KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,139
Maandamano makubwa yanatarajiwa kufanyika nchi nzima kumpongeza Rais Kikwete na kamati kuu ya CCM kiujumla kwa kufanya kuchukua maamuzi magumu ya kulifanyia mabadiliko makubwa baraza la mawaziri.
Rais kikwete ameamua kufanya maamuzi magumu hayo licha ya kwamba kuna jukumu zito la maandalizi ya bajeti za wizara na kwa hiyo ni changamoto kubwa kuingiza watu wapya kwa maana ya nafasi za mawaziri, lakini hata hivyo, hao wapya itabidi wategemee zaidi mihtasari ya watendaji watakaokuwapo katika kila wizara husika itakayoguswa na mabadiliko.
Wananchi mbalimbali nchini wamepongeza hatua hiyo ibnayotarajiwa kuchuliwa na rais kikwete huku wakisema kwamba hatua hiyo itaifanya ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iwe na nguvu kubwa ya kuisaidia serikali kupambana na ubadhirifu unaofanywa na mawaziri kwa kushirikiana na watendaji wa serikali wasio waaminifu.
Naye mbunge zitto kabwe ambae alishikia bango hoja ya kutaka bunge lipige kura ya kutokua na imani na waziri mkuu,akizungumza bungeni wiki juzi aliwapasha mawaziri kwa kuwaambia ''Mawaziri msimsingizie Raisi na kumchafua kwa uzembe wenu na ubaridhifu wenu wa kushindwa kusimamia mali na pesa za walipa kodi kwa manufaa yenu binafsi i lazima muwajibike na mchukuliwe hatua stahiki''
Rais kikwete ameamua kufanya maamuzi magumu hayo licha ya kwamba kuna jukumu zito la maandalizi ya bajeti za wizara na kwa hiyo ni changamoto kubwa kuingiza watu wapya kwa maana ya nafasi za mawaziri, lakini hata hivyo, hao wapya itabidi wategemee zaidi mihtasari ya watendaji watakaokuwapo katika kila wizara husika itakayoguswa na mabadiliko.
Wananchi mbalimbali nchini wamepongeza hatua hiyo ibnayotarajiwa kuchuliwa na rais kikwete huku wakisema kwamba hatua hiyo itaifanya ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iwe na nguvu kubwa ya kuisaidia serikali kupambana na ubadhirifu unaofanywa na mawaziri kwa kushirikiana na watendaji wa serikali wasio waaminifu.
Naye mbunge zitto kabwe ambae alishikia bango hoja ya kutaka bunge lipige kura ya kutokua na imani na waziri mkuu,akizungumza bungeni wiki juzi aliwapasha mawaziri kwa kuwaambia ''Mawaziri msimsingizie Raisi na kumchafua kwa uzembe wenu na ubaridhifu wenu wa kushindwa kusimamia mali na pesa za walipa kodi kwa manufaa yenu binafsi i lazima muwajibike na mchukuliwe hatua stahiki''