M/kiti wa CHADEMA mkoa wa Arusha akamatwa na kuswekwa rumande - kisa makala ya uchochezi

Mojawapoa ya quality za mwanamapinduzi halisi, ni utashi wa kutovumilia mmoja wa wale wanaofikiriwa kama wana Mapinduzi anapoonewa ama Kunyanyaswa.
Binafsi, nimesikitishwa sana na Mpigania haki Bwana Mwigamba kukamatwa na Mapolisi kwa Makala yake. Uko wapi Uhuru wa Kutoa Maoni unaohubiriwa katika Katiba.

Kiukweli Polisi wamedhihirisha uwezo wao wa kutofikiri kwa kumkamata Mwigamba, na kwa Mtindo huu hata mimi najiona Rumande siku si Nyingi.

Polisi wamekuwa kama wazinzi ambao kila siku wanaenda kanisani na kuhubiria kutozini, lakini akiwa palepale kanisani anamtamani muumini mwenzake, au mwanakwaya mwenye pete ya ndoa ati kwa kuwa ana sauti nzuri..Mfano wangu ukiufikiria kwa juu juu hutauelewa lakini kimsingi nimekumbuka nilivyomuuliza ndugu yangu askari polisi aliyetumwa kuwadhibiti wafuasi wa Chadema pale Shinyanga baada ya Kura za ubunge kuchakachuliwa, nilimuulliza hivi;
'Unadhani Chadema ilishinda? Akajibu 'Ndiyo',
Nikamuuliza tena wewe ulikuwa unalinda kura pale ofisini ulishuhudia uchakachuaji? akasema 'Ndiyo' ,
Nikamuuliza tena ulitambua kuwa Haki ya Mtanzania unapindishwa? Akasema 'Ndiyo'.
Nikamuuliza ulipoamriwa kuwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wadai kuibiwa kura uliwatawanya? akajibu 'Ndiyo'
Nikamuuliza unadhani ulitumia akili yako sawasawa? akakosa Jibu

Hilo ndilo analoongelea Mwigamba. Mojawapo ya watu wanaochelewesha Mapinduzi ya kidiplomasia katika Nchi zetu za Afrika ni Maaskari polisi!

Nikakumbuka pia nilivyohadithiwa na Rafiki yangu mmoja kule Tarime miaka fulani ya nyuma sana wakati Maaskari wanatafuta siraha, walikuwa wanawalazimisha wanaume kuwalala mama zao kama option ya kutaja Silaha ziko wapi..........'Uvunjifu Mkubwa wa Haki za Kibinadamu!


Okay Tuache porojo sasa
Suala la Msingi hapa ni kuwa je tuko tayari uona wana harakati wanakamatwa na kushitakiwa wakati tukiwa Kimya? Maana kama wewe ni mwanaharakati kweli ujue ni zamu yako......
Na kwa kuwa tunafumba macho na Kusikitika Kimoyomoyo kwa Mwigamba..basi Sheria ya katiba ikianza kutumika, sisi tunaojiita wanaharakati tutaozea jela .....na watu watasikitika kimoyomoyo tu na Maisha yao yataendelea

Hapo ndipo unapoona Akili zetu zilivyolala
Akili za Kusherekea Uhuru ambao watu wanaishi Maisha ya kiutumwa nchini mwao
Kuna Utumwa mkubwa zaidi ya umasikini?

Yaani nina Uchungu kwelikweli............................

Tuanzie kwako! Dhamana ilikuwa wazi, ww hukuwepo mahakamani? Huna hiyo mali ya mil 5 isiyohamishika?

Haya viongozi wa chadema wote hakukuwa hata na mmoja alikuwa tayari kuona huyo bwana halali selo?

Anza ww kuonyesha mfano wakumsaidia nasi tutakuja
 
Watanzania leo tunasherekea miaka 50 ya uhuru wa ilyokuwa Tanganyika. Wakati wa kupigania uhuru wananchi wote waliungana kuhakikisha kuwa mkoloni anaondolewa madarakani ili Watanganyika wajitawale wenyewe. Kujitawala wenyewe haikuwa na maana nyingine zaidi ya watu kujiamulia mambo yao wenyewe. Huo ndio ulikuwa msingi wa kupigania uhuru.

Leo tunapoadhimisha miaka 50 ya uhuru katika nchi huru yenye katiba yake iweje tunataka kurudi nyuma? Kwanini uhuru wa mawazo anaoutumia Mwigamba ambao umeruhusiwa na katiba ya nchi unyang'anywe? Kwani watu tulio huru kujiamulia mambo yetu tuburuzwe na serikali? Tukirejea matukkio ya uchaguzi mkuu mwaka 2010 yalitokea mengi yanayohuzunisha. Mojawapo lilikuwa la matokeo ya kura za wabunge kutokutangazwa hadi wananchi walipovamia wasimamizi wa uchaguzi. Aina hii ya uchaguzi ni ya uchaguzi katika nchi huru kweli? Lingine liliokuwa maarufu sana lilikuwa suala la uchakachuaji kura. Katika nchi huru ambayo ni ya kidemokrasia, kwanini kuwe na uchakachuaji wa kura?

Kuna haja ya kuangalia kwa makini huu mwelekeo wetu na uhuru wetu jinsi serikali na vyombo vyake wanavyoendesha mambo. Hata kama serikali itasema uhuru una mipaka, ni nini maana ya mipaka? Wananchi wakikusanyika na kuishangilia timu ya mpira hakuna tatizo lakini wakikusanyika na kujadili mambo yao chini ya mwamvuli wa chama wanavunja amani hata kama wanchojadili ni kwa ajili ya maslahi ya Taifa.

Tutambue kuwa kwa mwelekeo huu wa uongozi wa nchi hii, uhuru wetu tulioupata mwaka 1961 umetekwa na wajanja na hivyo wameanza kututawala. Tofauti kati ya watawala wa kikoloni na wa sasa ni rangi zao na kwamba wakoloni walikuwa wamtoka nje ya mipaka yetu ila hao wametoka humu humu. Hivyo wale walikuwa watawala wa nje lakin hawa wa sasa ni wa ndani. Wanatawala hawa wa sasa na wale wa kikoloni wanafana katika kutowajali raia, kutowasikiliza, kuwanyima uhuru wa kutoa maoni, kuwakandamiza na kuwafanya wanyonge.
 
Jmani ametolewa au ndio mpaka Jumatatu duh kweli wameamua lakini ipo siku watajuta.
 
Ukweli siku zote hujitenga na ukweli..c muda mrefu aibu iliyowafika kwa Muro itawaanika kwa mara nyingine tena jinsi askari wa Tanzania wanavyotumia akili za watu wengine kutekeleza majukumu yao. Ndio maana hata wakiambiwa ishi kwenye vibanda vya mbwa hawaoni hatari kutii amri..NDIO AFANDE! Ndio askari wetu jamani wengi wao ni zao la watu waliofeli na kukosa mwalekeo wa maisha kwa nini wasitii kila kitu..
 
Anayestahili kuhojiwa hapa ni mhariri wala si huyu bwana. Hata hivyo hakuna uchochezi hapa. Polisi wanautaratibu zao za kazi wala hawawezi kutegemea mawazo ya huyu bwana. Manumba Fanya kazi yako vizuri kwa kufuata sheria.
 
Hii nimeipenda na inanionyesha kuwa ukombozi wa Tanzania uko karibu.Usanii huu una mwisho kwani hata askari wetu hawaifurahii isipokuwa wachache wanaotumiwa kuwaburuza wenzao.Mungu yakwamishe mipango ya baradhuli hawa tuikomboe nchi yetu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Nasikia Manumba ni graduate, ni kweli???

Alafu alichoandika Samson ni kweli. Mwaka 2010 graduates waliotakiwa kwenda Polisi ni kama 50 hivi lakini baada ya kufika CCP sidhani kama walimaliza wote. Rafiki yangu mmoja aliyekuwa ka fail form six na kwenda Polisi alinidokeza kuwa walikuwa wana magraduate kibao lakini wengi walitoroka na kuacha mafunzo. Sababu?? nadhani ni upuuzi huu wa mafunzo yasiyo na dira zaidi ya kutii kila upuuzi.

Na nisingejua haya yote maana sikuwa nimesoma gazeti hili. Na nina hakika Polisi wengi watakuwa wamesoma ujumbe huu tokana na mtafaruku huu.

Hata hivyo kwa jinsi nijuavyo kwa sasa Polisi wengi wako upande wa wananchi. Ni muda tu, utathibitisha haya nisemayo. Wacha wacheze na moto.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Tuanzie kwako! Dhamana ilikuwa wazi, ww hukuwepo mahakamani? Huna hiyo mali ya mil 5 isiyohamishika?

Haya viongozi wa chadema wote hakukuwa hata na mmoja alikuwa tayari kuona huyo bwana halali selo?

Anza ww kuonyesha mfano wakumsaidia nasi tutakuja

Sikufahamu na sina nia ya kukutukana hata kama ningekuwa nakufahamu, ila acha nikujibu kama ifuatavyo na majibu haya Yanawalenga wote wenye mtizao,fikra na mawazo Finyu kama yako

Mtazamo wa Kwamba viongozi wa Chadema ndiyo Wahusike moja kwa Moja ni mtazamo hasi . Ili Nchi yetu iweze kufika kule tunakotakiwa kufika ni lazima kila mmoja achukue leading role. Iwapo utakuwa unasubiri Viongozi ndo wachukue hatua hutakuwa na tofauti na askari Polisi aliyemwongelea Mwigamba 'anayepokea amri pasipo na kutekeleza pasipo kufikiri'. Iwapo sisi tunaojiita wanamapinduzi tunawasubiri viongozi wachukue hatua pale mmoja wetu anapoonewa huo ni uanamapinduzi wa kinafiki na hufai kuitwa mwanamapinduzi. Mapinduzi ninayoongelea hapa si Mapinduzi ya mtutu wa Bunduki bali Mapinduzi ya Fikra. Tulipofikia sasa ni sawa na Maaskari walioko vitani na Kamanda wa jeshi ameshauliwa na ni kazi ya wanajeshi walobaki kuiokoa nchi. Katika hali kama hii kumpoteza mwanajeshi mwingine kwa uonevu wa kijinga na hasara, kwani kesho yaweza kuwa zamu yangu usipopigania haki kumwokoa. Nawe kesho utakamatwa kwa kosa fulani nasi tutakuangalia na kukusikitikia tukisubiri bosi wako akuokoe....Thats Cowardly ! Ili kuikomboa Tanzania tunahitaji uwanja wa kusema na kuwakemea wanaoturudisha nyumba tukiwa na uhakika wa Mazingira yanayojenga Impunity. Kwa mfumo wa kamatakamata huu uluianza...ni kuondoa uhuru wa kupigania haki, usawa na ustawi ktk Tanzania

Nirudi katika hoja yako ya 'Anza ww kuonyesha mfano wakumsaidia nasi tutakuja'
Hapa ndugu yangu ndo umeonesha utoto wa hali ya juu katika fikra. Kwa kuwa umesita 'kuanza' kuna Guarantee gani kwamba nikianza mimi wewe 'utafuata'? Je Sababu iliyokufanya Ushindwe kuanza itakusamehe ili ufuate nikianza?

Katika saikologia, 'Lack of self confidence' haijioneshi kwa tatizo moja tu, Ni sawa na kumwambia rafiki yako aanze kukutongozea binti halafu utaendelea. Tatizo kubwa liko katika kuanzisha tabia, iwapo unashindwa kuanzisha tabia fulani basi hesabu kuwa umeshashindwa hata kuwafuata wale ambao wanaitenda tabia hiyo. Hapa ndiyo maana nikasema umeonesha utoto na udhaifu mkubwa katika kufikiri na confidently naweza kusema wewe ni mwoga na mnafiki.... Ninyi ndo wale ambao tunakubaliana tuandamane halafu kesho hamuonekani barabarani au mkiona maaskari mwajifungia ndani.. Ninyi ndiyo mnauotusaliti katika maamuzi, kwa kuwa hamna uwezo wa kusimamia maamuzi yenu. Ninyi ndiyo mnaolirudisha nyuma taifa letu kwa Kuwa hamna uthubutu. Ninyi ndiyo mnaosubiri kuona jirani kaanzisha kibanda hapo mtaani ndo nawe unakukuruka kuanzisha hapo hapo mwisho wa siku mnapata hasara....watu wasio na uthubutu!

Kama nilivosema awali, sina nia ya kukutukana hata kama ningekuwa nakufahamu, naweza kuwa nimetumia maneno makali kwa kuwa tu nina uthubutu wa kuyatumia ili kufikisha ujumbe wangu kwako. Nin imani utauchukulia ujumbe huu kwa nia nema ili kubadili fikra zako

Kwa kujibu hoja yako ya Msingi, sikuwa mahakamani wala karibu na mkoa ilipo mahakama hiyo. ilikuwa na nia nzuri tu hata hivyo nimeshapata mawasiliano ya karibu na wahusika sasa najua nitamsaidia vipi.....

Aluta continua....
 
Serikali ya CCM ni ya kidhalimu na kikandamizaji ndiyo maana wanaona njia ya mkato ya kukabiliana na hoja za upinzani ni kutumia majeshi. Kikwete, kama Mungu aishivyo hutaweza kuzima nguvu ya umma hata siku moja, utauwa watu mamia kadhaa lakini hatimaye hao askari unaowafanya kama misukule yako watakataa kutii amri za kidhalimu na mwisho wake utawala wako utaanguka kwa kishindo.
 
Serikali ya CCM ni ya kidhalimu na kikandamizaji ndiyo maana wanaona njia ya mkato ya kukabiliana na hoja za upinzani ni kutumia majeshi.

Kikwete, kama Mungu aishivyo hutaweza kuzima nguvu ya umma hata siku moja, utauwa watu mamia kadhaa lakini hatimaye hao askari unaowafanya kama misukule yako watakataa kutii amri za kidhalimu na mwisho wake utawala wako utaanguka kwa kishindo.
 
Tuanzie kwako! Dhamana ilikuwa wazi, ww hukuwepo mahakamani? Huna hiyo mali ya mil 5 isiyohamishika?

Haya viongozi wa chadema wote hakukuwa hata na mmoja alikuwa tayari kuona huyo bwana halali selo?

Anza ww kuonyesha mfano wakumsaidia nasi tutakuja
Hapana, siyo kwamba viongozi hawakutaka kuhakikisha halali selo, kumbuka viongozi wote walitawanyika nchi nzima juu ya swala la katiba hivyo hakukuwa na mtu wa juu lakini viongozi wa chini walimpa msaada, walitumia muda huo kuhakikisha wanalipiza kisasi.
 
Back
Top Bottom