AzimiolaArusha
Senior Member
- Nov 9, 2011
- 141
- 88
Yaani hapa polisi wamechemsha, wanazidi kumpandisha chati na nafikiri sasa ndio ujumbe utafika kwa walengwa vizuri, sema tu pamoja na ufanyaji kazi wa kupendelea wa jeshi la polisi, bado kuna polisi wengi sana wanaowasupport wananchi!!! wapo wengi sana na very soon hawa wazee wa zamani watakubakubali kuwa jeshi lina vijana walio na mtazamo tofauti ambao hawawezi kuuona kwenye macho yao wala maneno yao wala tabia zao bali Mioyo yao!!!!Hivi huu si mwanzo wa wa udikteta? Uhuru wa mawazo unaolindwa na katiba uko wapi? Leo ni Samson Mwigamba kesho ni nani? Mimi niliyeandika makala ile kwa ufipi JF au ni mtandao wote wa JF?
Pili, Hivi ni haki serikali ya kutumia sheria ya uchochezi iliyotungwa enzi za ukoloni ambayo wameikopi na kuipaste na kwa faida ya nani? Tunaadimisha miaka hamsini ya uhuru gani kwa staili hii?