Waoga kibao wapo kazini. Mi nipo Muhimbili saivi naona mambo tambarare
Serikali ishindwe? waulize magwanda na wanafunzi wa mlimani.
Kukutana ni madaktari waliofanya dharau jana, Waziri Mkuu kawangoja hawakutokea, walitaka wabembelezwe? Mwanachi ataekuwa nyuma ya hawa na kuwaunga mkono huyo haitakii mema Tanzania.
Ktk hili sakata, Madaktari watashindwa.... Huwezi kucheza na Serikali ukabaki salama.
Nawahurumia wale wenzangu na mimi wanaofuata mkumbo na mwishowe kupoteza ajira.
RUDINI KAZINI.....otherwise ...Very soon mtagundua kuwa mlikuwa mnapoteza muda na imeshakula kwenu.
PM kasema madai yao ni ya msingi, asichukubali ni masharti ya kuambiwa yafanyike haraka. Hoja yao ni maslahi bora na mazingira bora ya kazi (vitendea kazi) haya yote ni kwa maslahi ya wanaohudumiwa. Wewe ni shahidi kuwa Kansa haikuletwa na CDM, ukitaka matibabu yake utawajibika kuja Dar, unawakuta na wenzako kutoka nchi nzima wamekusanyika, sasa daktari huyu asiye na motisha anafanyaje kazi kama sio kukulipua?Yetu macho hapo ni lazima utasikia tu Dr. Ulimboka na mwanachama wa CDM hivyo anatumiwa vibaya kufanya nchi isitawalike na kuingizwa CDM katika mgomo huo bila kuchuja hoja za Ma Dr. kama zina logic au la.