Maaskofu Tanzania watoa Tamko, wakemea udini, ukanda na ukabila!

adolay, JokaKuu,

Matatizo wa Waislam wa Somalia wala hayana uhusiano wowote na Uislam. Unaweza kuwa Muislam lakini kama haufuati mafundisho yake ni kazi bure.

Wasomali wameweka Uislam wao pembeni na kufuata mambo yao ya makabila na koo ndiyo maana unaona kila siku mauaji ya wenyewe kwa wenyewe, kila sehemu kuna kiongozi wa koo fulani kutoka kabila fulani mpaka ukafikia kabila fulani hawapati na kabila fulani. Wakati katika mafundisho ya Uislam hakuna kabila bora wala koo bora, mbora ni yule anayemcha Mwenyezi Mungu.

Hivi mauaji ya Rwanda yamesababishwa na Wakiristo? Mauaji ya Adolf Hitler, ya watu 12,000,000 mwaka 1939-1945 yana uhusiano na Ukiristo. Mauaji ya wa Congo 8,000,00 yaliyofanywa na Leopold II wa Belgium, yana uhusiano na Ukiristo? Mauaji ya Cambodia ya watu 1,700,000 yaliyofanywa na Pol Pot yana uhusiano na Ukiristo?

Huu ni mfano mdogo matatizo ya kibinadamu msitake kuyanasibisha na dini.

Umeongea point mkuu
 
Last edited by a moderator:
Umeongea point mkuu


Mhandisi 2009

Sifa kubwa ya mhandisi ni kusection na kuvitazama vitu kwa maana ya kuchakata hiden details . sijui umetumia taaluma ya jina lako vema?

Ameongea ukweli upi tusaidie wewe maana nimefafanua Suala la Somalia, kama ilivokuwa kwa mkuu wangu Sijali hapo chini. wewe soma kwa makini halafu utusaidie huo ukweli ulouona wewe kwaturejeshea majibu ya swali moja baada ya jengine mpaka chini kabisa.

quote_icon.png
By Sijali
<Mbona hoja zako Nyerere hazina mashiko wala mantiki? Bw Said anakupa kila kitu na ushahidi wewe unaropoka tu kihuni.Pia, kwa nini kuihusisha Somalia? Ni kwa sababu wataka kuonesha kuwa Waislamu ,naturally and inherently' hawasomi, hawapendi kusoma au hawawezi kuongoza Wizara au Idara za elimu? Umepata wapi dhana hiyo? Mbona hukuulizia juu ya nchi za Kiislamu zenye mifumo mizuri hata Wazungu huenda sasa kusoma huko, kama Emirates?




mkuu Sijali

Swali la kwanza nilikuuliza Nani kawazuia waislam kuwa na Mou yao, nikasema tukimaliza tutajzdili kwanini Mohamedi analalamikia

MOU ya wakristo.



Kuhusu somalia tumetokea mabali agalia hapo chini tumetokea wapi, isitoshe kama wanahistoria hatuwezi kujifungia humu ndaniya Tanzania bila kuangalia mifumo mingine, ilikuwa fair nimekariri mara kadhaa baada ya kudadisi na kuijadili somalia tutaenda nchi zingine, Syria, Libya, DRc, afghanstan nk. halafu tulinganishe na hapa kwetu. Huwezi kujifunza kwamba kunamakosa au mafanikio ukiwa umejifungia ndani ya nyumba yako. Inakupasa kutoka nje ya nyumba yako, tembea kwa majirani ujifunze halafu upime ubora wa mafanikio yako au udhaifu wako kujirekebisha. Sasa utakuwa umeelewa tunaweza kuendelea tukianzia na swali la kwanza hapo juu.

karibu mkuu wangu.




quote_icon.png
By Mohamed Said Kitabu changu kinaitwa, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika.''

Hakina uhusiano wowote na Somalia.
Kwa ajili hii ni vigumu kwangu kujibu maswali ya Somalia na Nyerere.





Ninakuulizen somalia na nyerere kwasababu waislam wa somalia wanamatatizo makubwa ya kijamii, kisiasa, kieliemu, afya nk

Nani mchawi maana hapa kwetu kwa mujibu wa hadithi zako ni Nyerere. (Tunaongelea matatizo ya waislamu na wanaowahujumu)

Watanzania (Waislam, wakristu pia wa imani zingine na wasio amini) wanamatatizo aghalabu si makubwa kama ya wasomali.

1. Kwanini useme waislam wa Tanzania ni hujuma za nyerere na kwanini wasiwe waislam wa somalia? kunatofauti ya uislam wa somalia na ule wa tanzania?



2. Ni mfumogani unaotawala somalia na kwanin na nani tumpe lawama kwa yanayoendelea?
 
Hao watumishi wa idara za serikali na mahakama anaowataja tayari walishakuwa viongozi waandamizi kwenye idara husika kabla ya rais Kikwete hajaingia madarakani.Kwa mtazamo wangu ni yeye huyo muhubiri ndio mdini na leo hii amemua kuonyesha ulimwengu kuwa nchi hii ni mfumo kristo kwa kutopenda kuona waislam kwenye nafasi za uongozi.
Mfumo kristo! 90% uongozi wa NCHI waislamu Tanzania Bara
Mfumo Kristo 100% uongozi wa tanzania visiwani waislamu.
Utakuwa mtindio wa ubongo ukifikiria hivi!
 
Ritz said:
Matatizo wa Waislam wa Somalia wala hayana uhusiano wowote na Uislam. Unaweza kuwa Muislam lakini kama haufuati mafundisho yake ni kazi bure.
Ritz said:
Wasomali wameweka Uislam wao pembeni na kufuata mambo yao ya makabila na koo ndiyo maana unaona kila siku mauaji ya wenyewe kwa wenyewe, kila sehemu kuna kiongozi wa koo fulani kutoka kabila fulani mpaka ukafikia kabila fulani hawapati na kabila fulani. Wakati katika mafundisho ya Uislam hakuna kabila bora wala koo bora, mbora ni yule anayemcha Mwenyezi Mungu.

Hivi mauaji ya Rwanda yamesababishwa na Wakiristo? Mauaji ya Adolf Hitler, ya watu 12,000,000 mwaka 1939-1945 yana uhusiano na Ukiristo. Mauaji ya wa Congo 8,000,00 yaliyofanywa na Leopold II wa Belgium, yana uhusiano na Ukiristo? Mauaji ya Cambodia ya watu 1,700,000 yaliyofanywa na Pol Pot yana uhusiano na Ukiristo?

Huu ni mfano mdogo matatizo ya kibinadamu msitake kuyanasibisha na dini.


Ritz,

..ushauri wako nimejaribu kuuzingatia sana maishani na hata ktk mijadala ya hapa JF.

..mimi huwa sipendi kujadili dini au imani za watu. sana sana ukinikuta ktk mijadala kama hii, huwa najaribu kuji-confine kujadili waumini wa dini hizo na matendo yao tu.

..mwisho, nadhani wa-Tanzania tujielekeze zaidi katika yale masuala yanayotuunganisha, na siyo yale yanayotutenganisha na kututofautisha.

..Wamarekani wana asili za majimbo tofauti tofauti, lakini kila mara wanapohitilafiana hawaishi kukumbushana kwamba wao ni Wamarekani kwanza. I wish wa-Tanzania tungekuwa na utamaduni huo wa kuupenda na kuuhifadhi u-Tanzania wetu kuliko kitu chochote kile.
 
Last edited by a moderator:

Ritz,

..ushauri wako nimejaribu kuuzingatia sana maishani na hata ktk mijadala ya hapa JF.

..mimi huwa sipendi kujadili dini au imani za watu. sana sana ukinikuta ktk mijadala kama hii, huwa najaribu kuji-confine kujadili waumini wa dini hizo na matendo yao tu.

..mwisho, nadhani wa-Tanzania tujielekeze zaidi katika yale masuala yanayotuunganisha, na siyo yale yanayotutenganisha na kututofautisha.

..Wamarekani wana asili za majimbo tofauti tofauti, lakini kila mara wanapohitilafiana hawaishi kukumbushana kwamba wao ni Wamarekani kwanza. I wish wa-Tanzania tungekuwa na utamaduni huo wa kuupenda na kuuhifadhi u-Tanzania wetu kuliko kitu chochote kile.

JokaKuu,

Maneno ni ya ujenzi na ni ujumbe tosha kwa watanzania wote wanaoitakia mema nchi yetu.
 
Last edited by a moderator:
Mimi nimeandika kitabu cha Abdu Sykes.
Unaniuliza kuhusu MUM.

Ingekuwa najua ningekujibu.
Ingekuwa bora swali hilo wakajibu wenyewe MUM.

Mimi nitafurahi sana iwapo itaandikwa historia mathalan ya mashujaa kutoka mikoani.

Hilo la haki na usawa halipo.
Usawa haupo ndiyo maana tunatahadharisha.

Hapa ishu siyo MUM bali ni ulinganifu wa chuo hiki na kile ambacho shehe hassan amir alikusudia kujenga wakati wa uhuru na matokeo ya chuo hicho kwa jamii hasa kipindi hicho ambapo nchi ilikuwa changa yenye migawanyiko ya aina mbalimbali na idadi kubwa ya raia walikuwa hata hawaongei lugha moja.
Ukiweka udini pembeni, ukafikiria kama binadamu wa kawaida, utaona waziwazi kuwa Nyerere (RIP) alikuwa sahihi na shehe Hassan bin Amir (sina uhakika kama bado yu hai au la) hakuwa sahihi kwa mazingira na mahitaji ya wakati huo.
That being said, mimi binafsi nitaendelea kukuombea wewe mzee Mohammad Said, ili siku moja uokoke na uione neema itokayo kwa Mungu baba, Mwana na Roho Mtakatifu na nuru ile ing'aayo ikitokea moja kwa moja Sayuni (Zion) penye maskani ya MUNGU.
 
Hapa ishu siyo MUM bali ni ulinganifu wa chuo hiki na kile ambacho shehe hassan amir alikusudia kujenga wakati wa uhuru na matokeo ya chuo hicho kwa jamii hasa kipindi hicho ambapo nchi ilikuwa changa yenye migawanyiko ya aina mbalimbali na idadi kubwa ya raia walikuwa hata hawaongei lugha moja.
Ukiweka udini pembeni, ukafikiria kama binadamu wa kawaida, utaona waziwazi kuwa Nyerere (RIP) alikuwa sahihi na shehe Hassan bin Amir (sina uhakika kama bado yu hai au la) hakuwa sahihi kwa mazingira na mahitaji ya wakati huo.
That being said, mimi binafsi nitaendelea kukuombea wewe mzee Mohammad Said, ili siku moja uokoke na uione neema itokayo kwa Mungu baba, Mwana na Roho Mtakatifu na nuru ile ing'aayo ikitokea moja kwa moja Sayuni (Zion) penye maskani ya MUNGU.

Ahsante kwa kheri zote ulizoniombea.
Naamini zinatoka moyoni.

Sheikh Hassan bin Amir amekufa mwaka 1979 na Nyerere alihudhuria khitma yake Msikiti wa Mtoro.

Katika mambo ambayo wengi wangependa Nyerere ayajibu ni hilo la Chuo Kikuu cha Chang'ombe na yeye kuivunja EAMWS.
Umemjibia kuhusu chuo hicho.

Nyerere hakupata kusema kuhusu sakata lile ingawa analaumiwa kwa udini kwa kuvunja EAMWS ili kuwakosesha Waislam chuo wapate kudhoofika.

Waislam wanahesabu kitendo kile ndio mwanzo wake wa vita dhidi ya Uislam.
 
Ahsante kwa kheri zote ulizoniombea.
Naamini zinatoka moyoni.

Sheikh Hassan bin Amir amekufa mwaka 1979 na Nyerere alihudhuria khitma yake Msikiti wa Mtoro.

Katika mambo ambayo wengi wangependa Nyerere ayajibu ni hilo la Chuo Kikuu cha Chang'ombe na yeye kuivunja EAMWS.
Umemjibia kuhusu chuo hicho.

Nyerere hakupata kusema kuhusu sakata lile ingawa analaumiwa kwa udini kwa kuvunja EAMWS ili kuwakosesha Waislam chuo wapate kudhoofika.

Waislam wanahesabu kitendo kile ndio mwanzo wake wa vita dhidi ya Uislam.

Mzee Mohammad Said, ninakuombea kheri kutoka moyoni bila kinyongo, natambua kuwa mjadala huu wakati mwingine unavuta hisia za wachangiaji, kwa upande wangu nimekuwa najaribu kuanisha hoja ili hasa tujue tunachokijadili ambacho kinaweza kuwa na manufaa kwa sisi watanzania wa leo na kwa vizazi vyetu vijavyo.
Asante kunifahamisha kuwa shehe Hassan bin Amir (RIP) hatunaye tangu 1979
 
Aliyeanzisha mambo ya udini Kikwete na kuukoleza kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 analialia sasa yamemtokea puani
 
Mohamed Said hayo unayoyasema hayalisaidii Taifa kwa sasa wala hayawasaidii waislamu wenyewe.

Kama Nyerere hakutaifisha shule ili waislamu wasome kumbe alifanya hivyo ili wasome akina nani. Wakristo tayari walikuwa na shule zao na mfumo wa elimu uliokuwepo tayari ulikuwa unawapendelea wao. Hivyo kama shule zingeachwa mikononi mwao ni wazi wao ndio wangeendelea kufaidika zaidi.

Nakubali kuwa waislamu kupitia EAMWS walianza kujenga shule zao, lakini ukweli ni kuwa wasingeweza kufikia ubora na idadi ya shule za kikristo. Tatizo lao la kwanza ilikuwa ni kupata walimu wa kufundisha shule hizo wenye sifa sawa na walimu wale wa shule za kikristo, pili ingekuwa ni uzoefu wa kuendesha shule hizo.

Wakati bado wanahangaika kutatua changamoto hizo wakristo huku wakijua kuna tishio la ushindani wangeongeza kasi zaidi kuwapa elimu waumini wao na darasani wangeeleza pia kuwa majirani zao wanashindana nao hivyo waongeze nguvu. Matokeo yake mshikamano wa kitaifa usingekuwepo kama unavyouona leo. Hasira ya waislam ingekuwa kubwa zaidi ya hii tunayoona.

Serikali inayoona mbali haiwezi kukubali hali hii kuendelea katika nchi. Mwalimu Nyerere alichukua hatua za haraka kuweka shule zote chini ya serikali ili kuepusha vurugu hiyo ambayo tayari ilikuwa iko wazi kutokea. Serikali ndiye "referee" ambaye angeweza kutenda haki katika mchezo na kwa kweli alitenda haki kwa mchezo huo.

Katika mchezo yule anayefanya juhudi ndiye hushinda mchezo, ukitegemea kushinda kwa kupendelewa hutafanya juhudi katika mazoezi. Mbona wapo waislam wengi waliosoma kipindi hicho tena kutoka familia maskini kabisa na wengine ni maprofesa leo. Je, hawa walifikaje huko? nani aliwapendelea? Naamini ukiwauliza watakujibu kuwa ni juhudi zao za kukazania masomo ndizo ziliwafikisha hapo.

Alichotaka kukifanya Prof. Kighoma Malima ni kuchezesha mchezo kwa upendeleo. Kuteua wakurugenzi wanne waislam kwa mara moja sijui alikusudia nini. Wakurugenzi waislam haikuwa tatizo kwani hakuna udini serikalini. Tatizo ni waraka wa siri aliomwandikia Rais kuwa kuna upendeleo katika mfumo wa elimu.

Hata hivyo alitendewa haki kwani huwezi kumhukumu mtu pasipo kumsikiliza. Alipoitwa kwenye NEC ya CCM naamini alipewa nafasi yakutetea hoja yake. Kwa kuwa hoja yake haikuwa na ushahidi hivyo ilikosa mashiko ndio maana hata waislam wenzake hawakumuunga mkono. Siamini kama angeweza kutoa ushahidi waislam wenzake wangekataa kumuunga mkono na hapo serikali ingekuwa imeumbuka.

Tuache kuleta chokochoko hizi. Huu sio wakati wa kulaumu, fursa ziko wazi kwa wote ni wajibu wa kila mtu kuzichangamkia. Hivi sasa wakristo wanaanzisha vyuo vikuu kwa wingi sana. wakatoliki hivi sana wana matawi mengi ya Vyuo vikuu karibu kila kanda. Huenda vitakuwa vingi kuliko vya serikali, Je, huo nao ni upendeleo? Walinyang'anywa shule zao lakini wameamua kutokulaumu historia wameanza kujipanga upya.

Nakushauri Mohamed Said kama sehemu ya wasomi wakiislam, kaeni kitako mjipange muweke mkakati maalum wa kushindana katika elimu. Uwanja uko "level" ni juhudi binafsi ya mtu ndiyo itakayompa ushindi.

Nyerere hakutaifisha shule ili Waislam wasome.

Hebu soma hii hapa chini:

Tarehe 5 Novemba, 1985 kabla hajastaafu urais, Nyerere aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam. Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo. Wazee hawa wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono Nyerere wakati wa kudai uhuru. Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru. Nyerere alisema kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:

Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo. Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho. Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo. Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.[1]

Hotuba hii ilikuwa ya ulaghai. Ukweli ni kuwa miongo mitatu baada ya uhuru Waislam hawajanufaika chochote wako katika hali ile ile aliyowaacha wakoloni au mbaya zaidi. Sivalon amefichua kuwa Kanisa limeweza kujenga himaya yake ambayo inahodhi asilimia 75% za viti katika Bunge la Tanzania. Kati ya viti hivyo 75% vipo mikononi mwa Wakatoliki na vilivyobaki vimegawika kati ya Waislam na Wakristo wa madhehebu nyingine.[1]Baada ya kupatikana uhuru, Kanisa lilipohisi wasiwasi, limeweza kwa urahisi kabisa kuwazuia na kuwadhibiti Waislam. Serikali imeweza kutumia nguvu iliyokuwanayo katika kudhibiti siasa kuzuia harakati za Waislam kudai fursa sawa na Wakristo katika kugawana madaraka katika serikali. Kanisa limehakikisha kuwa kupinduliwa kwa ukoloni si kizingiti kwa Ukristo, ingawa ingetegemewa kuwa Kanisa lingedhirika kwa kuanguka kwa ukoloni. Katika miaka yake zaidi ya mia moja, Kanisa lilikuwa limestarehe kama muokozi wa nafsi na watu wenyewe. Kanisa lilikuwa salama na halikupambana na msukosuko wowote kutoka kwa serikali kwa kuwa lilikuwa Kanisa ndilo lilishika hatamu ya serikali.

Baada ya kueleza hayo yote ni muhimu sasa kuangalia jinsi ukereketwa wa Kikristo unavyofanya kazi katika serikali na jinsi kazi hiyo inavyoathiri Uislam. Wizara ya Elimu inachukuliwa kama mfano kwa sababu ya umuhimu wake katika jamii. Katika wizara hii, inaweza kuonekana kwa uwazi kabisa jinsi Ukristo unavyofanya kazi na jinsi udini ulivyoshamiri katika kugawa nafasi muhimu kati ya Waislam na Wakristo. Ilikuwa katika wizara hii katika historia ya Tanzania ndipo kwa mara ya kwanza waziri Muislam alipochaguliwa kuongoza wizara, Kanisa likaingilia kati waziwazi kumpiga waziri vita na kuhoji nafasi nyingine za juu ambazo zilipewa Waislam. Serikali haikuweza kupingana na Kanisa na waziri huyo, marehemu Profesa Kighoma Ali Malima aliondoshwa katika wizara hiyo.

Mwaka 1987 Profesa Malima aliteuliwa kuwa Waziri wa Elimu akiwa Muislam wa kwanza kushika nafasi hiyo. Mawaziri wanane waliopita walikuwa Wakristo. Kulikuwa na malalamiko kutoka kwa Waislam kuwa wizara hiyo imegeuzwa jimbo la Wakristo, hasa pale padri alipoteuliwa na Julius Nyerere kuongoza wizara hiyo. Profesa Malima aliposhika wizara hiyo aliona upo umuhimu wa kufanya marekebisho kadhaa ili kurejesha imani ya Waislam katika wizara hiyo. Kulikuwa na tuhuma kuwa Wizara ya Elimu ilikuwa ikiwabagua vijana wa Kiislam kupata nafasi katika vyuo vya elimu ya juu na ilikuwa ikizuia kupanda vyeo kwa Waislam.

Profesa Malima alipoona dhulma ile iliyokuwapo katika wizara ile dhidi ya Waislam, Profesa Malima aliwateua Waislam wanne kushika nafasi katika kurugenzi mbalimbali na akaandika taarifa ya siri kwa Rais Ali Hassan Mwinyi [1]kumtaarifu udini [1]alioukuta katika wizara ile. Katika taarifa ile kwa rais,[1]Profesa Malima alieleza kuhusu kudumazwa kwa Waislam katika mgao wa elimu. Taarifa hii ilivuja kwa vyombo vya habari[1]na kwa Wakristo wengine. Katika watu walioipata taarifa hii ni Rais Mstaafu Julius Nyerere wakati ule akiwa Mwenyekiti wa chama tawala CCM.

Kuwekwa kando kwa Waislam kupo wazi kiasi ya kuwa mtafiti haihitaji hata kufanya utafiti wa kina unaopewa nguvu na takwimu. Mtafiti yeyote wa sayansi ya jamii hatoweza kushindwa kuona ukweli huu kwa macho tu. Hali hii inaonekana katika kila nyanja ya maisha. Utafiti wa kwanza katika tatizo hili la Waislam kudhulumiwa katika ugawaji wa madaraka ulifanywa na vijana wa Kiislam katika jumuiya yao iliyokuwa ikijulikana kama Warsha ya Waandishi wa Kiislam, kwa ufupi ikijulikana kama Warsha.

Kanisa kwa mara ya pili tokea mwaka 1963 ilipata wasiwasi kuhusu mabadiliko ambayo yalikuwa yanafanyika katika Wizara ya Elimu. Lakini katika miaka ya 1980, hali ya mambo yalikuwa yamebadilika sana. Waislam walikuwa wamejizatiti nje ya mfumo wa siasa kiasi ya kuwa hapakuweza kupatika kibaraka katika Waislam ambae angekuwa tayari kutumika kulihami Kanisa. Hali ya uhasama wa wazi kati ya Waislam na serikali ilikuwa imejitokeza wazi kabisa. Hata hivyo mawakala wa kanisa katika serikali walimshutumu Profesa Malima kwa kuwa Muislam mwenye ësiasa kalií. Profesa Malima akatakiwa ahojiwe mbele ya Kamati Kuu ya CCM kwa kuingiza hisia za kidini ambazo zimesababisha uadui baina ya waumini wa dini hizi mbili. Suala hili likajadiliwa Dodoma chini ya uenyekiti wa Julius Nyerere. Lakini badala ya kujadili suala la dhulma kwa Waislam na kulitafutia ufumbuzi, yule anaedhulumiwa ndiye aliyewekwa kizimbani badala ya dhalim anaedhulumu; msukumo wa mjadala ukawa katika uteuzi wa wakurugenzi wanne Waislam aliofanya Profesa Malima katika Wizara ya Elimu. Profesa Malima alionekana amekiuka mwenendo na taratibu zulizodumu katika wizara ile kwa kipindi kirefu ya kuwa ni Wakristo pekee wenye haki ya kushika nafasi za juu katika wizara za serikali. Kwa ajili hii profesa Malima akavuliwa madaraka kama Waziri wa Elimu. Rais Mwinyi alikuwa hana uwezo wa kuhimili nguvu ya Kanisa. Nchi inayodai kuwa ni ya kisekula ilikuwa imeshindwa kwa mara nyingine kuwapa Waislam haki yao waliyohakikishiwa na katiba ya Tanzania.

Kwa nchi ambayo inajigamba kuwa inajali usawa kwa wananchi wake inashangaza kuona kuwa Waislam wanabaki nyuma na juhudi zozote ambazo Waislam watafanya ili kuondoa upogo kati yao na Wakristo na kujiletea maendeleo zinapata upinzani na uadui kutoka na mfumo ule ule unajidai kuwa unasimamisha usawa na haki. Kitu cha kusikitisha ni kuwa hakusimama hata Muislam mmoja katika wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM kumuunga mkono Profesa Malima kwa dhulma ambayo wote walikuwa wanafahamu kuwa imedumu kwa kipindi kirefu. Hata ndani ya Bunge hakuna Muislam aliyekuwa na ujasiri wa kumtetea Profesa Malima.[1]Muislam mmoja, Mwenyekiti wa Mkoa wa Pwani, Masudi Mtandika, aliungana na kambi ya Wakristo katka Kamati Kuu ya CCM kumshambulia Profesa Malima. Msimamo wa Mtandika ulikuwa sawa na ule wa Rajab Diwani na Selemani Kitundu walipomshambulia Bibi Titi Mohamed wakati Kamati Kuu ya TANU ilipokuwa ikijadili EAMWS mwaka wa 1963. Kampeni ya chuki na propaganda dhidi ya Profesa Malima ikaanzishwa na vyombo vya habari ambavyo vyote vilikuwa chini ya miliki ya Wakristo na hivyo chini ya Kanisa.

Aboud Jumbe, [1]rais wa zamani wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa Tanzania, amefanya utafiti kuhusu nafasi ambazo wameshika Waislam katika serikali, Bunge na vyuo vya elimu ya juu. Takwimu alizoonyesha Aboud Jumbe zinatisha. Katika baadhi ya taasisi Waislam wanaonekana kwa kutokuwepo katika taasisi hizo. Utafiti wa Jumbe ulikuwa wa pili katika kueleza tatizo hili la Waislam na kuliweka wazi kwa matumaini ya kuwa labda serikali ingeweza kuhisi kuwajibika na kujaribu kusahihisha makosa hayo.

Majaribio mengine yamewahi kufanyika huko nyuma na watu kama Sheikh Abubakar Mwilima, wakati huo akiwa Mwenyekiti wa JUWATA na katika Kamati Kuu ya chama tawala CCM, alijaribu kuieleza serikali tatizo hili la Waislam. Kitu kimoja mashuhuri kwa wote waliojaribu kuliweka tatizo hili mbele ya serikali wote hao walimalizwa kisiasa. Maisha yao katika siasa yalikatizwa ñ Chifu Abdallah Said Fundikira, Tewa Said Tewa, Bibi Titi Mohamed, Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Mussa Kwikima, Sheikh Abubakr Mwilima, Profesa Kighoma Malima na wengine wengi. Ilikuwa kuanzia hapa ndipo Waislam walianza kunongíona kuhusu njama dhidi yao. Kuwepo kwa njama dhidi ya Waislam kulikuja kudhihirishwa pale watafiti wa Kikristo walipoanza kufanya utafiti kuhusu athari za Ukristo katika utawala wa dola; na bila kujali matokeo ya utafiti kwa hisia za Waislam wakawa wanaeleza jinsi Waislam kwa hila na msaada wa serikali walivyowekwa pembeni katika kugawana madaraka na Wakristo.
 
Mohamed Said hana anachoweza kuwasaidia waislam zaidi ya kuwadumaza kwa kuwawekea manung'uniko badala ya tija.

Wizara ya elimu inatumiwa sana kufanywa mfano wa ooh tumedhulumiwa hapa, mara pale kuhusu elimu. Mzee Mohamed Said, mtoto anapoanza darasa la kwanza, anahitaji kuidhinishwa na NECTA kuendelea darasa la pili na la tatu? Nauliza hivi kwa sababu, suala la kusoma halionekani kama sehemu ya ustaarabu wa Waislam. Watoto wengi wanaoishia darasa la 5, la 6, la 3 ni Waislam.

Tunaishi mitaani jamani, tunafahamiana. Kama unataka kuisaidia jamii ya kiislamu, basi weka mkazo ktk matatizo yaliyo ndani ya jamii na si kuwarushia maneno Wakristo. Suala la Wakatoliki kuwepo zaidi mashuleni na makazini ni urithi, Wakoloni walioleta dini waliiacha hali hiyo tofauti na Mwarabu aliyewaletea dini yenu kwani hata wao wenyewe hawasomi. Ama unao mfano mmoja wa shule ama zahanati iliojengwa kipindi cha Utawala wa Waarabu hapa East Africa?

Kama Waislam hawatazingatia uzazi wa mpango, basi matatizo yenu yatadumu milele. Hakuna wa kumlaumu ikiwa wenzenu walioamua kusoma wametokea upande wa pili. Kama mtu mmoja anazaa watoto 9 ambao hawezi kuwasomesha hata elimu ya msingi, unadhani kuna mmoja kati yao atainuka? Tena cha ajabu, aliye maskini zaidi ndie huzaa zaidi na huyo watoto wake shuleni hawafuatilii, lkn Sheikh Ponda anapoitisha maandamano dhidi ya NECTA naye ni wa mbele wakati watoto wake wameishia darasa huyu la 3, yule la 5, mwingine alimaliza la saba lkn hakufanya mtihani n.k

Mimi naamini ungetumia muda wako vizuri kushauriana na wenzako kwa yale yaliyo ya heri. Wakoloni walitudhulumu na kuendeleza nchi zao, Je Afrika kama dola, ikae chini kuwalaumu wakoloni au kusonga mbele? Ashakum si matusi, ni upumbavu kulalama miaka nenda rudi huku huchukui juhudi zozote za kusonga za kusogea mbele.

Hebu tazama chuo cha MUM, kinaenda mbele au nyuma? Ongea maendeleo mzee, sifa za kutafuta umaarufu hazina mashiko, unawadumaza wanaokuamini na kuwafanya waamini kuwa NECTA ikiongozwa na muislam watafaulu hata kama hawasomi.

Msione majengo ya Kanisa yanasimama, ni umoja na mazoea ya kuchangia. Kama jimbo zima au kanda inachangia Zahanati ya Parokia, lzm itamalizika tu, na tukishamaliza moja tunawachangia na wenzetu, hivyo ndio tumezoea, lkn kwenu ubinafsi na umaarufu kama wako ndio unatukuzwa. Ukiona msikiti unapendeza basi hapo ni mwarabu kajitolea, lkn nyinyi wenyewe hamna utaratibu wa kujitoa. Kama msikiti ni duni, wenye msikiti huo watajenga shule au Zahanati kweli?
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said,

..je, FEZA nao wanalalamikia utendaji wa NECTA?

..umewahi kufika FEZA ukaona mazingira wanayosoma??

..kwanini msiungane na FEZA mkafungua angalau shule 5 za kikanda zitoe cream ya Waislamu kwenda vyuo vya elimu ya juu??

..mimi nadhani malalamiko ya Waislamu dhidi ya NECTA au wizara ya elimu hayawezi kuzaa matunda mnayoyatarajia.

..Waislamu mnalalamikia teuzi za watendaji wakuu, badala ya kujielekeza ktk kulalamikia VIWANGO vya elimu vinavyotolewa kwa wa-Tanzania wote.

..sasa hivi wizara ya elimu ktk awamu hii ya JK kwa muda mrefu imekuwa ikiongozwa na Waislamu.

..Je, umeona kitu kimebadilika kuwa na ahueni, tangu waingie wakina Jumanne Maghembe, Mwatumu Mahiza, Shukuru Kawambwa, Hamisi Dihenga??

..si afadhali hata enzi za kina Tabitha Siwale wanafunzi walikuwa wanahitimu darasa la 7 wanajua kusoma na kuandika. Hii elimu wanayotoa wakina Jumanne, Shukuru, na Hamisi, tunapata wahitimu wa darasa la 7 wasiojua kusoma na kuandika.

..lakini hayo sijawasikia Waislamu wakiwaandama Shukuru na Hamisi pale wizarani kwamba kulikoni muongoze wizara ya elimu halafu kuna wahitimu std 7 hawajui kusoma na kuandika?? badala yake mnamuandama huyu mama wa NECTA kwasababu ya dini yake.

Jamani dhambi ya udini itatutafuna, tuvumiliane jamani
 
Mimi kimsingi historia ya uhuru wetu siijui vyema lakini naona sio busara kulaumiana kiasi cha kuandika vitabu kudhoofisha juhudi za waasisi wa taifa hili tusahau yalio kua mapungufu tuangalie mbele
 
Maaskofu kama wawakilishi wa wakristo wametimiza wajibu wao kwa kutoa dukuduku lao. Naamini pia na wawakilishi wa waislamu wamefanya hivyo au watafanya hivyo. Katika andiko la maaskofu, kitu mhimu kilichojitokeza ni hoja ya kila wanachoamini ni sawa na mapendekezo yao. Baadhi ya wachangiani wenzangu mnakebehi andiko la viongozi wenu wa dini mnavyotumia lugha ya kejeli na matusi dhidi ya wengine kwa kile mnachodhani ni kuunga mkono andiko la maaskofu. Watanzania hii changamoto ya udini inajitokeza kwa sura isiyo ya kawaida kwa mara ya kwanza sasa. Tunapaswa kuwa makini sana katika kauli zetu tukizingatia kwamba mgogoro wa kidini ni jambo zito sana linaloweza kuwa na madhara yasiyorekebishika. Tuwaunge mkono viongozi wa dini kwa kuliombea taifa letu kuendelea kuwa na amani na kuwaombea viongozi wa dola kuwa na hekima na busara zaidi kuweza kukabiliana na changamoto hii. Na hivyo hivyo kwa viongozi wetu wa dini na wananchi kwa ujumla.
 
Mohammed Said naomba pia utueleze kwanini mahali kote alikopita Mwarabu watu hawafanyi kazi kwa bidii ( Umwinyi). Mfano ukienda pwani utaona watu wanaongea kama chiliku na hawafanyi kazi. Nenda pale pangani uone kila nyumba inakibalaza cha kupigia soga, nini sababu. Nenda pwani umpe mtu kibarua shambani uone kama ataweza. Unadhani hao watu waliozoea kufunga msuli na kunywa kahawa hadi saa sita wanaweza kusoma?

Waarabu walijenga misikiti, wazungu makanisa, shule na zahanati. Utofauti wetu ni matokeo ya historia yetu tuacha kukamatana uchawi. Hata leo hii elimu ya waarabu, technolojia uwezi linganisha na wazungu au wayahudi. Mohammedi fanya utafiti na uache lawama
 
Back
Top Bottom