Mabishano ya kidini ni ujinga na kipimo cha uelewa mdogo

Infropreneur

JF-Expert Member
Aug 15, 2022
5,266
10,774
Habari wakuu wana jamii forums..

Moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu napenda kuzungumzia suala la mabishano ya kidini baina ya waumini wa dini mbalimbali hasa dini kuu mbili zenye wafuasi na waamini wengi duniani Ukristo na Uislamu...

Kwanza kabisa Binadamu yeyote anapozaliwa anakuwa hana dini,Hajui imani yeyote ile hadi pale anapofikia umri wa kujielewa na kuwa na ufahamu wa imani(Dini) inayomzunguka ndipo naye huanza kuingia kwenye imani hiyo kwa kufuata imani za watangulizi wake..Hapa watoto hufuata dini za wazazi wao na hufundishwa dini hiyo tangu wakiwa utotoni na kuendelea kukua nayo hadi ukubwani.Hapa kwa watoto wa dini ya ukristo huenda mafundisho ya kiimani ya ubarikio (Komunio, Ekaristi) na kipaimara pia watoto waislamu huenda madrassa kufundishwa pia imani yao ya kiislamu.

Kulingana na mafundisho ya dini zote mbili kila mtu huona dini yake aliyonayo ndio ya kweli na sahihi kuliko ya mwingine..mfano kwa dini ya kiislamu wana amini mtu yeyote asiye muumini wa dini ya kiislamu ni "kafiri" na hivyo hivyo kwenye ukristo wana amini yeyote asiye mkiri kristo kama mwokozi na mkombozi wa ulimwengu basi imani yake sio sahihi amepotoka kiimani.

Kutokana na mafundisho haya sasa,ndipo kumedumu na kushamiri "MABISHANO" makali kila siku miongoni mwa waumini wakibishana usahihi na ukweli wa dini zao.. mabishano haya ni sawa na mchezo wa "KUVUTA KAMBA" kila mtu hujaribu kuvutia na kutetea upande wake ili ashinde.

Hali ni tete zaidi kwa viongozi wa dini zote mbili,wengi wao huwafundisha na kuwa hubiria waumini wao kwamba imani au dini waliyopo ndio ya kweli na sahihi na endapo mtu yeyote yule atajaribu kuwashawishi kubadili dini au kuhama imani hiyo wapingane nae VIKALI mno, ikibidi kupoteza Maisha kabisa kutetea imani yao kwa kigezo eti ndio watapata thawabu na baraka za mwenyezi Mungu.Hii imepelekea vikwazo vingi sana kwa watu hasa kwenye suala la NDOA.. inakuwa ni vigumu sana kwa baadhi ya familia za kikristo na kiislamu kukubali utofauti wao kidini kwenye maswala ya ndoa hivyo inakuwa kikwazo kwa vijana wa dini mbili tofauti kufunga ndoa.

Kwa maoni, mtazamo na Ushauri wangu kwa jamii ni kwamba:Kila mtu anatakiwa aheshimu Dini (Imani) ya mwenzake kwa sababu kuu kwamba, kila mtu amezaliwa,amekulia, amefundishwa na kuaminishwa dini yake tangu utotoni na wazazi wake, hivyo asione dini ya mwingine "Haina ukweli na usahihi" maana hamna mwenye uthibitisho kamili wa "usahihi na ukweli" wa dini yake zaidi ya kuegemea na kujikita kwenye Maandiko ya kidini (Vitabu vya kidini,Biblia na Quran) vinavyo kinzana kwenye hoja mbalimbali hivyo kupelekea ubishi usio na mwisho.. nimalizie kwa kusema RELIGION IS NOT GOD.....

Karibuni kwa maoni, mitazamo na ushauri.kejeli na ubishi wa kuanza tena kutetea dini hapa haitasaidia kuelimishana...

Nawasilisha.kwenu wakuu!
 
ukijua kila kitu kina kinyume chake uwezi kuangaika na haya mambo.

Wema,ubaya
Giza,mwanga
Aman,vita

Kwaiyo hakuna dunia ambayo itakuja tokea tukawa upande mmoja.
Dunia tutakuwa upande mmoja tu kama kitatokea kitu kingine chenye kutumaliza sisi.

Kwaiyo mabishano lazima ya wepo cha muhimu ni uvumilivu tu kwanza huku amna mabishano ni kutukanana tu.

Kwanza ukifwata Dini akili zako uwezi zitumia nimeliona ilo hapa yani watu hunao waona wana hekima likija swala la Dini wanaweka akili pembeni
Ni kweli kabisa mkuu..Dini na Imani zetu hazitaki zihojiwe na ukijaribu kufanya hivyo inaonekana unapingana na dini au imani hiyo.. Faith prevents reasonable thinking...hili ni tatizo sana
 
Kuna kitu wewe unakosea kimoja!! Kama hukijui mpaka panazuka mijadala hii ya kidini ,panazuka mjadala kama huu jaribu kuangalia mashambulizi always yanaanzia wapi haswa kibongo ,tatizo lenu ni moja nawaambia ukiachana na nchi za nje ambao wanapigana kweny maslahi ya madaraka kwa vile kule walishaamua kuwa ivyo ...Mfano mada inatokea nje au mtu kalipua nje kwa hapa bongo hamna mtu alipuka na bomu basi mtu analeta nyuzi kumshambulia dini fulani ili kuonyesha chuki dhidi ya watu kuwapa majina mabaya..

Narudia kusema hatuvumilii ujinga sio wanyonge kama tunaweza kufuta mijdala tuwe tunadicus mambo ya maana Ntakupa mfano unasoma Uzi upate mbili tatu unakuta mtu kakoment labda dini yako wewe au kwenu Kuna magaidi au mashoga utakubali??

Huwaga watanzania na waafrica kwa kiasi kikubwa ni wapenda amani , hususani hapa Tz sema chokochoko ndo zinawacost ..

Nyuzi za humu dini, makabila, mikoa ujinga mtupu Mimi comment ila usitaje dini yangu ..
 
Kuna kitu wewe unakosea kimoja!! Kama hukijui mpaka panazuka mijadala hii ya kidini ,panazuka mjadala kama huu jaribu kuangalia mashambulizi always yanaanzia wapi haswa kibongo ,tatizo lenu ni moja nawaambia ukiachana na nchi za nje ambao wanapigana kweny maslahi ya madaraka kwa vile kule walishaamua kuwa ivyo ...Mfano mada inatokea nje au mtu kalipua nje kwa hapa bongo hamna mtu alipuka na bomu basi mtu analeta nyuzi kumshambulia dini fulani ili kuonyesha chuki dhidi ya watu kuwapa majina mabaya..

Narudia kusema hatuvumilii ujinga sio wanyonge kama tunaweza kufuta mijdala tuwe tunadicus mambo ya maana Ntakupa mfano unasoma Uzi upate mbili tatu unakuta mtu kakoment labda dini yako wewe au kwenu Kuna magaidi au mashoga utakubali??

Huwaga watanzania na waafrica kwa kiasi kikubwa ni wapenda amani , hususani hapa Tz sema chokochoko ndo zinawacost ..

Nyuzi za humu dini, makabila, mikoa ujinga mtupu Mimi comment ila usitaje dini yangu ..
Kwetu waafrika Udini ni utumwa wa kifikra mkubwa sana kiasi kwamba Akili zimesha athirika na Udini... Mfano mtu anapo tukana au anapo taja dini yako kwenye tukio baya anakuwa hana uelewa na ni mjinga anakuwa hajui na haelewi anacho kitetea, halafu ukimjibu kwa kubishana naye..Na wewe unakuwa tena una "Udini" unajaribu kutetea dini yako uliyo nayo kwa vile tu umesikia imetajwa,Mtu anapo taja dini yako kwenye tukio baya ukamjibu unakuwa anatetea kile ulicho aminishwa na viongozi wa dini na jinsi ulivyofundishwa na kuaminishwa kupitia maandiko yako ya kidini(Biblia, Quran) vitabu ambavyo ni maandiko ya kibinadamu yanayo daiwa eti kuandikwa kwa uvuvio wa roho mtakatifu na andiko lingine ati lilishushwa toka juu mbinguni vitu visivyo na uthibitisho kamili.
 
Kwa waislamu ndio hatari kabisa mtu akiacha uislamu anatatengwa, atauwawa, mzazi wake kabisa yupo radhi hata kumuua sema wanaogopa tu sheria za nchi, lakini wanawatenga na undugu unakufa kabisa na kufutwa kwenye ukoo. Tofauti na Wakristo ukiamua kuwa Muislamu Hakuna shida kabisa kwenye familia hata Jamii yako.
Pana Shehe Mkubwa kabisa nchini kwa watoto 10 yeye pekee ndie akaamua kuwa Muislamu hawa tisa Wakristo hawana shida kabisa undugu upo pale pale japo imani wametofautiana.
 
Wafia dini watakuja kuharibu huu uzi maana hawana jambo ndogo hata kidogo Wala mshipa wa aibu

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Na hao ndio hawana maendeleo kabisa kiuchumi wafia dini wengi (sio wote) wana umaskini mkubwa, wao kazi yao ni kukaa kwenye vijiwe wakibishana "Udini" wana amini kwamba miujiza itawasaidia kupata mafanikio..
 
Ni kweli kabisa mkuu..Dini na Imani zetu hazitaki zihojiwe na ukijaribu kufanya hivyo inaonekana unapingana na dini au imani hiyo.. Faith prevents reasonable thinking...hili ni tatizo sana
Kama hazitaki uhojiwe hapo pana shaka,imani ya kweli inahojika
 
Kwa waislamu ndio hatari kabisa mtu akiacha uislamu anatatengwa, atauwawa, mzazi wake kabisa yupo radhi hata kumuua sema wanaogopa tu sheria za nchi, lakini wanawatenga na undugu unakufa kabisa na kufutwa kwenye ukoo. Tofauti na Wakristo ukiamua kuwa Muislamu Hakuna shida kabisa kwenye familia hata Jamii yako.
Pana Shehe Mkubwa kabisa nchini kwa watoto 10 yeye pekee ndie akaamua kuwa Muislamu hawa tisa Wakristo hawana shida kabisa undugu upo pale pale japo imani wametofautiana.
Ndio "utumwa wa kifikra" (Mental slavery)..uliopo sasa mkuu..Udini ni sumu mbaya sana inayo sambaza chuki baina ya wanadamu.. Dini sio ya Mungu iwe ukristo au uislamu, Mungu hana dini.Dini zote ni za mwanadamu zilianzishwa na mwanadamu na kuwekwa kwenye maandiko na maandishi ya kibinadamu (Biblia na Quran) wakidai ndio maagizo ya Mungu.kumbe ni imani za kusadikika tu..
 
Kama hazitaki uhojiwe hapo pana shaka,imani ya kweli inahojika
Una uthibitisho wa "Imani ya kweli"tofauti na maandiko ya kidini (Biblia na Quran) unayo weza leta hapa kuthibitisha??...ukitumia Biblia na Quran unakuwa huna hoja tena zaidi ya kutetea Udini jinsi maandiko yako yalivyo kufunza.
 
Umewaza vema, maandiko yanasema "Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio Hali Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha" Zaburi 1:1, lakini pia maandiko hayo hayo yanasema yeye ajuaye kutenda mema na asitende Huyo anatenda dhambi, Kila mtu akomae na imani yake Ili atende mapenzi ya Mungu mwisho wa siku aurithi uzima wa mileke
 
Umewaza vema, maandiko yanasema "Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio Hali Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha" Zaburi 1:1, lakini pia maandiko hayo hayo yanasema yeye ajuaye kutenda mema na asitende Huyo anatenda dhambi, Kila mtu akomae na imani yake Ili atende mapenzi ya Mungu mwisho wa siku aurithi uzima wa mileke
Ni kweli kila mtu akomae na imani na dini kwa jinsi aonavyo yeye na asije akadhani Imani yake ndio sahihi zaidi kuliko ya mwenzake maana Mungu hana dini...ni wanadamu tunajaribu kumgawa Mungu kwenye Udini...
 
Ndio "utumwa wa kifikra" (Mental slavery)..uliopo sasa mkuu..Udini ni sumu mbaya sana inayo sambaza chuki baina ya wanadamu.. Dini sio ya Mungu iwe ukristo au uislamu, Mungu hana dini.Dini zote ni za mwanadamu zilianzishwa na mwanadamu na kuwekwa kwenye maandiko na maandishi ya kibinadamu (Biblia na Quran) wakidai ndio maagizo ya Mungu.kumbe ni imani za kusadikika tu..
Lakini Mungu uongea uonekana kupitia wanadamu.
Vimeandikwa kwa mikono ya wanadamu kwa maagizo ya Mungu
 
Lakini Mungu uongea uonekana kupitia wanadamu.
Vimeandikwa kwa mikono ya wanadamu kwa maagizo ya Mungu
Kama Mungu alia agiza maandiko ya kidini yaandikwe na wanadamu kwa maagizo yake mwenyewe iweje sasa aridhie uwepo wa maandiko mawili yanayo pingana yenyewe kwa yenyewe (Biblia na Quran zinapingana kwenye hoja)....?????
 
Back
Top Bottom