Maaskofu Tanzania watoa Tamko, wakemea udini, ukanda na ukabila!

1. Kwa hiyo, unataka tuamini Mkristo akipasi ina maana Mwislamu kadhulumiwa na akifeli ni haki yake na pia unataka tuamini Mwislamu akipasi ni haki yake na akifeli kadhulumiwa?
2. Sisi wengine ambao tumekaa sehemu za mwambao na baadhi ya mikoa ya Tanzania na tuna marafiki sehemu hizo 'experience' yetu ni kwamba Waislamu wanaamini elimu ya maana ni elimu ya dini na elimu dunia ni ya makafir. After all, haikuwahi kupewa kipaumbele na Waarabu waliotawala sehemu hizo. Na mara nyingi unasikia Waislamu wakisema: "Wakristo kwa elimu dunia wanajitahidi kweli lakini elimu ya dini hawana kabisa. Hii wawaachie Waislamu." Tembelea hiyo mikoa na uone kama kweli mwamko wa watu kielimu unapingana na takwimu zilizotolewa. Mtaa nikakokaa - utaona watoto wenye majina ya Ali, Salumu, Halima wakishatoka madrassa wanacheza mpira au michezo yao hadi wakati wa kwenda kulala usiku wakati wenye majina ya John, Maria, Titus wazazi wao wanawalazimisha kwenda tuition na wakitoka huko wanakalishwa chini kufanya homework. Obviously, matokeo ya darasani ya watoto kama hawa ni tofauti sana. Kwa upande mwingine, wazazi Waislamu ambao wako serious na elimu watoto wao wana'perform' vizuri. Nina family friends (couple) ambao mtoto wao walimpeleka shule ya mission (English Medium School ya Wakatoliki) na muda wote ambao amesoma hapo alikuwa akishika namba 1 (na maksi zake hakupewa Mkristo) na kwa bahati nzuri shule inaruhusu watoto wavae mavazi kulingana na jinsi wazazi wao wanavyowalea kiimani (wenye hijabu au kofia wanavaa pia) ila uniform yao ni moja ili kutoa utambulisho kuwa ni watoto wa shule fulani.
3. Mimi nimetembelea Wilaya ya Mkuranga na pia nawasiliana na baadhi ya walimu wanasema watu hawana mwamko kabisa wa elimu dunia bali elimu ya dini na ngoma za asili. Watoto wanasoma "kilele mama" na walimu wakiwakanya wazazi wao wanakuja juu.
4. Wakristo wao, elimu ya dini ni nzuri na elimu dunia ni nzuri pia maana havipingani provided elimu zote zinamfanya mwandamu ajitambue zaidi yeye ni nani na atoe mchango gani katika kuboresha maisha yake na ya wenzake na pia apate stahili mbele ya Mwenyezi Mungu. Kwa Wakristo in fact wazazi wanamkazania mtoto apate elimu dunia kwanza maana elimu ya dini ipo wakati wote.
5. Kwa hiyo, tafsiri ya hizo takwimu (kama zilivyoletwa humu) si tafsiri ya kuonesha nani kadhulumiwa na nani kadhulumu bali ni nani anachangamkia fursa na nani bado hana mwamko huo.
6. Nawapongeza baadhi ya viongozi wa Waislamu wanaowashauri waumini wapeleke watoto wao shule kuliko kulalamika tu. Maana wanajua suluhisho liko katika elimu hii ambayo baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wanaiita "elimu dunia" ambayo kwao si muhimu sana. Hata baadhi ya viongozi tu wanasema hivyo. "Elimu bora zaidi ni elimu ya dini. Hii nyingine waachieni makafir maana wao hawana dini." Sasa mtu akihubiri hivi halafu wafuasi wake wakifuata anachokihubiri na kuwaletea tatizo la kielimu alaumiwe yule mwingine ambaye anachangamkia fursa?
7. Ndiyo maana mimi huwa naona kama baadhi ya haya malalamiko yanatokana na kujiona kundi moja liko nyuma na kundi jingine mbele (kielimu na kiajira) na sasa badala ya kutafuta chanzo cha tatizo hitimisho linakuwa "lile kundi jingine linatudhulumu".
8. Hata kama kulibadilishwa majina na kutumia namba idadi ya Waislamu baadaye ilikuwa juu (kwani utafiti gani ulionesha ilikuwa juu kwa vile kule kudhulumiwa kulikwisha) na je kwa nini pamoja na kutumia namba bado kuna malalamiko? Pili, walimu wanasahihisha (nasikia) kila mwalimu mmoja swali moja na wako mchanganyiko na siyo kwamba ni wa dini moja na kwa vile ni namba tu zinazoonekana nani anakuwa anaweza kuona huyu ni Mwislamu apewe alama ndogo na huyu ni Mkristo apewe namba kubwa? Mbona wanafunzi Waislamu wanaofanya vizuri wanaendelea kufanya vizuri tu? Jamani tubadilike!

Unajua kina kitu kina shangaza sijui huelewi au unafanya kusudi.
Umepewa takwimu na mifano yakutosha kwamfano:
1. Nime kwambia baada ya Prof Malima kubadili taratibu na kutumia namba kutoa matokeo ya darasa la saba waislam kwaasilimia arubaini waliongezea, hii haikuwa bahati mbaya.
2. Nimekupa mfano wa matokeo ya Form six ya waislam yalio katwa hivi karibu jamaa wakadai ilikuwa computer lkn baada ya kufanya marekebisho yule alie kuwa kapata "D" kabla ya marekebisho akapewa "c" na aliekuwa na "E" akapewa "B" sasa huoni kama jamaa wamekaa ndani tu na kupika matokeo.
3. Bro Mohamed Said amekupa data za kufungwa seminary za kiislam, Nyerere alifanya hilo makusudi.
4.Nyerere alivunja umoja wa waislam uliokuwa namanufaa akaweka BAKWATA na kuweka vibaraka ili kuwaumiza waislam.

SASA WALETA HOJA KUWA WAISLAM HAWAPENDI KUSOMA MBONA KILA KUKIFANYIKA MABADILIKO MATOKEO NAYO YANABADILIKA?
 
Ukombozi kamili wa Waislam kokote waliko DUNIANI utatoka kwa Waislam wenyewe pale watakapokaa chini kutafakari na kubaini mapungufu yao wenyewe na DINI yao. Wakubali kuwashirikisha na Waislamu wengine wenye mawazo mbadala hata kama mawazo yao yatagusa kitabu chao kitukufu, Quran.

Vinginevyo kama wataendelea kuwalaumu watu wengine, kuwatafuta kuwaua, kuwajengea kashfa za kubumba, kujisikia kudhulumiwa kwa kila jambo, kutanguliza DINI yao kwa kila jambo, tutakesha na suluhu haitakuwepo.

Dunia hii na hususan TANZANIA hii ni yetu sote. Hakuna siku wala saa NCHI hii itaongozwa au kutawaliwa KIDINI. Kwa sisi wengine ni TANZANIA kwanza hayo mengine na hasa hayo ya kuletewa kama DINI yaje baadae yatusaidie namna nzuri ya kwenda mbinguni, kuzikana, kuoana na kutambika.
 
Kwani hiyo misamaha ya kodi waislam wamenyimwa? Kwanini mnawalalamikia wakristo kwa uzembe wenu wa kuchangamkia fursa zilizo sawa na wazi kwa madhehebu yote?
Fursa waislam wanachangamkia sana ila tatizo hawa maaskofu ndo wamekuwa mstari wa mbele kupinga kwa matamko mbalix2 tena ya vitisho, ambayo ndo yametufikisha hapa tulipo hadi tunakosa kuaminiana na kuvumiliana. unapoongelea mou ya wakristo, mnaona ni haki, lkn tunapoongelea mou ya waislam inakuwa sio haki, kwa hiyo hapo ni uzembe au mfumo kristo umeziba firsa na kukwamisha makusudi kwa visingizio ambavyo havina mashiko. ni vema mkaelewa waislamu sio wajinga ila upole na heshima na roho ya uvumilivu ndo imefanya TZ ifike hivi leo. lkn bila ya hivyo sidhani kama tungekuwa na tz ya hivi leo ilivyo.
 
Fursa waislam wanachangamkia sana ila tatizo hawa maaskofu ndo wamekuwa mstari wa mbele kupinga kwa matamko mbalix2 tena ya vitisho, ambayo ndo yametufikisha hapa tulipo hadi tunakosa kuaminiana na kuvumiliana. unapoongelea mou ya wakristo, mnaona ni haki, lkn tunapoongelea mou ya waislam inakuwa sio haki, kwa hiyo hapo ni uzembe au mfumo kristo umeziba firsa na kukwamisha makusudi kwa visingizio ambavyo havina mashiko. ni vema mkaelewa waislamu sio wajinga ila upole na heshima na roho ya uvumilivu ndo imefanya TZ ifike hivi leo. lkn bila ya hivyo sidhani kama tungekuwa na tz ya hivi leo ilivyo.
Ipi hiyo? Mbona jamaa(JK) aliwauliza kule kwenye baraza la Eid kama mmeomba halafu mkanyimwa?
 
Ipi hiyo? Mbona jamaa(JK) aliwauliza kule kwenye baraza la Eid kama mmeomba halafu mkanyimwa?
Bado wanahangaika na "dhulma" alizowafanyia Mwalimu mpaka kieleweke. Ikithibitika, Mwalimu avuliwe vyeo na nafasi zote alizowahi kushika nchi hii. Tuwatangaze akina Sykes, Plantan, Takadir,..., kwamba wao ndio walistahili nafasi hizi isingekuwa "dhulma" ya Mwalimu pamoja na utata wa URAIA wao!
 
Bado wanahangaika "dhulma" alizowafanyia Mwalimu mpaka kieleweke. Ikithibitika, Mwalimu avuliwe vyeo na nafasi zote alizowahi kushika nchi hii. Tuwatangaze akina Sykes, Plantan, Takadir,..., kwamba wao ndio walistahili nafasi hizi isingekuwa "dhulma" ya Mwalimu pamoja na utata wa URAIA wao!

Maskhara si mazuri wakati tunakuwa na mjadala huu uloletwa na Maaskofu.

Hawa ni watu wenye heshima zao ni lazima na sisi tuonyeshe heshima na
michango yenye adabu.
 
Bandugu, acheni kuwasemea marehemu...kwani mnazo references zozote zinazoonyesha prof Haroub Othman kwa maneno yake mwenyewe alisema alimuuliza nyerere mara nyingi bila kupata majibu?

Hapa si mahali pa utani kwa hiyo ndugu yangu kutuita sisi ''bandugu'' siyo mahali pake hapa. Hii ni JF kwa watu wa fikra. Soma hii hapa chini yaweza kukupa picha:

The late Prof. Haroub Othman after reading Sheikh Ali Muhsin's book Conflict and Harmony in Zanzibar and the writer's book The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 -1968 The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press, London 1998 and having come across hitherto unknown information on Nyerere was devastated because he was a great admirer of Nyerere as a patriot and a nationalist. The two books had painted him differently. Prof. Haroub confronted Nyerere and told him that the allegations in those two works have tarnished his image and he advised him to respond to them. Nyerere never did. Christian lecturers at Dar es Salaam University are discouraging students from making references to those two books. Dr. Harith Ghassany's book Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru, has also come up with more information on Nyerere hitherto unknown in the Zanzibar Revolution and the bloodbath which followed.
 
Akisoma tamko hilo kwa niaba ya Wengine Askofu Dr Martin F. Shao kwenye Ibada ya Taifa ya Christmass inayorushwa na TBC Kwaniaba ya Jukwaa la Kristo Tanzania amedai

1.Waislamu wanaeneza kashfa dhid ya Wakristo kwa kutumia chombo cha habari na kwa kutumia DVD, CD, KANDA, Mihadhara huku Serikali ikiwa Kimya bila kuchukua hatua ina maana inakubaliana nayo kwanini serikali iko kimya?

2. Kuhusu kuchoma Quruan jambo hilo linafanywa na waislamu wenyewe akatoa mfano ilitokea huko Zanzibar

3. Kuchoma makanisa Wakristo wachukue tahadhari maana Serikali si mbagala tu ilikuwa kimya wakadai hawakujua wakati waliambiwa.

4. Momerandamu wamesema walingia ubia kuendesha shule na afya na Serikali kama wanadai wanapendelewa serikali ijitoe izirudishe au izichukue. Kwanini hawalitolei ufafanuzi jambo hili wako kimya kashfa zinasamba

5.Madai ya waislamu nchi inaongozwa Kikristo wamesema ni 1 ya kashfa katiba hairusu.Pia wametolea mfano kwa kutaja Raisi,makamu,mkuu usalama,Jajimkuu na Zanzibar100% Waislamu
Wana Jamvi Hapo vp?

Funika KOmbe wanaharamu apite, aaskofu wacheni chokochoko.hivi sasa tumieni aman iliokuwepo kueneza neno la bWANA, MKIICHEZEA AMANI DINI YA uKIRSTO ITAKUJA KUA DINI YA MSITUNI.
Ushauri wa bure kwa Askofu Michael Hafidh kwa vile wewe ni ndugu yangu wa damu, usiwafate huo. kuwakiongozi kama aliyekutanguli Askofu Douglas SEif(toto) Wakiristo wa Zanzibar wanaishi vizui sana na waislamu. Matatizo wanaaanza kuyaleta hawa wakiristo wahamiaji kutoka bara ambao hafuati desturi na silka za watu wa zanzibar. wazazazi wako M ichael wapo zanzibar zamanina nakumbuka mama zako wadogo hawawzi kutoka nje na kutembea bila baibui, hizo ndio desturi za Wazanzibari. waisalamu zanzibar ni asilimia 99% ukiatoa wakiristo wakuletwa unategemea nini ktika safu ya uongozi Zanzibar. Jikumbushe wewe mwenyee ulivyowekewa vikwazo na wakirsto wa Bara usiwe Askofo kiongozi wa kanisa la Mkunzini umesahau? Ai Ubaguzi wa kidini huo msaada wa kupta wadifa huo si hao viongozi waislamu waiokusaidia? uwe na fadhila
Hivi nani anhatarisha amani wakirsto kutoka bara wanaopita nyumba kwa nyumba katika vitongoji vya mji wa zanzibar kuwalazimisha waislamu kusikilza neno la mungu majumbani ma na kuwacha vipeperushi?
Nani anahataruisha amani kulazimisha kujenga kanisa sehemu hat mkirsto mmoja hakuna

Hivi Dini ni moja ya mambo ya muungano? mbona kanisa CCT inaiandama zanzibar kila kukicha na kuingilia jinsi ya kuchaguana. Huo si uchochezi?
 
Bado wanahangaika na "dhulma" alizowafanyia Mwalimu mpaka kieleweke. Ikithibitika, Mwalimu avuliwe vyeo na nafasi zote alizowahi kushika nchi hii. Tuwatangaze akina Sykes, Plantan, Takadir,..., kwamba wao ndio walistahili nafasi hizi isingekuwa "dhulma" ya Mwalimu pamoja na utata wa URAIA wao!

Ukihamaki mtu unasema ovyo na matokeo yake unavuruga mjadala.
Kuna wakati nafurahi kupambana na wewe lakini sasa kwa mtindo huu
utanikatisha tamaa.

Sijapata hata mahali pamoja katika kitabu changu kusema kuwa Nyerere kafanya
khiyana katika nafasi ya urais wa TAA/TANU.

Ninachosema siku zote ni kuwa yeye Nyerere khiyana yake ipo katika kuficha ukweli
wa historia ya maisha yake kuanzia pale Mtaa wa Aggrey na Sikukuu walipokuwa wanafanya
mikutano ya siri nyumbani kwa Abdu hadi kufika Arnautoglo Hall April 17, 1953 alipomshinda
Abdu kwenye uchaguzi wa TAA.

Historia hii ndiyo aliyokuwa akiiogopa Nyerere na kwa bahati mbaya inakuchomeni sana.
Sijui sababu yake ni nini khasa.
 
Maskhara si mazuri wakati tunakuwa na mjadala huu uloletwa na Maaskofu.

Hawa ni watu wenye heshima zao ni lazima na sisi tuonyeshe heshima na
michango yenye adabu.
Heri yangu mimi ninayeleta maskhara kwa walio hai. Kuliko wewe unaeyaleta kwa Mwalimu aliyefariki zaidi ya miaka kumi iliyopita. Unajua mengi unayoyasema kuhusu Mwalimu ni UONGO wa hali ya juu kabisa. Unajisikiaje kwa mfano unapokanusha kuwa Mwalimu hakutaifisha shule za Wakristo ili Waislam nao wapate nafasi ya kusoma? Sio maskhara hayo?
 
Ipi hiyo? Mbona jamaa(JK) aliwauliza kule kwenye baraza la Eid kama mmeomba halafu mkanyimwa?
labda wanamfumo walikuwa hawajamfikishia, kwani sinimekwambia watendaji wako ndo wanaoziba lkn sidhani ile kauli kama atarudia tena kuitoa.
 
kama vipi munachomewa makanisa yenu ukiona hivyo hawawataki ondokeni kwetu nendeni kwenu
 
Ukihamaki mtu unasema ovyo na matokeo yake unavuruga mjadala.
Kuna wakati nafurahi kupambana na wewe lakini sasa kwa mtindo huu
utanikatisha tamaa.

Sijapata hata mahali pamoja katika kitabu changu kusema kuwa Nyerere kafanya
khiyana katika nafasi ya urais wa TAA/TANU.

Ninachosema siku zote ni kuwa yeye Nyerere khiyana yake ipo katika kuficha ukweli
wa historia ya maisha yake kuanzia pale Mtaa wa Aggrey na Sikukuu walipokuwa wanafanya
mikutano ya siri nyumbani kwa Abdu hadi kufika Arnautoglo Hall April 17, 1953 alipomshinda
Abdu kwenye uchaguzi wa TAA.

Historia hii ndiyo aliyokuwa akiiogopa Nyerere na kwa bahati mbaya inakuchomeni sana.
Sijui sababu yake ni nini khasa.
Mazungumzo ya uhakika ya Mwalimu na akina Abdu wewe ulisimuliwa tu. Haukuwepo. Aliyekusimulia alichagua sana ya kukueleza. Na wewe ukatumia kipaji chako cha usanii kuyahariri vizuri unavyotaka kwa maslahi yako na lengo lako. Waliokusimulia pia walishaanza kutofautiana na Mwalimu. Ni rahisi kufahamu walichokuambia kuhusu Mwalimu.

Mbaya zaidi, haukumshirikisha Mwalimu. Ukataka akisoma ulooyandika akujibu! Mwalimu atakuwa alikusoma akakupuuza. Mohamed, tofautisha HISTORIA na SIMULIZI. Sio kila simulizi ni historia. Ni vigumu sana kuamini HISTORIA iliyoandikwa na mtu mmoja. Hauwezi kujua alilenga nini kwenye historia ile.
 
Hapa si mahali pa utani kwa hiyo ndugu yangu kutuita sisi ''bandugu'' siyo mahali pake hapa. Hii ni JF kwa watu wa fikra. Soma hii hapa chini yaweza kukupa picha:

The late Prof. Haroub Othman after reading Sheikh Ali Muhsin's book Conflict and Harmony in Zanzibar and the writer's book The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 -1968 The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press, London 1998 and having come across hitherto unknown information on Nyerere was devastated because he was a great admirer of Nyerere as a patriot and a nationalist. The two books had painted him differently. Prof. Haroub confronted Nyerere and told him that the allegations in those two works have tarnished his image and he advised him to respond to them. Nyerere never did. Christian lecturers at Dar es Salaam University are discouraging students from making references to those two books. Dr. Harith Ghassany's book Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru, has also come up with more information on Nyerere hitherto unknown in the Zanzibar Revolution and the bloodbath which followed.
Wewe ndiyo unaleta utani. Mwenzako nilimuuliza ni wapi tunaweza kuona kwa maneno yake mwenyewe Prof Haroub Othman akisema alimuuliza Nyerere mara nyingi lakini Nyerere hakumjibu. Nyerere alifarikiri 14 October 1999. Prof Haroub Othman alifariki miaka karibu 10 baadaye , June 28 2009. Katika hiyo miaka kumi hatuwezi kupata nukuu yeyote kutoka kwenye gazeti au papers au media nyingine ikionyesha kwa maneno yake mwenyewe Prof Haroub Othman akisema alimconfront Nyerere ? Ni wewe peke yako uliyemsikia?
Ningependa kujua, hivi issue hii ya Prof Haroub Othmna kumconfront Nyerere ilikuwa tayari kwenye papers zako wakati Prof bado yupo hai au baadaye?
 
Wewe ndiyo unaleta utani. Mwenzako nilimuuliza ni wapi tunaweza kuona kwa maneno yake mwenyewe Prof Haroub Othman akisema alimuuliza Nyerere mara nyingi lakini Nyerere hakumjibu. Nyerere alifarikiri 14 October 1999. Prof Haroub Othman alifariki miaka karibu 10 baadaye , June 28 2009. Katika hiyo miaka kumi hatuwezi kupata nukuu yeyote kutoka kwenye gazeti au papers au media nyingine ikionyesha kwa maneno yake mwenyewe Prof Haroub Othman akisema alimconfront Nyerere ? Ni wewe peke yako uliyemsikia?
Ningependa kujua, hivi issue hii ya Prof Haroub Othmna kumconfront Nyerere ilikuwa tayari kwenye papers zako wakati Prof bado yupo hai au baadaye?
sweke34,
Prof Haroub Othmani ni mmoja kati ya MaProfesa wazuri mno Chuo Kikuu cha Dar kimepata kuwa nao. Hakuhangaika na DINI yake, hakuhangaika na UZanzibar wake. Tuliomzoea tulimwita "mzee na kadhalika", neno alilopenda kulitumia sana kila alipohojiwa. Mohamed anataka kumchafua tu.
 
Last edited by a moderator:
Hshima sana wanajamvi,

Upo mjadala mrefu na mpana hapa JF baina ya wanajamvi na Ustadhi Mohamed Said kwa wasiomjua mnaweza kubishana bila kufikia muafaka wa maana.Ninakumbuka kuna maswali aliulizwa na wanajamvi wafuatao Nguruvi3 Mzee Mwanakijiji JokaKuu Mkandara Mwita Maranya akaingia mitini (akala kona).
Muhimu sio majina ya waliomuuliza.Tunataka hayo maswali aliyoulizwa tuone kama kweli ni magumu.Nijuavyo mimi masuali ya maaskofu na ya kwenu huwa yana majibu rahisi sana.Yawezekana siku hiyo bro.Mohammed alikuwa ameshughulishwa na jambo fulani.Ukirejea maswali sisi wadogo zake tutajibu na yeye anaweza akasahihisha ikiwa tutakwenda kombo.
Inatia huruma kwa maaskofu wa madhehebu yote kuketi na kutoa tamko la majungu kama hili.
 
sweke34,
Prof Haroub Othmani ni mmoja kati ya MaProfesa wazuri mno Chuo Kikuu cha Dar kimepata kuwa nao. Hakuhangaika na DINI yake, hakuhangaika na UZanzibar wake. Tuliomzoea tulimwita "mzee na kadhalika", neno alilopenda kulitumia sana kila alipohojiwa. Mohamed anataka kumchafua tu.
Namfahamu vizuri sana. Alikuwa ni jirani yetu zaidi ya miaka 20 paple udsm. Inaniuma sana mtu ambaye ni kama mzazi wangu akiingizwa kwenye uchafu wa uchochezi.
 
Back
Top Bottom