Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Tunapoelekea uchaguzi tutaona mengi.
Tangu jana yamekua yakipita matangazo hapa mjini kwamba wana ccm watakuwa na maandamano ya kuunga mkono utekelezaji wa ilani za chama na utahutubiwa na mjumbe wa nini sijui wa umoja wa watoto (No nilimaanisha vijana) wa ccm taifa.
Kama ilivyo ada nadhani ilikuwa ni kujaribu kupiku yale yaliyofanyika hivi karibuni wakati Lwakatare akipokewa rasmi CHADEMA.
Pia nadhani kupoza hali tete iliyojitokeza tokana na hotuba ya Dr Slaa hapa Bukoba kuhusiana na hali tete ya udhibiti wa uchumi wa nchi yetu.
Nimeshangaa kuona kikundi si cha zaidi ya watu mia moja tu wakifanya maandamano hali isiyo ya kawaida.
Sasa najiuliza je hii inaonyesha ni kiasi gani watu wameanza kukata tamaa na chama hiki? Je kama hali ndiyo hii 2010 mambo si yatakuwa hatari zaidi?
Tangu jana yamekua yakipita matangazo hapa mjini kwamba wana ccm watakuwa na maandamano ya kuunga mkono utekelezaji wa ilani za chama na utahutubiwa na mjumbe wa nini sijui wa umoja wa watoto (No nilimaanisha vijana) wa ccm taifa.
Kama ilivyo ada nadhani ilikuwa ni kujaribu kupiku yale yaliyofanyika hivi karibuni wakati Lwakatare akipokewa rasmi CHADEMA.
Pia nadhani kupoza hali tete iliyojitokeza tokana na hotuba ya Dr Slaa hapa Bukoba kuhusiana na hali tete ya udhibiti wa uchumi wa nchi yetu.
Nimeshangaa kuona kikundi si cha zaidi ya watu mia moja tu wakifanya maandamano hali isiyo ya kawaida.
Sasa najiuliza je hii inaonyesha ni kiasi gani watu wameanza kukata tamaa na chama hiki? Je kama hali ndiyo hii 2010 mambo si yatakuwa hatari zaidi?