakati huo huo madaktari wakazi waliitwa na senate ya BUGANDO na kulazimishwa kurudi kazini lakini walikataa mbele ya senate hiyo hivyo wakaambiwa watafutiwa udahili wao na wote kwa pamoja wakapiga makofi wakisema wako tayari kwa hilo.
Habari zaidi zinazidi kupasha kuwa hospitali ya Mwananyamala wameletewa fomu za kujaza kama wako tayari kuendelea na kazi au la,ila madaktari wamesimamia msimamo wao huo kuwa mgomo uko pale pale.
Katika hatua nyingine CHUO CHA TIBA BUGANDO NA KILE CHA MUHIMBILI VIKO MBIONI KUFUNGWA kutoka na walimu wao ambao ni madaktari kugoma na mazingira kutokuwa rafiki kwa kujifunzia.
Wakati hayo yakiendelea taarifa zinasema hsopitali ya Tanga BOMBO imeingia rasmi kwenye mgomo na ile ya MOUNT MERU
Habari zaidi madaktari wanajiandaa kwa mass resignation muda wowote
Wakati huo huo madaktari wakazi waliitwa na senate ya BUGANDO na kulazimishwa kurudi kazini lakini walikataa mbele ya senate hiyo hivyo wakaambiwa watafutiwa udahili wao na wote kwa pamoja wakapiga makofi wakisema wako tayari kwa hilo.
Habari zaidi zinazidi kupasha kuwa hospitali ya Mwananyamala wameletewa fomu za kujaza kama wako tayari kuendelea na kazi au la,ila madaktari wamesimamia msimamo wao huo kuwa mgomo uko pale pale.
Katika hatua nyingine CHUO CHA TIBA BUGANDO NA KILE CHA MUHIMBILI VIKO MBIONI KUFUNGWA kutoka na walimu wao ambao ni madaktari kugoma na mazingira kutokuwa rafiki kwa kujifunzia.
Wakati hayo yakiendelea taarifa zinasema hsopitali ya Tanga BOMBO imeingia rasmi kwenye mgomo na ile ya MOUNT MERU
Habari zaidi madaktari wanajiandaa kwa mass resignation muda wowote