Maandamano ya Aprili 26, 2018: Yanayojiri kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi

Status
Not open for further replies.
mkuu, kuna analysis nyingi sana

mange kafuta maandamano yote yajayo pia!!
Ukiendekeza mbwa atakufuata mpaka msikitini. Serikali imechezeshwa ngoma na huyu dada. Kuna watu watakuwa wanafurahi kuwa Mange na kundi lake wameshindwa lakini mimi naona kama aliyepoteza hapa ni serikali and co! Wamepoteza kwa sababu wameonyesha dalili zote za kugwaya kwa mtu ambaye yupo mbali na anatumia vidole tu ku-type. Hebu fikiria upande mmoja yuko mwanamke mmoja tena mwenye mwili mdogo mdogo amejikali kwenye computer/simu ana-type na upande mwingine wamekaa makundi kwa makundi ya maaskari wanaruka ruka na kuzunguka mitaani kama vichaa! Kulikuwa na umuhimu wa kufanya hayo yote isipokuwa ni over-reaction ya vyombo vya usalama? Yaani mpaka yeye nadhani hakuwa anaamini kama anaweza kuwapelekesha namna hii! Na mbaya zaidi amenogewa... anasema sasa hivi anavizia serikali ifanye tukio lolote baya (kwa bahati mbaya au kwa uzembe kwa makusudi) ili akiamshe tena! Huoni hapo ameiweka serikali kwenye mtihani mkubwa? Hii inanikumbusha kuishi sehemu zenye vibaka... Unakuwa umejenga nyumba yako nzuuuuri lakini usiku na mchana huna raha kwa wasiwasi wa kuvamiwa! Tafakari!
 
Ukiweza kuchunga ng'ombe huwezi shindwa kuongoza watanzania, Kwa hali hii kweli slow yuko Right hakuna mbunge wa upinzani atakaerudi bungeni,labda wajisalimishe tu kuunga mkono wakitaka kurudi
Unakosea kufikiri kuwa maandamano haya yalikuwa ya wapinzani..., yaani Chadema au CUF.. Kumbuka Mange alionya sana kuhusu kujihusisha kwao...
Lakini kwa kusema ukweli.., kama maandamano haya yangeitishwa na vyama vya upinzani..., hali ingekua tofauti..
 
Ukweli mchungu...
Wapinzani mkubali tu rais Magufuli kawashika sehemu mbaya mno. Its a time to let him be na wananchi wanamuelewa mno. Maana ingekuwa rais hakubaliki ukweli mchungu tungeona hata rasharasha kwenye mikoa ya Arusha na Mbeya ambapo ufipa wanapaona ni nyumbani, Nasema haya.

Hakuna siku tuliowachache tulitegemea viongozi wa upinzani mngempa sapoti huyo mwenyekiti wenu mpya(Mange) kuhoji mahali trilioni 1.5 zilipo kama leo. Kwa kuingia barabarani. Rejea twitter ya Msigwa kuhusu haya maandamano

Hakuna siku wale wafia upinzani mostly wale wa mtandaoni wangetoa sapoti kwa mwenyekiti na msemaji wa upinzani (Mange) kuhoji yale yote ambayo mmekuwa mkiitisha press kuyahoji.

Sasa najiuliza mtaweza vipi kutushawishi sisi wananchi kuanzia kesho kuhusu hizo trilioni 1.5. Kama tu kelele zenu zimeshindwa kuwapa hasira wananchi including nyie wenyewe...?

Serious ukweli lazima tuseme kwa sasa hamueleweki huyu jamaa kawashika vibaya. 2020 hamtazidi 5 bungeni. Mwenye uhakika ni Prof...Jay.....
Na ndio msahau tena habari za MAANDAMANO kwenye utawala huu....mmeharibu mno
Wenye kujitambua wamekuelewa!
 
Wewe na Mange kwa matusi hamna tofauti kwahiyo nitakuacha hivyo hivyo kama ulivyo kwani nikikutukana na mimi nitakuwa kama nyinyi!! Serikali imetumia muda na mali nyingi kujaribu kuthibiti maandamano ambayo yalitakiwa kupuuzwa na busara zitumike kusikiliza malalamiko ya wananchi na kutafuta ufumbuzi!!
UKIJIBIZANA NA MWENDAWAZIMU NA WEWE UTADHANIWA MWENDAWAZIMU PIA!!!
Narudia kukuambia ficha upumbavu wako
Serikali imsikilize anaye t
 
Mimi nilichojifunza kwa utulivu uliokuwa
mjini leo ni kwamba tukiwa na siku tatu
mfululizo kama leo,lazima tutasikia
malalamiko kutoka kwa wafanya biashara.
 
Kwa tarifa yako CHADEMA wamehusika sana kuratibu haya maandamano nyuma ya PAZIA...Kukuthibitishia hili rejea twiter ya msigwa
Mkaona muizime na jamii forums
Mnaogopa Nini
Polis wameandamana kwa hisani ya mange Kimambi
 
Phase II ni Kukokotoa. Mjinga ni mjinga tu kama Phase I ilikuwa ya kutishia mbona hamkuweka wazi . Mi na jua mtoto mchanga akikunja ngumi huyo amejipanga NENDA MAZIMA. Thats how Serkali imefanya
 
Kwa tarifa yako CHADEMA wamehusika sana kuratibu haya maandamano nyuma ya PAZIA...Kukuthibitishia hili rejea twiter ya msigwa
True
Alafu wakisha shindwa jambo huliruka futi elfu walahi!
 
Sio kwamba yamezuiwa kwa nguvu ila ni waandamanaji wameamua kutoandamana
Hata wangetokeza zamira ya kuzima ilikuwa iko tayari na imara. Kipindi hichi, kilikuwa sio cha kutania, usalama walijipanga vilivyo.
 
Nimeziona mkuu, ufipa ni shida! Walitanda lila kona ya nchi, hawa jamaa na kamanda wao mange ni mashujaa wa kuigwa.
Boya anapokejeli huku haki zake zinaminywa..nyie sio wanaume bali ni majike yenye sura za kiume..subirini kupimwa matezi dume tu..maana hakuna jinsi..i wish Nyerere was alive to witness..this coward..in state house..mungu amrehemu shujaa wa kweli!
 
Kwanza umemwelewa mleta thread?? Kauliza swali kwamba; Pilika pilika za majeshi yetu zisizo za lazima na hadi sherehe fupi fupi za Sikukuu yetu tena bubu, Je tuone kama mafanikio kwa Mange?? Ni swali tu ila usimpinge kwa hoja zisizoendana na mada. Si ungemjibu Hapana au ndiyo kwa sababu kadhaa?? Mfano, Wadhani kuwa migari yote, pikipiki na masilaha waliyoonesha majeshi yetu mitaani ni gharama kidogo?? Nadhani huy dada ni wa kudhibiti kwa hali yeyote ile. Amelitia taifa hasara kubwa. Nalaani wazo lake lililotufanya tutumie fedha iso na mpango leo. Nisingependa aungwe mkono kwa vyovyote
Nimemwelewa vizuri sana mtoa mada. Na kwa nyongeza tu kama lengo la kuitisha hayo maandamano ilikuwa ni kufanya surbotage of our resources basi anatakiwa kuchukiwa na kila anayeliombea mema taifa hili.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom