Maandamano pekee yanatosha kuonesha utekelezaji wa 4R na Demokrasia kukua nchini?

Precious Diamond

JF-Expert Member
Jun 9, 2023
397
993
Wakuu,

Baada ya polisi kutoa tamko la maandamano kufanyika nchini, kila kona ni sifa tu kuwa 4R zimefanyiwa kazi, demokrasia imekuwa nchini, mama ametenda na kadha wa kadha, huku pongezi za akina Mbowe, Sugu zikitumika kama rejea ya kuwa hata wapinzani wenyewe wanakubali kuwa sasa Tanzania Demokrasia imekua kwelikweli.

Swali ni je, Maandamano haya pekee yanatosha kuwa kipimo cha demokrasia iliyokomaa nchini?

Uhuru wa vyombo vya habari bado ni changamoto kubwa, uhuru wa kujieleza bado nako, Watanzania wanakimbia kuwekeza nchini na kwenda nchi jirani sababu mazingira ya kuwekeza nchini ni mabovu, kodi chungu mzima zinazoongeza mzingo mzito kwa wananchi, ubadhirifu wa mali ya umma uko juu mpaka wanaambiwa wale kwa urefu wa kamba zao ripoti za CAG zinakuwa kama karatasi za makumbusho, bidhaa ziko juu na maisha yanaendelea kuwa magumu, huduma za kijamii mbovu mpakaka leo baada ya miaka 60+ bado tuna kampeni za kumtua mama ndoo, umeme changamoto maji safi shida nk, polisi hawana haki ya kuzuia maandamano kufanyika, jukumu lao ni kutoa ulinzi na kama ikitokea siku iliyotakiwa kufanya maandamano kuna kitu kinazuia polisi wanatakiwa kutoa siku nyingine.

Maandamano, mikutano ya hadhara sio hisani kusema Rais amefanya jambo kubwa kuleta kitu ambacho katiba hakikua imeruhusu, hakupaswa kuhushukuriwa kwa kurudisha au kuruhusu kitu ambacho tayari kimeruhusiwa na katiba, ilitakiwa awajibike kwa kwenda kinyume na Katiba!

Maandamano pekee yanatosha kuonesha utekelezaji kabambe wa 4R za Rais? Maandamano pekee yanatosha kuonesha Demokrasia imekua nchini?
 
Baada ya polisi kutoa tamko la maandamano kufanyika nchini, kila kona ni sifa tu kuwa 4R zimefanyiwa kazi, demokrasia imekuwa nchini, mama ametenda na kadha wa kadha, huku pongezi za akina Mbowe, Sugu zikitumika kama rejea ya kuwa hata wapinzani wenyewe wanakubali kuwa sasa Tanzania Demokrasia imekua kwelikweli.
Naa kama yangezuiwa wewe binafsi ungekuja na statement gani?
 
Yale yaliyokuwa yakizuiwa yalikua on which grounds
Ubabe ulitumika na Katiba ilivunjwa, kusema hiki sio kipindi cha kufanya siasa tufocus kwenye kujenga nchi ni matumizi ya mabavu yaliyotakiwa kupigiwa kelele. Sasa tuko hapa, turudi kwa mada, maandamano pekee ndio kiashiria cha demokrasia na 4R kutimizwa wakati mengine yako ovyo na kuchechemea?
 
Maandamano, uhuru wa kukusanyika kwa amani, uhuru wa kujieleza, na kadhalika, ni haki zilizopo kwenye katiba.

Yote hayo si hisani ya Samia, kama zilivyo pesa za walipa kodi, siyo pesa zake huyo Samia.

Tuko deprived sana kiasi kwamba hata haki zetu za msingi tunaona ni miujiza ya Rais Samia.

Ignorance plus deprivation = dumbass people.
4R ya Samia Inatekelezwa Kwa vitendo na Machadema
 
maandamano pekee ndio kiashiria cha demokrasia na 4R kutimizwa wakati mengine yako ovyo na kuchechemea?
Viashiria muhimu ni Wananchi wote kupata haki zetu zote za msingi kama maji, umeme, elimu, afya, miundombinu, ajira, mazingira rafiki ya biashara na kilimo pamoja na uwezo wa kuchagua viongozi.
 
Wakuu,
Baada ya polisi kutoa tamko la maandamano kufanyika nchini, kila kona ni sifa tu kuwa 4R zimefanyiwa kazi, demokrasia imekuwa nchini, mama ametenda na kadha wa kadha, huku pongezi za akina Mbowe, Sugu zikitumika kama rejea ya kuwa hata wapinzani wenyewe wanakubali kuwa sasa Tanzania Demokrasia imekua kwelikweli.

Swali ni je, Maandamano haya pekee yanatosha kuwa kipimo cha demokrasia iliyokomaa nchini?

Maandamano, mikutano ya hadhara sio hisani kusema Rais amefanya jambo kubwa kuleta kitu ambacho katiba hakikua imeruhusu, hakupaswa kuhushukuriwa kwa kurudisha au kuruhusu kitu ambacho tayari kimeruhusiwa na katiba, ilitakiwa awajibike kwa kwenda kinyume na Katiba!

Maandamano pekee yanatosha kuonesha utekelezaji kabambe wa 4R za Rais? Maandamano pekee yanatosha kuonesha Demokrasia imekua nchini?
Tanzania bado ni demokrasia changa, haki zilizotolewa kwenye katiba yetu zimegeuzwa ni hisani kwa watawala, niliuliza humu Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini? ?.

Maandamano ni haki, na tunamshukuru sana Rais Samia awamu hii, amerejesha haki ya mikutano na haki ya kuandamana kwa kuzingatia ushauri huu Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu

Huu ni mwanzo mzuri, ila safari ya kuelekea kwenye demokrasia ya kweli na haki za kweli bado ni ndefu!. Haki ya kuchagua na kuchaguliwa bado imefinyangwa!, tunamuomba Rais Samia atekeleze na hili Ombi kwa Rais Samia: Japo wengi wape, wachache pia wasikilizwe, Hoja ya kufanya minimum reforms za Katiba ni hoja ya msingi sana kuliko hata Sheria!.
P
 
Tanzania bado ni demokrasia changa, haki zilizotolewa kwenye katiba yetu zimegeuzwa ni hisani kwa watawala, niliuliza humu Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini? ?.

Maandamano ni haki, na tunamshukuru sana Rais Samia awamu hii, amerejesha haki ya mikutano na haki ya kuandamana kwa kuzingatia ushauri huu Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu

Huu ni mwanzo mzuri, ila safari ya kuelekea kwenye demokrasia ya kweli na haki za kweli bado ni ndefu!. Haki ya kuchagua na kuchaguliwa bado imefinyangwa!, tunamuomba Rais Samia atekeleze na hili Ombi kwa Rais Samia: Japo wengi wape, wachache pia wasikilizwe, Hoja ya kufanya minimum reforms za Katiba ni hoja ya msingi sana kuliko hata Sheria!.
P
Umesema vyema Mkuu
 
Back
Top Bottom